JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Promota ana rekodi tata
Mwanzoni nilisikia taarifa juu ya Promota, kwamba wana tuhuma za kutowalipa mabondia, baada ya makubaliano tukakubaliana kuwa kazi ifanywe kwa kushirikiana ili kila upande uwe na haki ya kuleta wadhamini.
Kwa maana hiyo nilikuwa na haki ya kuleta mabondia ambao walikuwa upande wangu ili wapigane.
Baadaye Promota akakwama katika suala la fedha, hivyo wakahitaji msaada wa kutoka upande mwingine kitu ambacho ni kinyume na makubaliano yetu kwa kuwa wao walitakiwa kusimama mpaka mwisho.
Baadaye wakaingia mkataba na Promota ambaye sisi (timu ya Mwakinyo) hatuna uhusiano naye mzuri, nikawauliza wakasema hizo taarifa hazina ukweli.
Baadaye nikabaini hakuna ukweli katika mazungumzo yake (Promota), ikabidi nianze kurekodi mazungumzo yetu yote kuhusu tukio hilo.
Promota akasema kuwa alishirikisha kampuni nyingine kwa kuwa fedha ya kulipia mkada haikuwepo, ikabidi mimi ndio nilipie mkanda kwa Dola 4,000.
Mpinzani Mkenya ajitoa
Kuhusu mpinzani wangu wa awali (Rayton Okwiri) nadhani aliambiwa na watu kuwa anaenda kupigana na bondia mkubwa, hivyo akapandisha dau ikashindikana kwake.
Wakatafuta mpinzani mwingine kwa haraka, ofa yake ikawa juu zaidi ya waliyokuwa nayo, tukakubaliana kuwa Promota atoe nusu ya pesa nasi tutoe ili aongezewe bondia mpya.
Ilivyofika siku ya kupima uzito nikawaona watu ambao hawakuwa kwenye mipango yetu, wakadai kuwa baada ya kumaliza vipimo tutazungumza.
Baada ya vipimo hakukuwa na kikao chochote, nikapiga simu naambiwa nimeshauzwa, nifanye ninachotaka.
Promota alinichukulia poa labda kwa kuwa aliona amenizidi umri a hakujua misimamo yangu.
Walitaka wauze tiketi kwa kutumia jina langu, labda walitaka mimi nikae kimya ili niharibikiwe.