Plato
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 420
- 94
Maigizo ya Halima Mdee kuchukuliwa fomu ya kugombea BAWACHA ni ya hatari sana kwa CHADEMA. hiyo ni njama tu ya kutaka chama kinakuwa mikononi mwa watu walewale wa kulekuleee. kwanza Halima bado ni kijana kuliko mwanamke. hatujui kama hata amekwisha kuolewa wala kama ana mtoto. Kwa haiba hiyo tunadhani hafai kuwa mwenyekiti wa BAWACHA.
Ninaheshimu sana uwezo wake wa uongozi kama mbunge na uwezo binafsi wa uongozi. lakini nadhani asinge kufustrate chama kwa nafasi hiyo. nimetumia neno ku frustrate kwa sababu chama kitakuwa kinakumbuka kilichotokea uchaguzi wa bawacha uliopita. wakati chama kilikuwa kinataka kuwapitisha akina Grace Kihwelu, wajumbe hawakuwa wanataka kuwachagua.
kwa kweli hicho ndicho kilisababisha uchaguzi kufutwa na muda wote BAWACHA haikuwa na mwenyekiti. hata leo, mgombea yeyote ambaye ni Mbunge hatachaguliwa katika nafasi hizi.waacheni wamama wengine kama Sophia Mwakagenda au Anna Mughwira wawe viongozi badala ya kutaka kujishindilia vyeo juu ya vyeo.
Ninaheshimu sana uwezo wake wa uongozi kama mbunge na uwezo binafsi wa uongozi. lakini nadhani asinge kufustrate chama kwa nafasi hiyo. nimetumia neno ku frustrate kwa sababu chama kitakuwa kinakumbuka kilichotokea uchaguzi wa bawacha uliopita. wakati chama kilikuwa kinataka kuwapitisha akina Grace Kihwelu, wajumbe hawakuwa wanataka kuwachagua.
kwa kweli hicho ndicho kilisababisha uchaguzi kufutwa na muda wote BAWACHA haikuwa na mwenyekiti. hata leo, mgombea yeyote ambaye ni Mbunge hatachaguliwa katika nafasi hizi.waacheni wamama wengine kama Sophia Mwakagenda au Anna Mughwira wawe viongozi badala ya kutaka kujishindilia vyeo juu ya vyeo.