Hadithi ya Kweli: Jini wa Daraja la Selander

Mwachiluwi

JF-Expert Member
Mar 10, 2022
17,796
32,148
JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.1

Majira ya saa nane za usiku msichana Suzana alikuwa akitoka kujirusha katika ukumbi wa Bilicanas. Kilichomshtua kilikuwa kutoweka kwa mpenzi wake Sammy ambaye aliondoka bila kumuaga. Wazo lake la kwanza lilikuwa Sammy kaondoka na msichana mwingine akijua kabisa yeye ndiye mchumba wake.

Akiwa amekasirika kwa kitendo cha Sammy kuondoka na kumuacha peke yake, kila alipopiga simu yake iliita bila kupokelewa kitu kilichoonesha dharau. Aliamua kurudi nyumbani kwake japo alipanga siku ile kwenda kulala kwa Sammy. Aliendesha gari akiwa amefura kwa hasira huku machozi yakimtoka kutokana kitendo alichotendewa na mpenzi wake ambaye ndiye aliyemtoa kitandani alipokuwa amekwisha kulala. Suzana awaliza mengi juu ya kitendo cha mpenzi wake kumwita klabu na kumkimbia.

Wakati akitoka Bilicanas mvua ilianza kunyesha, hakutaka kuisubiri aliamua kwenda nayo ili awahi kunyumba angalau alale kwa muda mchache ili asubuhi awahi kanisani misa ya kwanza.

Mvua ilikuwa kubwa iliyoambatana na upepo mkali kitu kilichomfanya ashindwe kuona mbele ilimbidi alisimamishe gari pembeni ya daraja ya Salenda ili kusubiri upepo upungue ndipo aendelee na safari yake. Upepo ule haukuchukua ulitulia na mvua ilikuwa imekatika.

Alipowasha gari liligoma kuwaka, alirudia zaidi ya mara tano kuzungusha funguo lakini liligoma kuwaka. Kuteremka kwenye gari alishindwa kutokana na hali ya kiza cha kutisha nje. Wasi wasi ulimtawala na kujiuliza atatokaje pale au ndio atalala mpaka asubuhi.

Hasira zilizidi kumpanda Suzana kutokana na kukimbiwa na mpenzi wake na kuharibikiwa na gari. Kutokana na hofu aliyokuwa nayo alihakikisha milango na vioo vyote vimefungwa vizuri. Alijikuta akipiga dua kumuomba Mungu amuokoe la janga lile kwa kupata msaada wa watu wenye gari kumsaidia kuwasha gari lake. Lakini kwa muda ule hakukuwa na dalili ya gari lolote kupita.

Akiwa ameinama mikono ameikutanisha kifuani kwake alishtushwa na upepo makali uliovuka toka baharini na kulifanya gari lake kuyumba na kusogea kidogo. Kwa woga uliompata Suzana alijikuta akitokwa na haja ndogo bila kuelewa. Alitamani kulia lakini aliamini sauti yake haitasaidia lolote kwa vile hakukuwa na wakumsaidia.

Aliinama kwa woga hakutaka kuangalia popote zaidi ya kusubiri chochote kitakachomtokea. Baada ya muda hali ile ilitulia, Suzana alinyanyua kichwa taratibu ili achukue simu ampigie baba yake amfuate eneo lile ambalo lilikuwa limemuweka katika hali ya hatari.

Aliponyanyua uso achukue simu iliyokuwa kwenye kwenye dash board, alishtushwa na mwanga mkali kama jua la saa saba mchana. Aliangalia katikati ya bahari palipokuwa kunatoka mwanga ule. Alituliza macho baada ya kumuona mwanamke aliyekuwa amevaa gauni jeupe lilikuwa liking’aa kutokana na mapambo yake.

Hali ile ilimfanya asahau yalitomtokea muda mfupi na kutuliza macho kumuangalia yule mwanamke aliyekuwa akitembea juu ya maji huku nyuma akisindikizwa na wasichana walikuwa wamebeba vikapu vidogo vilivyokuwa na maua ambayo walimwagia kila hatua ilivyopigwa huku wakiimba nyimbo nzuri.

