Ziada Mwana
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 201
- 22
Hodi wana JF. nimekuwa ni msomaji maarufu sana lakini nikawa nashindwa kuchangia hoja kwa kuwa sikuwa member wa jamvi.lakini nimelazimika kujiunga nanyi ili tuwe pamoja.ila nasikitika kuwaarifu wana chadema kuwa mimi ni gamba laini (ngozi) ambayo kila mtu anayo,kwa hiyo sisi sote ni watu wa magamba ila magamba hayo yanapokuwa magumu kama ya nyoka au kenge basi upo umuhimu wa kuyavua ili libaki gamba laini.Sasa ndugu yangu ,kama serikali itawaacha watu wafanye watakalo,nchi hii hatafika popote.walevi wataenda kuvamia TBL ili wapate bia za bure,majangili watavamia mbuga wapate meno ya ndovu na kila mtu atafanya ki vyake.hebu fikiria kama polisi wasingefanya hivyo walivyofanya,leo hii mgodi huo ungekuwaje.hebu niambie hao chadema wakichukua nchi watawanyanganya polisi SMG zote wa wabakiwe na virungu? wahalifu ni wahalifu tu hata kama watakuwa ni ndugu zako wa tumbo moja.Tusikumbatie ujinga, hakuna nchi au serikali inayopenda kuua watu wake, lakini pia hakuna serikali inayokubali kundi la wahuni kuvuruga utawala wake,hao watashughulikiwa kwa nguvu zote.subirini chadema ichukue nchi ili mukagawane hizo dhahabu na wanyama huko serengeti,miaka 100 sio mingi mutatawala tu.