MTENDAHAKI
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 4,013
- 1,443
Siasa ni mchezo mzuri sana ambao umejaa maigizo na vituko, mbwembwe na visa, Fitna na majungu lakini pia Ujuzi na umakini wa hali ya juu mno kuliko DRAFT!Kila kauli kwenye siasa ina maana sana!Kabla mtu hajagundua adui yake ninani hawezi kuwa salama na hata katika siasa ni hivyo hivyo; Yaani kama hujaambiwa mapungufu yako kabla hujaingia kwenye uchaguzi basi ujue una wakati mgumu sana kujua utakumbana na changamoto gani! Ndio maana namuona SAMUEL SITA kama mtu makini sana kwenye siasa !Nasema hivi kwa sababu naanza kuamini kuwa ana nia ya kweli ya kutaka kugombea urais. Awali nilijua ni mpambanaji tu ndani ya CCM hasa baada ya kukosa uspika!Kumbe hapana alikuwa akiwachokonoa wenzake wamwambie mapungufu yake ndani ya chama chake. Baada ya mivutano ya muda mrefu ndani ya ccm Sita anaona kama ameshinda vita ndani ya chama chake ndio maana ameamua kuhamishia vita kw wapinzani wake wakuu yaani CHADEMA kwa kuwachokonoa makusudi ili wamwambie mambo yanayoweza kuwa kikwazo kwake,bomu kwake na pingamizi katika kupata ridhaa ya kuongoza nchi iwapo chama chake kitamuamini kwenye nafasi ya kuwa mgombea urais!NI wazi kuwa CHADEMA hupata uungwaji mkono mkubwa wa wananchi kutokana na style yao ya kuumbua madudu ya wapinzani wao na ni wazi kutokana na siri nyingi walizokuwa nazo CHADEMA juu ya SITA ingekuwa rahisi kummaliza kama angeteuliwa na chama chake hapo baadae bila kujijua anaweza kukabiliana na nini! Ndio maana nasema kwa hili chadema mmeingia mkenge!USHAURI WA BURE ni kujibu maswali mliyoulizwa tu au kuuliza yale mliyopanga kuuliza na sio kucheza "MUZIKI WA SITA"!waache CCM waucheze mziki wenu na sio kinyume! HII INAITWA FORCE KINGI style maarufu kabisa kwenye drafti!LA sivyo mnasafisha njia ya mtu tu!