Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,170
Kesi ya Mpesya dhidi ya `Sugu` kusikilizwa Januari 19
Wanasheria naomba mtusaidie, maana kwa hoja hizo tatu na eti ndiyo kuu kuna kesi hapa????
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya inatarajia kuanza kusikiliza kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya CCM, Benson Mpesya, dhidi ya Mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu Januari 19 mwaka huu.
Katika kesi hiyo, Mpesya analamikia mambo makuu matatu ambayo anaona yalimfanya ashindwe na Mbilinyi katika kinyanganyiro cha ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka jana.
Katika uchaguzi huo, Mpesya ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo alibwagwa na mgombea wa Chadema, Mbilinyi, ambaye alipata kura 46,411 huku mgombea huyo wa CCM akipata a kura 24,236, hatua iliyomfanya aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo, Dk.Samweli Lazaro, kumtangaza Mbilinyi kuwa ndiye mshindi.
Mpesya katika kesi yake hiyo ambayo hata hivyo bado haijapangiwa jaji wa kuisikiliza,
1. anadai kuwa Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Monica Saile, ambaye wakati wa uchaguzi alikuwa msimamizi wa uchaguzi, alikuwa na maslahi na Chadema kutokana na kuwa miongoni mwa wanachama wa chama hicho cha upinzani waliopendekezwa kugombea ubunge wa viti maalum.
2. Madai mengine aliyoyatoa Mpesya katika kesi hiyo ni kwamba, wakati wa mchakato wa kampeni, Mbilinyi, alikuwa akitoa maelezo ya uongo kwamba yeye (Mpesya) amejenga shule ya sekondari mkoani Dodoma, hali iliyowafanya wananchi wamuelewe vibaya na hivyo wakashindwa kumchagua.
3. Sababu ya tatu iliyotolewa na Mpesya ni kwamba Mbunge wa Chadema, wakati wa kampeni alikuwa akieleza maneno ya uongo kuwa yeye (Mpesya) amejenga vilabu vya kuuzia pombe za kienyeji hali iliyomchafulia sifa kwa wapiga kura ambao walimuona kuwa si mpenda maendeleo kwani fedha alizozitumia kujenga vilabu hivyo angeziwekeza katika kujenga hospitali na shule.
Mpesya katika kesi hiyo anatetewa na wakili wa kampuni ya Mkumbe and Company Advocate.
Wanasheria naomba mtusaidie, maana kwa hoja hizo tatu na eti ndiyo kuu kuna kesi hapa????
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mbeya inatarajia kuanza kusikiliza kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa Mbeya Mjini kwa tiketi ya CCM, Benson Mpesya, dhidi ya Mbunge wa sasa wa jimbo hilo, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu Januari 19 mwaka huu.
Katika kesi hiyo, Mpesya analamikia mambo makuu matatu ambayo anaona yalimfanya ashindwe na Mbilinyi katika kinyanganyiro cha ubunge wa Jimbo la Mbeya Mjini katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 31 mwaka jana.
Katika uchaguzi huo, Mpesya ambaye alikuwa akitetea nafasi hiyo alibwagwa na mgombea wa Chadema, Mbilinyi, ambaye alipata kura 46,411 huku mgombea huyo wa CCM akipata a kura 24,236, hatua iliyomfanya aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi katika jimbo hilo, Dk.Samweli Lazaro, kumtangaza Mbilinyi kuwa ndiye mshindi.
Mpesya katika kesi yake hiyo ambayo hata hivyo bado haijapangiwa jaji wa kuisikiliza,
1. anadai kuwa Afisa Utumishi wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya, Monica Saile, ambaye wakati wa uchaguzi alikuwa msimamizi wa uchaguzi, alikuwa na maslahi na Chadema kutokana na kuwa miongoni mwa wanachama wa chama hicho cha upinzani waliopendekezwa kugombea ubunge wa viti maalum.
2. Madai mengine aliyoyatoa Mpesya katika kesi hiyo ni kwamba, wakati wa mchakato wa kampeni, Mbilinyi, alikuwa akitoa maelezo ya uongo kwamba yeye (Mpesya) amejenga shule ya sekondari mkoani Dodoma, hali iliyowafanya wananchi wamuelewe vibaya na hivyo wakashindwa kumchagua.
3. Sababu ya tatu iliyotolewa na Mpesya ni kwamba Mbunge wa Chadema, wakati wa kampeni alikuwa akieleza maneno ya uongo kuwa yeye (Mpesya) amejenga vilabu vya kuuzia pombe za kienyeji hali iliyomchafulia sifa kwa wapiga kura ambao walimuona kuwa si mpenda maendeleo kwani fedha alizozitumia kujenga vilabu hivyo angeziwekeza katika kujenga hospitali na shule.
Mpesya katika kesi hiyo anatetewa na wakili wa kampuni ya Mkumbe and Company Advocate.