Suzana alijikuta akipata ujasiri wa ajabu kwa kufungua dirisha kidogo ili aweze kusikia watu wale walikuwa wakiimba kitu gani. Zilikuwa sauti nzuri kama za kaswida zilizoibwa kwa lugha ya kiarabu. Nyimbo zile zilimvutia na kujikuta akiwa na hamu ya kuwaona watu wale waliokuwa wakitembea juu ya maji huku kwa mstari mbele akitangulia yule mwanamke ambaye usoni kwake kulikuwa kunawaka kama taa na kushindwa kuiona sura yake vizuri.

Suzana alijikuta akisahau kama wale watu walikuwa wakitembea juu ya maji zaidi ya kushangazwa na sherehe ile ambayo toka azaliwe hajawahi kuona sherehe ya aina ile ya mtu mmoja kutangulia mbele wengine kumfuata nyuma huku wakimuwagia maua na kumwimbia nyimbo nzuri.

Baada ya muda watu wote walikaa mstari mmoja, kisha yule mwanamke aliyekuwa amepeneza kuliko wote alipita katikati yao na kupigiwa vilegele huku akitupiwa maua. Manukato ya maua yalisambaa mpaka ndani ya gari la Suzana alilokuwa amefungua kioo kidogo kusikia nyimbo alizokuwa anaimbiwa yule mwanamke ambaye alionekana kama bibi harusi lakini muda wote hakumuona bwana harusi wala mwanaume kwenye kundi lile.

Yule mwanamke alipita kwenye mstari mpaka mwisho alitembea peke yake bila kufuatwa na mtu kisha aligeuka na kuwapungia mkono wenzake ambao nao walimpungia huku wakimrushia maua. Baada ya kutembea kidogo Suzana alimshuhudia yule mwanamke alikunja gauni lake usawa na kifua na kushangaa kumuona akitembea ndani ya maji yaliyokuwa yamemfika tumboni.

Suzana alijikuta akishtuka na kujiuliza yupo ndotoni au anaona kweli, kilichomshangaza ni umbali aliotoka yule mwanamke akitembea juu ya maji. Lakini cha kushangaza alipokaribia ufukweni alionekana yupo ndani ya maji yaliyomfikia tumboni.

Aliendelea kumtazama amuone anakwenda wapi, yule mwanamke baada ya kutoka ndani ya maji alitembea juu ya mchanga kulifuata lile gari. Kila hatua ilivyokuwa akipiga ilizidi kumtisha Suzana, alijikuta akimshangaa kutaka kuijua sura yake. Alituliza macho yake kwenye uso wa yule mwanamke aliyekuwa akiisogelea gari huku manukato makali yakizidi kujaa ndani ya gari.

Kilichomshangaza zaidi ni sura ya yule mwanamke alikuwa akifanana naye kwa kila kitu umbile na sura. Suzana alishtuka na kufunga kioo haraka ili mtu yule ambaye yeye alimuona wa muujiza asiingie kwenye gari. Yule mwanamke alisogea kwenye gari na kuligusa, ajabu baada ya kuligusa lile gari alitoweka ghafla.

Suzana akiwa anatetemeka alijaribu kuwasha gari kwa mara nyingine, ajabu ya Mungu gari liliwaka aliondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi. Alipofika nyumbani kulikuwa kumekucha, alikwenda kuoga haraka ili awahi kanisani kwani muda ulikuwa umekwenda.

Baada ya kuoga alirudi ndani, lakini alishtushwa na harufu ya manukato ambayo aliyasikia muda mfupi darajani gari lake lilipozima na kuenea hadi ndani ya gari lake. Hakutaka kulifikiria sana lile kwa muda ulikuwa umekwenda, alikwenda kwenye kabati kubadili nguo ili awahi kanisani.

Baada ya kumaliza kubadili nguo alijikuta akiingiwa na uvivu na kwenda kukaa kwenye kitanda haikupita muda. Usingizi mzito ulimshika na kulala bila kujielewa, aliposhtuka usingizini alishtuka kuiona familia yake yote imesimama mbele yake. Alijiuliza kuna nini, alipojiangalia alijiona alikuwa amevaa nguo za kuendea kanisani.

“Suzana upo sawa?” Mama yake alimuuliza.
“Mbona unaniuliza hivyo? Halafu mbona kama wote mlikuwa mnalia kuna nini mbona mnanitisha?

Nini kimemtokea Suzana mpaka familia yake ikusanyike mbele yake huku wakitokwa na machozi. Kuyajua yote fuatana nami katika simulizi hii mpya ya kusisimua..
 
Yule mwanamke alipita kwenye mstari mpaka mwisho, alitembea peke yake bila kufuatwa na mtu kisha aligeuka na kuwapungia mkono wenzake ambao nao walimpungia huku wakiendelea na zoezi la kumrushia maua. Baada ya kutembea kidogo Suzana alimshuhudia yule mwanamke akikunja gauni lake usawa wa kifua na kushangaa kumuona akitembea ndani ya maji yaliyokuwa yamemfika tumboni.

Suzana alijikuta akishtuka na kujiuliza yupo ndotoni au anaona kweli, kilichomshangaza ni umbali aliotoka yule mwanamke akitembea juu ya maji. Lakini cha kushangaza alipokaribia ufukweni alionekana yupo ndani ya maji yaliyomfikia tumboni.

Aliendelea kumtazama amuone anakwenda wapi, yule mwanamke baada ya kutoka ndani ya maji alitembea juu ya mchanga kulifuata gari lake. Kila alivyopiga hatua Suzana alizidi kutishika, alijikuta akimshangaa na kutamani kuijua sura yake. SASA ENDELEA...

Alituliza macho yake kwenye uso wa yule mwanamke aliyekuwa akiisogelea gari huku manukato makali yakizidi kujaa ndani ya gari.

Kilichomshangaza zaidi umbile la yule mwanamke ambaye mwanzo alionekana kama mrefu tena mweupe lakini kila alivyomsogelea sura na umbile la yule mwanamke lilibadilika na kufanana naye kwa kila kitu. Suzana alishtuka na kufunga kioo haraka ili mtu yule ambaye yeye alimuona wa muujiza asiingie ndani ya gari.

Yule mwanamke alisogea kwenye gari na kuligusa, ajabu baada ya kuligusa, alitoweka ghafla. Suzana akiwa anatetemeka alijaribu kuwasha gari kwa mara nyingine, ajabu ya Mungu gari liliwaka aliondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi. Alipofika nyumbani kulikuwa kumekwisha pambazuka, alikwenda kuoga haraka ili awahi kanisani kwani muda ulikuwa umekwenda sana.

Baada ya kuoga alirudi ndani, lakini alishtushwa na harufu ya manukato ambayo aliyasikia muda mfupi darajani gari lake lilipozima na kuenea hadi ndani ya gari lake. Hakutaka kulifikiria sana lile kwa sababu muda ulikuwa umekwenda, alikwenda kwenye kabati kubadili nguo ili awahi kanisani.

Baada ya kumaliza kubadili, alijikuta akiingiwa na uvivu na kwenda kukaa kwenye kitanda haukupita muda usingizi mzito ulimshika na kulala bila kujielewa, aliposhtuka usingizini alishtuka kuiona familia yake yote imesimama mbele yake. Alijiuliza kuna nini, alipojiangalia alijiona alikuwa amevaa nguo za kuendea kanisani.
“Suzana upo sawa?” Mama yake alimuuliza huku akifuta machozi.

“Mbona unaniuliza hivyo? Halafu mbona kama wote mlikuwa mnalia kuna nini mbona mnanitisha?
“Suzana,” mama yake alimwita tena akiwa bado anamshangaa..
“Abee mama.”
“Upo sawa?” Mama yake alimuuliza huku akimkagua mwanaye kwa kumshika kila kona ya mwili.

“Nipo sawa mama, kwani vipi?”
“Siamini kweli Mungu wa ajabu.”
“Mama mbona sikuelewi nilitokewa na nini?” Suzana alizidi kushangaa.

“Hebu nyanyuka kwanza.”
Suzana alinyanyuka kitandani kuonesha yupo sawa, wote waliokuwa mule ndani walishukuru Mungu.
“Kwani muda huu ni saa ngapi?”

“Saa kumi na moja.”
“Jamani ina maana sikwenda kanisani?” Suzana alizidi kujishangaa.
“Kwani ilikuwaje?” Mdogo wake wa kike alimuuliza huku akionesha kumshangaa dada yake.

“Hata najua, nashangaa kuwaona mpo mbele yangu mkitokwa na machozi kwani nilikuwa kwenye hali gani?”
“Mmh, haielezeki.”
“Mbona mnanitisha.”
“Ulitaka kwenda kanisani misa ya ngapi?”

“Ya kwanza, ooh, nimekumbuka nilihisi uchovu na kuja kujilaza kilichoendelea sikujua, kwani mama nini kimenitokea?”
“Tumepigiwa simu na shoga yako kuwa upo katika hali isiyoeleweka, ndipo tulipozoana na wadogo zako kuja hapa. Tulipofika tumekukuta umepoteza fahamu hujitambui hata mapigo yako ya moyo yalionesha kusimama.”
“Mungu wangu!” Suzana alishtuka sana.

“Basi tulichanganyikiwa, lakini sikutaka kuamini kama kweli utakuwa umekufa, ndipo tulifanya maombi ambayo yamekufanya unyanyuke na kuonesha kama ulikuwa katika usingizi mzito. Hatuamini kama huna tatizo lolote.”
“Ni ajabu kulala muda mrefu kiasi hicho sijawahi kutokewa na kitu kama hicho, lakini nipo sawa kama uchovu ni wa kawaida tu.”

“Mmh, haya ni maajabu makubwa sana, kuna umuhimu wa kwenda kwanza hospitali kuichunguza afya yako.”
Suzana hakutaka kubishana na familia yake, walimchukua na kumpeleka hospitali ya TMJ. Walipofika walimueleza daktari hali waliyomkutana nayo na baada ya maombi kuamka kama alikuwa usingizini.

Alichukuliwa vipimo vyote ambayo havikuonesha ugonjwa wowote, waliruhusiwa kurudi nyumbani. Siku ile alichukuliwa kwenda kulala kwa wazazi wake, usiku kwake ulikuwa mrefu kuwaza yote aliyokutana nayo na hali iliyomtokea. Mpaka siku ya pili inaingia hali ya Suzana ilikuwa nzuri hakuonesha mabadiliko yoyote.

Siku hiyo aliondokea kwa wazazi wake kwenda kazini, alipofika kazini alikuwa mtu mwenye mawazo mengi juu ya matukio yaliyomtokea toka alipokimbiwa na mpenzi wake kwenye ukumbi wa Club Bilicanas, matukio ya ajabu aliyoyaona baharini kwenye sherehe ya ajabu.
Kingine hali waliyomkutanayo kama mtu aliyekuwa amefariki, na kushangazwa na jinsi alivyoamka na kukutwa hana ugonjwa wowote zaidi ya uchovu wa usingizi. Alijiuliza hali ile imemtokea kwa sababu gani, akiwa katika dimbwi la mawazo shoga yake kipenzi Sharifa aliingia.

“Vipi shoga mbona leo sikusomi?”
“Mmh, shoga wee acha tu kuna mambo yamenitokea yananichanganya.”
“Yapi? Hebu kaa chini nikueleze yaliyonisibu najuta kwenda club usiku.”
“Yepi tena hayo shoga?”

Suzana alimueleza yote aliyokutatana nayo usiku na hali iliyomkuta baada ya kumaliza kuoga ili aende kanisani na alipoamka na kukukuta watu wamemzunguka na kumueleza walimkuta akiwa kama amekufa.
“Haa! Shoga unayosema ni kweli?”
“Kweli kabisa.”

“Huyo mtu unasema umemuona wapi?”
“Daraja la Salenda”
“Mmh!” Sharifa aliguna.
“Mbona unaguna?”
“Mbona tukio linafanana kama langu.”
Sharifa naye alikutana na tukio gani linalo fanana na Suzana?
 
LIPOISHIA;
Kingine, hali waliyomkutanayo kama mtu aliyekuwa amefariki dunia na kushangazwa na jinsi alivyoamka na kukutwa hana ugonjwa wowote zaidi ya uchovu wa usingizi. Alijiuliza hali ile imemtokea kwa sababu gani. Akiwa katika dimbwi la mawazo shoga yake kipenzi, Sharifa aliingia.
“Vipi shoga mbona leo sikusomi?”

“Mmh, shoga wee acha tu kuna mambo yamenitokea yananichanganya.”
“Yapi? Hebu kaa chini nikueleze yaliyonisibu najuta kwenda klabu usiku.”
“Yapi tena hayo shoga?”

Suzana alimueleza yote aliyokutana nayo usiku na hali iliyomkuta baada ya kumaliza kuoga ili aende kanisani na alipoamka na kukukuta watu wamemzunguka na kumueleza walimkuta akiwa kama amekufa.
“Haa! Shoga unayosema ni kweli?”
“Kweli kabisa.”

“Huyo mtu unasema umemuona wapi?”
“Daraja la Salenda”
“Mmh!” Sharifa aliguna.
“Mbona unaguna?”
“Mbona tukio linafanana na kama langu.” SASA ENDELEA...

“Lako?”
“Eeeh.”
“Tukio gani?”
“Unajua kuna mtu nilimueleza akasema eti ni uongo na uzushi, si unakumbuka kuna tukio moja lilitamba katika vyombo vya habari?”
“Tukio gani?”

“Lile la msichana kuota manyoya baada ya kumpa msaada ombaomba kwenye Daraja la Salenda?”
“Ndiyo.”

“Mimi nilikuwa mmoja ya watu walio kataa katakata kuwa ni uzushi, Suzana mimi ni mbishi sana kukubaliana na jambo linaloonekana ni la kusadikika.”
“Mh.”

“Basi wiki iliyopita katika majira ya saa kumi na mbili jioni nikiwa narudi nyumbani, si unajua foleni za Dar. Toka pale Palm Beach magari yalikuwa yakienda taratibu sana, tulipofika katika Daraja la Salenda magari yalisimama. Niliendelea kusubiri huku nikisikiliza nyimbo za Injili.

“Nje ya magari kulikuwa na ombaomba wachache, sikushughulika nao, niliendelea kusikiliza muziki nikisubiri foleni isogee. Nilishtushwa na dirisha kugongwa kwa nje, niliponyanyua macho nilimuona ombaomba wa kike akitaka msaada kwangu.

“Huruma iliniigia, nilifungua dirisha kidogo na kumpa noti ya elfu moja, halafu nilifunga dirisha na kuendelea kusikiliza muziki. Nilishtushwa tena dirisha kugongwa, nilipoangalia nilimuona yule yule ombaomba wa kike. Nilijiuliza ana shida gani ya kugonga tena, safari hii nilijikuta nimefungua kioo mpaka chini na kumuuliza:

“Una shida gani tena?”
Yule ombaomba aliyekuwa ameinama na uso wake kuzibwa na nywele nyingi alinyanyua uso wake na kunitazama, alionesha kama kunishangaa. Nilijiuliza mbona amenishangaa huenda kanifananisha na mimi nilikaza macho kumwangalia.

Kilichonishangaza zaidi ilikuwa sura yake iliyofanana sana na yangu kama pacha. Moyo ulinilipuka ajabu, kuna kitu nilikiona kikitoka kwenye macho yake na kupiga kwenye macho yangu na ghafla alitoweka.”
“Weee!” Suzana alishtuka.

“Ndiyo maana nikasema tukio kama langu japo tofauti yake ni ndogo sana. Baada ya foleni kuanza kutembea, niliondoa gari na kwenda moja kwa moja nyumbani. Amini Suzana tukio lile wala sikulitilia maanani kwa vile sikulielewa na pia sikuwa muumini wa mambo ya kishirikina.”
“Mh!”

“Basi shoga, siku ile nyumbani nilikutana kimwili na mume wangu. Kama kawaida mzunguko wa kwanza ulikwenda vizuri, ajabu wa pili hakuwa na nguvu. Kila alivyojitahidi nguvu zake za kiume ziligoma.”
“Mmh!” Suzana aliguna na kujitengeneza vizuri kwenye kiti chake.
“Tokea siku ile mpaka leo mume wangu hana nguvu za kiume.”
“Usiniambie!”

“Kweli kabisa.”
“Sharifa unataka kuniambia ombaomba yule ndiye aliyesababisha yote hayo?”
“Sasa napata picha kuwa sehemu ile kweli kuna kitu kinafanyika.”
“Kwa hiyo unataka kusema ni kweli pale kuna jini kama watu wanavyoamini?”

“Sina uhakika kama ni jini lakini kuna kitu kibaya.”
“Kwa hiyo hata ya mwanamke kuota manyonya ni kweli?”
“Inawezekana.”
“Mmh! Kama ni kweli basi tuna hatari, kwani yule mwanamke alipatikana?”
“Nilisikia alionekana ufukweni akiwa uchi na akili zake kama chizi.”
“Unataka kuniambia ndiye aliyetutokea?”

“Huenda.”
“Basi kuna umuhimu wa kulifanyia kazi jambo hili.”
“Ngoja tutafute ushauri wa watu wazima.”
“Kwani mumeo ulimueleza uliyokutana nayo?”
“Sikumueleza kwa kuamini hali ile imetokana na yeye kutoka nje ya ndoa.”
“Una uhakika gani?”

“Suzana, sasa naingiwa na imani hiyo kutokana na tukio lililokutokea wewe.”
“Sharifa kabla ya kutafuta ufumbuzi mbadala kwa nini usikae chini na mumeo kutafuta sababu ya yeye kuwa vile?”
“Suzana mume wangu namfahamu vizuri, hata kama anatembea nje haijawahi kutokea, ninaye mwaka wa kumi sasa.”

“Mmh! Bado haijawa sababu, kwani yeye anasemaje?”
“Kwa kweli nyumba yetu imeingia matatizo ya kulaumiana huku nikimlaumu mume wangu na yeye kusema haelewi sababu ile inatokana na nini.”
“Mmekwenda hospitali?”
“Suzana wazo hilo sikuwa nalo, akili yangu yote niliielekeza kwenye lawama.”

“Sharifa hasira siku zote haijengi ulitakiwa kumsikiliza mwenzako.”
Wakiwa tukiwa katikati ya mazungumzo Brighton mpenzi wa Suzana aliingia. Baada ya kusalimiana Sharifa aliwaaga na kuwaacha wapendanao wazungumze. Baada ya kuondoka Sharifa alimuangalia Brighton kwa jicho la hasira.
“Vipi sweet, mbona unaniangalia hivyo?”

“Brighton wewe wa kunifanya hivyo, nimepungukiwa nini mwilini mwangu kufikia hatua ya kunidhalilisha kiasi hicho,” Suzana alimlalamikia mpenzi wake.
 
JINI WA DARAJA LA SALENDA.......EP.4.


ILIPOISHIA;
“Sikumueleza kwa kuamini hali ile imetokana na yeye kutoka nje ya ndoa.”
“Una uhakika gani sababu ya mumeo kuwa hivyo ni kutokana tukio lile?”
“Suzana sasa naingiwa na imani hiyo kutokana na tukio lililokutokea.”

“Sharifa kabla ya kutafuta ufumbuzi mbadala kwa nini usikae chini na mumeo kutafuta sababu ya yeye kuwa vile?”
“Suzana mume wangu namfahamu vizuri, hata kama anatembea nje haijawahi kutokea ninaye mwaka wa kumi sasa.”

“Mmh! Bado haijawa sababu, kwani yeye anasemaje?”
“Kwa kweli nyumba yetu imeingia matatizo ya kulaumiana huku nikimlaumu mume wangu na yeye kusema haelewi sababu ile inatokana na nini.”

“Mmekwenda hospitali?”
“Suzana wazo hilo sikuwa nalo, akili yangu yote niliielekeza kwenye lawama.”
“Sharifa hasira siku zote haijengi ulitakiwa kumsikiliza mwenzako.”

Wakiwa katikati ya mazungumzo Brighton mpenzi wa Suzana aliingia, baada ya kusalimiana Sharifa aliwaaga na kuwaacha wapendanao hao wazungumze. Baada ya kuondoka Sharifa alimuangalia Brighton kwa jicho la hasira.

“Vipi Sweet mbona unaniangalia hivyo?”
“Brighton wewe wa kunifanya hivyo, nimepungukiwa nini mwilini mwangu kufikia hatua ya kunidhalilisha kiasi hicho?” Suzana alimlalamikia mpenzi wake. SASA ENDELEA...

“Suzana nimekufanya nini tena mpenzi wangu?”
“Hujui...hujui eeh, juzi umenifanya nini Bilicanas?”
“Sasa Suzana nani wa kulaumiwa kati yangu na wewe?”
“Brighton unachukua mwanamke unaniacha club peke yangu, nilikulazimisha kuwa na wewe siku hiyo, si ni wewe ndiye uliyenipigia simu nije tujumuike wote kisha nikalale kwako.

Kama ulijua una miadi na mwanamke mwingine kwa nini uliniita?” Suzana alijisahau kama yupo ofisini na kujikuta akitokwa na machozi ya uchungu.
“Mimi?”
“Kwani nazungumza na ukuta?”

“Suzana juzi si nilikuacha unakunywa mimi nikapanda juu kuzungumza na Shakoor, nilipoteremka nilishangaa kukuta meza nyeupe na vinywaji vipo kama nilivyoviacha. Nilijua umekwenda msalani lakini muda ulipokwenda sana ilibidi nitoke nje kukutafuta. Kilichonishangaza sikukuta gari lako ilibidi nikodi teksi hadi nyumbani kwa kuamini umekwenda huko.

“Kila nilipopiga simu yako iliita bila kupokelewa, nilipofika nyumbani kwangu sikukuta, nilisubiri kwa saa moja mpaka saa tisa na nusu. Baada ya kutokukuona niliamua kukufuata kwako, nilikuta mlango umefungwa. Nilipomuuliza mlinzi aliniambia hujarudi.

“Hapo nilichanganyikiwa, nilijiuliza utakuwa wapi? Huwezi kuamini mpaka kunakucha nilikuwa sijapata jibu. Simu yako kila nilipopiga iliita bila kupokelewa, nilirudi nyumbani na kuamua kujilaza kidogo niende kanisani misa ya pili kutokana na uchovu wa kutopumzika.

“Amini usiamini nimeamka saa tatu usiku toka saa moja asubuhi nilipoweka ubavu, toka nizaliwe na kuwa na akili zangu timamu sijawahi kutokewa na usingizi wa ajabu kama ule. Hata nilipoamka nilikuwa kamsa mlevi niliyekunywa pombe nyingi, sikunyanyuka kitandani niliendelea kulala, huwezi kuamini nililala bila kula kwa saa 24 na nilipoamka leo asubuhi nilikuwa na nguvu kama sijatokewa na kitu chochote.

“Nilipitia kwako mlinzi alinieleza kama ulirudi, lakini kuna kitu kilitokea kilichoonesha kuna jambo limekupata na kuchukuliwa na familia yako. Mimi kiguu na njia mpaka kwenu, nilipofika niliambiwa umekuja kazini na afya yako ni salama. Kwani ulitokewa na nini?”
“Yangenitokea bila wewe?”

“Bila mimi kivipi Suzana?”
“Eeh, kama ningekwenda kwako unafikiri ningekutana na mauzauza, Brighton uliondoka na mwanamke unajitetea tu,” Suzana alizidi kulakamika.
“Suzana mpenzi wangu tuna muda gani juzi nifanye hivyo?”
“Si umenichoka.”

“Suzana naapa kwa jina la Yesu Kiristo uliniacha juu sikutoka na mwanamke muulize hata Shakoor kama nilitoka na mwanamke au muulize mlinzi wako nimefika kwako saa ngapi?”
“Itanibidi nikubali kwa vile nakupenda.”

“Suzana mpenzi wangu niamini siwezi kwenda kunyume na ahadi yetu, nakupenda na sitakusaliti hata siku moja.”
“Basi yamekwisha lakini uliniumiza sana.”
“Mh, eti ulipatwa na nini?”

“Samahani Brighton toka niingie ofisini sijafanya kazi yoyote, naomba unipe muda baada ya kazi nikitoka hapa nikakuja kwako moja kwa moja tuzungumze, ni mazungungumzo marefu.”
“Nigusie hata kidogo”
“Ni kuhusu nilipotoka Bilicanas na mambo niliyokutata nayo njiani.”
“Mambo gani?”

“Nimekueleza nitakueleza au unataka nifukuzwe kazi?”
“Basi mpenzi wangu nimekuelewa.”
Waliagana Brighton na mpenzi wake Suzana na kumuacha akifanya kazi. Baada ya kuondoka Brighton, Suzana alijikuta akihamia kwenye maelezo ya Brighton juu ya hali iliyomtokea ya kulala zaidi ya saa kumi na nne. Alijiuliza kama yeye alikutana na maajabu yale, Brighton alikutana na kitu gani.

Kazi kwake ilikuwa nzito siku ile, aliomba ruhusa na kurudi nyumbani kupumzika, kabla ya kutoka alimjulisha mpenzi wake kuwa anatangulia nyumbani kwake.

Baada ya kutoka kazini alikwenda moja kwa moja nyumbani kwa mpenzi wake, kwa vile alikuwa na funguo za nyumba alifungua na kuingia ndani. Alipoingia alishangaa kukuta chumbani kumesafishwa tofauti na siku zote, mara nyingi usafi wa nyumba ile alikuwa akifanya yeye.

Ile haikumsumbua akili yake aliamini kutokana na msongo wa mawazo hali ya usafi ya nyumba ingemfanya asisumbue mwili wake zaidi ya kwenda moja kwa moja chumbani kujilaza. Hali ya hewa ndani ilikuwa nzuri tofauti na siku zote huku harufu ya manukato aliyowahi kuyasikia alipokutana na maajabu ya dalaja la Salenda.

Upepo mwanana uliompuliza ulimfanya apitiwe na usingizi bila kujijua, katikati ya usingizi alishtushwa na Brighton akimpapasa.
“Aah, mpenzi umerudi zamani?”
“Kama robo saa.”

Kwa vile Brighton alikuwa amekwishaoga Suzana naye alikwenda kuoga na kujumuika wote kitandani. Kama kawaida walisafiri katika meli ya wapendanao, safari ya kwanza ilianza vizuri kila mmoja aliifurahia. Baada ya safari ya kwanza kwisha Suzana hamu ilikuwa bado haijamuisha alitaka asafiri safari moja zaidi ndipo wapumzike.

Ajabu kila alipomgusa mwenzake jogoo alikataa kuwika kitu kilichomshtua Suzana.
“Vipi mpenzi mbona hivi?”
“Hata mimi nashangaa.”
Nini kimempata Brighton? Au ndiyo yaliyompata mume wa Sharifa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom