Amicus Curiae
JF-Expert Member
- Sep 12, 2012
- 4,971
- 6,520
MAWAZO YANGU:
Mimi nafikiri hakuna uhusiano wowote kati ya Ufisadi (Matumizi ya mali ya umma kwa manufaa binafsi) na Chama cha huyo anayefanya/aliyefanya Ufisadi, tuamini kwamba Ufisadi ni tabia ya mtu mwenyewe, kwa mantiki hiyo basi, fisadi anaweza kutoka CHADEMA, CCM, CUF, CWT (Chama cha Walimu Tanzania) au hata SACCOSS.
Siamini kwamba CCM yote imejaa mafisadi, wapo viongozi kutoka CCM wenye hofu na Mungu na wala si mafisadi, halikadhalika si kweli kwamba CHADEMA wote si mafisadi, miongoni mwao wapo mafisadi pia. Tofauti ninayoiona hapa ni idadi ya mafisadi, huenda CCM ikasemekana ina mafisadi wengi kuliko Vyama vingine.
Naamini pia kwamba ufisadi wa CCM unajidhihirisha zaidi kwasababu ni Chama Tawala, tofauti na ufisadi wa Vyama vingine ambavyo havihusiki na utendaji wa moja kwa moja Serikalini.
Nimemaliza...
Mimi nafikiri hakuna uhusiano wowote kati ya Ufisadi (Matumizi ya mali ya umma kwa manufaa binafsi) na Chama cha huyo anayefanya/aliyefanya Ufisadi, tuamini kwamba Ufisadi ni tabia ya mtu mwenyewe, kwa mantiki hiyo basi, fisadi anaweza kutoka CHADEMA, CCM, CUF, CWT (Chama cha Walimu Tanzania) au hata SACCOSS.
Siamini kwamba CCM yote imejaa mafisadi, wapo viongozi kutoka CCM wenye hofu na Mungu na wala si mafisadi, halikadhalika si kweli kwamba CHADEMA wote si mafisadi, miongoni mwao wapo mafisadi pia. Tofauti ninayoiona hapa ni idadi ya mafisadi, huenda CCM ikasemekana ina mafisadi wengi kuliko Vyama vingine.
Naamini pia kwamba ufisadi wa CCM unajidhihirisha zaidi kwasababu ni Chama Tawala, tofauti na ufisadi wa Vyama vingine ambavyo havihusiki na utendaji wa moja kwa moja Serikalini.
Nimemaliza...