Hapa kweli kuna kesi????

Nyambala

JF-Expert Member
Oct 10, 2007
4,465
1,170
Kesi ya Mpesya dhidi ya `Sugu` kusikilizwa Januari 19


Wanasheria naomba mtusaidie, maana kwa hoja hizo tatu na eti ndiyo kuu kuna kesi hapa????


Sugu(4).jpg





Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya inatarajia kuanza kusikiliza kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya CCM, Benson Mpesya, dhidi ya Mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Joseph Mbilinyi maarufu ‘Sugu’ Januari 19 mwaka huu.

Katika kesi hiyo, Mpesya analamikia mambo makuu matatu ambayo anaona yalimfanya ashindwe na Mbilinyi katika kinyang’anyiro cha ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka jana.

Katika uchaguzi huo, Mpesya ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo alibwagwa na mgombea wa Chadema, Mbilinyi, ambaye alipata kura 46,411 huku mgombea huyo wa CCM akipata a kura 24,236, hatua iliyomfanya aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo, Dk.Samweli Lazaro, kumtangaza Mbilinyi kuwa ndiye mshindi.

Mpesya katika kesi yake hiyo ambayo hata hivyo bado haijapangiwa jaji wa kuisikiliza,

1. anadai kuwa Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Monica Saile, ambaye wakati wa uchaguzi alikuwa msimamizi wa uchaguzi, alikuwa na maslahi na Chadema kutokana na kuwa miongoni mwa wanachama wa chama hicho cha upinzani waliopendekezwa kugombea ubunge wa viti maalum.


2. Madai mengine aliyoyatoa Mpesya katika kesi hiyo ni kwamba, wakati wa mchakato wa kampeni, Mbilinyi, alikuwa akitoa maelezo ya uongo kwamba yeye (Mpesya) amejenga shule ya sekondari mkoani Dodoma, hali iliyowafanya wananchi wamuelewe vibaya na hivyo wakashindwa kumchagua.

3. Sababu ya tatu iliyotolewa na Mpesya ni kwamba Mbunge wa Chadema, wakati wa kampeni alikuwa akieleza maneno ya uongo kuwa yeye (Mpesya) amejenga vilabu vya kuuzia pombe za kienyeji hali iliyomchafulia sifa kwa wapiga kura ambao walimuona kuwa si mpenda maendeleo kwani fedha alizozitumia kujenga vilabu hivyo angeziwekeza katika kujenga hospitali na shule.

Mpesya katika kesi hiyo anatetewa na wakili wa kampuni ya Mkumbe and Company Advocate.
 
Kesi ndogo sana hiyo...
Bwana Mdogo Sambwee Shitambala hata usingizini anaimaliza hiyo kesi, na itatupiliwa mbali...
Hivi msimamizi wa uchaguzi anateuliwa na CHADEMA?...So whats that got to do with Mr Two?
 
Ground ya kwanza ina weight kidogo but the rest are Crap

Hata hiyo ya kwanza naona bado iko weak kwa sababu atatakiwa kuithibitishia mahakama ni namna gani huyo afisa utumishi aliinfluence ushindi, je ni kwa kuiba kura, kukampeni, kuhujumu kura za Mpesya? Na kama hii argument itaonekana kuhold water basi kesi nyingi sana zitaibuliwa kutoka wabunge wa CCM kwaniwakurugenzi wa wilaya ambao ni wasimamizi wa uchaguzi ni wanaCCm and it can be proved.
 
Kesi ndogo sana hiyo...
Bwana Mdogo Sambwee Shitambala hata usingizini anaimaliza hiyo kesi, na itatupiliwa mbali...
Hivi msimamizi wa uchaguzi anateuliwa na CHADEMA?...So whats that got to do with Mr Two?


Hata mimi nashangaa...au walimwachia sugu ateue?

Ukichoka kufikiri bwana, hata maiti inakuwa na nafuu, maana imepumzika imetulia
 
Kesi ya Mpesya dhidi ya `Sugu` kusikilizwa Januari 19


Wanasheria naomba mtusaidie, maana kwa hoja hizo tatu na eti ndiyo kuu kuna kesi hapa????


Sugu(4).jpg





Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya inatarajia kuanza kusikiliza kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya CCM, Benson Mpesya, dhidi ya Mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Joseph Mbilinyi maarufu ‘Sugu’ Januari 19 mwaka huu.

Katika kesi hiyo, Mpesya analamikia mambo makuu matatu ambayo anaona yalimfanya ashindwe na Mbilinyi katika kinyang’anyiro cha ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka jana.

Katika uchaguzi huo, Mpesya ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo alibwagwa na mgombea wa Chadema, Mbilinyi, ambaye alipata kura 46,411 huku mgombea huyo wa CCM akipata a kura 24,236, hatua iliyomfanya aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo, Dk.Samweli Lazaro, kumtangaza Mbilinyi kuwa ndiye mshindi.

Mpesya katika kesi yake hiyo ambayo hata hivyo bado haijapangiwa jaji wa kuisikiliza,

1. anadai kuwa Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Monica Saile, ambaye wakati wa uchaguzi alikuwa msimamizi wa uchaguzi, alikuwa na maslahi na Chadema kutokana na kuwa miongoni mwa wanachama wa chama hicho cha upinzani waliopendekezwa kugombea ubunge wa viti maalum.


