Hakuna malipo ya NSSF, PPF hadi umri wa kustaafu ufike!

allydou

JF-Expert Member
Apr 16, 2009
1,603
1,060
Habari wana JF

Ni muda sasa, tangu mwezi wa sita hivi nimekuwa nikisikia kwamba Serikali ipo katika hatua za mwisho za kuzuia wafanyakazi wa sector binafsi kuchukua NSSF zao mpaka wafikishe umri wa kustaafu uliowekwa na seerikali, like 60yrs.

nilisikia kwamba mpango huu ulikuwa uanze mwaka huu mwishoni, lakini ikashindikana kutokana na maandalizi kutokuwa yamekamilika vizuri.

Nimesikia tena leo mjadala huu ukiendelea kwenye forum moja ya watu wanaofanya kazi kampuni mmoja through outlook mails kwamba mpango huu utakuwa implemented kuanzia 1st march 2012 bila kukosa.

Nilisikia pia kupitia wana forum hao kwamba bunge lilipisha muswada huu na Rais kuusaini kinyemela tangu mwaka jana, kitu ambacho kinaniumiza kichwa, inakuwaje muswada nyeti kama huu upitishwe kwenye bunge hili la sasa la ushindani wa kisiasa na hoja zenye mantiki kutoka upinzani bila wanachi kufahamu.

mwenye uhakika na suala hili please naomba unifahamishe vizuri.

Itakuwa ni vizuri zaidi kama utaleta na official data kuleta uhakika zaidi.

Aksanteni.
Na Hellen Mwango | 23rd July 2012

Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), imesema kuanzia sasa mwanachama wa mfuko wowote hataruhusiwa kuchukua mafao yake kutokana na sababu yoyote mpaka hapo atakapofikisha miaka 55.

Hata hivyo, licha ya kuzuia fao la kujitoa na kutoruhusiwa kuchukua mafao yao, mwanachama wakiwamo wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) na Mfuko wa Pensheni ya Mashirika ya Umma NSSF) atapata fursa ya kupata mikopo ya nyumba kwa kutumia dhamana ya michango yake kama ilivyoelezwa kwenye sheria ya SSRA.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa SSRA, Irene Isaka, mabadiliko hayo yametokana na sheria za mamlaka hiyo kufanyiwa marekebisho na kupitishwa na Bunge Aprili 13, mwaka huu na kwamba imeshasainiwa na Rais Jakaya Kikwete na imeanza kutumika rasmi.

Kwa mujibu wa marekebisho hayo fao la kujitoa yamefutwa na kuanzia sasa hayatakuwepo.

"Mafao hayo yalikuwa yanatolewa pale mwanachama alipokuwa anaacha kazi lakini kuanzia sasa mwanachama wa mfuko atapata mafao yake pale atakapofikisha umri wa kustaafu kwa hiari (55) au kwa lazima (60) au pale anapopata ulemavu wa kudumu" ilisema taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana na kufafanua kuwa:

"Marekebisho hayo kuhusu kuzuia mafao ya kujitoa yamefanyika ili kutimiza lengo na madhumuni ya hifadhi ya jamii ambayo ni kuhakikisha kuwa mwanachama anapostaafu anapata mafao bora yatakayomwezesha kumudu maisha ya uzeeni.

Taarifa ya Mkurugenzi huyo iliendelea kusema kuwa mafao ya kujitoa yanapunguza na kuondoa kinga ya mfanyakazi pale anapoumia kazini au anapofika uzeeni.

Hata hivyo, ilisema pamoja na kuzuia fao la kujitoa, mafao mengine ambayo ni muhimu kwa sekta ya madini yataendelea kutolewa kama kawaida ikiwemo kuumia kazini pamoja na fao la ulemavu.

Ilisema wanachama wanatakiwa kuwa watulivu kuhusiana na mabadiliko hayo na kwamba maslahi yao yatalindwa na hakuna atakayepunjwa kutokana na utaratibu huo.


CHANZO: NIPASHE

Ufafanuzi Kutoka Mamlaka ya Usimamizi na Udhitibi wa Hifadhi ya Jamii

UFAFANUZI KUHUSU FAO LA KUJITOA KATIKA MAREKEBISHO YA SHERIA ZA MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII.

Ufuatao ni ufafanuzi mfupi kuhusu marekebisho ya Sheria za Mifuko hasa kuhusu fao la kujitoa.

20 JULAI, 2012

1. Kama mtakumbuka Sheria za Mifuko ya Hifadhi ya Jamii pamoja na Sheria ya Mamlaka zimefanyiwa marekebisho na kupitishwa na Bunge tarehe 13 Aprili, 2012. Sheria hiyo tayari imeshasaininiwa na Mheshimiwa Rais na imeanza kutumika rasmi. Marekebisho haya yanawahusu wafanyakazi wote nchini mwetu bila kubagua sekta yoyote ile.

2. Kwa mujibu wa marekebisho hayo fao la kujitoa (withdrawal benefits) yamefutwa na kuanzia sasa hayatakuwepo. Mafao hayo yalikuwa yanatolewa pale mwanachama alipokuwa anaacha kazi. Sasa mwanachama wa Mfuko atapata mafao yake pale atakopfikisha umri wa kustaafu kwa hiari (miaka 55) au kwa lazima (miaka 60) au pale anapopata ulemavu wa kudumu.

3. Kwa kuzuia fao la kujitoa mwanachama anapata fursa ya kupata mikopo ya nyumba kwa kutumia dhamana ya michango yake kama ilivyoelezwa kwenye Sheria ya SSRA kipengele cha 38.

4. Marekebisho hayo kuhusu kuzuia mafao ya kujitoa yamefanyika ili kutimiza lengo na madhumuni ya hifadhi ya jamii ambayo ni kuhakikisha kuwa mwanachama anapostaafu anapata mafao bora yatakayomwezesha kumudu maisha ya uzeeni wakati ambapo nguvu ya kufanya kazi tayari imeshamwishia.

Mafao ya kujitoa yanapunguza na hata kuondoa kabisa kinga ya mfanyakazi pale anapoumia kazini au anapofika uzeeni.

5. Tunawaomba muwaelimishe wafanyakazi umuhimu na madhumuni ya mafao ya hifadhi ya jamii. Hifadhi ya jamii ni nyenzo mahususi iliyowekwa kuwasaidia wafanyakazi kuendesha maisha yao wakati wanapokuwa wameishastaafu tayari. Umasikini wa kipato wakati wa uzee ni mojawapo ya changamoto ngumu kukabiliana nazo kwa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. Tunawasihi tena muelimishe wafanyakazi kuhusu jambo hili. Tafadhali msisite kuwasiliana na Mamlaka pale ufafanuzi zaidi utakapohitajika

6. Kwa kuwa marekebisho hayo yamesainiwa na kuanza kutumika rasmi kama sheria, mafao ya kujitoa hayawezi kutolewa tena na wafanyakazi watakaoacha kazi kwa sababu ya marekebisho ya kipengele hicho watakuwa hawajaijitendea haki wao wenyewe na pia itakuwa ni kunyume cha Sheria.

Mamlaka inaandaa kanuni za mafao ambayo lengo lake ni kuboresha maslahi ya wanachama, kanuni hizo zitajadiliwa na wadau wakiwemo vyama vya wafanyakazi na waajiri ili kupata maoni yao.

7. Tafadhali muwaelimishe wafanyakazi kwamba pamoja na kuzuia fao la kujitoa, mafao mengine ambayo ni muhimu kwa sekta ya Madini yataendelea kutolewa kama kawaida. Mafao hayo ni Kama vile kuumia kazini pamoja na fao la ulemavu

8. Tumesikia kwamba tayari kuna hofu imejijenga kwa wanachama kuhusiana na fao la kujitoa. Ikumbukwe kwamba baadhi ya Mifuko ilikuwa inatoa fao hilo kinyume cha Sheria kwani katika Sheria zao hakuna fao la kujitoa. Tunapenda kusisitiza kwamba wanachama wawe watulivu wakisubiri miongozo.

9. Tunapenda kuwahakikishia kwamba katika hili maslahi ya wanachama yatalindwa na hakuna mwanachama atakayepunjika kutokana na utaratibu huo.

Mamlaka imepanga kutembelea wafanyakazi wa sekta ya madini katika juma la kwanza la mwezi Agosti 2012 ili kutoa ufafanuzi zaidi kwa wanachama wote.

Tunatanguliza shukrani za dhati kwa ushirikiano.

Wenu.
Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Hifadhi ya Jamii

Irene Isaka
MKURUGENZI MKUU

 
Hi wana JF,

Nimesikia kuwa kuna sheria imepitishwa kuwa HAKUNA TENA kuchukua hela za NSSF ukiacha kazi HADI UMRI wa kustaafu
ufike.

Mwenye kujua UKWELI atuhabarishe zaidi (NSSF au watunga sheria wetu).

Wafanyakazi wa sekta binafsi mnalijua hili?
 
Bargain,

Hii sio tetesi maana haijawa kama hivyo. Lakini umefanya vizuri kuleta hii habari katika kipindi hiki na kuwafanya waajiriwa wote Tanzania wakae mkao wa kula.

Ukweli ni kwamba serikali ina mpango wa kupeleka bungeni marekebisho ya muswada wa sheria wa mafao ya wafanyakazi kama ulivyopitisha ba bunge ili sasa kufanya wafanyakazi wote wanaokatwa akiba ya mafao (PPF,NNSF, PSPF,LAPF,GEPF n.k) kulazimika kutopata mafao yao kama hawajatimiza umri wa kustaafu(55-60).Mpango huu unaletwa kwa sababu serikali yenu haina namna ya kufanya na ingependa kupata boost ya mapato toka mifuko hii ili kuleta pesa kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Mpango huu wa aibu na kandamizi utawaathiri wafanyakazi zaidi ya 700000 serikalini lakini kwa kipekee utaathiri na kuua ndoto za wafanyakazi zaidi ya 3000000 walio katika sekta binafsi kama vile makampuni, NGOs na wale waliojiajiri wenyewe na ambao wanatumia mifuko hii.

(Una imani kubwa kwamba wabunge wetu hasa wa upinzani wataupigia ngumu mpango huu nyonyaji ambao ni wa aina yake katika nchi zote za Afrika. Hii pia inatoa fursa kwa wafanyakazi wote nchini (hasa vijana) kutafakari na kuona jinsi serikali yenu inavyopanga kufifisha mipango yenu ya muda mfupi na ile ya kati. Kazi kwenu simameni na Chukueni Hatua Sasa.

HABARI NDO HIYO
 
Hi wana JF,

Nimesikia kuwa kuna sheria imepitishwa kuwa HAKUNA TENA kuchukua hela za NSSF ukiacha kazi HADI UMRI wa kustaafu
ufike.

Mwenye kujua UKWELI atuhabarishe zaidi (NSSF au watunga sheria wetu).

Wafanyakazi wa sekta binafsi mnalijua hili?

naona sasa wanataka tuwashkishe ukuta.

anywayz nimechukuwa cheki yangu jusi baada ya kusungushwa karibu miezi miwili.
 
Jamii forums inawachangiaji mbalimbali wakiwemo wataalamu kutoka kwenye mashirika yanayohusika na mifuko ya jamii.Naamini katika mashirika haya kuna maafisa mahusiano ambao wanapaswa kutolea ufafanuzi mabo mbalimbali likiwepo hili.,kwa fursa hii mnaombwa kutufahamisha wafanyakazi na wananchi kwa ujumla .
 
Usawa haki na maisha bora kwa wafanyakazi wa tanzania unakaribia kufutika maana haina maana yoyote ya kufanya kazi kwa mkataba ktk mashirika binafsi. Tutaishi maisha ya kufikirika tabu na mateso ndiyo furaha ya serikali yetu
 
Tatizo la hii mifuko ya hifadhi za jamii ni kwamba, waliwekeza sana kwenye vitaga uchumi ambavyo rejesho la uwekezaji ni la muda mrefu sana hivyo hawana jinsi.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Mnwele

Asante kwa ufafanuzi.

Shida ni kuwa likishafika BUNGENI watasema NDIOOOOOOOOO wale wabunge wa CCM na kwa kweli hali haitakuwa nzuri hasa kwa sekta binafsi.

Wafanyakazi tulio PRIVATE toeni michango yenu ya mawazo nini kifanyike kuzuia udhalimu huu unaotaka kufanyika.
 
Last edited by a moderator:
Hii sheria ikipitishwa itawaadhiri wafanyakazi wengi wa sekta binafsi na itakuwa imeharibu ndoto za vijana wengi wenye nia ya kujiajiri labda serikali nayo ipunguze umri wa kustaafu kutoka miaka 55 kwa hiari hadi miaka 45 na hii inatokana na wastani wa umri wa mtanzania kuishi ni miaka 45 tu.
 
Hi hatari sana tena sana kama wabunge wakipitisha hilo basi nitajua wabunge ni washezi na hawafai itakuwa ni haki kuwapinga maye,mi nilitegemea waweke sheria ya mtu kuacha kazi au kufukuzwa kazi alipwe mara moja mafaao ya NSSF sio kuzungushwa kama ilivyo sasa, ni tabu sana kuipata hela ya NSSF ni usumbufu wa hali ya juu.

Kwanza ukiacha kazi eti usubili mpk miezi 6 ndio uanze kudai,lakin walivyo wajinga kwa wafanyakazi wa BARRICK MINING eti ukiacha kazi unalipwa ndani ya wiki 2,sasa hio ni akili au matope,hilo la BARRICK MINING nina ushahidi kwani nilishakuwa mfanyakazi wa barrick,tutapinga kwa nguvu zote wao wapitishe waone.
 
Hi wana JF,

Nimesikia kuwa kuna sheria imepitishwa kuwa HAKUNA TENA kuchukua hela za NSSF ukiacha kazi HADI UMRI wa kustaafu ufike.

Mwenye kujua UKWELI atuhabarishe zaidi (NSSF au watunga sheria wetu).

Wafanyakazi wa sekta binafsi mnalijua hili?
Kwa life expectancy ipi? Waache wenye pesa wajichukulie pale wanapotaka.
 
Wana JF kumbukeni,

Bunge lilipitisha WAFANYAKAZI WA SERIKALI hawalipi kodi kwenye ALLOWANCES lakini PRIVATE lazima ulipe kodi ya allowances zote (eg house allowances e.tc).

Je TUKINYAMAZA katika hili la HELA ZETU si nalo litapitishwa?

Tuamke tutake kuelezwa ukweli na Serikali.
 
Kama itapita hakika itakuwa kilio kwa wafanyakazi wengi;
Kwa maisha ya sasa yalivyo na ugumu wa kila hali; magonjwa ya kila aina , BP, kisukari, HIV/AIDS , TB , malaria etc. Bado wanategemea watu tufike 55- 60yrs old. ..............Eeh Mungu tusaidie waja wako.
 
Kwanza ukiacha kazi eti usubili mpk miezi 6 ndio uanze kudai,lakin walivyo wajinga kwa wafanyakazi wa BARRICK MINING eti ukiacha kazi unalipwa ndani ya wiki 2,sasa hio ni akili au matope,hilo la BARRICK MINING nina ushahidi kwani nilishakuwa mfanyakazi wa barrick,tutapinga kwa nguvu zote wao wapitishe waone.

Hapo kwenye nyekundu, hii ni KASHFA ya wazi. WHY BARRICK??????
 
Back
Top Bottom