Hali ya usafiri jijini kwa sasa.

kakuruvi

JF-Expert Member
Sep 2, 2009
770
256
Wadau kuna jambo limenipa matumaini, jana jioni nilipanda daladala pale posta hakukuwa na kugombania sana labda kwa wale waliozoea. Leo asubuhi hali ilikuwa pia sio mbaya, tumetumia dakika 30 tuka Ubungo-Posta kwani huwa tunatumia mara nyingi si chini ya saa 1.

Sasa wadau nime-note kwamba kumbe kuna idadi kubwa sana ya wanafunzi wanaosoma katikati ya mji wakitokea sehemu mbalimbali za mji, hii inamaanisha pia kuna walimu na wafanyakazi wa mashuleni wanaokuja na kurudi toka katikati ya mji ila kwa sasa wengi wamefunga shule. Kwa jinsi idadi yao ilivyo kubwa ndio inapelekea foleni kubwa hapa mjini japokuwa kuna sababu nyingine nyingi ila hii ni muhimu.

Wadau, wakifungua shule hali itarudia vile vile, nini kifanyike ili wanafunzi wasome karibu na wanakoishi bila kutumia magari (daladala)? kwa jinsi wengi wanavyopata tabu ya usafiri kinachowaleta shule za katikati ya mji nini haswa? Asanteni kwa hoja mtakazo changia.
 
Wanafunzi huwa wanaongezaje foleni?


Wanafunzi wengi wanasoma mbali na wanakoishi, hivyo ni lazima wapande magari, kwa jinsi walivyo wengi kwa idadi kunakuwa na msongamano kwenye magari na barabarani, kwa sasa wako likizo kuna afadhali kidogo kwenye magari (daladala) na barabarani pia, nini kifanyike wanafunzi wasisome mbali na wanakoishi? hii italeta ahueni barabarani, umenielewa Bujix2?
 
hapana watu wengi wenye fujo wanatoka Arusha na moshi sasa wote wamekwenda Chrismas na new year. Subiri kuanzia tarehe 3 Jan utaona fujo barabarani zimeanza.
 
hapana watu wengi wenye fujo wanatoka Arusha na moshi sasa wote wamekwenda Chrismas na new year. Subiri kuanzia tarehe 3 Jan utaona fujo barabarani zimeanza.

unatuonea kwa hiyo fujo zipo moshi na arusha saa hizi au unasemaje??? sis watu poa sana tena watulivu njoo kwetu uone HM Hafif
 
hapana watu wengi wenye fujo wanatoka Arusha na moshi sasa wote wamekwenda Chrismas na new year. Subiri kuanzia tarehe 3 Jan utaona fujo barabarani zimeanza.
..Aiseee! Mbona unatupiga dongo bwa sheee??!!
 
hapana watu wengi wenye fujo wanatoka Arusha na moshi sasa wote wamekwenda Chrismas na new year. Subiri kuanzia tarehe 3 Jan utaona fujo barabarani zimeanza.

Da! Uwezo wako wa kufikri ni finyu sana sawa na punje ya mchele uzao wako utakuwa na IQ ndogo sawa na punje ya ulezi.
 
nini kifanyike ili wanafunzi wasome karibu na wanakoishi bila kutumia magari (daladala)? kwa jinsi wengi wanavyopata tabu ya usafiri kinachowaleta shule za katikati ya mji nini haswa? Asanteni kwa hoja mtakazo changia.

mkuu kakuruvi,

nadhani hii ni changamoto ambayo iko hapa to stay, si kwamba nakatisha tamaa mjadala huu bali najaribu kuwa mkweli wa nafsi yangu kwani sitaki kujipa matumaini kwa kitu ambacho hakielekei kupatiwa suluhu ya karibuni....

moja ya sababu ni kufuata shule bora na si bora shule...mfano shule ya msingi bunge..darasa lina watoto 45-50 wakati makurumla pale mwembechai ni 60-70. walimu wa bunge bado wako makini kiasi kwa hiyo mzazi atampeleka mwanae bunge badili ya makurumla matokeo yake ni hayo hapo juu...au tazama hii..mtoto anaishi kitunda...amesoma primary kipunguni...amefaulu form one anatakiwa kwenda azania/jangwani/kisutu...hakuna school bus..huyo ni lazima utakutana nae kwenye daladala.

kama tutaweza kumaliza inflow ya watu kuja Dsm kutoka mikoani au hapa hapa dar majority kuelekea posta au kariakoo kufanya shughuli za kutafuta rizki basi na hili tutaweza kulimaliza vinginevyo tusubiri masiha kutoka mbinguni.

ni mtazamo tu..
 
Wadau kuna jambo limenipa matumaini, jana jioni nilipanda daladala pale posta hakukuwa na kugombania sana labda kwa wale waliozoea. Leo asubuhi hali ilikuwa pia sio mbaya, tumetumia dakika 30 tuka Ubungo-Posta kwani huwa tunatumia mara nyingi si chini ya saa 1.

Sasa wadau nime-note kwamba kumbe kuna idadi kubwa sana ya wanafunzi wanaosoma katikati ya mji wakitokea sehemu mbalimbali za mji, hii inamaanisha pia kuna walimu na wafanyakazi wa mashuleni wanaokuja na kurudi toka katikati ya mji ila kwa sasa wengi wamefunga shule. Kwa jinsi idadi yao ilivyo kubwa ndio inapelekea foleni kubwa hapa mjini japokuwa kuna sababu nyingine nyingi ila hii ni muhimu.

Wadau, wakifungua shule hali itarudia vile vile, nini kifanyike ili wanafunzi wasome karibu na wanakoishi bila kutumia magari (daladala)? kwa jinsi wengi wanavyopata tabu ya usafiri kinachowaleta shule za katikati ya mji nini haswa? Asanteni kwa hoja mtakazo changia.
kama wewe ni mbongo kweli utajua kwamba wanafunzi huwa wananyanyaswa sana ktk daladala. ki2 kingine...wanafunzi wa 5 wanaweza panda gari 1 sasa hiyo foleni inahusiana vp? je unamaanisha kwamba waalimu ndio wanaomiliki magari huko city centre? hiyo research yako mmmh, embu interprete data zako vizuri...kama ulitumia saa 1 leo umetumia dkk 30 je gari hilo jana lilikuwa na wanafunzi wangapi na leo lilibeba wanafunzi wangapi? je wanafunzi ndio wanasababisha gari/daldala liende polepole?
 
unatuonea kwa hiyo fujo zipo moshi na arusha saa hizi au unasemaje??? sis watu poa sana tena watulivu njoo kwetu uone HM Hafif
bht upo mama?mbona kimya? nilidhani umeenda moshi maana hata jf jukwaa la mahusiano limepoa kweli,sijui ndio wapwa wengi ni waarusha na moshi?
 
mkuu kakuruvi,

nadhani hii ni changamoto ambayo iko hapa to stay, si kwamba nakatisha tamaa mjadala huu bali najaribu kuwa mkweli wa nafsi yangu kwani sitaki kujipa matumaini kwa kitu ambacho hakielekei kupatiwa suluhu ya karibuni....

moja ya sababu ni kufuata shule bora na si bora shule...mfano shule ya msingi bunge..darasa lina watoto 45-50 wakati makurumla pale mwembechai ni 60-70. walimu wa bunge bado wako makini kiasi kwa hiyo mzazi atampeleka mwanae bunge badili ya makurumla matokeo yake ni hayo hapo juu...au tazama hii..mtoto anaishi kitunda...amesoma primary kipunguni...amefaulu form one anatakiwa kwenda azania/jangwani/kisutu...hakuna school bus..huyo ni lazima utakutana nae kwenye daladala.

kama tutaweza kumaliza inflow ya watu kuja Dsm kutoka mikoani au hapa hapa dar majority kuelekea posta au kariakoo kufanya shughuli za kutafuta rizki basi na hili tutaweza kulimaliza vinginevyo tusubiri masiha kutoka mbinguni.

ni mtazamo tu..

Al Zagawi asante sana kwa mchango wako, kumbe kuna haja pia ya kuboresha hata huduma za jamii hukohuko watu wanakotoka, bila shaka hilo pia itasaidia kupunguza watu wanaotoka nje ya mji na vitongojini kufuata huduma hizo.
 
kama wewe ni mbongo kweli utajua kwamba wanafunzi huwa wananyanyaswa sana ktk daladala. ki2 kingine...wanafunzi wa 5 wanaweza panda gari 1 sasa hiyo foleni inahusiana vp? je unamaanisha kwamba waalimu ndio wanaomiliki magari huko city centre? hiyo research yako mmmh, embu interprete data zako vizuri...kama ulitumia saa 1 leo umetumia dkk 30 je gari hilo jana lilikuwa na wanafunzi wangapi na leo lilibeba wanafunzi wangapi? je wanafunzi ndio wanasababisha gari/daldala liende polepole?

Pape yaelekea hukunielewa, bora uelewe mada kwanza ndipo uchangie, ni hivi! Huduma ya jamii yoyote ikitolewa kwa watu wachache inakuwa bora kuliko huduma hiyo hiyo ikitolewa kwa watu wengi, ubora wake unapungua. Kipindi hiki wanafunzi wanapokuwa likizo kwa kiasi fulani usafiri unakuwa afadhali, kumbuka hata wasiopanda daladala gari ya nyumbani inayowapeleka shule inapumzishwa hivyo kupunguza idadi ya magari barabarani, na foleni pia kwa kiasi fulani.

Wanafunzi wasingesoma mbali na wanapoishi, wasingetumia magari na barabara, huoni hii ingesaidia? Au research ipi unataka, au data zipi unataka, au wewe huoni, au unakaa kijiji cha Nyagwa mbali na Dar na huji katikati ya Jiji?
 
hapana watu wengi wenye fujo wanatoka Arusha na moshi sasa wote wamekwenda Chrismas na new year. Subiri kuanzia tarehe 3 Jan utaona fujo barabarani zimeanza.

Kwani shule zinafunguliwa lini huko Tanzania especially dar es salaam.

Vp sasa kuna foleni kule Sinza na mbezi beach ( mBagamoyo rd)maana yake huko wachaga wengi sana.



Tuangalie kama wachaga wakirudi toka Xmas misongamano itapungua.
 
Back
Top Bottom