2. Madai mengine aliyoyatoa Mpesya katika kesi hiyo ni kwamba, wakati wa mchakato wa kampeni, Mbilinyi, alikuwa akitoa maelezo ya uongo kwamba yeye (Mpesya) amejenga shule ya sekondari mkoani Dodoma, hali iliyowafanya wananchi wamuelewe vibaya na hivyo wakashindwa kumchagua.

3. Sababu ya tatu iliyotolewa na Mpesya ni kwamba Mbunge wa Chadema, wakati wa kampeni alikuwa akieleza maneno ya uongo kuwa yeye (Mpesya) amejenga vilabu vya kuuzia pombe za kienyeji hali iliyomchafulia sifa kwa wapiga kura ambao walimuona kuwa si mpenda maendeleo kwani fedha alizozitumia kujenga vilabu hivyo angeziwekeza katika kujenga hospitali na shule.

Mpesya katika kesi hiyo anatetewa na wakili wa kampuni ya Mkumbe and Company Advocate.

Hana cha kupoteza anatekeleza agizo la Katibu Mkuu wa CCM kuwa wana CCM wote walioshindwa Ubunge/Udiwano wafungue kesi na CCM italipa gharama za kesi, possibly from DOWANS ICC proceedings
 
Kisiasa kesi ipo,zinaweza kuwa weak arguments ukiziangalia but si za kudharauliwa kwenye nchi amabyo rushwa,mabavu ni moja ya njia za ushindi,hata waliongalia ile ya Liyumba walisema hana Kesi tena akiwa na mwanasheria anayeheshimika kama Magafu.......hakuna haja ya dharau kwenye suala kama hili.........na kwenye hiyo ya kwanza kweli kuna conflict of interest ya huyo msimamizi wa uchaguzi....ila ni kesi inayoshindika.
 
Mbilinyi, ambaye alipata kura 46,411 huku mgombea huyo wa CCM akipata a kura 24,236

mtu umeachwa kwa mbali hivi lkn bado tu unang'ang'ania
 
Ni haki yake kikatiba. Mwache ajaribu kwa majaji hawa ambao siku hizi nao wamejaa u-ccm kwa kuwa tu aliyewachagua ni m-ccm labda anaweza kusikilizwa. Lakini kwangu sijaona lolote la maana kwenye malalamiko yake.
 
Kesi ya Mpesya dhidi ya `Sugu` kusikilizwa Januari 19


Wanasheria naomba mtusaidie, maana kwa hoja hizo tatu na eti ndiyo kuu kuna kesi hapa????


Sugu(4).jpg





Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya inatarajia kuanza kusikiliza kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya CCM, Benson Mpesya, dhidi ya Mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Joseph Mbilinyi maarufu ‘Sugu’ Januari 19 mwaka huu.

Katika kesi hiyo, Mpesya analamikia mambo makuu matatu ambayo anaona yalimfanya ashindwe na Mbilinyi katika kinyang’anyiro cha ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka jana.

Katika uchaguzi huo, Mpesya ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo alibwagwa na mgombea wa Chadema, Mbilinyi, ambaye alipata kura 46,411 huku mgombea huyo wa CCM akipata a kura 24,236, hatua iliyomfanya aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo, Dk.Samweli Lazaro, kumtangaza Mbilinyi kuwa ndiye mshindi.

Mpesya katika kesi yake hiyo ambayo hata hivyo bado haijapangiwa jaji wa kuisikiliza,

1. anadai kuwa Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Monica Saile, ambaye wakati wa uchaguzi alikuwa msimamizi wa uchaguzi, alikuwa na maslahi na Chadema kutokana na kuwa miongoni mwa wanachama wa chama hicho cha upinzani waliopendekezwa kugombea ubunge wa viti maalum.


2. Madai mengine aliyoyatoa Mpesya katika kesi hiyo ni kwamba, wakati wa mchakato wa kampeni, Mbilinyi, alikuwa akitoa maelezo ya uongo kwamba yeye (Mpesya) amejenga shule ya sekondari mkoani Dodoma, hali iliyowafanya wananchi wamuelewe vibaya na hivyo wakashindwa kumchagua.

3. Sababu ya tatu iliyotolewa na Mpesya ni kwamba Mbunge wa Chadema, wakati wa kampeni alikuwa akieleza maneno ya uongo kuwa yeye (Mpesya) amejenga vilabu vya kuuzia pombe za kienyeji hali iliyomchafulia sifa kwa wapiga kura ambao walimuona kuwa si mpenda maendeleo kwani fedha alizozitumia kujenga vilabu hivyo angeziwekeza katika kujenga hospitali na shule.

Mpesya katika kesi hiyo anatetewa na wakili wa kampuni ya Mkumbe and Company Advocate.

Sisi wa huku Mbeya tunajua kuwa Mpesya amesaidia sana ujenzi wa vilabu vya pombe. Huu ni ukweli!
 
Back
Top Bottom