Hamad Masauni: Kamera zenye Mfumo wa utambuzi wa Sura kufungwa Dar es Salaam, Arusha na Dodoma

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 35 leo Mei 29, 2023.



Ufungaji wa kamera za Ulinzi
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Hamad Masauni amesema Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi limekamilisha mradi wa ujenzi wa mji salama utakaotumia kamera zenye mfumo wa utambuzi wa Sura.

Katika awamu ya kwanza, kamera hizo zitafungwa Katika mkoa wa Arusha, Dar es salaam na Dodoma. Hii ni sehemu ya kuongeza nguvu katika kubaini na kuzuia vitendo vya kihalifu nchini.

Hali ya Magereza Nchini
Akizungumzia hali ya magereza nchini, Waziri Masauni amesema hadi Mei 2023, jumla ya wahalifu 30,901 walikuwepo kwenye magereza yote nchini ambapo wafungwa wapo 18,887 na mahabusu 12,014.

Pia, Utekelezaji wa adhabu Mbadala umekuwa unafanyika ambapo wafungwa wenye kifungo cha nje wapo 780 na waliohukumiwa kutumika vifungo vyao kwa kutoa huduma kwa jamii wakiwa 3,719.

Matukio 14,184 ya ukatili wa kijinsia yameripotiwa Polisi
Kutoka Julai 2022 hadi Mei 2023, jumla ya mashauri 14,184 ya matukio ya ukatili wa kijinsia na Watoto yalitolewa taarifa katika vituo va Polisi ikilinganishwa na matukio 12,642 yaliyotokea kipindi kama hicho mwaka uliopita.

Matukio ya Ajali za Barabani ni 1,283
Hali ya usalama barabarani imeimarika kutokana na Jeshi la Polisi kusimamia Sheria za Usalama Barabarani.

Amesema “Katika kipindi cha Julai 22, 2022 hadi Mei 23, 2023 matukio ya ajali yalikuwa 1,283 tofauti na mwaka mmoja uliopita ambapo yalikuwa 1,731, hivyo yamepungua kwa 25.9% sababu ikiwa ni kuimarika kwa usimamizi wa Sheria, kufanyika kwa oparesheni maalum Nchi nzima na elimu kutolewa kwa makundi yote.”

Waziri Masauni: Magereza yote nchini yana wahalifu 30,901
Akizungumzia hali ya magereza Nchini, Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni amesema hadi Mei 2023, jumla ya Wahalifu 30,901 walikuwepo kwenye magereza yote, kati yao wafungwa ni 18,887 na mahabusu ni 12,044.

Amesema utekelezaji wa adhabu mbadala umekuwa unafanyika ambapo wafungwa wenye kifungo cha nje wapo 780 na waliohukumiwa kutoa huduma kwa jamii ni 3,719, ameeleza kipindi kama hiki kwa Mwaka 2021/22 kulikuwa na Wahalifu 32,671 gerezani
 
Nchi za watu wenye akili hawafanyi double investments. Sehemu nyingi za biashara zinazo kamera tayari. Wanachokifanya ni kushirikiana na wamiliki pale ushahidi unapohitajika.

Badala ya kuanza kuingia gharama nyingi zisizo na ulazima unaweza tu kufuta kodi kwa muda kwenye vifaa hivyo na kuhamasisha watu wote wenye biashara ndogo na kubwa kufunga camera kwa usalama wao.

But again, ukifanya hivyo haupati 10% yako kwenye manunuzi 😢.
 
Nchi za watu wenye akili hawafanyi double investments. Sehemu nyingi za biashara zinazo kamera tayari. Wanachokifanya ni kushirikiana na wamiliki pale ushahidi unapohitajika.

Badala ya kuanza kuingia gharama nyingi zisizo ja ulazima unaweza tu kufuta kodi kwa muda kwenye vifaa hivyo na kuhamasisha watu wote wenye biashara ndogo ka kubwa kufunga camera kwa usalama wao.

But again, ukifanya hivyo haupati 10% yako kwenye manunuzi 😢.
Hili ni suala la upigaji. Tunahitaji kamera wakati watu wengi wanafariki kwa magonjwa ya kutibika? Wanaofariki kwa uhalifu wanafikia hata 1/100 ya wanaokufa kwa kukosa mahitaji muhimu? Kwa taarifa yao ni kuwa kamera kama hizi haziwezi kuzuia uhalifu hasa kwenye mazingira kama yetu.
 
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 11, Kikao cha 35 leo Mei 29, 2023.



Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhe. Hamad Masauni amesema Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Polisi limekamilisha mradi wa ujenzi wa mji salama utakaotumia kamera zenye mfumo wa utambuzi wa Sura.

Katika awamu ya kwanza, kamera hizo zitafungwa Katika mkoa wa Arusha, Dar es salaam na Dodoma. Hii ni sehemu ya kuongeza nguvu katika kubaini na kuzuia vitendo vya kihalifu nchini.

Akizungumzia hali ya magereza nchini, Waziri Masauni amesema hadi Mei 2023, jumla ya wahalifu 30,901 walikuwepo kwenye magereza yote nchini ambapo wafungwa wapo 18,887 na mahabusu 12,014.

Pia, Utekelezaji wa adhabu Mbadala umekuwa unafanyika ambapo wafungwa wenye kifungo cha nje wapo 780 na waliohukumiwa kutumika vifungo vyao kwa kutoa huduma kwa jamii wakiwa 3,7

Wahalifu hawako barabarani bali wako ndani ya ma V8 ya serikali wakiiba kila mtu kwa urefu wa kamba yake
 
Sawa sawa...Jiongezee wigo wa malisho....hakuna kuingiliana.....kila wizara ibuni namna ya kurefusha kamba.
 
Hili ni suala la upigaji. Tunahitaji kamera wakati watu wengi wanafariki kwa magonjwa ya kutibika? Wanaofariki kwa uhalifu wanafikia hata 1/100 ya wanaokufa kwa kukosa mahitaji muhimu? Kwa taarifa yao ni kuwa kamera kama hizi haziwezi kuzuia uhalifu hasa kwenye mazingira kama yetu.
Sasa mtu kama anaumwa na haiendi hospital unataka serikali ikamteke Impeleke hospital?
 
Nchi za watu wenye akili hawafanyi double investments. Sehemu nyingi za biashara zinazo kamera tayari. Wanachokifanya ni kushirikiana na wamiliki pale ushahidi unapohitajika.

Badala ya kuanza kuingia gharama nyingi zisizo na ulazima unaweza tu kufuta kodi kwa muda kwenye vifaa hivyo na kuhamasisha watu wote wenye biashara ndogo ka kubwa kufunga camera kwa usalama wao.

But again, ukifanya hivyo haupati 10% yako kwenye manunuzi .
Serikali lazima iwe na mfumo wake kwenye makutano ya barabara ili kusaidia katika kupata waharifu, magari etc.
Huwezi sema utakuta mtu binafsi kaweka kamera pale Selander.
 
Watu wengi washafungwa cams zao binafsi kitambo tu
Nyie serikali mmechelewa sana

Ova
Serikali inaenda funga Camera Tambuzi, maana yake zitakuwa linked na NIDA.
Hizo za majumba yenu haziko networked
 
Back
Top Bottom