Hakuna malipo ya NSSF, PPF hadi umri wa kustaafu ufike!

Bargain,

Hii sio tetesi maana haijawa kama hivyo. Lakini umefanya vizuri kuleta hii habari katika kipindi hiki na kuwafanya waajiriwa wote Tanzania wakae mkao wa kula.

Ukweli ni kwamba serikali ina mpango wa kupeleka bungeni marekebisho ya muswada wa sheria wa mafao ya wafanyakazi kama ulivyopitisha ba bunge ili sasa kufanya wafanyakazi wote wanaokatwa akiba ya mafao (PPF,NNSF, PSPF,LAPF,GEPF n.k) kulazimika kutopata mafao yao kama hawajatimiza umri wa kustaafu(55-60).Mpango huu unaletwa kwa sababu serikali yenu haina namna ya kufanya na ingependa kupata boost ya mapato toka mifuko hii ili kuleta pesa kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Mpango huu wa aibu na kandamizi utawaathiri wafanyakazi zaidi ya 700000 serikalini lakini kwa kipekee utaathiri na kuua ndoto za wafanyakazi zaidi ya 3000000 walio katika sekta binafsi kama vile makampuni, NGOs na wale waliojiajiri wenyewe na ambao wanatumia mifuko hii.

(Una imani kubwa kwamba wabunge wetu hasa wa upinzani wataupigia ngumu mpango huu nyonyaji ambao ni wa aina yake katika nchi zote za Afrika. Hii pia inatoa fursa kwa wafanyakazi wote nchini (hasa vijana) kutafakari na kuona jinsi serikali yenu inavyopanga kufifisha mipango yenu ya muda mfupi na ile ya kati. Kazi kwenu simameni na Chukueni Hatua Sasa.

HABARI NDO HIYO
Je kama mimi ni mwanachama nafanya sekta binafsi nimefukuzwa kazi na nipo kijiweni je mimi nitakuwa kundi gani??je na pesa yangu ndiyo itakaa huko hadi nifikishe miaka 55???au inakuwaje?
 
Jamani wana JF mbona mnakuwa kama sio GTs. Hata ukisoma kwenye utanguliza wa DG wa SSRA amesema hii SHERIA IMESHAPITISHWA NA BUNGE tangu 13 April 2012. WABUNGE WETU wameshaipitisha.

Mimi ninajiuliza hivi itakuwa je kwa wafanyakazi wanaofanya kazi kwa contract za miaka 2,3,5 .... etc
Contract imekwisha hajaiwa renewed na wewe una miaka 40, utasubiri hadi ufikishe miaka 55 au 60 ndiyo upate mafao yako.

Mbona wabunge wao wakimaliza mda wao wa miaka 5 wanachukiwa kila kilicho chao? Kwanini nao hawasubiri hadi wafikishe miaka 60 kwa wale ambao hawajafikisha?

Wafanyakazi wanaofanya kazi kwenye NGOs, Private sectors hawa wote sio penshionable wanafanya kazi kwa CONTRACT. Nao watasubiri hadi wafikishe miaka 55 ua 60? Wafanyakazi kwenye MIGODI na hasa MINERS, WANAJESHI na POLISI ambao ni JUNIOR staff wao umri wao wa kustaafu sio miaka 55 is less than that.

Hii SSRA ilianzishwa hasa kutokana na dai la wafanyakazi kutaka mifuko yote i-harmonise formula ya ukokotoaji wa mafao ya uzeeni, hasa baada ya kuona mfuko wa serikali kuu PSPF unalipa mafao mazuri kulinganisha na mafao duni yanayotolewa na NSSF na PPF. Ndiyo chanzo hasa cha kuundwa SSRA.

Lakini ajabu badala ya SSRA kufanyia kazi hili DAI kubwa la wafanyakazi, wao wamerukia mambo mengi ambayo sio KERO ya wafanyakazi. Indeed badala ya kupunguza kero, sasa SSRA imeongeza kero kwa wafanyakazi.

Kama kuna mfanyakazi yeyote Tanzania aliyempatia kura Kikwete na Mbunge wa CCM basi ALAANIWE kwani pamoja na JK kusema hana haja na kula za wafanyakazi bado kuna eti-mifanyakazi na familia zao walitoa kura kwa CCM. Sasa ngoja tukipate cha MOTO.

Pesa zetu zote za NSSF na PPF zimekopwa na serikali/CCM na kughalamikia WHITE ELEPHANT PROJECTS sasa mifuko haina pesa ndiyo wanawatumia SSRA kuleteta hii sheri ya kijinga.

Kule France serikali iliongeza MIAKA YA KUSTAAFU kwa wafanyakazi, France nzima iliwaka moto kwa maandamano ya kupinga. Pia hiyo ni mojawapo ya sababu zilizomu cost Sarkozy urais. Lakini eti hii Tanzania nchi ya AMANI, MIFANYAKAZI tumekaa kimya, hata TUCTA inashindwa kutoa tamko. KWELI Watanzania tuna laana!
 
Urgent public call for @J.Mnyika, Zitto HKigwangalla, @Tundi Lisu (Sijui kama yupo humu)

Tunaomba ufafanuzi hii sheria ya kuzuia withdraw benefit imepitishwa lini imekuwaje na nyie
mkakubali hii sheria ipitishe?

Wabunge wetu wakishidwa kutoa ufafanuzi wa kusadia wananchi wake napendekeza MASS STRIKE

hii mbona ni kinyume na ILO conversion minimum benefit standard N0.102???

Hii sio haki kabisa. Nyie SSRA toka lini mmeteuliwa na MUNGU kujua ni lini binadamu wa Tanzania wanaochangia mifuko ya hifadhi watakufa? Na kwa nini mtu asubiri mpaka miaka 55 au 60? Ni nani aliyewiaambia kuwa baada ya kustaafu mtu atategemea tu hizo pesa za hifadhi? Je ni nani aliyewaambia kuwa mtu akistaafu hawezi tena kufanya kazi? Mbona Serikali yenyewe iliwaita Madaktari wastaafu wakati ule wa mgomo wa Madaktari?

Hii sheria yenu imepitwa na wakati, nadhani suala hili ilikuwa muamue kama watu wanataka kujiunga na hifadhi iwe huru na si lazima. Iwe ni michango ya hiari.

Irene Isaka, nadhani utajenga uhasama na wafanyakazi walio wengi. Hembu kajipange na uje kwa upya.
 
eh..eh..eh...hili ni bomu la B52.....mbona wanazilia mingo hela za wanyonge kiasi hiki??
 

Hii sio haki kabisa. Nyie SSRA toka lini mmeteuliwa na MUNGU kujua ni lini binadamu wa Tanzania wanaochangia mifuko ya hifadhi watakufa? Na kwa nini mtu asubiri mpaka miaka 55 au 60? Ni nani aliyewiaambia kuwa baada ya kustaafu mtu atategemea tu hizo pesa za hifadhi? Je ni nani aliyewaambia kuwa mtu akistaafu hawezi tena kufanya kazi? Mbona Serikali yenyewe iliwaita Madaktari wastaafu wakati ule wa mgomo wa Madaktari?

Hii sheria yenu imepitwa na wakati, nadhani suala hili ilikuwa muamue kama watu wanataka kujiunga na hifadhi iwe huru na si lazima. Iwe ni michango ya hiari.

Irene Isaka, nadhani utajenga uhasama na wafanyakazi walio wengi. Hembu kajipange na uje kwa upya.

Irene Isaka katumwa na William Erio wa PPF aliyekuwa boss wake kuwa afute hilo fao maana mfuko wa PPF ungekufa hivi karibuni kama hilo fao la kujitoa lingeendelea.

PPF hadi sasa hivi inatakiwa kuwa PROVIDENT FUND sio Pension Fund maana imepoteza sifa hiyo kisheria, ni maiti inayotembea. Wamefilisi pesa yote kwa kugawana kila mwaka wakurugenzi. Wanaochangia walio katika ajira za kudumu PPF ni 30% tu wakati wale ambao wanaweza kujitoa wakati wowote ni 70% na kulipwa withdrawal benefit.

Zitto hana ubavu wa kumwambia chochote DG wa PPF maana amewekwa mfukoni, kila wakati yuko naye eg sabasaba, nanenane etc na kila akija lazima akilimiwe na ktitita. Alionyesha ujasiri kwenye suala la Group Endowment lakini kaishia mfukoni mwa Erio
 
Iseeee inawezekana hii sheria imepitishwa zamani

Kichwa kinauma maana nilitaka kuchukua mafao yangu kujiwezesha kimradi

Maz^^^^&f**ck
 
Ktk hili serikali ime-target kutumbua mihela ya NSSF maana ndiyo fuko ambalo limetuna kuliko mifuko yote na huko ndo wanakokopaga hata kulipia mishahara ya watumishi wake wa umma
 
sijaelewa nchi inaezaje kubadili sheria nyeti kama hizi kiholela..mi nafikiri ifike mahali na wachanganiaji nao wawe na sauti ktk hii mifuko..haiwezekani tunapelekwa tu kama ndama machinjioni wakti sisi ni watu wazima wenye fikra kamili..kama wanataka kupeleka mambo kwa staili ya ngomani basi mifuko hii iwe hiari maana naona inatumika ndivyosivyo kama fimbo ya kuwachapia wafanyakazi..
 
Kila siku mmnaambiwa jiajirini wenyewe hamsikii..haya sasa oneni yanayowakuta. Mwenzenu nimejiajiri na nachangia kwenye voluntary scheme. Naweza kujitoa saa yoyote cuz sheria hainibani.
usiwe myopic..kama uso wote ungekua pua wapi lingekaa sikio na mdomo..ficha upumbavu wako.
 
[h=1]CAG: NSSF hatarini kufilisika[/h]
6db9d786bc77dd73357197bb3040a188.jpg

Na Reginald Miruko - Imechapwa 18 April 2012

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) uko hatarini kufilisika na kupoteza fedha za wanachama wake.
Hii inatokana na serikali kushindwa kurejesha katika mfuko huu, mabilioni ya shilingi iliyokopa au kudhamini katika miradi mbalimbali.
Kwa mujibu wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya 2010/2011, fedha za wanachama, hata katika mifuko mingine ya jamii, ziko hatarini kupotea.
Mbali na NSSF, mifuko mingine inayotajwa kuwa katika hatari hiyo ni Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF); Mfuko wa Wafanyakazi wa Serikali Kuu (PSPF), Mfuko wa Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (LAPF) na Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF).
Kulingana na taarifa ya CAG, sehemu kubwa ya fedha za wanachama ambazo hazijarejeshwa, zilikopeshwa kwa serikali kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Katika chuo hiki, NSSF peke yake iliingiza Sh. 234.1 bilioni. Mifuko iliyosalia ilitoa jumla ya Sh. 181.3 bilioni.
Katika ujenzi wa UDOM, PPF ilitoa Sh. 39.99 bilioni, PSPF (Sh. 105.9 bilioni), LAPF (Sh. 22 bilioni) na NHIF (Sh. 13.4 bilioni). Fedha hizo na riba yake hazijarejeshwa.
Ripoti ya CAG, Ludovick Utouh, inasema kutorejeshwa kwa mikopo hiyo, iliyochukuliwa au kudhaminiwa na serikali, ni kinyume cha sheria ya udhamini ya mwaka 1974.
"Kutolipika kwa mikopo hii iliyodhaminiwa na serikali kunaiweka mifuko hii ya hifadhi katika hatari ya kupoteza fedha za wanachama na kuhatarisha uwezo wa mifuko kufanya uwekezaji zaidi," anasema na kuongeza:
"Kushindwa kulipa madeni taasisi hizi ambazo baadhi yake zilipata udhamini wa serikali, kunatia shaka iwapo upembuzi wa kina wa wakopaji ulifanywa na mifuko ya kijamii kabla ya kutoa mikopo hiyo."
Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dk. Ramadhan Dau hakupatikana kwa maelezo kuwa alikuwa kwenye mkutano mkoani Mbeya.
Lakini Meneja Kiongozi Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume amesema mikopo kwa serikali imetolewa kwa uangalifu na inalipwa bila matatizo na kwa misingi ya kibiashara.
"Mikataba ya kisheria imesainiwa kukidhi mazingira mbalimbali ikiwa ni pamoja na iwapo itacheleweshwa…. Hakuna hatari yoyote ya fedha kutolipwa wala kupoteza fedha za wateja," amesema Chiume.
Lakini CAG katika taarifa yake ya kurasa 183, anasema, "Ukubwa wa kibiashara kati ya serikali na mifuko unatia shaka kutokana na kusuasua kwa serikali katika ulipaji madeni yake. Hii inahatarisha uendelevu wa mifuko hii."
Katika ukaguzi wake, CAG amebaini kuwa NSSF ilitoa Sh. 234.1 bilioni kwa mradi wa UDOM, lakini mkataba uliosainiwa ni wa Sh. 35.2 bilioni tu. Hii ni hatari kwa fedha za wafanyakazi na wastaafu.
Akifafanua suala la fedha kwenye mkataba kutofautiana na fedha zilizotolewa, Chiume alisema mkataba ulitakiwa kuwa mmoja ambao ulisainiwa wakati wa awamu ya kwanza.
Chiume alisema kwa awamu ya pili, kilichotakiwa ni kusaini addendum (makubaliano ya nyongeza), ambayo "yako mbioni kukamilika."
Utouh anaripoti, "Majengo kwa ajili ya awamu ya kwanza yalikamilika na kuwekwa katika matumizi mwezi Septemba 2008. Mpaka wakati wa ukaguzi 2010/2011, mfuko ulikuwa haujafanikiwa kukusanya malipo ya pango kutoka serikalini.
Kwa msingi huo, hadi sasa limbikizo la riba limefika thamani ya Sh. 14 bilioni," anasema Utouh.
Mkopo huo ulitolewa kwa utaratibu wa kubuni, kujenga, kumiliki na kuhamisha ambapo mfuko ungepokea kodi iliyokokotolewa kwa riba ya asilimia 15 kwa kipindi cha miaka kumi.
Vilevile CAG amebaini kuwa majengo yaliyojengwa kwa mkopo huo, hayako kwenye vitabu vya UDOM wala katika vitabu vya NSSF, kutokana na uelewa tofauti uliopo kati ya pande mbili zinazohusika.
Kuna mikanganyiko katika uelewa kwa serikali na mifuko ya hifadhi, ameeleza CAG. Wakati mifuko inasema fedha zilizotumika kujenga majengo hayo zilikuwa mikopo kwa serikali, yenyewe serikali inadai fedha hizo ni uwekezaji wa kawaida wa mifuko hiyo.
Mbali na UDOM, serikali pia haijalipa jumla ya Sh. 19.77 bilioni zilizotumika katika ujenzi wa ukumbi wa bunge, ambazo hazilipwi kulingana na makubaliano. Hadi wakati wa ukaguzi, NSSF ilikuwa inadai Sh. 8.96 bilioni, PPF (Sh. 7.9 na LAPF Sh. 2.91.
Pia upo mkopo mwingine wa NSSF wa Sh. 5.33 bilioni na riba ya asilimia 15 kwa miaka kumi, uliotolewa kwa ajili ya ujenzi wa "taasisi ya serikali ya kiusalama" mwaka 2007.
Mfuko mwingine uliowekeza katika mradi huo ni PSPF uliotoa Sh. 6.4 bilioni.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, NSSF kwa udhamini wa serikali ilikopesha taasisi kwa shughuli mbalimbali.
Kwa mfano, ujenzi wa nyumba za polisi kwa Sh. 20 bilioni na Sh. 12. 9 bilioni kwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam mwaka 2007 kwa ajili ya ujenzi wa Machinga Complex, Ilala.
 
Hii kitu imekaa vibaya sana.. hela yangu mwenyewe mnipangie siku ya kuichukua? Mateso mnayotupa nyie CCM yanatosha jamani au mnataka mpaka tufe kabisa ndio mfurahi? hela mnazopiga kwenye Meremeta,kagoda, EPA haziwatoshia saa mnataka mapaka hata hichi kidogo tunachokatwa kila siku? sasa life expectancy miaka 52 nyie mnaweka eti Mpaka 55 ili iweje?

Tuhurumiane jamani.. mtu akiacha kazi apewe hela yake ajue anaifanyia nini wengine tu akazi za mikataba ya miaka miwili miwili.. sasa mnategemea mkataba ukiisha nisubiri mpaka miaka 55?
 
Hawa jamaa wanadhani wataweza kubadilisha hizi sheria mpaka lini? Je hawajui kuwa leo watabadili sheria kwa kuona mwanya na kesho waone kuwa mifuko ina hela na kuendelea kukopa hatimae kijikuta wanakopa zaidi, je wataendelea kubadili sheria ili wastaafu wasubiri mpaka mfuko utakapo lipwa na serikali? Sisiem tafakarini sana, acheni kutumia mabavu katika kufikiri na kufanya maamuzi yasiyo kuwa na tija kwa walalahoi.
 
utapeli mwingine, nani atafika miaka 60? and if they want to do that basi watoe fursa ya mikopo kwa wanachama wao otherwise wizi mtupu.
 
