Hadithi: Mpangaji

CK Allan

JF-Expert Member
Aug 14, 2013
2,729
5,923
Karibuni Tena katika story hii
Kama kawaida ni mwanzo mpaka mwisho hakuna kuishia njiani

Kutoka "madam president" na ",kesi ya Mzee Mnyoka"

Ssa Leo tunaanza kisa kingine Cha Mpangaji
Mtunzi ni Mimi mwenyewe CK Allan

(0746 Mia mbili sitini na sita mia mbili sitini na Saba)


MPANGAJI 01
Hakuna mpangaji yoyote ambaye alikuwa anafahamu asili ya Yule mpangaji mwenzao, hata jina lake la ‘Sele’ wapo waliosema halikua jina lake halisi, lakini yote kwa yote Sele kama unavyoweza kusema alikua mpangaji wa kudumu wa mzee Mhina, miaka ilikatika na sio mzee Mhina wala wapangaji ama watoto wake walijua kazi halisi ya Sele.

Wapo waliosema sele alijihusisha na kazi ya kuzibua vyoo huko mjini mbali na hapo, wengine walisema sele Alikuwa mtu wa ‘kitengo” na kama ilivyo kawaida ya wabongo basi wengine walizua kuwa sele ni jahili mzoefu,
Kwanza Sele asingetoka nje ya chumba chake bila kuitwa, na kwakuwa chumba chake kilikua ni selfu basi huwezi kujua kama sele yupo ndani au ametoka.

Mama mwajuma hawezi kusahau yeye na wapangaji wenzake walivyoumbuka siku hiyo walitumia masaa zaidi ya mawili kumsengenya Sele kwa sauti ya juu kabisa.

“Tena nakuambia huyu Sele itakuwa anafuga majini, mwanaume gani huwezi kumkuta yuko nje na wenzake, nyumba haina redio wala tivii halo halooo!”.

“halafu hata siku moja sio mwanaume wala mwanamke aliwahi kuingia hicho chumba!”

“hakuna hata ndugu yake mmoja aliyewahi kuja hapa nakuambia mwaka wa sita huu mimi niko hapa!” wapangaji wenzake walikua wakiendelea kumzodoa sele,

Mama Mwajuma alikua amekazana kuongoza maongezi hayo bila kujua sele alikua ndani akiwasikiliza tu,
Ni mpaka pale waliongea hadi wakachoka ndipo Sele alitoka akiwa na mkoba wake.

Alimsalimia mama Mwajuma kwa heshima kama ilivyokuwa kawaida yake kisha akatoa elfu tano na kumpa mama Mwajuma ambaye alishikwa na kigugumizi.

“hii hela ya umeme utampa kaka Efraimu hapo tutaonana baadae” alisema Sele akitoka zake..
Huku nyuma wale wanawake waliangua kicheko
“tumeumbuka shoga, umbea huuu”
Alisema aisha akirudi ndani kwake..

****************************
Kama kawaida siku hiyo saa tatu usiku Sele alirejea zake nyumbani kwake aliwapita wanawake kadhaa waliokuwa bado hawajamaliza kupika vyakula vyao vya usiku, aliwasalimia kana kwamba hakuna chochote kilichotokea asubuhi ile kisha akafungua mlango na kujitosa ndani.

Huku nyuma vicheko vilisikika kama kawaida lakini aliwapotezea, hakuwa na muda wa kubishana nao kwanza ukimtoa Ephraim, wapangaji wengine walimkuta akiwa pale, kwanini ahangaike nao.

Usiku wa manane Sele alistushwa na kelele za wapangaji huko nje ya chumba chake alijaribu kutega sikio kusikiliza vizuri na kugundua ulikua ugomvi wa mke na mume tu, kama kawaida hakujishughulisha na ugomvi usiomhusu akavuta shuka lake na kulala.

Alfajiri alistuka mlango wake ukigongwa kwa nguvu na Ephraim , alimtambua sauti yake
“labda ni pesa ya umeme” aliwaza akitoka akivaa “malapa” yake na tisheti kisha akafungua mlango na kutoka
‘OI, broo’ alisema Sele
‘kuna kikao mshkaj njoo chap ‘ alisema Ephraim akirudi zake, kwa muda wote aliokaa pale hakuwahi kumuelewa Sele, kuna wakati alijaribu kumzoea lakini alijikuta akishindwa na hakuna hata siku moja alifanikiwa kukaa nae zaidi ya dakika tano.

Hata kwenye vikao vya usafi, umeme na maji, Sele hakuchangia chochote alisubiri makubaliano tu kisha alitoa pesa yoyote itakayokubaliwa.

Hata mzee Mhina alikua akimtolea mfano kuhusu ulipaji kodi, haijawahi kutokea Sele akapitisha mwezi bila kulipa kodi ya pango.

Tofauti na vikao vingine , siku hiyo mzee Mhina na balozi wa nyumba walikuwepo kwenye kikao cha siku hiyo kidogo sele alistuka lakini hakuonyesha mshangao wake wazi akasogea na kukaa kwenye mkeka kama wenzake.

“nadhani wotetupo sasa tuendelee ili wengine waende kutafuta riziki”
Alisema mzee Mhina. Wote waliitikia kisha Balozi akamkonyeza mzee Mhina kumuashiria atoe hoja kikao kianze
“ sasa ndugu zangu nimepata malalamiko kuhusu Bwana Sele hapa” alianza Mzee Mhina,

‘Jana usiku kulikua na ugomvi miongoni mwa wapangaji na walitoka na kupigana bado kidogo wauane, wapangaji wote walitoka kuamua na kusaidia lakini ndugu yetu Sele yeye wala hakujisumbua kutoka, sio jana tu lakini hata wakati ule chumba cha mama Isa kilipopata hitilafu Bwana Sele pia hakutoka kabisa.

Nakumbuka pia hata wakati wa sherehe ambayo niliandaa mimi mwenyewe wakati binti yangu Rehema akifunga ndoa Bwana Sele pia hakuhudhuria hivyo kwa mazingira haya naona kabisa kuna kitu huyu mwenzetu anacho anajaribu kutuficha nikaona balozi uje kidogo utusaidie,” alimaliza Mzee Mhina huku wapangaji wote wakipiga jicho kwa Sele.

‘ ooh Kijana wangu Sele, hebu niangalie, hivi kweli leo hii hata nikikuambia unitajie majina ya wapangaji wenzako utawajua kweli?’ aliuliza Balozi huku wapangaji wengine wakicheka.

“huyu anamjua Ephraim tu ndio mwenzake huyoo” alidakia mama Mwajuma.

‘ Hapana nawajua wote!” alidakia Sele kisha akaendelea.

‘wewe ni mzee Lota, una watoto wanne , watatu wa kike na mdogo wa mwisho wa kiume, Yule ni Aisha na mumewe Mkude, Yule ni mama Mama Mwajuma na mume wake Ngoda, pale ni Isa, kule ni John na hapa ni kaka Ephraim na mke wake mama Joan’ alimaliza Sele huku akiwaacha wapangaji wote mdomo wazi, hususani huyu mpangaji John ambaye alikua na siku ya pili tu!

“Wewe mwana wewe, umejuaje mpaka hawa wapangaji wapya? Umeona sasa Balozi tukisema sisi tunaishi na zimwi.. zimwi..” alidakia mama Mwajuma huku wapangaji wote wakiangua kicheko.

“ Mama Mwajuma, tumalize kikao ili usichelewe kumuandalia mgeni wako Ester anayekuja leo kutoka Lindi!” alisema Sele akitoka zake kurudi chumbani!

‘Bwana sele hatujamaliza lakini!” alisema Mzee Mhina lakini sele alirudi zake chumbani kumalizia usingizi wake,
“makubwa haya, makubwa haya sasa kuhusu Huyu Ester huyu Sele kajuaje jamani” alisema mama Mwajuma huku akiondoka.

Kikao kile kilivuruga kabisa mtazamo wao kuhusu Sele, wapangaji waligawanyika huku wengine wakitaka afukuzwe, na wengine wakisema hawajaona kosa
“sasa afukuzwe kwa kosa gani?

Bili zote analipa, usafi analipa, kodi ya watu analipa, hawajawahi kugombana na mtu kaka wa watu, muacheni bhana!”

Alisema Ngoda na kisha kikao kikaishia hapo

Inaendelea
 
MPANGAJI 02
Ilipita wiki moja na hali ikawa shwari kabisa kwa wapangaji wa mzee Mhina, siku hiyo usiku Sele alikua anarudi zake na kwa bahati mbaya siku hiyo alikua amechelewa kupita siku zote na hivyo ilibidi agonge geti na kusubiri kidogo, alikua amevaa begi lake kama kawaida na mkononi akiwa na mfuko wa chipsi na soda yake tayari kabisa kuingia ndani, mara nyingi alikua akichelewa alifunguliwa mlango na kaka Ephraim au mzee Ngoda,

siku hiyo ilikua tofauti sana kwani wakati geti linafunguliwa Aliona sura ngeni kabisa machoni pake ya msichana mrembo umri wa miaka 25-28 hivi, Sele alijikuta akishikwa na kigugumizi na akili yake ikasimama kidogo akiwa ameduwaa pale getini.

“ingia ndani kaka Sele!” alisema Yule msichana nae akiduwaa

“ah ah, bila Shaka wewe ni Ester?” alisema Sele sasa akiingia ndani

“umejuaje?” aliuliza Ester akimalizia kufunga geti.

“ah mama yake alisema utakuja wiki iliyopita kwahiyo nimeona wewe ndio mgeni tu hapa vipi mbona hujalala mpaka sasa hivi!” aliuliza Sele akieleka mlangoni kwake.

“ah kuna tamthilia naangalia kwahiyo niliposikia unagonga nikaona nikufungulie na nikuone maana nasikia tu sele! Sele!” alisema akitabasamu

“ohoo ushasikia umbeya tayari!” alisema sele sasa akiingia chumbani kwake,
Sele aliingia ndani kwake huku mawazo yake yakiwa kwa Ester ni kweli alikua anakutana na wasichana wengi kila siku, na hata hapo walikuja wapangaji wengi tu wa kike na kuondoka lakini haijawahi kutokea msichana aliyeubamba moyo wake kama ilivyokuwa kwa Ester,

“siamini kama nimekamatika hivi!” alijisemea Sele akifungua soda yake na kunywa,
Pamoja na kuwa ilikua ni mara ya kwanza wanaonana na binti Yule Sele alijiapiza kabisa Yule binti ameushika moyo wake.

Ester nae kwa upande wake aliona kitu cha tofauti kwa sele, kwanza zile hadithi alizokuwa amesikia kwa mama yake pamoja na wapangaji wengine kuhusu sele alitaka kuthibitisha kwa macho yake, na hivyo baada ya kusoma ratiba ya sele na kukosa kumuona mara kadhaa ndipo sasa siku hii akaamua kujitahidi kuwahi nafasi ya kufungua mlango ili amuone sele.

Haikua sababu ya mapenzi wala nini Ester alitaka tu kuona huyo Sele ni mtu wa namna gani, ni jini kweli? Au ni mtu wa namna gani! Na pengine akirudi kazini kwake Lindi basi angekuwa na kitu cha kusimulia walimu wenzake au pengine hata wanafunzi wake.

Ester alikua mwalimu wa sekondari ya kata ya kibaoni akifundisha Kiswahili na Historia, ni mwaka mmoja tu ulikua umepita toka aajiriwe katika shule hiyo baada ya kumaliza chuo cha aualimu huko Butimba Mwanza , kulikua na tetesi kuwa mama Mwajuma alikua amemficha mtoto wake huyo kwa mume wake baada ya yeye kuja Dar, na ndio maana hakuwahi kufika hapo nyumbani, na baada ya kukusumbuliwa sana na Ester mwenyewe ndipo sasa hakuwa na jinsi isipokuwa kumleta Ester amuone mama yake na baba yake wa Kambo,
Hivyo ester alitumia likizo ile ya pasaka kuja kumtembelea mama yake na ndipo sasa akasikia kuhusu Sele,
“kwakweli huyo Sele ni kama jini mwanangu yaani hapa pengine anatusikia!” ester alikumbuka maneno ya mama yake mchana huo na kisha akatabasamu tu akivuta shuka kulala katika chumba cha mwajuma,

Siku hiyo sele Alijikuta anachelewa makusudi kutoka ili tu amuone Ester ni kweli alimaliza kujiandandaa kabisa na kisha akawa anasikiliza huko nje kama atasikia sauti ya wanawake na ester akiwemo ndipo akatoka na begi lake na kuangaza huko na huko.

“za asubuhi shemeji!’ alikuwa aisha akimsalimia Sele

“ah poa tu vipi hajambo kaka!” alisema sele akiangaza macho huko na huko na hatimaye akamuona Ester akitoka.

“kaka Sele za asubuhi! Nataka leo twende huko mjini na mimi niangaze macho jamani, si unajua nimetokea kijijini jamani!” alisema Ester huku akiongeza mwendo kuelekea kule Sele aliko.

“dah Litakufa jitu leo” aliwaza Sele.

“ooh twende basi nikutembeze” alisema sele nae akiwa siriasi

Wapangaji wengine walitoka kuchungulia kwani hakuna aliyewahi kuongozana na Sele hata siku moja!

“kweli mtu na mtuwe!’ alisema mama Mwajuma akiwa ameshika mdomo

‘mama baadae jamani natoka na kaka Sele!” ester alisema kwa sauti..

“sele unafanya nini ?” alisikia sauti ikimwambia kwenye hisia zake.

‘unafanya makosa Sele’.

“ACHA UFALA SELE wewe ni mwanaume!” sauti nyingine ilimwambia.

Hakujali aliendelea kupiga hatua akiwa sambamba na Ester ambaye alikua na mkoba wake na simu yake ya Samsung galaxy.

“mh kwahiyo tunaanzia wapi? Kazini kwako au mtaani kwanza?” aliuliza ester!

“wewe umesemaje kwani?” Sele nae aliuliza

“nilisema tukaangalie mji” alisema ester

“Basi sasa leo nitakutembeza mpaka miguu iume!” alisema Sele

“kwahiyo kazini kwako hatufiki?” aliuliza Ester

“hapana mama, leo utembee uone mji kama ulivyotaka!” alisema Sele kwa upole

“kwahiyo kaka Sele nimesababisha wewe usiende kazini jamani!” aliuliza Ester

“mh mbona umekazania kazi! Kaz! Kwani umeambiwa nafanya kazi gani! Hahaha?” Sele aliulizahuku akimtazama Ester.

“hamna Bwana, si unajua tu mjini hapa kazi ni muhimu sana!” alisema Ester.

“basi kama ulivyosema hapa ni mjini sio kila kazi lazima uende” alisema Sele na sasa walikaribia kufika Stendi
“kariakoo, posta, kivukoni!” ilikua sauti ya konda akinadi dala dala.

“twende zetu” alisema Sele kisha wakaingia kwenye gari
Njiani walipiga hadithi za hapa na pale na Sele alijisikia vizuri sana na wakati mwingine alicheka hadi abiria wengine waligeuza shingo zao kuwatazama, kwa yoyote aliyewaona hakika alijua tu hawa ni wapenzi wapya ama wanandoa ambao wanakwenda kula fungate, kwani wakati mwingine Ester alimlalia mabegani sele,


Ester alimkumbuka mpenzi wake Ima, ambaye alianza nae mahusiano akiwa chuo cha ualimu , walikua na ndoto nyingi za kuishi pamoja bila kujua ima alikua na mpenzi wake mwingine aliyekuwa nae, siku ya mahafali yao Msichana huyo alikuja chuoni na kisha Ima Akamtambulisha mbele yake kuwa ni mchumba wake, ni bahati tu rafiki zake Ester waliwahi kumuweka “chini ya ulinzi” vinginevyo siku ile ingekuwa ya mwisho kwa ester,
Na kutoka pale Ester alijiapiza hatakuja kupenda tena mwanaume katika maisha yake, na ndio maana walimu wenzake pamoja na maafisa elimu aliwatolea nje mchana kweupe na hakutaka mazoea na yeyote, sasa alipopata habari za Sele kidogo zilimstaajabisha hususani aliposikia hajawahi kutembelewa na mwanamke yoyote,

Ester alikuwa anakumbuka hayo yote sasa wakiwa karibu kabisa kufika kariakoo

Walifika na kushuka na kuanza kutembea huko na huko, na kununua vitu vidogo vidogo,

Baadae walifika kwenye mgahawa na kuagiza supu, walimaliza kisha wakaedelea na mizunguuko kutoka kariakoo hadi posta na kuendelea na mizunguuko mpaka kufika saa 7 mchana Ester alikuwa hoi taabani wenyewe wanasema aliomba poo.

“hahaha hapa ujue nataka tuunge mpaka Temeke tushuke taifa tukaangalie mechi ya taifa starz” alisema sele
“no no no Sele nimechoka” alisema Ester.

“okay tumchukulie mama Mwajuma zawadi basi tugeuke ila mimi nitakuacha home siwezi kubaki nyumbani sasa hivi! Ujue” alisema Sele

“haya bhana turudi tuu” alisema Ester kisha wakarudi kituoni na kupanda dala dala,
“kweli leo nimetembea mjini, ila Dar ni nzuri kwakweli!’ alisema Ester huku akishushia na fanta yake
“yeah mzee baba Kajitahidi kuweka mji vizuri” alisema Sele

“hivi una mishe gani Lindi!’ aliuliza Sele

“mimi ni mwalimu jamani Sele si nilikuambia!” alisema Ester

“ ah kweli asee nakumbuka, kwahiyo unakula likizo sio!”

“yeah, wewe ndio umegoma kabisa kuniapeleka kazini kwako!” alisema ester

“hahaha si upo bhana tutaenda siku moja!’ alisema Sele sasa akichukua mizigo na kushuka!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom