Nimesoma Uzi mmoja humu kwenye hili jukwaa ukielezea matumaini mapya waliyo nayo WanaCCM juu ya kukifuta Chama cha CHADEMA katika ramani ya Siasa Nchini.Hii inafuatia kikao chao cha Siri walichokifanya huko Dodoma hivi karibuni.Tunafahamu fika kabisa kwamba kikao walichokifanya huko Dodoma kinahusiana na mikakati yao ovu ya muda mrefu ya kuimaliza CHADEMA,Kiuhalisia kile walichokijadili kule Dodoma si kigeni kama ambavyo wangependa kutuaminisha kwasababu mikakati yao tayari imeshaanza kufanyiwa kazi muda hata kabla ya kikao chao.Walianza na ruzuku za Vyama,Wakaja na machafuko kule Mbeya rejea kauli ya Sofia Simba na sasa hili suala la Mbowe na nyumba yake ya Arabuni.Haya matukio yote haya yanatokea katika umoja wake.Huu mkakati maalum wa CCM na CHADEMA tujiandae kwa mengi zaidi huko mbeleni kutoka kwa hawa watu wasio na roho.Maadam tumeshajua wapi wamepanga kupeleka mashambulizi ili kutekeleza mkakati wao huo ovu ningependa kuwatoa hofu WanaCHADEMA kwamba bado tunayo kete ya kuwapoteza CCM,Nayo ni Uchaguzi.