Ndio madhara ya vijana wa kitanzania kupelekeshwa na mtukio. Wakati mswada huu unajadiliwa watu waliconcentrate kufuatilia vitimbi vya mijadala ya mswada wa katiba. Kumbe Bunge kila linapokaa kuna kitu cha msingi cha kufuatilia, sio mpaka mbunge anapotolewa nje na spika. Sasa imeshakuwa sheria. Hata hivyo, its not too late, marekebisho yanaweza kufanyika.
Kwa Tanzania kumwambia mtu angoje mpaka miaka 60 wakati life expectancy ya watu wengi wa sasa ni miaka 45, ni kudhulumu tu wafanyakazi.
 
hapa ssra ilitakiwa kuzuia serikali kukopa kutoka kwenye mifuko na mafisadi wasikope huko, kuliko kulizunguka tatizo kwa kuondoa mafao ya kujitoa, ikumbukwe pamoja na sheria za pension, bado kwa upande wa haki za binadam pesa hizo zimetafutwa na kuwekwa na wafanyakazi kutoka kwenye jasho lao, hivyo wanauhuru wa kuzitumia.
 
eh..eh..eh...hili ni bomu la B52.....mbona wanazilia mingo hela za wanyonge kiasi hiki??

Unaposikia akina mzee Mwanakijiji wanasema kuna mifumo ya kifisadi nchini mwetu inatuongoza hii ndo mifano yake mkuu. Mwisho wa siku watazikopa wao kufanyia biashara zao na kuendelea kuneemeka na familia zao na watajenga daraja la kigamboni kwa ajili ya mji mpya! Hebu niambie, una mtoto/watoto wanasoma na ghafla unapoteza kazi yako inayokuingizia kipato, una miaka labda 35 na kwa maana hiyo huwezi kuchukua vijisenti vyako na umeshindwa kupata ajira mpya. Hawa watoto wataishia kufukuzwa shule na familia inaweza kukosa hata mahitaji kwa sababu mishahara tunayoipata ndani ya ajira haitunziki! Sheria za namna hii zinalipeleka wapi taifa hili? Wanataka kila mtu awe mwizi katika sehemu yake ya kazi ili ajilimbikizie kwa ajili ya matumizi baada ya ajira? Nashindwa kuwaelewa kabisa!
 
Ukimbuka nyuma kidogo, sheria za pension (wakati huo zikiwa tofauti) zilifanyiwa mabadiliko kwa kupunguza umri wa kustahili pension kutoka 45 hadi 55 na 60 kwa lazima, hii yote kuhakikisha mifuko inakaa na pesa za wachangiaji muda mrefu, hivyo ni mwendelezo tu wa mambo, mwisho itapitishwa sheria ya wananchi kutolipwa pension!!!!!
 
Irene Isaka katumwa na William Erio wa PPF aliyekuwa boss wake kuwa afute hilo fao maana mfuko wa PPF ungekufa hivi karibuni kama hilo fao la kujitoa lingeendelea.

PPF hadi sasa hivi inatakiwa kuwa PROVIDENT FUND sio Pension Fund maana imepoteza sifa hiyo kisheria, ni maiti inayotembea. Wamefilisi pesa yote kwa kugawana kila mwaka wakurugenzi. Wanaochangia walio katika ajira za kudumu PPF ni 30% tu wakati wale ambao wanaweza kujitoa wakati wowote ni 70% na kulipwa withdrawal benefit.

Zitto hana ubavu wa kumwambia chochote DG wa PPF maana amewekwa mfukoni, kila wakati yuko naye eg sabasaba, nanenane etc na kila akija lazima akilimiwe na ktitita. Alionyesha ujasiri kwenye suala la Group Endowment lakini kaishia mfukoni mwa Erio

Unataka kusema hii sheria imeletwa na PPF? Vipi ulisoma report ya CAG?

Serikali ndio mkopaji mkubwa kwenye hii mifuko, na kwa jinsi hali ilivyo haiwezekani kuendelea kutumikia vyote, serikali na watu wanaojitoa. Kwa bahati mbaya Tanzania hakuna unemployment benefit ambayo ingetakiwa itoke serikali kuu. Hivyo anayekuwa nje ya ajira kabla ya miaka 55 ana-hang hadi hapo atakapopata kazi nyingine au afikie umri wa kustaafu.
 
Back
Top Bottom