Hassan Mwakinyo walitaka nikae kimya ili wanichafue

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
Akizungumzia pambano lake dhidi ya Bondia Julius Indongo wa Namibia katika kuwania Mkanda wa IBA Intercontinetal, Bondia Hassan Mwakinyo amesema tatizo limeanzia kwa promota ambaye ameenda kinyume na makubaliano yao.

Promota ana rekodi tata
Mwanzoni nilisikia taarifa juu ya Promota, kwamba wana tuhuma za kutowalipa mabondia, baada ya makubaliano tukakubaliana kuwa kazi ifanywe kwa kushirikiana ili kila upande uwe na haki ya kuleta wadhamini.

Kwa maana hiyo nilikuwa na haki ya kuleta mabondia ambao walikuwa upande wangu ili wapigane.

Baadaye Promota akakwama katika suala la fedha, hivyo wakahitaji msaada wa kutoka upande mwingine kitu ambacho ni kinyume na makubaliano yetu kwa kuwa wao walitakiwa kusimama mpaka mwisho.

Baadaye wakaingia mkataba na Promota ambaye sisi (timu ya Mwakinyo) hatuna uhusiano naye mzuri, nikawauliza wakasema hizo taarifa hazina ukweli.

Baadaye nikabaini hakuna ukweli katika mazungumzo yake (Promota), ikabidi nianze kurekodi mazungumzo yetu yote kuhusu tukio hilo.

Promota akasema kuwa alishirikisha kampuni nyingine kwa kuwa fedha ya kulipia mkada haikuwepo, ikabidi mimi ndio nilipie mkanda kwa Dola 4,000.

Mpinzani Mkenya ajitoa
Kuhusu mpinzani wangu wa awali (Rayton Okwiri) nadhani aliambiwa na watu kuwa anaenda kupigana na bondia mkubwa, hivyo akapandisha dau ikashindikana kwake.

Wakatafuta mpinzani mwingine kwa haraka, ofa yake ikawa juu zaidi ya waliyokuwa nayo, tukakubaliana kuwa Promota atoe nusu ya pesa nasi tutoe ili aongezewe bondia mpya.

Ilivyofika siku ya kupima uzito nikawaona watu ambao hawakuwa kwenye mipango yetu, wakadai kuwa baada ya kumaliza vipimo tutazungumza.

Baada ya vipimo hakukuwa na kikao chochote, nikapiga simu naambiwa nimeshauzwa, nifanye ninachotaka.

Promota alinichukulia poa labda kwa kuwa aliona amenizidi umri a hakujua misimamo yangu.

Walitaka wauze tiketi kwa kutumia jina langu, labda walitaka mimi nikae kimya ili niharibikiwe.
 
π™Ώπš›πš˜πš–πš˜πšπšŠ πš”πšŠπšπš‘πš’πš‹πš’πšπš’πšœπš‘πšŠ π™Όπš πšŠπš”πš’πš—πš’πš˜ πšŠπš—πšŠπšŒπš‘πšŠπšπšžπšŠ πš–πšŠπš‹πš˜πš—πšπš’πšŠ πš—πš’πšŠπš—πš’πšŠ ,πš πšŠπš”πš’πš–πšπšŠπšπšžπšπš’πšŠ πš–πšŠπš‹πš˜πš—πšπš’πšŠ 𝚠𝚊 πš–πšŠπšŠπš—πšŠ πšŠπš—πšŠπš πšŠπš”πšŠπšπšŠπšŠ πš‘πšŠπšπšŠ πš’πšžπš•πšŽ πš–πš”πšŽπš—πš’πšŠ πš’πš•πš’πš‹πš’πšπš’ πš πšŠπš‹πšŽπš–πš‹πšŽπš•πšŽπš£πšŽ πšœπšŠπš—πšŠ πšŒπš‘πšŠπš–πšŠ πšŒπš‘πšŠ πš—πšπšžπš–πš’ πšŠπšπš›πš’πš”πšŠ πš’πš•πš’ πš”πš’πš”πšžπš‹πšŠπš›πš’ πšŠπš™πš’πšπšŠπš—πšŽ πš—πšŠ πš–πš πšŠπš”πš’πš—πš’πš˜ πš”πš πšŠπš—πš’ πš‘πšŠπš”πšžπš πšŠ πš—πšŠ πšœπš’πšπšŠ
 
Akizungumzia pambano lake dhidi ya Bondia Julius Indongo wa Namibia katika kuwania Mkanda wa IBA Intercontinetal, Bondia Hassan Mwakinyo amesema tatizo limeanzia kwa promota ambaye ameenda kinyume na makubaliano yao.

Promota ana rekodi tata
Mwanzoni nilisikia taarifa juu ya Promota, kwamba wana tuhuma za kutowalipa mabondia, baada ya makubaliano tukakubaliana kuwa kazi ifanywe kwa kushirikiana ili kila upande uwe na haki ya kuleta wadhamini.

Kwa maana hiyo nilikuwa na haki ya kuleta mabondia ambao walikuwa upande wangu ili wapigane.

Baadaye Promota akakwama katika suala la fedha, hivyo wakahitaji msaada wa kutoka upande mwingine kitu ambacho ni kinyume na makubaliano yetu kwa kuwa wao walitakiwa kusimama mpaka mwisho.

Baadaye wakaingia mkataba na Promota ambaye sisi (timu ya Mwakinyo) hatuna uhusiano naye mzuri, nikawauliza wakasema hizo taarifa hazina ukweli.

Baadaye nikabaini hakuna ukweli katika mazungumzo yake (Promota), ikabidi nianze kurekodi mazungumzo yetu yote kuhusu tukio hilo.

Promota akasema kuwa alishirikisha kampuni nyingine kwa kuwa fedha ya kulipia mkada haikuwepo, ikabidi mimi ndio nilipie mkanda kwa Dola 4,000.

Mpinzani Mkenya ajitoa
Kuhusu mpinzani wangu wa awali (Rayton Okwiri) nadhani aliambiwa na watu kuwa anaenda kupigana na bondia mkubwa, hivyo akapandisha dau ikashindikana kwake.

Wakatafuta mpinzani mwingine kwa haraka, ofa yake ikawa juu zaidi ya waliyokuwa nayo, tukakubaliana kuwa Promota atoe nusu ya pesa nasi tutoe ili aongezewe bondia mpya.

Ilivyofika siku ya kupima uzito nikawaona watu ambao hawakuwa kwenye mipango yetu, wakadai kuwa baada ya kumaliza vipimo tutazungumza.

Baada ya vipimo hakukuwa na kikao chochote, nikapiga simu naambiwa nimeshauzwa, nifanye ninachotaka.

Promota alinichukulia poa labda kwa kuwa aliona amenizidi umri a hakujua misimamo yangu.

Walitaka wauze tiketi kwa kutumia jina langu, labda walitaka mimi nikae kimya ili niharibikiwe.
Bongo dalisalama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
π™Ώπš›πš˜πš–πš˜πšπšŠ πš”πšŠπšπš‘πš’πš‹πš’πšπš’πšœπš‘πšŠ π™Όπš πšŠπš”πš’πš—πš’πš˜ πšŠπš—πšŠπšŒπš‘πšŠπšπšžπšŠ πš–πšŠπš‹πš˜πš—πšπš’πšŠ πš—πš’πšŠπš—πš’πšŠ ,πš πšŠπš”πš’πš–πšπšŠπšπšžπšπš’πšŠ πš–πšŠπš‹πš˜πš—πšπš’πšŠ 𝚠𝚊 πš–πšŠπšŠπš—πšŠ πšŠπš—πšŠπš πšŠπš”πšŠπšπšŠπšŠ πš‘πšŠπšπšŠ πš’πšžπš•πšŽ πš–πš”πšŽπš—πš’πšŠ πš’πš•πš’πš‹πš’πšπš’ πš πšŠπš‹πšŽπš–πš‹πšŽπš•πšŽπš£πšŽ πšœπšŠπš—πšŠ πšŒπš‘πšŠπš–πšŠ πšŒπš‘πšŠ πš—πšπšžπš–πš’ πšŠπšπš›πš’πš”πšŠ πš’πš•πš’ πš”πš’πš”πšžπš‹πšŠπš›πš’ πšŠπš™πš’πšπšŠπš—πšŽ πš—πšŠ πš–πš πšŠπš”πš’πš—πš’πš˜ πš”πš πšŠπš—πš’ πš‘πšŠπš”πšžπš πšŠ πš—πšŠ πšœπš’πšπšŠ
Hata Mimi nimemsikiliza vizuri, mwakinyo kazingua kwenye hili.

Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
 
Huyu jamaa siku hizi anatrend zaidi kwa porojo kuliko kazi yake ulingoni. Yuko na "big fat ego" pamoja na ulimbukeni mwingi.

Asipokua makini, anaweza kujichimbia shimo ambalo hataweza kutokamo!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom