CK Allan
JF-Expert Member
- Aug 14, 2013
- 2,729
- 5,923
KESI YA MZEE MNYOKA 01
Mzee Mnyoka alikua na kawaida ya kuchelewa kurudi nyumbani kwake, Mzee Mnyoka hakua mlevi au mchawi lakini tuseme tu hakua na mazoea ya kurudi nyumbani mapema.
Siku ya Alhamis Kama ilivyo kawaida yake Mzee Mnyoka alikua akirudi nyumbani kwake majira ya saa 4:45 hivi usiku. Akiwa mita kadhaa kabla ya kufika kwake kwa mbali alimuona mwenyekiti wake wa Kijiji akiwa anaburuta ng'ombe dume.
Mzee Mnyoka kwanza alijifanya hajamuona mwenyekiti, Mzee Mkude, lakini baadae Mzee Mkude alimuona Mzee Mnyoka , hivyo wakaonana macho kwa macho! Na ndipo Mzee Mkude akastuka sana na kutahayari!
“Kwanza Mzee Mkude hakuwa anafuga hata kuku nyumbani kwake! Lakini pia hakuwahi kufanya biashara ya nyama! Na hivi karibuni hajatangaza sherehe yoyote! Sasa huyu ngo'mbe usiku huu anampeleka wapi?”
Nahisi hicho ndicho kilichomstua Mzee Mkude! Mzee Mnyoka aligundua mfadhaiko wa mwenyekiti lakini hakuona Kama Kuna umuhimu wowote wa kuendelea kushangaa Mambo yasiyo mhusu! Mzee Mnyoka akajiendea zake nyumbani.
Kesho yake ijumaa habari zikaanza kusambaa kwa Kasi kuwa Mzee Pembe ameibiwa dume lake alilopewa Kama malipo ya mahari baada ya kumuoza binti yake Asha!
Msako ukaanza ili kumbaini mwizi wa lile dume, hatimaye siku ya jumamosi Mzee Mnyoka na Mzee Mkude wakakutana! Walipotazama hakuna aliyeongea kitu lakini macho yao yalizungumza!
Macho ya Mzee Mnyoka yalisema wazi wazi "najua mwizi Ni wewe" Huku macho ya Mzee Mkude yakisema "Ole wako unitaje!" Hatimaye wakasalimiana na Mzee Mnyoka akaaga na kuondoka kwa haraka, huku Mzee Mkude akipigwa na mshangao! Maskini Mzee Mnyoka alijilaumu kuona mpaka Sasa mwizi akiwa bado hajakamatwa, lakini ilimuuma Sana kuona huyo mwizi Ni mwenyekiti wake wa Kijiji,
Mzee Mnyoka alichoka!
****
Mzee Mnyoka alikuwa na kawaida ya kuchelewa kurudi nyumbani ndio, lakini siku za jumapili na mwisho wa mwezi Mzee Mnyoka alikua anawahi Sana! Na pengine siku nyingine hakutoka kabisa!
Siku hiyo jumapili baada ya siku tatu kupita tangu wizi utokee Mzee Mnyoka akiwa nyumbani kwake akisuka mkeka alipokea wageni wa kustaajibisha.
Polisi! Ndio, polisi walifika na kumueleza Mzee Mnyoka kuwa yupo chini ya ulinzi kwa tuhuma za kuiba Ng'ombe dume wa Mzee Pembe!
Mzee Mnyoka alikataa Kata Kata! Lakini polisi wakambeba msobe msobe na kwenda kumuweka lupango, huku wakimtolea maneno mazito kuwa atakoma, na huo ndio mwisho wa wezi kama yeye.
**********
Mzee Mnyoka alipiga kelele huku machozi yakimtoka "Jamani mnanionea! Mnanionea! Sijaiba Mimi! Sijaiba Mimi!" Wale polisi waliendelea kucheka na kupiga stori zao huku wakimuamuru Mzee Mnyoka kuacha makelele.
"We Mzee, hakuna mtu aliletwa hapa akakubali kosa kirahisi, wewe tuachie makelele yako hapa sio nyumbani kwako" Polisi mmoja aliongea huku wenzake wakimuunga mkono.
Nyumbani kwa Mzee mnyoka, mkewe hakupata usingizi, pamoja na tabia yake ya kuchelewa kurudi lakini Mzee Mnyoka aliishi vizuri na majirani, jioni Ile nyumbani kwa Mzee Mnyoka mtaa mzima ulihamia kwake, mkewe alikuwa amesharudia kuhadithia jinsi mumewe "alivyodakwa" na polisi, na Sasa mama Alli alikua amechukua jukumu la kusimulia kuhusu kukamatwa kwa Mzee Mnyoka.
"jamani Mzee Mnyoka sio mwizi, sote tunajua, haiwezekan wamchukue, twendeni huko polisi" Waliongea majirani. Hata hivyo mpaka saa 2 usiku bado hawakufikia muafaka na hatimaye usiku , mwenyekiti wa kitongoji ambaye ni kijana tu alifika Nyumbani kwa Mzee Mnyoka kutoa taarifa kuwa Mzee Mnyoka anaweza kupata dhamana kesho yake jumatatu na hivyo wasijisumbue kwenda usiku kule polisi na badala yake kesho waende kumuona!
Hakika Mzee Mnyoka Hakupata tabu peke yake Bali mkewe, na mtaa mzima walipata tabu. Kwanza Nani alienda kumshtaki Mzee Mnyoka? Mbona Mzee Mnyoka hajawahi kuiba hata kuku pale mtaani?
********
Mzee Mnyoka alilala mahabusu huku akiwa anaelewa kwanini Yuko pale! "Mkude mwanaharamu wewe labda nisitoke hapa !" Mzee Mnyoka alipaza sauti akiwa lupango...."Mkude , mshenzi Sana wewe, uibe Ng'ombe mwenyewe halafu unisingizie Mimi? Nikitoka hapa nakuua mshenzi wewe!" Mzee Mnyoka alikuwa anaropoka tu, na kupelekea polisi kuja kumtuliza ...
"We Mzee ukiendelea na hayo makelele yako tutashindwa kukuvumilia" alisema Afande mmoja aliyeitwa Paul. Mzee Mnyoka Hakupata usingizi kwani selo ilijaa harufu Kali ya kinyesi, na giza Totoro, huku mbu wakiwa wanapiga kelele za furaha, Mzee Mnyoka nguvu zilimuishia
*******
Mzee Mnyoka alishindwa kusimama na akajikuta anakaa chini na ndipo Sasa Mzee Mnyoka akapigwa na butwaa, Naam macho yake Sasa yalianza kuzoea giza la pale ndani baada ya kuwa alitoka kwenye mwanga mkali, Na ndipo Mzee Mnyoka akang'amua kuwa hakua peke yake pale ndani!
Ndio,
Mahabusu Tena mwishoni mwa wiki haiwezekan ikawa tupu! Kwa haraka haraka walikuwa Saba mle ndani, huku wa Nne wakiwa wamesimama na watatu wamelala! Mzee Mnyoka alijikuta akicheka!
Ndio alicheka kicheko Cha uchungu! Inawezekaje mtu apate usingizi katika chumba kile ambacho Mzee Mnyoka hakuelewa Kama anatakiwa kuziba pua au mdomo? Inawezekaje mtu apate usingizi katikati ya sherehe za mbu?
Mzee Mnyoka Sasa alitambua kuwa bila shaka wale waliolala, Ni watu wa Aina mbili, mosi,
Wameamua kusamehe na kujisamehe wao wenyewe na kusahau shida zote na kuamua kulala fofofo, ama Ni watu waliozoea Yale mazingira pale ndani! Lakini kwa namna yoyote Ile Mzee Mnyoka asingepata usingizi,
Kwanza alimkumbuka mke wake , mama Monica, pamoja na watoto wake,
Lakini pia Mzee Mnyoka aliwaza kesi iliyoko mbele yake, Kesi ambayo alikua hajui anaanzaje kujitetea. Ni kweli hakufanya, Ni kweli alimjua mhusika, lakini Nani atamuamini? Mzee Mnyoka machozi yalimtiririka.
************
Asubuh na mapema kituo Cha polisi mama Monica na majirani wengine walifika kumjulia Hali Mzee Mnyoka,
Polisi alienda kumtoa Mzee Mnyoka. Ambaye alijikaza huku akijilazimisha kutabasamu baada ya Kumuona mkewe. Alipata wasaa wa kuongea na mkewe na akapewa masharti ya dhamana, hivyo mkewe akishirikiana na majirani walienda "kuchakarika" kuhakikisha Mzee Mnyoka anapata dhamana, siku ile Ile ya jumatatu!
Baada ya mipango yote kukamilika ikiwemo kuuza mbuzi wake wawili na kuweka rehani cherehani yake , mama Monica alifanikiwa kupata dhamana ya mumewe saa 11 jioni! Na safari ya kurudi kijijini ikaanza!
Inaendelea
Mzee Mnyoka alikua na kawaida ya kuchelewa kurudi nyumbani kwake, Mzee Mnyoka hakua mlevi au mchawi lakini tuseme tu hakua na mazoea ya kurudi nyumbani mapema.
Siku ya Alhamis Kama ilivyo kawaida yake Mzee Mnyoka alikua akirudi nyumbani kwake majira ya saa 4:45 hivi usiku. Akiwa mita kadhaa kabla ya kufika kwake kwa mbali alimuona mwenyekiti wake wa Kijiji akiwa anaburuta ng'ombe dume.
Mzee Mnyoka kwanza alijifanya hajamuona mwenyekiti, Mzee Mkude, lakini baadae Mzee Mkude alimuona Mzee Mnyoka , hivyo wakaonana macho kwa macho! Na ndipo Mzee Mkude akastuka sana na kutahayari!
“Kwanza Mzee Mkude hakuwa anafuga hata kuku nyumbani kwake! Lakini pia hakuwahi kufanya biashara ya nyama! Na hivi karibuni hajatangaza sherehe yoyote! Sasa huyu ngo'mbe usiku huu anampeleka wapi?”
Nahisi hicho ndicho kilichomstua Mzee Mkude! Mzee Mnyoka aligundua mfadhaiko wa mwenyekiti lakini hakuona Kama Kuna umuhimu wowote wa kuendelea kushangaa Mambo yasiyo mhusu! Mzee Mnyoka akajiendea zake nyumbani.
Kesho yake ijumaa habari zikaanza kusambaa kwa Kasi kuwa Mzee Pembe ameibiwa dume lake alilopewa Kama malipo ya mahari baada ya kumuoza binti yake Asha!
Msako ukaanza ili kumbaini mwizi wa lile dume, hatimaye siku ya jumamosi Mzee Mnyoka na Mzee Mkude wakakutana! Walipotazama hakuna aliyeongea kitu lakini macho yao yalizungumza!
Macho ya Mzee Mnyoka yalisema wazi wazi "najua mwizi Ni wewe" Huku macho ya Mzee Mkude yakisema "Ole wako unitaje!" Hatimaye wakasalimiana na Mzee Mnyoka akaaga na kuondoka kwa haraka, huku Mzee Mkude akipigwa na mshangao! Maskini Mzee Mnyoka alijilaumu kuona mpaka Sasa mwizi akiwa bado hajakamatwa, lakini ilimuuma Sana kuona huyo mwizi Ni mwenyekiti wake wa Kijiji,
Mzee Mnyoka alichoka!
****
Mzee Mnyoka alikuwa na kawaida ya kuchelewa kurudi nyumbani ndio, lakini siku za jumapili na mwisho wa mwezi Mzee Mnyoka alikua anawahi Sana! Na pengine siku nyingine hakutoka kabisa!
Siku hiyo jumapili baada ya siku tatu kupita tangu wizi utokee Mzee Mnyoka akiwa nyumbani kwake akisuka mkeka alipokea wageni wa kustaajibisha.
Polisi! Ndio, polisi walifika na kumueleza Mzee Mnyoka kuwa yupo chini ya ulinzi kwa tuhuma za kuiba Ng'ombe dume wa Mzee Pembe!
Mzee Mnyoka alikataa Kata Kata! Lakini polisi wakambeba msobe msobe na kwenda kumuweka lupango, huku wakimtolea maneno mazito kuwa atakoma, na huo ndio mwisho wa wezi kama yeye.
**********
Mzee Mnyoka alipiga kelele huku machozi yakimtoka "Jamani mnanionea! Mnanionea! Sijaiba Mimi! Sijaiba Mimi!" Wale polisi waliendelea kucheka na kupiga stori zao huku wakimuamuru Mzee Mnyoka kuacha makelele.
"We Mzee, hakuna mtu aliletwa hapa akakubali kosa kirahisi, wewe tuachie makelele yako hapa sio nyumbani kwako" Polisi mmoja aliongea huku wenzake wakimuunga mkono.
Nyumbani kwa Mzee mnyoka, mkewe hakupata usingizi, pamoja na tabia yake ya kuchelewa kurudi lakini Mzee Mnyoka aliishi vizuri na majirani, jioni Ile nyumbani kwa Mzee Mnyoka mtaa mzima ulihamia kwake, mkewe alikuwa amesharudia kuhadithia jinsi mumewe "alivyodakwa" na polisi, na Sasa mama Alli alikua amechukua jukumu la kusimulia kuhusu kukamatwa kwa Mzee Mnyoka.
"jamani Mzee Mnyoka sio mwizi, sote tunajua, haiwezekan wamchukue, twendeni huko polisi" Waliongea majirani. Hata hivyo mpaka saa 2 usiku bado hawakufikia muafaka na hatimaye usiku , mwenyekiti wa kitongoji ambaye ni kijana tu alifika Nyumbani kwa Mzee Mnyoka kutoa taarifa kuwa Mzee Mnyoka anaweza kupata dhamana kesho yake jumatatu na hivyo wasijisumbue kwenda usiku kule polisi na badala yake kesho waende kumuona!
Hakika Mzee Mnyoka Hakupata tabu peke yake Bali mkewe, na mtaa mzima walipata tabu. Kwanza Nani alienda kumshtaki Mzee Mnyoka? Mbona Mzee Mnyoka hajawahi kuiba hata kuku pale mtaani?
********
Mzee Mnyoka alilala mahabusu huku akiwa anaelewa kwanini Yuko pale! "Mkude mwanaharamu wewe labda nisitoke hapa !" Mzee Mnyoka alipaza sauti akiwa lupango...."Mkude , mshenzi Sana wewe, uibe Ng'ombe mwenyewe halafu unisingizie Mimi? Nikitoka hapa nakuua mshenzi wewe!" Mzee Mnyoka alikuwa anaropoka tu, na kupelekea polisi kuja kumtuliza ...
"We Mzee ukiendelea na hayo makelele yako tutashindwa kukuvumilia" alisema Afande mmoja aliyeitwa Paul. Mzee Mnyoka Hakupata usingizi kwani selo ilijaa harufu Kali ya kinyesi, na giza Totoro, huku mbu wakiwa wanapiga kelele za furaha, Mzee Mnyoka nguvu zilimuishia
*******
Mzee Mnyoka alishindwa kusimama na akajikuta anakaa chini na ndipo Sasa Mzee Mnyoka akapigwa na butwaa, Naam macho yake Sasa yalianza kuzoea giza la pale ndani baada ya kuwa alitoka kwenye mwanga mkali, Na ndipo Mzee Mnyoka akang'amua kuwa hakua peke yake pale ndani!
Ndio,
Mahabusu Tena mwishoni mwa wiki haiwezekan ikawa tupu! Kwa haraka haraka walikuwa Saba mle ndani, huku wa Nne wakiwa wamesimama na watatu wamelala! Mzee Mnyoka alijikuta akicheka!
Ndio alicheka kicheko Cha uchungu! Inawezekaje mtu apate usingizi katika chumba kile ambacho Mzee Mnyoka hakuelewa Kama anatakiwa kuziba pua au mdomo? Inawezekaje mtu apate usingizi katikati ya sherehe za mbu?
Mzee Mnyoka Sasa alitambua kuwa bila shaka wale waliolala, Ni watu wa Aina mbili, mosi,
Wameamua kusamehe na kujisamehe wao wenyewe na kusahau shida zote na kuamua kulala fofofo, ama Ni watu waliozoea Yale mazingira pale ndani! Lakini kwa namna yoyote Ile Mzee Mnyoka asingepata usingizi,
Kwanza alimkumbuka mke wake , mama Monica, pamoja na watoto wake,
Lakini pia Mzee Mnyoka aliwaza kesi iliyoko mbele yake, Kesi ambayo alikua hajui anaanzaje kujitetea. Ni kweli hakufanya, Ni kweli alimjua mhusika, lakini Nani atamuamini? Mzee Mnyoka machozi yalimtiririka.
************
Asubuh na mapema kituo Cha polisi mama Monica na majirani wengine walifika kumjulia Hali Mzee Mnyoka,
Polisi alienda kumtoa Mzee Mnyoka. Ambaye alijikaza huku akijilazimisha kutabasamu baada ya Kumuona mkewe. Alipata wasaa wa kuongea na mkewe na akapewa masharti ya dhamana, hivyo mkewe akishirikiana na majirani walienda "kuchakarika" kuhakikisha Mzee Mnyoka anapata dhamana, siku ile Ile ya jumatatu!
Baada ya mipango yote kukamilika ikiwemo kuuza mbuzi wake wawili na kuweka rehani cherehani yake , mama Monica alifanikiwa kupata dhamana ya mumewe saa 11 jioni! Na safari ya kurudi kijijini ikaanza!
Inaendelea