Hadithi fupi ya mapenzi

Reshmail hayupo? mbona jana alikuwa hapa ofisin?" mwalimu wa zamu alikuwa anamuuliza mwanafunzi aliyeagizwa kumuita Reshmail baada ya mama yake kuwa amefika,"Hata mi sijui mwalimu"

"Hapana sio jambo la kawaida reshmail kutokuwa mazingira ya shule tena jumatatu! hebu mwambie time-keeper agonge kengere mara moja" aliamrisha mwalimu.

******

Hakuwa hata na chembe ya utani Reshmail wa watu,majira ya saa moja asubuhi tayari alikuwa kwenye gari la KIMOTCO ninalotoka Arusha kwenda Musoma kwa kupitia Mugumu Serengeti,kitu kinachoitwa hofu moyoni hakikuwepo hata kwa mbali,ndani ya kipochi chake kidogo alikuwa na pesa taslimu za kitanzania shiling laki mbili zikisindikizwa na kadi ya viza ya CRDB iliyokuwa na uwezo wa kutoa shiling laki tano kwa siku mara nne yaani milioni mbili zilikuwa zimehfadhiwa katika acount yake ya akiba.Mamaa wa shughuli (Eveline) alikuwa pembeni ya Reshmail,hofu kwake haikuwepo wala hakuiwaza tayari alikuwa mzoefu wa mambo hayo."Eveline yani akili ndo inakuja sasa hivi eti kwa nini tusingepanda ndege dah! gari linaenda taratibu hilo jaman" alilalama Reshmail kwa wananch wa kawaida waliomsikia walidhani ni mashauzi na majigambo ya watoto wa kike

"Mh? shoga ulivyokuwa na hamu ungekumbuka hayo,tutafika weye acha papara"

Gari lilizidi kuchanja mbuga za ngorongoro kwa kasi ya kawaida hadi majira ya saa saba tairi chakavu za gari hili zilikuwa tayari kwenye mbuga za Serengeti,Resh alikuwa macho anatazama safari inavyokwenda huku akihesabu masaa yanavyokatika kwa kasi huku mwisho wa safari ukiwa haufiki.Eve yeye alikuwa ameuchapa usingzi huku akiwa amejifunika uso wake kwa kofia yake nyeusi ambayo vumbi ilikuwa imeibadili rangi yake na kuwa ya ugoro.(Brown).

"Eve Eve Eve,amka uone wewe" Resh alikuwa anamwamsha kwa fujo."Angalia hii sms imeingia sasa hv" "Resh mazako kaja unatafutwa uko wap?" jasho jembamba likaanza kumtoka Resh lakin Eve hakushtuka sana.Walikuwa wametumiwa ujumbe mfupi na mmoja wa viranja."Eve tumeisha tumeisha"


* * * * * * * *


Ulikuwa mshikemshke wa ghafla pale shuleni mwalimu aliamuru kila mmoja aje mstarini hata kama ni mgonjwa,viranja walitii amri na kuita wanafunzi wote kwa haraka hakuna hata mwanafunzi mmoja aliyebaki ndani ya bweni.

Wakiwa hawajui nini kinachoendelea mwalimu wa zamu aliyeitwa Mwl.Chipeta alikuwa mbele ya wanafunzi waliokuwa kimya kumsikiliza yeye.”Kabla sijatoa tangazo hili,ni nani anatambua mwanafunzi ambaye hayupo eneo hili? (Kimya)

"Nani anaumwa na amepewa ruhusa?" (Kimya)

"Kwa hyo wote mpo?" (Ndiooo)

"Haya mchepuo wa H.G.E wote pita mbele" aliamuru mwalimu Chipeta na kwa haraka wakaanza kujongea mbele."Mamaaaaa," ghafla kelele ilisikika kuna mwanafunzi aliyekuwa mgonjwa alikuwa ameanguka chini kwa sababu ya kizunguzungu.Ustaarabu ukatoweka pale ghafla kila mwanafunzi akawa anasema lake,mara hivi mara vile. Hata mwalimu Chipeta alitimua mbio kuelekea kwenye tukio.

Ni wakat huohuo Joyce ambaye alikuwa kiranja alipata mwanya wa kutuma ujumbe kwa Reshmail kumpa taarifa.

*****

Roho ilikuwa inamdunda Reshmail kwa kasi sana,aliamin kila kitu kitakuwa wazi na atafukuzwa shule,"Eve watanielewaje wazazi mie mh! nimerokoroga" alijisemea Reshmail.

"Upo na steringi lazima tushinde haka kavita kadogo" Eve alimpa moyo wa ujasiri Resh,"Naomba hiyo simu si ina salio kidogo"

"Imo elfu tatu"Alijibu huku akimpa simu Eve.

"Sihitaji zote hizo natumia shiling 60 tu hapa"Alijibu kwa jeuri Eve huku akionekana kujiamini zaidi.

"Sasa hyo 60 itafanya nini shogangu au umesema elfu sitini?"Alitania Resh na wote wakajikuta wanacheka.

"Dakika tano nyingi majibu mazuri yatakuja,chukua simu yako ikiingia meseji uisome mi nalala bibie tuliza roho yako hii sio movie ya kihindi eti stering anauwawa,hili picha la kichina stering anachomwa kisu bado anapona" alimaliza Eve na kushusha kofia yake ikafunika macho.

Ni kama alivyosema dakika tano zilikuwa nyingi sana ujumbe kujibiwa

"Na ufanye kweli mi narekebisha mambo nyie tanueni kwa raha zenu na pia kuhusu yule wa H.G.L vipi?" ulisomeka ujumbe."Mungu wangu amakweli Eve steringi jamani yaani kirahisi hvyo" alijisemea Resh kwa sauti ya chini akidhani Eve amelala tayari "Futa sms ya huyo mjnga nitamalizana nae" kwa saut ya kivivu Eve alimwambia Resh.

****

Ndege ya Precion Air ilikuwa inaondoka kutoka Musoma kwenda Dar-es-salaam kupitia Mwanza majira ya saa kumi na moja wakati basi la KIMOTCO lilifika saa kumi na nusu jioni,Resh aliona akipanda gari anaweza kuchelewa kwa Adam Mwanza japo hata umbali wa Musoma kwenda Mwanza hakuufahamu."Resh ndege ya wapi tunapata sasa hv jaman" Eve alimuuliza Resh wakiwa ndani ya 'Teksi’ kutokea stendi kuu ya Musoma maeneo ya Bweri."Tunajaribu steringi wangu"

"Haya!! utamu na uchungu wa mapenzi mwachie aliyeyabeba" alitoa fumbo Eveline.

"Dereva dereva zuia kidogo tafadhali" ghafla Resh alimwomba dreva naye bila hiana akazikanyaga breki bila kuuliza kulikoni. Mbio mbio Resh akashuka akaanza kutimua mbio kurudi nyuma huku akiwa peku viatu ameacha garini Eve,Dereva na wananchi wengine wakabaki kumshangaa.

Mwalimu Chipeta aliongoza zoezi zima la kumshughulikia mwanafunzi aliyeanguka pale mstarini,shule ya Arusha international ilisifika sana kwa kujali afya za wanafunzi hivyo tukio lile lilisababisha Mwalimu Chipeta kumsahau kabisa Bi.Gaudencia mama yake Reshmail na kwenda kushughulika ipasavyo kwenye lile tukio,aliyekuwa ameanguka alikuwa Naomi Holela mwanafunzi aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kifua na pale kilikuwa kimembana hasa kutokana na baridi iliyokuwepo nje. Gari ya shule ilifika haraka Mwalimu Chipeta na viranja wawili pamoja na 'matron' walimsindikiza Naomi hospitali. Akiwa ndani gari Mwalimu Chipeta alisikia simu yake ikitoa mlio wa kupokea ujumbe mwanzoni alipuuzia kutokana na ubize uliokuwa ukimkabili lakini punde alitoa simu yake na kufungua ujumbe ulioingia

"Niaje ticha mi Wa ukweli nipo na Resh mbali kimtindo kama vipi rekebisha mambo huko mi nikija nakuletea geto yule Amina wa H.K.L,niandalie tu mapene yangu" uso wake ulisahau matatizo yote yaliyokuwa mbele yake,ni muda mrefu sasa tangu Mwalimu Chipeta muhitimu wa shahada ya elimu ya fasihi andishi katika chuo kikuu cha Dodoma alikuwa amemfukuzia binti mrembo wa kawaida tu Amina bila mafanikio tegemeo lake alikuwa ni Eve au Wa ukweli kama walivyomzoea,bila kupoteza muda Chipeta alifungua sehemu ya ku'forwad' meseji na akaituma kwa Mwalimu.Madege ambaye wote lao lilikuwa moja,alikuwa ni mwalimu Madege aliyeijibu ule ujumbe na kuulizia kuhusu yeye na mpango wa kumpata binti wa H.G.L.

"Samahani wewe ndio mama yake na Reshmail "Mwalimu Madege aliuliza baada ya Bi. Gaude kuingia katika ofisi ya makamu mwalimu wa zamu .

"Ndio ni mimi baba"

"Kwanza samahan sana kwa usumbufu uliojitokeza"

"Usijali na mimi niwape pole kwa matatizo yaliyojitokeza hapa"

"Tunashukuru ndio mambo ya shule haya,eeh! mama nimepokea ujumbe sasa hivi kwamba mwanao yupo katika mbuga za Serengeti ambapo wanafunzi watano waliofanya vizuri walipelekwa kufanya utalii wa siku tano" alidanganya mwalimu Madege.

"Jaman huyu mtoto mbona hakuniambia?... baba yake atafurahi sana akisikia maendeleo ya mwanae"mama Resh alijieleza kwa furaha iliyozidi wasiwasi aliokuwa nao.

"Tuliwashtukiza hawakuwa na taarifa hata wao wameshangaa mno" aliendelea kupanga maneno huku akichorachora mezani kwa kutumia karamu isiyokuwa na wino.

Moyo wa mama Reshmail uliridhika japo mwili ulikuwa na kinyongo kwa kukosa haki yake. Ilimbidi siku hiyo hiyo afunge safari kurudi jijini Dar na zawadi alizokuwa amemletea mwanae zikiwa mikononi mwake.


* * * * * *


A.T.M ya N.B.C aliyoiona maeneo ya Nyasho ilimkumbusha kuwa kadi yake ni 'VISA' inafanya kazi mashine ya A.T.M ya benki yoyote bila kujali macho ya watu alitimua mbio pekupeku hadi kwenye mashine ambapo kwa bahati nzuri hapakuwa na foleni na mtandao ulikuwepo "You can withdraw up to 1000000 with your A.T.M card daily N.B.C WE CARE" kijitangazo kwenye kioo cha mashne kiliibua tabasamu la Reshmail,na bila ajizi akabonyeza chaguo la kutoa laki tano kwa mikupuo miwili na kutimiza kiasi cha milioni moja, kisha kwa mwendo wa mbio kama alivyoingia akatoka akisindikizwa na miluzi ya wauza mitumba wa Nyasho ambayo kwake haikuwa na madhara hata chembe

"Samahani safari yenu imeahirishwa tafadhali hadi kesho asubuhi!" sauti nyororo ya mwanadada wa mapokezi aliyehusika na masuala ya Booking aliwaeleza mwanaume mmoja aliyekuwa na mpenzi wake wakitegemea kusafiri muda mfupi ujao kwenda Mwanza.
Sura zao zilizokuwa na furaha zililegea na kuwa kama watakavyokuwa pindi wakipata wajukuu,"Haiwezekani huu ni upumbavu tena ujinga ujinga ujinga,yani safari yangu inahairishwa ghafla kama vile safari za baiskeli,hapana sipo tayari nas...."

"shhhhh!!" kwa ishara ya kidole kimoja kuziba mdomo alinyamazishwa yule baba aliyetaka kuugeuza ukumbi ule uwanja wa mapambano na matusi. Kwa ishara nyingine yule dada akamwita akasogea pale alipo akamnon'goneza "Unawaona wale wasichana wawili,mmoja kimada wa mtoto wa raisi mwingne mtoto wa kamanda wa jeshi ni simu kutoka ikulu,kwa usalama wako acha kelele" alimwambia huku akimwelekezea walipo Resh na Eve. Bila kuhoji huku uoga ukimtawala hadhi yake ikashuka haraka haraka akamvuta mkewe wakaondoka wakawapisha kwa mbali Resh na Eve kama vile wanatema cheche za moto.
* * * * *
Ni kweli nafasi zilikuwa zimejaa lakini pesa iliongea nafasi ya mtu mwingine wakapewa wao tena harakaharaka,huku mtendaji wa jambo hilo akiweka shilingi laki mbili na nusu kibindoni. Huku Resh na Eve wakipata nafasi katika ndege ya Precision Air kiulaini,kwa mara ya kwanza Eve anapanda ndege "Mh! ushoga nao raha wakati mwingine” alijisemea wakati muhudumu wa ndani ya ndege akitoa maelekezo madogomadogo.
Ilikuwa kama safari ya kutoka Kimara Dar kwenda Mbagala,tayari walikuwa jiji la Mwanza

"Eve rushwa tamu wewe,naamini haitaisha ona sasa tupo Mwanza tayari" Resh alimwambia Eve wakati wanasafisha macho yao wajue nini cha kufanya baada ya kushuka kutoka kwenye ndege.
"Hoteli yenu ni nzuri?" Eve alimuuliza muhusika aliyekuwa ndani ya kigari kidogo kilichoandikwa Millenium Hotels kilichokuwa hapo kwa lengo la kutafuta wateja wanaotua na ndege uwanjani hapo,"Ni nzuri sana hautajuta kuwa pale.”

"Mh! haya,Resh twende giza linaingia" Eve alimwita Resh wakajitoma ndani ya gari na safari ikaanza.
"Darling umetoka kwenye michezo tayari pole mpenzi" ulikuwa ujumbe mfupi kutoka kwa Adam kuja kwa Resh,tabasamu pana likameza mdomo wake looh! lilikuwa tabasamu lililoelezea furaha ya moyo.
Adam alituma ujumbe huo akijua Resh yupo shuleni tena ilikuwa siku ya michezo ambayo Resh alipenda kushiriki hasahasa mpira wa kikapu.
"Mamaaaaa!!"Resh alipiga kelele ghafla gari ikayumba huku na huko,dereva akajaribu kwa uwezo wake wote kuirudisha barabarani "Paaaa!!" mlio mkubwa ukasikika.

*******************

Adam alipokea ujumbe kutoka kwa Reshmail akiwa maeneo ya kijiweni barabara ya lami kuelekea chuo kikuu cha mtakatifu Augustino,kupitia shule ya wasichana ya Ngaza.Adam alikuwa pamoja na rafiki yake (Huha) katika pikipiki ya rafiki yao aliyekuwa amewaazimisha wazungukiezungukie maeneo.

"Huha hebu endesha twende hapo Nyegezi kona kuna mtu nataka kuonana naye mara moja" Adam alimwomba Huha.
"Tayari Halima ametuma meseji mwambie hatuna mafuta atufate na gari yake bwana" Alitania Huha huku akianza kuiondoa pikipiki taratibu

"Ungejua hata usingesema wewe twende ukajionee maajabu ya mwaka" alijibu Adamu huku pikipiki ikizidi kushika kasi.
Ndani ya dakika tano tayari walikuwa Nyegezi kona ambapo Huha alipaki pembezoni kidogo na barabara iendayo stendi kuu ya Nyegezi jijini Mwanza,Adam alielekea dukani kununua vocha,na Huha akasogea pembeni kidogo aweze kuvuta sigara yake.
 
Dereva akiwa mwingi wa mawazo yake binafsi yasiyomuhusu Reshmail wala Eve na hata kama yangekuwa yanawahusu ule haukuwa muda muafaka wa kuwaambia.Macho ya Reshmail yalikuwa yamekutana na bango kubwa lililoandikwa "KARIBU CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AUGUSTINO" kwa hamu kubwa aliyokuwa nayo ya kumwona Adam ambaye alikuwa pia mwanafunzi ndani ya chuo hicho ndio sababu kuu ya kujikuta akipiga kelele kwa nguvu hali iliyomshtua dereva kutoka katika mawazo mazito na kujikuta akiyumbisha gari huku na huko hadi ilipokutana na pikipiki iliyokuwa imepakiwa pembezoni mwa barabara na kuirusha umbali ambao si wa kutisha sana,iligeuka vurumai madereva wa teksi na bodaboda za pikipiki walikuwa wakali sana hawakutaka kusikia la mtu,wengine hasira za kukosa abiria tangu waingie kijiweni asubuhi walizihamishia katika tukio hilo. Usingekuwa upole wa yule dereva basi mawe waliyobeba wananchi yangeigeuza ile gari kuwa mkweche. Eveline alitelemka garini kwenda kumsaidia dereva kujitetea lakini Reshmail uoga ulimtawala akawa amejibana kwenye viti vya nyuma vya ile gari huku akitetemeka. "Mh! Adam hawezi kukosa mwenyeji maeneo haya ngoja nijaribu kumpigia,ah! hii safari imetawaliwa na mikosi dah!" aliwaza Resh huku akichukua simu yake kutoka katika kipochi chake.
Lakini kelele zilizokuwa pale aliamini hawezi kusikilizana vizuri na upande wa pili,taratibu huku akitetemeka alifungua mlango akashuka na kuanza kutembea kuelekea pahali ambapo kidogo pametulia. Zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wenye hasira eneo lile wakageuza vichwa vyao kuangalia kazi ya Mungu ilivyotendeka vyema katika mwili wa Reshmail,badala ya kumpigia kelele dereva,miluzi mikali ikiongozwa na dereva mkongwe wa teksi eneo lile ndugu Sanya Bonda ikahamia kwa Reshmail,Resh akajifanya kama hasikii vile "Ilikuwa haki ya dereva kupotea njia jamani" Bonda alisema kwa sauti ya juu na kugeuza hasira za watu kuwa vicheko. Resh taratibu akaufikia mti mdogo mbali na eneo la tukio akabonyeza namba za Adam. Simu iliita muda mrefu bila kupokelewa. Alipopiga mara ya pili simu ilipokelewa."Helow Resh subiri nisogee pembeni nakupigia kuna tatizo limenipata" alijibiwa na Adam katika simu.
"Hata mi....." kabla hajamalizia kauli yake Reshmail simu ilikatwa akiwa bado anaduwaa kama dakika mbili pembeni yake alizengea kijana mmoja ambaye Resh hakutaka hata kumwangalia machoni,alijua ni walewale waliokuwa wakipiga miluzi na kumwita majina waliyotaka. Resh taratibu akajisogeza pemben."Vipi dada mbona wanikimbia au mi nanuka halafu we mrembo haya basi umebarikiwa sana najua unataka kusifiwa" aliongea yule kijana lakini Resh hakujibu.Simu yake ya mkononi iliyokuwa katika mfumo wa kimya(Silence mode) ilikuwa inatoa mwanga kuashiria aidha kuna ujumbe umeingia au kuna simu inaingia,lakini kwa jinsi alivyoandamwa na yule kaka kwa maneno hata hakuweza kugundua.
Baada ya dakika kadhaa akaondoka yule kaka ndipo kuangalia simu akagundua ilikuwa imeita mpaka imekata na hakuwa mwingine bali ni Adam alikuwa amepiga,harakaharaka akapiga tena. Ulikuwa mshangao wa hali ya juu sana Reshmail hakuamini alipomwona yule kijana aliyekuwa ametokea pale dakika chache zilizopita kuelekea kwenye zile vurugu ndio anapokea simu."Resh mbona nimekupigia hupokei mamaa" alimshuhudia yule kaka akiongea kwenye simu huku akirejea lile eneo kukwepa kelele,kama ilivyo kwa mtu aliyenaswa na umeme Reshmail alikuwa ametulia tuli na simu sikioni huku yule kaka akizidi kulikaribia eneo lile “Reshmail mbona huongei!!” aliendelea kuuliza bila kupata majibu."Adam" alijitutumua Resh na kutamka akiwa jirani naye kabisa,bila kujua yule kijana akaangusha simu yake hakuamini msichana aliyetoka kuongea nae dakika kadhaa ndio Reshmail wa Arusha.
***
Vurumai lilisawazishwa haraka sana Adam na Huha ndio waliokuwa wamiliki wa ile pikipiki iliyogongwa na gari waliyokuwemo akina Reshmail."Jamani huyu hapa ni dada yangu,ndio alikuwa amenipigia simu tuonane hapa naomba haya mtuachie sisi" Adam aliuambia umati ule ambao hasira zao zilikuwa zimeanza kupoa na haraka walimwelewa wakaacha kumzonga dereva.Reshmail bila kupoteza muda akamwongoza Adam wakaingia garini akampa pesa taslimu shilingi laki tatu kwa ajiri ya matengenezo ya ile pikipiki naye Adam akamkabidhi Huha kisha akajumuika na Eve pamoja na Reshmail katika gari,huku Reshmail akiwaacha watu hoi kwa uzuri wake wa asilia ambao hata Adam alikuwa amechachawa nao na kukubaliana na ukweli kwamba picha zilizotumwa zilikuwa za Resh kweli.

***
Bi Gaudensia alifika Dar-es-salaam majira ya saa tatu usiku,bado alikuwa hajaridhika kumaliza siku yake bila kuongea na mwanae,hivyo punde tu baada ya kuingia chumbani mwake aliamua kujaribu kupiga namba za simu za Reshmail ambazo zilikuwa hazipatikani siku nzima. Furaha aliyoipata ilikuwa haisimuliki,pale simu ilipoita upande wa pili"Mh! kalala nini huyu?" alijiuliza simu ilivyoita kwa muda mrefu bila kupokelewa,lakini mara ikapokelewa
"Helow! samahani Reshmail amelala" sauti ya kiume ilijibu baada ya kupokea kisha simu ikakatwa na kuzimwa. Mama Resh hakuamini kuwa amesikia sauti ya kiume katika simu ya mwanae alidhani amekosea namba lakini alipohakikisha zilikuwa zenyewe,wivu mkali ukamshika,akajaribu kupiga mara nyingi lakini bado hali ilikuwa ileile simu ilikuwa imezimwa usingizi ulipaa,alitokwa na jasho,hisia mbaya zikamvuruga na kufanya kichwa chake kiume sana,mama huyu alikuwa amejisahau kabisa kuwa Reshmail ni mwanae wa kumzaa, alizurura kama mtu anayetafuta kitu ambacho amesahau alipokiweka pale chumbani,alitamani kupiga kelele lakini aliamini hazitasaidia kitu.
***
Reshmail akiwa usingizini Adam pembeni yake,yeye(Resh) alikuwa hoi kwa uchovu wa safari na misukosuko yote waliyopitia,na alipomaliza kuoga tu na kupata chakula alisinzia,hata simu yake ilipoita hakuisikia hata kidogo na hata angeisikia asingeweza kunyanyuka kupokea "Resh ni kipetito anapiga" Adam alimuuliza Resh aliyekuwa hoi kitandani."Ah! ni rafiki yangu mwambie nimelala" alijibu kwa taabu akiwa hata hajui anachokiongea. Naye Adam bila kugundua kwamba Resh hajui anachokisema na ile namba ni ya mama yake Resh alipokea na kuzungumza
Kitendo cha Adam kumkuta Reshmail akiwa bado ni bikra kilimzuzua sana,mapenzi yake kwa Halima yalipungua sana na kuisha kabisa hatimaye. Siku tatu mfululizo walizotumia pale Millenium Hotel zilitosha kuvunjilia mbali penzi la Adam na Halima na kujenga penzi imara kati ya Adam na Reshmail.
"Mwezi wa pili uje ujitambulishe nyumbani Adam yaani siwezi kusubiri kwa kweli nakupenda Adam wewe ni mwanaume wangu wa kwanza na ninakuahidi nitajitunza kwa ajili yako" Reshmail alikuwa anamsisitiza Adam siku alipokuwa amewasindikiza uwanja wa ndege tayari kwa wawili hawa kurejea Arusha shuleni.
"Mama anapiga! Eve" Resh alimwambia Eve pale simu yake ilivyoita."He! usiniambie huyo ndio mama,sasa mbona ulikubali niongee nae usiku ule? aliduwaa Adam.
"Eti! uliongea nae? Yesu wangu!" alishtuka Resh lakini Eve akamshauri azime simu kwanza mengineyo watajua mbele kwa mbele naye Resh akatii amri hiyo haraka akaizima simu bila kupokea Resh kwa kiasi kukuwa alikuwa amemzoea na kumwamini Eve.
Adam,Resh,na Eve waliagana kama watu waliofahamia na kukaa pamoja siku nyingi sana,Resh alimkumbatia Resh alimkumbatia Adam kwa muda mrefu hadi Eve alipowatenganisha na kuambiana Kwaheri.
***
Ilikuwa imebaki miezi minne wafanye mtihani wa kumaliza kidato cha tano,Resh akiwa amekolea katika penzi la Adam na kusahau kuhusu
Mama yake ambaye alikuwa amezuiwa na mwanaye huyo kwenda pale shuleni kumsalimia kwa madai kwamba yeye(Reshmail) anataka ajikite zaidi katika masomo. Reshmail kwa maksudi akabadilisha namba yake ya simu ili mama yake asiweze kumpata mara kwa mara badala yake muda mwingi akawa anawasiliana na Adam.
Mwezi wa pili ilikuwa ni likizo ya mwezi mzima kwa wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita na pia wakati huohuo wanafunzi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino huwa katika mapumziko mafupi baada ya kumaliza muhula(Semister) ya kwanza. Kwa Reshmail ulikuwa wakati muafaka wa kumtambulisha Adam kwa wazazi wake jambo ambalo aliamini lingesaidia kupunguza makali ya mama yake. Tangu akiwa mtoto kamwe hakuwahi kuwakwaza wazazi wake kwa sababu ya wanaume hata siku moja hivyo alitegemea hawatampinga.
Ilikuwa siku ya furaha kubwa sana kwa Bi. Gaudencia na familia yote kwa ujumla kumwona tena Reshmail nyumbani baada ya miezi mingi tena akiwa mwingi wa furaha. Lakini tofauti na mama yake alivyofikiria kwamba mwanae huyo anafurahia kurudi katika ulimwengu wao wa mapenzi haramu yeye(Reshmail) alikuwa anafuraha ya kumtambulisha Adam ndani ya siku chache.
Kwa kujua wazi kabisa mama yake atachukizwa na maamuzi yake hayo,Reshmail aliamua kulifikisha hilo mbele ya Mzee. Manyama ambaye ni baba yake.
"Kwa sababu ni uchumba tu na hakupeleki popote hamna tatizo hata kidogo,mlete tu mwanangu mlete una maamuzi mazuri sana sio kama wasichana wengine wanafanya upuuzi kimyakimya mambo yanapokuwa mabaya ndio wanasema" alijibu mzee.Manyama huku akimshika mwanae huyo shavuni,Resh akatabasamu na kumkumbatia baba yake "I love you dad(Nakupenda baba)" Resh akamwambia kwa furaha tele mzazi wake huyo,huku moyoni akijiaminisha kwamba hapatakuwa na kikwazo tena kwa mama yake kwani baba ndiye kichwa cha familia.
Baada ya siku tano Adam aliwasili ndani ya kasri la mbunge huyu.Alikuwa anaogopa na hakuamini kama angepokelewa na kama angepokelewa alijua yatakuwa mapokezi mabaya sana kwani katika simulizi mbalimbali anazozisikia kwa watu zilimwonyesha kwamba ni vigumu sana kwa wazazi kumwelewa mtoto wa kike linapokuja suala la kumtambulisha mwanaume kama mchumba wake.
"Da Rosemary nina hofu mie" Adam alimwambia dada yake kipenzi waliyekuwa wameongozana naye "Acha uoga bro mbona hata sisi babu yetu alikuwa chifu? kwani chifu na mbunge nani zaidi" alitania Rosemary kumwondoa hofu kaka yake.Mapokezi waliyoyapata kutokea kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha Ubungo yaliwashangaza mno waliwakuta watu wa kuwapokea na kwenda nao kwenye gari mbili walizokuja nazo,waliwafikisha hadi getini ambapo kina dada wawili kwa heshima kabisa waliwaongoza hadi sehemu maalum iliyoandaliwa kwa ajili yao,japo usoni waliuficha mshangao wao lakini moyoni uliwajaa tele.Adam akiwa ndani ya suti nyeusi wanazotumia wanasheria katika shughuli zao na Rosemary aliyevaa suti pia walielekezwa wapi walipo wazazi wa Reshmail wakaenda kutoa salamu zao,ilikuwa ni hafla kubwa sana ndugu,jamaa na marafiki wapatao miamoja walikuwa wamealikwa na mheshimiwa huyu. Ilikuwa kama harusi kwa asiyejua lakini ulikuwa utambulisho tu.
Bwana na bibi Manyama walipendeza kwelikweli na walikuwa na kila haki ya kuitwa wakwe na Adam. Furaha ya Bi. Gaudencia ilificha chuki aliyokuwa nayo moyoni dhidi ya Adam kwa kumchukua mwanae ambaye ndio alikuwa anampa raha zote za dunia.
Hadi hafla inafikia tamati majira ya saa mbili usiku kila mtu alikuwa amepata furaha kubwa sana,wabunge na madiwani ambao ni marafiki wa karibu wa Manyama walitoa zawadi nyingi kwa wawili hawa huku babu yake Reshmail akitoa mawaidha yenye maana kubwa sana katika maisha waliyotarajia kuyaishi Reshmail na Adam siku za usoni.
Mzee Manyama kwa ombi la mwanae aliwasiliana na wazazi wa Adam kuwa muda wa mapumziko ya siku tano alizobakiza Adam amalizie katika familia yake,hapakuwa na kinyongo wala kipingamizi chochote walikubali kwa moyo mmoja na Adam akaendelea kuishi pale huku dada yake akirejea Mwanza kwa usafiri wa ndege ambao gharama zote zilikuwa juu ya mheshimiwa Manyama. Kila alipowasiliana na wazazi wake Adam hakusita kuelezea upendo wa kipekee anaoupata kutoka familia ya Reshmail hata wao walifarijika sana.
***
Ilikuwa jumapili moja tulivu sana baada ya kutoka kanisani familia yote akiwemo pia Adam,baba yake Reshmail aliongozana na mwanae kwenda mjini kwa lengo kuu la kuonana na walimu mbalimbali wa masomo ya ziada(Tution) watakaompendeza Reshmail basi waweze kumfundishia nyumbani.
Huku nyuma alibaki Adam pamoja na mkwewe (Mama Reshmail) baada ya kupata kifungua kinywa Adam alimwaga mkwewe kuwa anaenda kuzungukazunguka bustanini "Tena nilitaka nikwambie leo unataka uondoke hata bustanini hujawahi kufika,afadhali nenda mwanangu" alijibu mama Reshmail.
Ulikuwa mpango kabambe uliosukwa na Bi. Gaudencia,kwa dhumuni kuu la kumwondolea mamlaka Adam ya kuwa na Reshmail. Kwa kuwatumia vijana kutoka katika ngome ya vigogo,ngome maalum iliyokuwa inatumiwa na watu wenye pesa zao kwa ajili ya kuwatenda vibaya watu wanaoonekana kuingilia mambo yao aidha kimapenzi au kibiashara.Alipoaga anaenda bustanini Gaudencia alitumia fursa hiyo kupiga simu kwa wanaume hao wa shoka ambao tayari alikiwa ameelewana nao bei.
"Ndani ya dakika tano tutakuwa hapo” ndio jibu lililotolewa upande wa pili
Bila kuongezea lolote Bi.Gaudencia alikata simu yake na kutoka nje.
"Babu kwa mama Veneranda si unapajua?" alitoa swali hlo Bi. Gaudencia kwenda kwa mlinzi wao wa getini.
"Ndio si yule mama anayesuka pale mbele"
”Hapo hapo haya haraka nenda kaniangalizie kama kuna foleni kubwa" aliamrisha Bi. Gaude na mlinzi akatii amri hiyo haraka haraka akaondoka katika lindo lake akaenda kutimiza amri ya bosi wake.
Baada ya dakika takribani kumi alirejea mlinzi yule "Yupo mmoja tu anamaliziwa" alileta taarifa hiyo kwa furaha.
"Haya mi ninatoka nimemwacha Adam ndani amelala akiamka mwambie nimetoka kidogo" alisema mama Reshmail huku akiondoka.
“sawa bosi nitamwambia”
Masaa mawili badae alirejea akiwa amesukwa tayari nywele zake,ni muda huohuo Reshmail na baba yake walikuwa wametoka mizungukoni,walimkuta Gaudencia anatokea ndani. "Babu Adam alivyoamka ameenda wapi? au bustanini?"Aliuliza Gaudencia na kuongezea "Maana nimegonga chumbani kwake kimya,hebu Reshmail ingia ukamwangalie ndani mwake humo huenda amelala bado" kwa mwendo wa maringo lakini harakaharaka Reshmail alijongea ndani.
"Babu unasema Adam hajatoka?" Resh aliuliza baada ya kurejea akiwa na hofu kidogo usoni.
"Hajatoka na mimi hapa sijatoka tangu mama alipoenda kusuka na kumwacha Adam amelala" alijieleza mlinzi yule jibu lililopokelewa kwa furaha na Bi.Gaudencia.
Jambo gumu zaidi kwa ambao hawakujua janja ya mama huyu ni kwamba simu ya Adam ilikuwa haipatikani hali hiyo ilileta wasiwasi sana,walisubiri huenda atarudi hadi jioni hali ilikuwa tete ndipo mzee Manyama alipoamua kupiga simu kituo cha polisi maeneo ya jirani kwa sababu alikuwa mbunge msako ulianza usiku huohuo.
Siku tatu zilipita bila taarifa yoyote kutoka katika kituo cha polisi,Reshmail alikuwa amepooza sana kupita maelezo mara kwa mara alimpigia baba yake simu na kuuliza kulikoni lakini jibu bado lilikuwa lilelile kuwa hajapatikana.
"Mama niache tafadhali,tena niache nasema upuuzi wako siutaki tena niache!" alifoka Reshmail pale mama yake alivyomkuta amekaa sebuleni na kujaribu kumpapasa huku akimpa pole ya kupotelewa na Adam wake ghafla.
"Mwanangu usiwe na hasira kiasi hicho polisi watafanikisha upelelezi na watamrejesha Adam akiwa mzima wa afya" alibembeleza Bi. Gaudencia lakini Reshmail hakujibu kitu akajiondokea akiwa ameuvuta mdomo wake sana.
Siku ya tano polisi waliopewa jukumu la kufanya upelelezi huo walirejea na taarifa yao huku wakiambatana na ushahidi. Zilikuwa nguo aliyokuwa amevaa Adam kwenda kanisani ikiwa na matundu sita ya risasi na ikiwa imetapakaa damu pote,suruali ilikuwa na matundu matatu ya risasi.
"Hapana hawezi kuwa Adam hata kidogo nasema hawezi kuwa yeye" alifoka Manyama huku akiwa wimawima mbele ya mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai jiji la Dar-es-salaam Chacha Boniphace au maarufu kama Chacha B.
"Mheshimiwa lakini huu ni upelelezi wa awali tunaendelea zaidi na zaidi tutazidi kutoa taarifa kadri tunavyopata majibu mapya" alijieleza kwa utulivu bila wasiwasi kabisa jambo ambalo kidogo lilirejesha amani ya Manyama japo hofu tayari ilishaukumba moyo wake kwamba huenda Adam ameuwawa tena kikatili.
Ilikuwa ni shughuli pevu kwa Reshmail kuamini kile ambacho alikuwa anaelezwa na baba yake kwamba Adam anadhaniwa kuuwawa kwa risasi nane kisha mwili wake hauonekani. Bi. Gaudencia tayari alikuwa anaangua kilio kikubwa hata kabla maelezo hayajaisha ikawa kazi kwa mumewe kumbembeleza.
"Mke wangu Adam hajafa ila inadhaniwa pia upelelezi bado unaendelea jamani,ukilia hivyo unakuaribisha msiba mama watoto sawa" alibembeleza mzee Manyama huku amemkumbatia mkewe.
"Baba haiwezekani baba haiwezekani nguo za Adam zipatikane katika hali hiyo halafu mnasema hajafa,jamani Adam wangu wamemuua" alipiga mayowe Reshmail ikamlazimu mzee Manyama kufanya kazi mara mbili jambo ambalo lilimtoa jasho mzee huyu.
"Reshmail mwanangu,tulia hiyo siyo taarifa rasmi jamani ni majibu ya awali mbona mnanifanyia hivyo au mnataka nipate presha nife?" alijieleza Manyama huku akijifuta jasho kwa kutumia shati lake. Reshmail mbio mbio akaondoka pale sebuleni akaanza kuzipanda ngazi kuelekea chumbani kwake huku akilia,mzee Manyama nae huyo nyuma yake.
"Reshmail mwanangu,njoo malkia wangu,njoo mwanangu" aliyazungumza hayo huku akimkimbiza kwa nyuma. Wakati huo Bi. Gaudencia tayari alikuwa amenyamaza kimya kabisa,akijaribu kupikicha
macho yake.Reshmail hakusimama hadi chumbani kwake akajifungia,baba yake alibembeleza mpaka akachoka hakupata jibu zaidi ya kilio cha kwikwi kutoka ndani.
"Baba Resh twende chumbani mume wangu,twende utakaa hapa hadi saa ngapi cha msingi tumwombe Mungu asije akajidhuru mwanetu" Gaudencia alimnyanyua mumewe wakajikongoja kuelekea chumbani kwao,Manyama akiwa amelegea kabisa.
Asubuhi ya siku iliyofuata naibu waziri wa ulinzi na usalama,alifika na msafara wake wa magari matano kwa mbunge Manyama kuja kutoa pole ya kutokewa tukio hilo lenye utata kwa mwenzao. Shughuli ngumu iliyokuwa mbele yao ni jinsi gani watawaeleza wazazi wake Adam ambao hadi dakika hiyo waliamini Adam yupo salama na mwenye furaha kwa mchumba wake Reshmail,Manyama alimuomba waziri ashughulikie hilo suala na bila kupoteza muda alinyanyua simu yake ya mkononi na kutoa taarifa hiyo kwa mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mwanza pamoja na mawasiliano anayoweza kumpata baba yake Adam. Ilikuwa vigumu sana kwa baba Adam kuelewa anachoelezwa lakini kwa kadri ya uwezo wake na taaluma yake mkuu huyo alifanikiwa kumwelewesha ambapo baba yake Adam aliondoka akiwa na matumaini kwamba ipo siku Adam atapatikana.
Nyumba nzima ya kina Adam ilipooza sana dada yake Adam (Rosemary) alikuwa analia muda wote kwa uchungu hakuamini kwamba siku ile pale uwanja wa ndege alivyosindikizwa na familia nzima ya mhe.Manyama ndio ilikuwa mara ya mwisho kumwona kaka yake kipenzi(Adam).
Uongozi wa polisi uliifikisha taarifa hiyo pale chuoni ambao pia walipokea kwa simanzi kubwa.
"MAUAJI YA KUTISHA", ndivyo mandishi meusi kabisa kwenye magazeti mbalimbali yalisomeka,hali hiyo ilithibitisha kabisa kuwa Adam hayuko hai tena. Picha yake iliyoambatanishwa na habari hizo akiwa na mtoto wa mbunge iliteka na kuumiza mioyo ya watu wengi hasahasa vijana."Tumempoteza mwanasheria" ndilo neno la pamoja walilosema wasomi wa chuo kikuu cha mtakatifu Augustino Mwanza katika misa ya pamoja kumwombea mema Adam kama yupo hai au kumtakia pumziko jema la milele kama tayari Mungu ameichukua roho yake,kila uso ulikuwa na simanzi kubwa ilikuwa kama tamthilia.
Reshmail alikuwa kama zezeta,hamwelewi mtu yeyote,roho yake ilimwambia kwamba mama yake mzazi anahusika kwa namna moja au nyingine katika tukio hili lililojaa utata. Lakini ataanzia wapi kumweleza baba yake,atajisikiaje mzee Manyama akigundua kwamba mke na mtoto wake walikuwa katika ndoa haramu ya siri ndani ya nyumba yake."Hapana sitaki kuongeza tatizo juu ya tatizo nitasubiri liwalo na liwe,kama Mungu alimpanga Adam awe wangu naapa sitaolewa na mwingine kamwe,lakini kama hakuwa halali yangu basi ataletwa mwanaume duniani kwa ajili yangu tena"Alijipa ujasiri wa hali ya juu Reshmail huku akijipigapiga kifuani."Nitarejea shule na nitasoma tena kwa bidii sana,sitamwaza mwanaume yeyote tena alikuwa Adam na atabaki kuwa Adam hadi Mungu aamue tena" aliendelea kujipa matumaini."Bibi yangu aliniambia maneno ya mdomo huumba halisi,na nina uhakika ninachokiongea kwa mdomo wangu Mungu ataniumbia" aliendelea kuongea huku machozi yakifumba macho yake na kitambaa alichokuwa anatumia kujifuta kilikuwa kimelowana tayari kwa wingi wa machozi alikuwa kama yatima vile,Resh alikuwa akifungasha baadhi ya mizigo yake tayari kwa kurejea shuleni tena,tangu tukio la Adam kupotea hakuna aliyetegemea hata siku moja Resh atawaza kurudi tena shuleni kwani waziwazi akili yake ilionekana kuathirika kwa kiasi kikubwa kwa kumpoteza Adam katika mazingira yasiyoeleweka.
"Baba kesho narejea shule si unajua tayari shule imefunguliwa?" Reshmail alimkurupua mzazi wake huyo kutoka alipokaa kwa mshangao
"Umesema nini malkia wangu!" alihoji Manyama huku akiwa wima
"Narejea shule kesho" kwa msisitizo na tabasamu alijibu Reshmail. Mzee Manyama hakuamini kwani alikuwa akiwaza ni namna gani atamshawishi mwanae aweze tena kurejea shuleni baada ya matatizo yote yaliyojitokeza kwa mchumba wake Adam ambaye hadi wakati huo bado mwili wake ulikuwa haujapatikana wala taarifa yoyote zaidi ya nguo zikiwa na matundu ya risasi na damu."asante sana mwanangu nakupenda sana" mzee Manyama aliongea kwa furaha huku akimkumbatia mwanae.
Tangu kupotea kwa Adam aliyehisiwa kuwa tayari amekufa kulipokelewa kwa hisia tofauti na wananchi huku asilimia kubwa ikiegemea upande wa imani potofu za kishirikina wakihusisha tukio hilo na utajiri alionao Mh. Manyama na uchaguzi uliokuwa mbele yake
 
Wamemtoa mwanangu kafara ili waongeze utajiri,nilimwambia Adam aoe msukuma mwenzake ona sasa,watoto wa siku hizi wabishi wanajifanya wanajua sana na elimu yao inawadanganya" mama yake Adam alikuwa analaani vikali mbele ya mume wake wakiwa ndani ya nyumba yao maeneo ya Igoma kwa 'one-way'
"Usiseme hivyo mama Adam kumbuka sisi ni wakristu,tumwachie Mungu yeye ndio atajua nini cha kufanya" Babaye Adam alimtuliza mkewe huku akimgongagonga mgongoni kwa kutumia kiganja cha mkono wake wa kuume.
Mawasiliano baina ya familia hizi mbili ya Adam jijini Mwanza na ya Reshmail jijini Dar-es-salaam yalikuwa yamekatika licha ya baba yake Adam (mzee Michael) kutangaza kuwa kutoka moyoni mwake amesamehe yote yaliyotokea na anaamini ni mipango ya Mungu lakini kinyongo kilionekana dhahiri kwa matendo,upendo wa zamani haukuwepo tena jambo hilo lilimfadhaisha sana mzee Manyama kiasi cha kukondeana na kukosa umakini katika utendaji wake wa kazi jambo lililoishusha sana heshima yake kama mbunge aliyekuwa anaheshimika sana kuanzia bungeni hadi jimboni kwake,wapinzani walitumia fursa hiyo kumchafua hasahasa na kweli uchafu huo ukakubalika kwa wananchi kwa ujumla Manyama hakuwa na lake tena pale,wananchi walimpuuzia sana tofauti na zamani na hata hiyo miaka miwili iliyobaki wananchi waliiona kama ni mingi sana kuwa na kiongozi wa aina yake.
Kuliko fedheha yote hiyo Mh. Manyama kwa hiari yake mwenyewe alipitisha kura ya maoni ya wananchi kuhusu imani waliyonayo kwake kama mbunge wao. Asilimia 70 ya waliopiga kura walidai hawana imani naye huku asilimia kumi na nne tu ndio wakidai bado wana imani naye na kura zilizobaki zikiharibika,rasmi Manyama akawa ametolewa bungeni na katika uchaguzi mdogo uliofanyika akachaguliwa mbunge kutoka chama cha upinzani na maisha yakaendelea huku Mh.Manyama akiendelea na biashara zake mikoani.
* **
Adam akiwa pale bustanini alivamiwa ghafla na wanaume wawili wa shoka wakiwa na bunduki,ishara ya kidole mdomoni ilimfanya atulie tuli kisha wakamwonyesha ishara kwamba awafuate alifanya kama walivyotaka hadi kwenye gari iliyokuwa imepaki pembeni kidogo ya nyumba yao Adam alishangazwa sana na ukimya uliokuwepo hakuwepo mlinzi wala mama mkwe wake.Safari yao ilikwenda mpaka Iringa gari iliyokuwa na vioo vyeusi 'tinted' ilimzuia Adam kujua ni wapi alipo,gari ilizimishwa ndani ya jumba kubwa sana ambapo alipelekwa kwenye chumba kikubwa tu,hofu kubwa ilimtawala hakujua kwa nini yuko pale,hakupigwa wala kupewa bughudha yoyote,hali hiyo ilzidi kumshangaza "au ndio wachuna ngozi" alijiuliza Adam kwa hofu tele.
Hayo ndio masharti ambayo mama Reshmail alitoa kwa vijana aliowapa tenda hiyo ya kumtorosha Adam pale nyumbani. Shida yake haikuwa kumtesa Adam bali kumweka mbali na mwana (Reshmail) ambaye alikuwa amempagawisha ipasavyo katika mapenzi ya jinsia moja.Suala la pesa halikuwa tatizo hata kidogo alichohitaji ni kutimiziwa alichotaka. Mkataba wa miaka mitano ndio alioingia na watu hawa kukaa na Adam bila kumruhusu kutoka nje ya jingo.Bi Gaudencia aliamini kwamba kwa kutokomea Adam mbele ya uso wa Reshmail ilikuwa fursa nzuri ya kurudisha tena uhusiano wake na Reshmail ambao ulikuwa unaelekea kufa lakini kinyume chake alikuwa ameibua chuki kubwa baina yake na mwanae “heri wote tukose kama ni hivyo” alijiapiza mama Reshmail baada ya kuona dalili za kumshawishi Reshmail hazipo tena
Alikuwa ni Reshmail mwingine kabisa mkasa uliomkumba ulimbadilisha sana na kuitanua akili yake sana,Eveline naye alisikitishwa na yaliyomkumba shoga yake akajitahhdi sana kuwa karibu naye kumpa moyo huku akijiepusha sana kufanya vitendo ambavyo vitamkumbusha Resh jinsi alivyoweza kukutana na Adam. Ni katika kujiepusha na kumkera rafiki yake huyo kipenzi Eveline akajikuta amefuta picha za uchi na filamu za ngono katika kompyuta yake akawa si mtu wa kutoroka shule,hakuwa tena mtu wa wanaume na hatimaye akawa Eveline wa kuigwa na wanafunzi wenzake jambo hilo liliwaduwaza sana wanafunzi pale shuleni lakini ndio hivyo Eve alikuwa amekubali mabadiliko katika maisha yake. Juhudi zao katika masomo ziliendelea kuwaweka katika nafasi nzuri ya kufanya vizuri mtihani wao wa mwisho. Hawakuyazungumzia tena yaliyopita tena walijadili mapya na yanayowanufaisha "Eveline wewe ni kama dada yangu nakupenda sana"
"Nakupenda pia Reshmail umebadili maisha yangu moja kwa moja nina maisha mazuri sasa" alijibu Eva kwa upole huku akimwangalia Reshmail aliyekuwa anaishusha chandarua yake aweze kulala. Ni kweli walitokea kupendana wawili hawa.
"Hivi Resh una mpango bado wa kusomea uhasibu mi lazima niwe mhasibu"
"Mh! unavyojiaminisha utadhani tumefaulu tayari" alijibu Resh.
"He! mi najua sisi kufaulu kwetu sio swali ni jibu,swali ni je tunaenda chuo gani na kusomea nini." alijiaminisha Eveline.
"ok! nilidhani nitasomea uhasibu lakini kwa heshima ya Adam nitasomea sheria" alijibu Reshmail kwa furaha.
"Mh! na upole wako huo na mambo ya kutoa hukumu wapi na wapi? mwenzio naangalia ankara" alisema Eva.
"Wala hata siendi kuhukumiana naenda kwa heshima tu" alisisitiza Reshmail.
"Mh! haya mheshimiwa hakimu napenda kujitetea kama ifuatavyo" Eve alitania akifuatiwa na kicheko kikubwa kutoka kwa Reshmail.
* * *
Maisha yaliendelea vyema sana tu japo yalikuwa maisha ya mashaka Adam aliruhusiwa kuongea na kuuliza kila kitu kasoro swali moja tu "Kwa nini niko hapa?",ndio hakuruhusiwa kuliuliza hata kwa mbali,watu wote pale hawakuwa na ubaya nae hata kidogo,hawakumtesa,hakugombezwa wala hakufanya kazi,alipewa huduma zote za msingi,aliweza kutoka nje na kwenda bustanini lakini nje ya geti hakuruhusiwa. Tayari aliyazoea maisha haya lakini kumbukumbu ya jinsi alivyochukuliwa ndani ya jumba la wakweze bila kupata msaada wowote ule "Nani atakuwa nyuma ya haya yote mlinzi alikuwa wapi? Mama Resh je?" alijiuliza sana bila kupata wa kumpa jibu.
"Hivi unaitwa dada nani vile?" Adam alimuuliza dada mmoja ambaye kila baada ya siku tatu alikuja kufanya usafi katika chumba chake.
"Naitwa Beatrice Cosmas niite Bite" alijibu huku anafuta vioo kwa dirisha la chumba cha Adam.
"Una jina zuri wewe mh!"Alisanifu Adam.
"Asante wewe ni Adam eeh!" aliongezea yule binti huku akiwa ameacha shughuli yake aliyokuwa anafanya.
"Ndio mimi ni Adam! samahani nikuulize maswali machache"
"Uliza tu lakini sitakujibu sasa hivi"
"Kwa nini?"
"We uliza yote ndo nitakwambia kwa nini"
"Hivi hapa ni wapi? kwa nani? na kwa nini nipo hapa?"
"Ndio hayo matatu tu?...sawa nitakujibu kwa sharti dogo sana yaani"
"Sharti gani hilo mi nipo tayari"alitoa uhakika Adam bila hata kulijua sharti lenyewe.
"Sikia Adam sina haja ya kuzunguka zunguka nina mwaka wa pili hapa kitu kinaitwa mwanaume katika mwili wangu ni kama ndoto sasa ni wewe wa kutii kiu yangu na mimi nitajibu maswali yako" alijieleza Bite,jambo ambalio lilikuwa zito na la kumshangaza Adam.
"Mh! au ndo mtego tena kutoka kwa Reshmail? dah! ikiwa hivyo nitaaibika kweli mimi"Alijiwazia Adam kwa mashaka makubwa kabla ya kujibu.
"Basi utakuja kunijibu baadaye!" alisema Adam.
"Haya usiku na wewe jiandae" alijibu na kuaga Bite.
Hayawi hayawi mara yakawa usiku wa saa tatu,Bite tayari ndani ya chumba cha Adam ndani ya khanga moja peke yake.
"Haya nipe nikupe hakuna longolongo hapa" alizungumza Bite.
"Subiri taratibu basi,sikiliza" alianza kujitetea Adam wakati Bite anajisogeza kitandani,Adam alikuwa amechelewa tayari joto la Bite lilipenya katika mwili wake na kumchanganya hadi kujikuta akifanya kinyume na alivyotarajia kwamba atafanikiwa kutegua mtego wa Bite badala yake alikuwa ameshafanya mapenzi na Bite. Kwa Bite ulikuwa ushindi mkubwa sana kwani tangu aletwe hapo kuwa msaidizi wa kazi za ndani ya vyumba hakuwahi kutoka nje ya jengo hilo,sio kwamba alikuwa amefungwa hapana kila kitu kilikuwepo ndani kila siku pia alikuwa ameridhika kuwa hapo.
"Hapa ni Iringa,nimejibu swali lako la kwanza tuendelee tena nikujibu swali la pili na tatu" alisema Bite kwa shauku kubwa sana.
"Hapana Bite imetosha kwa leo sijisikii vizuri,siku nyingine basi sawa!" alidanganya Adam na Bite hakuwa mbishi akambusu Adam shavuni akajiondokea zake.
Ilimchukua takribani siku tano Bite kugundua kwamba tayari ameshika ujauzito jambo ambalo halikuruhusiwa katika jumba hilo na alipewa onyo kali wakati anaingia hapo. Kwa usalama wake na Adam alifikiria suala la kutoroka lakini haya yote aliyafanya baada ya kuongea na Adam na kumweleza hali halisi. Ni katika wasaa huo alimweleza Adam chanzo ambacho kinaweza kuwa kimemsababishia yeye kuwepo pale "Umemchukulia kigogo mpenzi wake,umemendea mtoto wa kizito au umemkataa kimapenzi mtu maarafu" hizo ndizo zilikuwa baadhi ya sababu alizoorodheshewa na Bite,lakini kwake yeye aliona hakuna hata moja inayomuhusu kwani wazazi wote wawili wa Reshmail walimpenda sana hakuwa tayari kuweka hisia kwamba pengine moyoni wanamchukia.
"Usijali lakini hutakaa milele humu,huwa unafika
Muda aliyekuweka humu akiridhika unatoka.
"Nitamlea mtoto,napenda watoto hata kama usipokuwa mpenzi au mume wangu nitampenda sana na nitamwita....."
"Christian akiwa mvulana au Christina akiwa msichana" alidakia Adam ambaye kwa mbali alianza kumtamani Bite kimapenzi.
* * *
Biashara za baba yake zilikuwa zinaendelea vizuri na skendo lake lilikuwa linafifia taratibu. Hadi anamaliza kidato cha sita Reshmail mapenzi kwa wazazi wake yalikuwa palepale na japo hakutaka kumwongelea Adam jena alikuwa na picha yake waliyopiga pamoja siku moja kabla ya tukio lile la kushangaza na kuumiza. Reshmail kwa ruhusa ya wazazi wa Eveline alienda nae mpaka kwao ambapo walikaa wote kwa siku tano kisha akarejea tena Arusha. Urembo wa Reshmail ulipagawisha kila mwanaume na hata baba yake ilifikia kipindi akakiri kwamba kweli pale alizaa mtoto mmoja wa kipekee na kweli alikuwa wa kipekee. Mama Resh bado alikuwa na matamanio lakini kwa ssa alimwogopa sana Reshmail tofauti na miaka mingi iliyopita.
"Baba na mama wiki ijayo nataka kwenda Mwanza kwa wazazi wa Adam" Resh alitoa hoja yake wakiwa mezani wanakula.
"Wapi? Mwanza! hawatakuelewa mwanangu utakuwa kwa maksudi kabisa unafufua shari iliyopoa tayari.
Tayari"Kwa busara tele na upole mzee Manyama alimweleza mwanae ambaye pia aliyapokea kwa nidhamu ya hali ya juu na kichwa chake kuyakubali kuwa yana maana kubwa ndani yake."Nimekuelewa baba sitaenda tena" alijibu kwa unyenyekevu sana Reshmail.
Muda mwingi wakati anasubiria matokeo aliutumia kuimba na kusikiliza muziki na mara chache sana kwenda kutembelea rafiki zake walioishi jirani naye.
* * * *
Matokeo ya kidato cha sita yalipotoka hayakuwa ya kushangaza sana kwa upande wake kwani alikuwa amevuna alichokipanda. Reshmail alikuwa amepata daraja la kwanza na ndivyo alivyotarajia,furaha yake iliongezeka baada ya kumwona katika orodha Eveline Maige rafiki yake kipenzi naye akiwa amepata daraja la kwanza huku wakitofautiana pointi kadhaa. Akiwa anajiandaa kumpigia simu tayari simu yake iliwakawaka na kuandika "pacha" jina ambalo alikuwa amemwandika Eve katika simu yake,badala ya kuongea wote kwa pamoja wakaanza kucheka,walicheka sana hadi simu ilipokatika. Zilikuwa ni furaha kutoka moyoni,kwa nini wasifurahi wakati ndoto zao zilikuwa zinatimia?
Tanzania Commission of Universities (T.C.U) ilipotoa uchaguzi wa kwenda vyuoni Reshmail kama alivyopenda alichaguliwa chuo kikuu cha mtakatifu Augustine Mwanza kwa masomo ya sheria huku Eveline Maige akipelekwa Mzumbe chuo kikuu kwenda kuchukua masomo ya uhasibu shahada ya juu.
"Ndugu hakimu naomba kujitetea!" Eve alimtania Resh utani wao wa shuleni siku walipokuwa wanaagana.Walikuwa wametenganishwa hatimaye lakini mawasiliano yao yalidumu
Kama alivyojiwekea kiapo chake cha kutopenda hovyohovyo ni hivyohivyo alivyoingia pale chuoni,hakuringia uzuri wake lakini hakutaka pia usumbufu unaopitiliza kutoka kwa wanaume yaani kwa kifupi alikuwa na msimamo mkali sana,ni rafiki yake (Eve) pamoja na wazazi wake ambao wangeweza kubashiri sababu hasa inayomfanya binti huyu awe hivi na si mtu mwingine pale chuoni.
Maringo yake yalifichwa na werevu wake darasani,kwani ilikuwa ni warembo wachache sana wa aina yake waliofanya vizuri kimasomo,jambo hilo lililowavutia waalimu wengi sana na wanafunzi ambao wanapenda maendeleo kimasomo. Reshmail hakuwa mtu wa mambo mengi hakunywa pombe wala kwenda kumbi za starehe usiku starehe yake ilikuwa ni kusoma na michezo.
Mnamo mwezi wa pili michezo ya FAWASCO ilipoanza michezo hiyo inayohusisha vitivo vyote pale chuoni,kwa maksudi alichaguliwa kuwa mhamasishaji kwa wasichana wajibu alioufanya vizuri ipasavyo na kikubwa zaidi akawa pia mdhamini mkubwa sana. Moyo wake wa kujitolea uliwavutia sana wanadarasa wenzake ambao baadhi walimpenda huku wengine wakidai ana maringo, msimamo wa Reshmail ulibaki palepale.
Mwaka wa pili pale chuoni ndio ulikuwa mbaya kwake. Darasa walilolitumia mwaka wa pili wanafunzi wa kitivo cha sheria,lililojulikana kama Mombasa Raha kwa mbele lilikuwa na picha kubwa sana ya Adam ambayo ilikuwa pembeni ya ubao wa kufundishia hiyo ikimaanisha kwamba kila atakapoingia darasani lazima aione,"ADAM THE GREAT" yaliandikwa maandishi haya chini ya picha kubwa ya Adam. Amani,ikatoweka kabisa moyoni mwake kumbukumbu mbaya za kumpoteza mpenzi wake Adam zikaanza kumrejea kwa kasi sana.Reshmail akaanza kujihisi yeye ndiye chanzo cha yote hayo,tofauti na waalimu wake hakuna mwanafunzi aliyemfahamu Adam zaidi ya kujua tu historia ya yaliyomkuta na wengi kuichukulia kama simulizi tu ya kusadikika. Reshmail alianza kuwa mtoro darasani na hata alipoingia badala ya kumwangalia na kumsikiliza mwalimu,mawazo yake yote yalivutwa na picha ya Adam yenye tabasamu pana mara zote aliamini inamuangalia yeye na kumlaumu kwa kumkatisha masomo yake kwa penzi la mtandaoni. "Adam stop blaming me!!(Adam usinilaumu)" alipiga kelele kwa nguvu Reshmail bila kujitambua,mwalimu alimshangaa na hakuelewa kilikuwa kimemsibu nini "Is she dreaming? (Anaota?)" aliuliza mwalimu Sijjo aliyekuwa anawafundisha somo la mawasiliano (Communication skills),darasa zima likacheka kwa fujo sana,lakini Reshmail alikuwa analia huku akitetemeka sana,kwa ghadhabu akasimama na kutoka nje. Japo ulikuwa ni mwezi mmoja tu tangu waanze masomo ya mwaka wa pili lakini
tabu na mateso aliyokuwa ameyapata yalitosha kumshawishi kuwa huenda amesoma hapo kwa miaka kumi.Wazazi wake hawakuwa na la kufanya,Eveline alibaki kumwonea huruma shoga yake huyu alijaribu mara kwa mara kumpigia simu lakini haikuwa tiba ya tatizo la Reshmail. Ni kweli Reshmail asingeweza kujilazimisha kuwa na furaha kwani ni yeye aliyemshawishi Adam awe nae kimapenzi na ni yeye huyuhuyu alimshawishi Adam aende kwao kwa ajili ya kujitambulisha na safari hiyo ikawa ya mwisho ya Adam. "Nikiwaambia waalimu wangu watanielewaje,na hata wakinielewa itakuwaje wanafunzi wenzangu wakijua siri hii? watajenga picha gani tena kuhusu mimi,mh! niepushe na hali hi bwana,kama uliweza kuniondolea mawazo haya hadi nikamaliza kidato cha sita vyema hebu baba na sasa ondoa tena na hili jaribu zito mbele yangu na jina lako lisifiwe." aliweka ombi fupi Reshmail katika mawazo yake hayo. Lilikuwa ni jambo gumu sana kwa Reshmail alikonda sana na punde si punde maneno ya wakosaji yakaanza tena "Mh! kumbe ndio maana anakataa wanaume kumbe anaishi kwa matumaini maskini,dada mrembo kama huyu" yalisikika maneno hayo katika vijiwe vya wanafunzi pale chuoni. Ilikuwa ni kero kubwa kila alipokatiza vidole vilimwelekea yeye umaarufu wake wa awali kwamba ni mrembo ukaongezeka maradufu karibia chuo kizima lakini wakati huu ilikuwa ni sifa mbaya kwamba ana virusi vya UKIMWI hata yeye aliyasikia maneno hayo yalikuwa yakivuma kwa kasi,hakuwa na uwezo wa kuzuia tetesi hizo "Wangejua kwamba mi ni bikra na wanayoyasema yote ni uongo,hata wasingenyanyua midomo yao michafu kuropoka upuuzi huo,lakini bila Adam watajuaje?" alijiuliza Reshmail akiwa chumbani mwake katika hosteli ya Ngulelo aliyokuwa amepanga chumba alichoishi peke yake. Marafiki zake taratibu wakaanza kumtenga wakiamini ameathirika,hilo halikumuumiza kichwa kwani alilitegemea sana hasa hasa dhana ya unyanyapaa kwa waathirika iliyokuwa inatawala chuoni hapo.
 
Bite alifanikiwa kutoroka katika ngome ile kubwa aliyokuwa amehifadhiwa Adam. Kwa jinsi alivyokuwa amezoeleka pale haikumchukua muda mrefu kumshawishi mlinzi amfungulie geti atoke kidogo na ndio ikawa jumla hakwenda mbali sana na mkoa wa Iringa bali aliweka kambi yake maeneo ya Uyole Mbeya mkoa uliopo jirani na Iringa ambapo kipesa kidogo alichoondoka nacho pale ndani alifungua kibanda chake sokoni na kupanga nyumba eneo jirani la Igawilo akianzia maisha ya kulala chini hadi aliponunua godoro.Biashara ya kuuza nyanya

na mbogamboga ilimkimu sana maisha yake kwani wazo wala tegemeo lake halikuwa kununua gari,au kujenga nyumba hapana lengo lake lilikuwa uhai pekee,na shilngi elfu moja alizozipata zilikuwa zinamtosha kabisa. Alikuwa mchangamfu na mstaarabu sana,wateja walivutika kwake kwa kasi kufaidi ukarimu wake katika biashara.Tumbo lake lilianza kukua taratibu,kina mama sokoni wakaanza kuhisi tayari Bite kapata mjanja Mbeya amemjaza mimba,lakini miezi yake ya kujifungua ndiyo ilifungua akili za waliokuwa na maswali na kugundua kwamba ile mimba alikuja nayo pale na sio kwamba aliipatia pale. Salama bin salmin Bite alijifungua mtoto wa kiume miezi tisa ilipowadia.

"Mh! baba yake atafurahi tena alimpa jina pale tu nilipomwambia nimeshika mimba" Bite kwa furaha tele aliwaambia kina mama wa pale sokoni,akiwemo jirani yake mama wawili,ni hao ndio walikuwa ndugu zake."Hongera Bite,sijui ndio unakuwa mama nani vile" Bite alihojiwa na mama wawili

"Mwanangu anaitwa Christian" alijibu Bite huku akibusu kichanga chake hicho ambacho kilikuwa kinarusharusha miguu na mikono yake huku na huko.

Christian alizaliwa akiwa na afya tele na hakusumbuliwa na magonjwa wakati wa ukuaji wake mwaka wa kwanza,ilikuwa furaha kubwa kwa mama yake.
***

Miaka ilizidi kukatika wazo la Bi. Gaudencia kumtoa Adam katika jumba lile lilikuwepo kichwani mwake kwani udhaifu alioupata Reshmail pamoja na kashfa mbaya anazozipata pale chuoni zilimsononesha sana lakini ataanzia wapi kuificha aibu yake pale ambapo Adam,akasababisha uovu wa mama huyu uwekwe hadharani. Ni jambo hilo lililomuumiza kichwa mama huyu. Reshmail na baba yake watanielewaje kwa mabaya niliyowafanyia,nimeishusha heshima ya mume wangu aliyekuwa na heshima kubwa bungeni" alizidi kuwaza
Huku Iringa maeneo ya Ruaha Adam alikuwa anauanza mwaka wa tatu,akiishi kama nyumbani kwake,lakini hakuridhika hata kidogo maisha hayo ya ufungwa. Miaka mitatu ilikuwa mingi sana "Mama na baba yangu wanahisi niko wapi? vipi kuhusu mpenzi wangu Reshmail,hapana imetosha nahitaji kutoka hapa,lakini lazima nijiulize nitatoka vipi hapa katika ngome hii" alijisisitiza Adam japo ulinzi madhubuti ulioongezwa kutokana na kutoroka kwa Bite katika mazingira ya kutatanisha pale ngomeni

***

Mwaka wa pili uliisha hivyohivyo kimateso makali yaliyojawa na kumbukumbu mbaya na isingekuwa kuhamishwa kwa darasa la sheria mwaka wa pili kwenda katika maghorofa ya Mwanjonde chuoni hapo basi Reshmail angefeli vibaya masomo yake kutokana na msongo wa mawazo.

Akiwa mwaka wa tatu afya yake ilirejea tele kwani hakuwa akiiona tena picha kubwa ya Adam machoni pake hali hiyo ya afya kurejea ilizusha msemo mpya tena,tofauti na mwanzo walivyosema ana Ukimwi,sasa walisema "Akikonda ana virusi,akinenepa ameanza kutumia dozi" yote hayo alituhumiwa Reshmail lakini kamwe hakuwahi kuthubutu kunyanyua mdomo wake kujibu vijembe hivyo yeye alikuwa mkimya huku akipambana na masomo hadi alipoumaliza mwaka wake wa nne vyema.
Mnamo mwezi wa kumi na moja familia yake yote ilisafiri kuelekea jijini Mwanza kusheherekea kwa pamoja mahafali ya mtoto wao,Eveline ambaye tayari alikuwa kazini baada ya kuwa amemaliza miaka yake mitatu chuoni na kufaulu vizuri pia alijumuika katika kukamilisha furaha hii ya rafiki yake mpenzi huku akiongozana na mchumba wake Benjamin Simon. Reshmail alifurahishwa sana na ujio wa Eve kwani alizidi kudhihirisha kuwa ni kiasi gani yeye ni rafiki wa kweli.
Yalikuwa ni mahafali makubwa na ya kipekee kuliko yote yaliyowahi kutokea ambapo chuo cha Mt.Augustino kilifanya mahafali ya pamoja na matawi yake yote Tanzania,yaani Iringa,Mtwara na Tabora. Kwa ufupi yalikuwa yamefana.
Ni katika pirikapirika na pitapita za huku na huko

za sherehe hiyo ndipo Reshmail akiwa na Eveline ana kwa ana anakutana na familia ya Adam yaani baba na mama yake,aliwatambua kwa uwepo wa Rosemary yule mdogo wake Adam. Rosemary alikuwa ndio kwanza amehitimu shahada ya elimu katika chuo kikuu cha mtakatifu Augustino tawi la mtwara hivyo yeye na familia yake pia walikuwepo katika viwanja vya Raila Odinga kusheherekea mahafali yale."Mchawi...mchawi!" alianza kupiga kelele mama yake Adam wakati Reshmail akisogea taratibu katika eneo walilokuwepo kwa furaha "Uuuwii" alipiga makelele kwa sauti ya juu jambo lililovuruga usikivu katika eneo lile na watu kuanza kumwangalia yeye kama mtu aliyechanganyikiwa,Reshmail na Eve walikuwa wameganda tu na mama Adam akizidi kupiga kelele,jitihada za baba yake Adam kumtuliza mkewe hazikufua dafu,mara ghafla mama Adam akakurupuka akiwa na chupa iliyokuwa na soda ambayo haijafunguliwa bado na kwa kasi akaenda kumkabili Reshmail ambaye akili yake ni kama ilikuwa imesimama na umati uliokuwa umemkazia macho kwa kitendo cha kuitwa mchawi ulimzidishia hofu na fedheha kwake,Eve alimshika mkono Reshmail na kujaribu kumvuta watoke eneo lile lakini tayari mama Adam alishawafikia na kwa nguvu kabisa akaituliza chupa ile juu ya kichwa cha Reshmail palepale akaenda chini huku damu nyingi ikimtoka kichwani. Wanaume watatu akiwemo pia baba yake Adam walifika na kumbeba juu juu,mama Adam ambaye alionekana dhahiri kuwa bado hajaridhika na kipigo alichotoa kwa Reshmail kwani bado alikuwa anaangaza huku na huko kama palikuwa na silaha nyingine. Alikuwa kama mwendawazimu

Wengine walimbeba Rshmail ambaye joho lake la kipekee kabisa lilikuwa limechafuliwa vibaya na vumbi la uwanja wa mpirawa miguu wa Raila Odinga ambapo ndio sherehe zilifanyika. Hali ya sintofahamu ilitawala sherehe zile kwa takribani nusu saa nzima hadi Reshmail alivyoondolewa na familia yake kuelekea hospitali na mama Adam kutiwa katika nguvu ya dola

***

Halikuwa jeraha kubwa sana nyuzi mbili zilipita katika kichwa chake kushona jeraha lile

“kwa nini mama mkwe wako akutende hivi” eve alimuuliza Reshmail akiwa pale kitandani

“ni haki yake hata kunipiga risasi mimi ni chanzo cha maumivu haya wanayoyapata” alijibu Resh huku akilazimisha tabasamu

“kwa hio hapa amenionea huruma sana mimi ni sawasawa na muuaji tena wa kukusudia na haki yangu ni kuuawa pia” aliendelea Reshmail huku akitoa tabasamu hafifu tena

“usiseme hivyo mamii sio wewe uliyetaka iwe hivyo ni Mungu pekee” aliongea kwa upole Eve huku akivibinyabinya vidole vya Reshmail

“mama mwambie baba afatilie mama mkwe asije kulazwa selo hata kwa saa moja hana kosa lolote” Reshmail alimwambia mama yake alipoingia katika chumba cha hospitali ya Agha khan aliyokuwaelazwa kwa ajili ya matibabu maneno hayo yalimshangaza sana mama yake aliyetegemea Reshmail atakuwa na hasira ya kutendwa vile mbele ya hadhara

Nafsi ilikuwa inamsuta sana mama reshmail,moyo uliomba msamaha lakini mdomo ulikuwa mzito sana kufanya hivyo. Hali hiyo ilimkondesha sana na kumkosesha raha ndani kwa ndani unene wake wa asili uliyafunika yote hayo na hakuna aliyejua jambo zito alilobeba mama huyu.

Kweli badala ya bwana na bibi Manyama kuegemea upande wa mashtaka ili mama Adam apewe adhabu la wao waliunga mkono kwamba Reshmail alikuwa na makosa mahakama ikatupilia mbali mashtaka hayo na mama Adam akawa huru,jambo hilo badala ya kurudisha undugu liliongeza chuki na uadui

“si nilikwambia ukabisha?? Kama hawajamtoa mwanetu kafara kwanini sasa wamekubali niachiwe huru??” mama Adam alimwambia mumewe jambo ambalo wakati huu hata yeye alikubaliana nalo kuwa motto wao mkubwa wa kiume(Adam) alitendwa vibaya na familia ya reshmail . kuamini kwa mzee Michael baba yake Adam ni sawa na familia nzima kuamini kabisa na sumu ya chuki ikamwingia kila mwanafamilia na kuwa aadui wakubwa wa familia ya mzee Manyama.




* * * * * * * * * * *

Siku mbili alizokaa pale hospitali hakuja hata mwanafunzi mmoja kutoka pale chuoni kuja kutoa pole kwa Reshmail wote waliogopa wakiamini alikuwa mshirikina . Eve hakukubaliana hata kwa mbali na shutuma hizo kwani alimwamini sana Reshmail hivyo aliendelea kuwa pale hospitalini pamoja na mchumba wake kumuuguza Reshmail ambaye alitoka siku tatu baadaye.

“baba mimi nitaenda na Eve kwake nitakaa siku tano ndio nitakuja huko” Reshmail alimpa taarifa hiyo baba yake naye hakupinga kwani amani aliyokuwa nayo Resh akiwa na Eve ilikuwa kubwa mno hali iliyowapa faraja hata wazazi wake hivyo walimruhusu bila kusita.

Siku hiyohiyo walipanda ndege kwa gharama za mchumba wa Eveline aitwaye Benjamin Simon,kuelekea Iringa ambapo Eve alikuwa amepata ajira katika benki ya N.B.C tawi la hapo.

Maisha yao yalikuwa mazuri sana kwani Benny alikuwa mwalimu wa shule ya sekondari hivyo katika majukumu waliweza kusaidiana na upendo wa dhati kati yao ulipendezesha zaidi nyumba yao.Reshmail alivutiwa sana na maisha hayo na kumkumbuka sana Adam wake “laiti angekuwepo tungeishi hivi siku moja “ alijiwazia Reshmail wakati akiwaangalia Eve na Benny wakiwa kwenye kochi wamebebana kwa furaha huku wakitaniana

Ilikuwa jioni moja Reshmail na Eve wakiwa katika mizunguko ya hapa na pale mizunguko ambayo kwa namna moja au nyingine iliibua ghafla safari ya kuingia sokoni,waliingia hapo kununua matunda matunda,zilikuwa zimepita siku tano na tofauti na alivyowahaidi wazazi wake hata hakuwa amefikiria kurudi Dar maisha ya Iringa yalikuwa yamempendeza sana .

“Eveline ona eveline jamani angalia kale katoto!!!” Reshmail alimgusagusa begani Eveline huku akimwonyesha kikundi fulani cha watoto pale sokoni

“wewe achana hao machokoraa walionikwapua pochi langu sina hamu nao hata kidogo,kisimu changu cha mchina na shilingi elfu thelathini zikapotelea hewani looh!! Wabaya hao” aliongea kwa hasira Eve huku akisitisha zoezi la kula chungwa aliliokuwa anafanya kwa wakati ule.

“mh!! Eve jamani achaga uongo yaani katoto kama kale jamani hebu kaone kale kadogo “Reshmail alizidi kusisitiza lakini Eve alionyesha bado ana uoga na uchungu moyoni wa kuibiwa vitu vyake na watoto aliowaita machokoraa

“Reshmail shauri zako vitakuliza hivyo we endelea kusema ni vitoto………..mh!! Resh lakini kale kadogo kazuri kweli” aliongea Eve alipokaona kale katoto ambako Reshmail alisisitiza sana.

“toto zuri jamboo!!”

“sijambo shkamoo!!” kalijibu katoto kale kwa uchangamfu sana baada ya Reshmail na Eve kukasogelea na kukasalimia.

“marahaba mtoto mzuri mbona upo hapa! Mwenyewe au hawa ni kaka zako?” Resh alimuuliza

“a a sio kaka zangu mi namsubiri mama ameondoka na watu wameenda huko amesema anarudi nimsubiri” alijibu tena kwa sauti ya kitotototo

“umekula??” aliuliza Eve.

“looh!! Eve hujaacha tu maswali yako ya kichoyo ya uchagani kwenu mh! Unataka aseme amekula ili umnyime au ?” Reshmail alimshushua Eve kiutani

“mh! Limeniganda shoga,una mashushu wewe!!” alijibu Eve kiaibuaibu huku akimpa yule mtoto chungwa lililokwisha menywa tayari.

“mama anarudi saa ngapi??” Reshmail alimuuliza yule mtoto tena

“sijui nimemsubiri hata hajaja amenipa chai tu akaondoka na wale wanaume wawili” alijieleza vizuri motto yule

“mh!! Mjini mjini tu katoto kanajieleza utadhani mtu mzima dah!” Eve alimnon’goneza Reshmail

“haya twende ukale eti motto mzuri!” Reshmail alimwambia yule motto naye akakubali kwa ishara ya kichwa,akiwa pekupeku akafuatana na Reshmail hadi kwenye mgahawa ulioandikwa “MAMA FRED MGAHAWA” uliokuwa pembeni kidogo ya soko kuu la Iringa.

“utamsalimia mama eeh!!” baada ya kumnunulia chakula walilipa na kumuaga

“haya mamdogo!” alijibu yule motto

“unaitwa nani vile”Eve akamuuliza

“naitwa Christian motto wa mama Bite” alijibu na wote kwenye mgahawa wakacheka





Kuifananisha na picha ya Adam,dimplez za yule mtoto zilimfananisha kabisa na Adam,achilia mbali rangi yake ya maji ya kunde na ucheshi wake.
"Eve hapana,mbona kesho naenda kumtafuta Christian ili nimjue baba yake anavyofanana,haiwezekani kufanana kwa kiasi hchi hapana "Aliongea Resh huku akiifunika album ile . Eve alikubaliana naye na siku iliyofuata majira ya saa nne,walikuwa katika hoteli ya yule mama ambapo walimwacha Christian.
"Nyie watoto ni kesi gani hyo mmetaka kuniachia jana" mama mnene kiasi mmiliki wa mgahawa wa Mama Fred aliwapokea kwa maneno hayo makali huku akifunga kanga yake vizuri kiunoni. Resh na Eve hawakuwa na jibu la kutoa walidhani amewafananisha labda "Mama ni nini tena,mbona sisi...." alijaribu kujieleza Eve huku akiishiwa maneno ya kujieleza.
"Mmenitekelezea mtoto hapa anaanza kunililia hapa usiku he! jamani mnataka mniuwe kwa presha mkurya wa watu mie" aliongea kwa ghadhabu na mshangao mkubwa sana yule mama.
"Mama sisi tumempata hapo sokoni,ndio kumleta hapa kwako kwa ajili ya kupata chakula tu mama yangu" Reshmail alinyanyua mdomo wake na kuzungumza kwa sauti iliyojaa mshangao pia.
"He! mauzauza gani haya jamani,mi nimempeleka pale kituo cha polisi usiku uleuule ndugu







**************************************


* * * ** ** ** ** *


Baridi kali ya Mbeya ilikuwa imemkataa motto wa Bite (Christian) kwa hali hiyo alipotimiza miaka miwili waliondoka na kurudi tena Iringa ambapo Bite alitaka kukaa kidogo halafu aende Mwanza kuweka makazi mapya huko. Jambo la kushangaza licha ya baridi ya Iringa hali ya Christian ilianza kuwa njema kama awali jambo lililosababisha Bite aendelee kukaa katika mkoa huo.hadi anatimiza miaka mine hali yake kiafya ilikuwa njema sana na tayari Bite alikuwa amesahau suala la kwenda Mwanza.akaanzisha genge la kuuza uji na karanga mida ya jioni na mihogo ya kukaanga majira ya asubuhi. Ilikuwa biashara ndogo lakini iliyomuingizia kipato kizuri tofauti na matarajio yake.aliweza kupanga nyumba ya chumba kimoja na sebule aliyoishi na mwanae kwa furaha sana tu bila masumbufu yoyote hadi siku hiyo asubuhi alipokuwa anauza mihogo yake ambapo wanaume wawili ambao sura zao hazikuwa ngeni machoni pake walipofika eneo la biashara yake.Aliwapokea kwa furaha sana na bashasha kama wateja wengine aliozoeana nao.”Bite tukuone pembeni kidogo samahani lakini’ wawili wale walimvuta pembeni Bite

“mh! Mikopo asubuhi asubuhi hamna kwakweli mtadhalilisha hizo suti zenu” aliongea Bite kwa utani huku akiwafata walipo wawili hao

“funga biashara tunaondoka na ukithubutu kupiga kelele au kukimbia nasambaratisha ubongo wako nadhani hujawahi kufikiria kifo cha namna hiyo,hivyo basi fanya kama unavyoagizwa” aliambiwa Bite na wale wanaume huku mmoja akifunua koti lake jeusi la suti na kumwonyesha Bite kitu ambacho hakujiuliza mara mbili mbili kuwa ile ilikuwa ni Bunduki,kwa kuutambua uoga alioupata Bite,yule mwenye bunduki alimbandika kitu mfano wa kishikizo cha nguo na kumwambia “hiyo ni sound recorder nenda ukawaambie wateja wako sisi ni ndugu zako tumekuletea taarifa za msiba nitakuwa nakusikiliza hapa,ole wako nasema ole wako usifuate maelekezo” alipewa masharti hayo ya uongo Bite ambaye laiti isingekuwa pensi yake ya jinsi ambayo huwa anavaa kwa ndani ili kuhifadhia pesa zake za mauzo basi mkojo uliopenya bila yeye kujua ungemwagika palepale hadharani na wala asingepatwa ma aibu yoyote ile.Kama alivyoagizwa aliwaeleza wateja wake wawili waliokuwa wanamalizia kuitafuna mihogo waliyokuwa wameinunua,wakampa pole za dhati . jasho lilikuwa linamtoka alitamani kutumia ishara kuwaambia kwamba yupo katika hatari lakini alipowazia mdomo wa bunduki alikaa kimya kabisa,bila kificho Bite aliiogopa sana bunduki na hakupenda kumwacha Christian katika umri ule.Tayari akili ilisharudi nyuma akatambua hasa,hao watu alikutana nao wapi,walikuwa ni baadhi ya wafanyakazi katika ile ngome aliyekaa miaka miwili na ni hao waliomleta Adam pale ngomeni “nimekwisha mimi Beatrice” alijiwazia Bite huku akitetemeka.

Baada ya kuifunga biashara yake aliwafuata akiwa na mwanae amemshikilia mkono.

“nadhani unajua hatuhitaji mtoto!!! Tunakuhitaji wewe tena sasa hivi” aligombezwa Bite na bila kujijua akajikuta akimwacha mwanae pale “Christian narudi sawa nisubirie pale sokoni sawa mwanangu! “haya mama alijibu Christian kwa furaha kwani alijua amepata fursa kubwa na ya kipekee kwenda kucheza na watoto wenzake pale mtaani

“ulidhani unaweza kutuzidi ujanja sisi,umepotea sisi hatupimiki hata kidogo umeumia tena umeumia sana aliambiwa Bite na wale wanaume wakiwa kwenye gari kuelekea kwenye gari kuelekea kule katika ngome jambo hilo Bite hakulitamani hata kidogo,japo alimpata Christian kwa bahati mbaya lakini alikuwa akimpenda sana kutoka moyoni na hakuwa tayari kutenganishwa naye kwa namna yoyote ile.Alijiuliza maswali mengi sana ni nani atakayempa chakula mwanaye siku hiyo na nyingine zitakazoendelea wakati yeye hayupo,michezo ya kukimbizana aliyoipenda Chriss pia ilimtia hofu Bite na kuhisi huenda mwanae anaweza kupoteza uhai wake kwa kugongwa na gari. Funda la hasira lilimkaba kooni alitamani kufanya lolote lile wakati huo lile jambo liwe ndoto kwake, machozi yaliyotoka ndio yaliyeyusha lile fundo japo kidogo,hasira kali ilikuwa imemkaba Bite aliyekuwa amekaa siti ya nyuma na jamaa mwenye Bunduki katika koti lake lakini maskini hakuwa na la kufanya hadi gari lilipoingia ndani ya ngome ile


* * * * *

Macho ya Reshmail yalitawaliwa na taswira ya yule mtoto Christian,zilikuwa ni siku nyingi zimepita tangu afungue album yake kumwangalia mpenzi wake (Adam) aliyeaminika kuwa tayari ni marehemu.Ni katika usiku huu alipokuwa akipitia album ya Eveline ndipo tena anakutana na picha ya Adam ambayo yeye (Adam) alimpa Eveline walipoenda Mwanza.”Eveline,Eveline,Eve……….huyu hapa ni nani???”

“we umechanganyikiwa tena eti hebu acha mambo yake ya ajabu huyu Adam” Alijibu Eve kwa uoga.

“ na tuliyemwona leo kule sokoni ni nani??” aliuliza Reshmail

“we Reshmail jamani wanafanana Mungu wangu mbona wamefana hivyo lakini eeh!! Eve alijikuta picha ya mtoto Christian ikiumbika kichwani mwake na



Zangu kwa sababu nimekaa naye hadi saa nne tumemsubiri huyo mama yake aje wapi!! Nikaona isiwe shari ngoja nimpeleke polisi penye usalama kuepuka balaa kumbe na nyie hamjui ni wa nani he!!” alitoa maelezo hayo yule mama na kueleweka vyema kwa Reshmail na Eveline.

“hicho kituo cha polisi umesema kipo wapi?” aliuliza Eve

“kile pale kinaonekana hata kwa hapa,lile jingo la bluu nyuma yake” alielekeza yule mama

Ndani ya dakika tano tayari Reshmail na shoga yake walikuwa mbele ya mapokezi ya kituo cha polisi Iringa mjini

,na walikuwa kwenye foleni wakisubiri zamu yao ya kuhudumiwa ifike.

“nyie ni ndugu zake? Au mmoja wenu ndio mama yake?”

“hapana sisi si ndugu zake ila……”aliishia njiani katika maongezi yake Resh baada ya kukatishwa na yule askari “ila nini? Yaani nyie wanawake wa siku hizi suala la kujali watoto wenu hamtaki kabisa kulisikia mnachojali ni urembo tu wa sura zenu”

“jamani sio kwamba kuna ndugu yake hapa kati yetu ila sisi tumemkuta jana kule sokoni ndio tumemnunulia chakula halafu tukajiondokea zetu,leo hii ndio tunapita pale kwa mama Fred yule mwenye mgahawa yeye ndiye ametupatia taarifa hiyo tukaona sio vibaya nasi tukifika kumwona huyo motto” aliongea Eve aliyeonekana kutokuwa na hofu na kituo cha polisi lakini Reshmail alikuwa ana uoga kwa mbali kama vile anatuhumiwa kwa lolote lile.

“haya yupo tumemuhifadhi na tumepeleka taarifa kwenye vyommbo vya habari wataanza kutangaza kama mama yake bahati mbaya haya atakuja kumchukua na kama amemtelekeza akajiandae kwenda kuishi kwa watoto yatima sisi hatuna uwezo wa kuhifadhi watu hapa zaidi ya mahabusu” alijieleza askari yule huku akijipepea joto kwa kutumia kofia yake iliyochakaa

Majuma mawili yalipita bila mama wala ndugu wa motto kupatikana licha ya kituo cha redio maarufu mjini iringa cha Ebon fm kutangaza kila siku bila kukoma

“eve naenda kumchukua yule motto nafsi yangu inanishauri hivyo na ni lazima nifate ambacho nafsi yangu inaniamuru” Reshmail alimwambia Eve siku moja wakiwa wamekaa sebuleni wakiangalia habari katika luninga.Eve alikuwa amejenga tabia ya kutobishana na rafki yake huyo kwani furaha yake ilikuwa ni kumwona Reshmail akiwa na furaha tele

“lakini Resh,mama yake si atamtafuta ssana??”

“Eve yaani imetangazwa hivyo redioni na hajajitokeza leo hii mie tu kumchukua ndipo ajitokeze? Looh! Acha nae ahangaike kidogo” alijibu Reshmail kwa jeuri

“mh! Haya sikuwezi mwanasheria wangu”

Polisi hapakuwa na usumbufu ni wazi kwamba walikuwa wamechoshwa na matukio ya watoto kutelekezwa na wazazi wao pasipo sababu zilizo wazi,hivyo kitendo cha Resmail kuamua kumchukua Christian ilikuwa ahueni kwao.aliandiokishwa maelezo mafupi tu kabla ya kuruhusiwa kondoka na mtoto ambaye alikuwa dhaifu tayari kutokana na lishe duni na upweke wa kutomuona mama yake kwa siku hizo zote.

Reshmail alikuwa ameyafurahia sana maisha ya Iringa,kampani kubwa kutoka Eveline na mchumba wake ilibeba nusu ya furaha yake huku nusu nyingine ikikamilishwa na uwepo wa Christian mikononi mwake,mara kwa mara alipenda kuwa naye karibu huku akimwita mume wako jambo lililompa faraja kubwa moyoni
”Eve jamani nitakumiss kipenzi changu lakini nitarudi tena asanteni sana kwa ukarimu wenu mlionionyesha tangu mwanzo nimeishi kwa furaha kubwa sana hapa” Reshmail aliyazungumza hayo alipokuwa anawaaga Eve na Benny usiku ambapo kesho yake alitegemea kurejea Dar-es-salaam akiwa ameandamana na Christian mtoto aliyempata katika mazingira ya kutatanisha

Kwa Christian safari ya kutoka Iringa kwenda Dar ilikuwa safari yake ya kwanza ndefu zaidi kuwahi kusafiri

Siku iloyofuata wawili hawa walikuwa ndani ya basi la ‘budget’ litokalo Mbeya kwenda Dar likipitia Iringa.

“Mama alisema baba yupo pale kwenye ile nyumba, tushuke nikamsalimie!” Chriss aliongea hayo huku akielekezea kidole chake kwenye jingo lililoonekana kwa mbali mno kutokea pale barabarani na hapakuwa na dalili ya kuishi mtu pale hivyo Reshmail akachukulia kuwa ni akili ya utoto imemtuma Chriss kuzungumza akaamua kupuuzia

“chriss alikwambia nani we muongo!!”

“alinambia mama siku moja hivi tulipita hapa ,halafu mama alinikataza kusema uongo ni dhambi” alijieleza Christian haraka haraka

“mh! Haya tutakiuja siku nyingine sawa mfalme wangu” Reshmail alimjibu Chriss ili kumlidhisha kwa aliyokuwa anasema


** ** ** **

Nyumba tulivu kabisa ya mh.Manyama ililipuka kwa furaha kwa kurejea kwa Reshmail akiwa mwenye furaha tele “umetuletea na mjukuu!!” alitania mama Resh.”mtoto wa Eve huyu anamwita mama mdogo” Resh naye akdanganya “kazuri kweli kama………………” alisita kumalizia baba yake “ni kama Adam baba usiogope kufananisha wamefanana kweli” alimtoa baba yake wasiwasi huku akimkumbatia baba yake kasha mama yake.

“mh!! Tulikuwa wapweke kweli jamani dada” msaidizi wa kazi za ndani aliyeitwa Fatuma alimwambia Reshmail huku akimkumbatia na kumbusu shavuni

“na huyo mtoto kama mwanao vile hebu kaone” aliendelea Fatuma

“sio kama wa kwangu ila ni wa kwangu humwoni alivyonifanana?” alijibu kimzaha na wote wakacheka kwa pamoja

** ***** *****

Hali ya sintofahamu iliwakumba wale wafanyakazi wa lile jumba (ngomeni) alipokuwa anatunzwa Adam. Mkuu wa ngome hiyo bwana Lwebe alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila mbua alikuwa na ghadhabu kubwa sana,kila kitu kilikuwa shaghala baghala kila mara aliongea kwenye simu hukuakitoa vitisho vikali sana na hata kutishia kuua. Wafanyakazi hawakumwelewa lolote walizitambua hasira za bosi wao huyo ambaye mara chache anazokuwa katika hali kama hiyo humalizia hasira zake kwa kutoa roho ya mtu

“mlete Adam hapa mara moja !!” aliamrisha huku akijikuna ndevu zake kwa kutumia mdomo wa bunduki aliyokuwa nayo

“maskini Adam sijui amekosa nini” alijiuliza aliyekuwa anaenda kumwita. Bila wasiwasi wowote Adam akamfikia Lwebe D kwa ishara ya mkono akamwamrisha kumfuata,pamoja na mabaunsa wawili waliotinga suti nyeusi . lwebe hakuongea neno lolote hadi walipofika kwa nje,tayari kigiza cha saa mbili kilikuwa kimetawala

“mlete na yule mwingine wa nyumba ya chini” alitoa amri nyingine tena baada ya tano walioagizwa wakarejea na mtu mwingine

“we kinyamkera una bahati sana aliyekuleta hapa amesema haujasambaza taarifa zozote mbaya laiti kama ungethubutu ningeiondoa shingo yako sasa hivi. Nakuacha uende tena lakini tambua mtandao wangu upo popote katika nchi hii sasa ole wako uthubutu kunyanyua mdomo wako kutangaza ujinga” aliambiwa yule binti aliyeletwa pale huku akionyeshwa njia ya kutokea

“we kidume kwa jeuri ya bosi wako kujaribu kunidhurumu pesa yangu wakati wewe unakula na kulala bure hapa;lazima nimwonyeshe mimi ni nani na ni wewe utakayeumia” aliongea Lwebe huku akipuliza moshi wa sigara hewani.

**********

Ilikuwa ni mwezi mmoja tangu Bite arejeshwe kwenye ile ngome lakini katika chumba kingine,hakuwa msaidizi wa kazi tena bali mtuhumiwa na hakupata fursa ya kuonana na Adam hata siku moja . siku alipotolewa nje usiku na kwa mahesabu ya miaka mitano ambayo Adam angekaa pale machale yalimcheza,alivyopewa uhuru wa kuondoka hakwenda mbali sana alifika eneo moja kwenye mtaro na kuanza kusubiria ni nini kitatokea japo hakusikia vizuri maneno lakini alisubiri hata vitendo

Mkataba wa miaka mitano alioandikishana Bi.gaudensia na Lwebe wa Adam kuhifadhiwa pale ulikuwa umeisha tayari na miezi mitatu zaidi ilikuwa imepita,suala hilo la kuchelewesha pesa lilimkera sana Lwebe na pia ahadi za uongo kutoka kwa Gaudencia zilichochea sana hasira za Lwebe kufikia hatua ya kuamua kuzipooza kwa huyo Adam aliyehifadhiwa hapo.ni usiku huo alipoamua kwa mkono wake mwenyewe Adam duniani kama kisasi kwa Bi.Gaudensia

“paa!! Paa!!” mlio mkali wa risasi ulisikika na kumzindua Bite ambaye alikuwa amepitiwa na usingizi pale kwenye mtalo,kidogo apige kelele lakini viganja vya mkono wake vikawahi kuuziba haraka sana. Hakusikia hata chembe ya kilio na baada ya dakika kama saba akasikia milango imefungwa

Kwa ujasiri na tahadhari kubwa Bite akajisogeza hadi karibu kabisa na eneo ambalo aliamini hakika ndipo mlio wa risasi umetokea huku kichwani kwake akiwa ana jibu la “nimesahau saa yangu” iwapo atakutana au kushtukiwa na mlinzi,kwa hofu alizurura katika lile eneo dakika tatu bila kuona chochoten”au wameingia nae ndani??” alijiuliza bila kupata jibu

“koh!! Koh!! Alishtuliwa na sauti ya kikohozi nyuma yake,mawazo yake alidhania ni mlinzi eneo lile lakini alipogeukz hakuwa mlinzi tena ni mwili wa binadamu ukiwa chini,hakutambua mara moja yule ni nani hadi macho yake yalipolizoea giza la pale “Adam!!!!!”

“we ni nani??” alijibiwa kwa sauti ya chini sana iliyokuwa inaunguruma kama mnyama anayechinjwa

“Bite mimi jamani Adam”

“ondoka watakuua hao Bite ondoka niache mi nife hapa” alijibu Adam

“hapana Adam usife,usife Adam twende tukamtafute mwanetu Chrstian anatamani sana kukuona,usife Adam tafadhali” Bite alibembeleza

Risasi mbili zilizopenya katika paja lake la kulia zilikuwa zimemsababishia Adam kuvuja sana damu na mbele yake alichokitarajia ni kifo hakuna kinginelakini maneno ya Bite nguvu zilirejea upya kabisa tena kwa kasi”Bite ulijifungua,mtoto wangu yuko wapi? Ni wa kiume au wa kike?” alihoji maswali mfululizo Adam huku akijitutumua kusimama kwa nguvu alizokuwa amezipata

“ni stori ndefu na hapa sio mahali pake tuondoke tafadhali jitahidi kuna hatari kubwa kama unampenda mwanao jitahidi tuondoke” aliongea Bite huku akiuweka mkono wa Adam katika bega lake na kuanza kumkongoja kutoka eneo lile huku (Adam) akitumia mguu mmoja na ule uliojeruhiwa ukiwa juu juu.kutoka pale walipokuwa hadi barabarani haukuwa umbali mrefu sana na walifanikiwa kufika,kwa giza nene lililokuwepo hawakuweza kuonekana na mtu yeyote,nguvu zilikuwa zinamwishia Adam kutokana na kuvuja damu lakini alijikaza kijasiri sana na kuendelea mbele

********* ******* *******

Lwebe na kundi lake baada ya kumpiga risasi mbili Adam waliamini katu asingeweza kunyanyuka kutoka katika eneo lile,na hata angeweza kuinuka hakuwa na pa kwenda hakuujua mkoa huo hata kidogo. Waliingia ndani na kupiga simu kwa Bi.Gaudensia kwamba mtu wake tayari ana risasi mbili mwilini

“msimuue jamani,tafadhali sana kesho naileta pesa yenu mapema kabisa”

“nimechoshwa na ahadi zako mheshimiwa jiandae kuchukua maiti yako siku yoyote utakayotaka utaikuta nimeihifadhi na kama na kuizika nitakusaidia” alijibu kwa ghadhabu kasha akakata simu

Bi Gaudencia akapiga tena

“nakusikiliza”

“basi nielewe kwa leo na hili ni ombi la mwisho tafadhali usimuue kesho asubuhi sana nakuja huko,ninaondoka huku saa nane usiku tafadhali” alibembeleza

“na iwe hivyo atalala nje leo na hata kula hadi utakapokuja

“sawa mkurugenzi” alijibu kwa unyenyekevu Gaudensia

Akini ya Bi.Gaudensia ilifanya kazi haraka haraka akapekua kila kona katika chumba anacholala na mumewe na kwa bahati nzuri kwa akakutana na kadi ya benki ya mume wake ambayo alikuwa akifahamu vizuri kabisa namba zake za siri. Bila kupoteza muda akampigia dereva wake wa siri ambaye huwa anampeleka Iringa naye haraka haraka bila kuhoji akatii amri aliyopewa.bila Reshmail kujua Bi.Gaudensia akaondoka majira saa saba usiku,nafsi ilikuwa ikimuhukumu juu ya baya lolote litakalomkuta Adam “damu ya Adam ipo juu yangu”

“naenda kwa rafiki yangu ameugua ghafla “ mama Reshmail alimuaga mlinzi wa getini

“sawa bosi” alijibu mzee yule wa makamo huku akifunga geti baada ya mama kuwa ametoka nje

Kwa kasi ya ajabu gari iliondoka jijini Dar-es-salaam kwa kuwa ilikuwa usiku sana vizingiti vya watu wa usalama pamoja na foleni havikuwepo sana hivyo dereva alikimbiza gari kwa kadri ya uwezo wake. Breki ya kwanza ilikuwa ni katika benki ya C.R.D.B maeneo ya Ubungo ambapo mama Reshmail alishuka na kuvuta pesa kutoka katika akaunti ya akiba ya mzee Manyama

Badala ya masaa matano kwa gari binafsi kufika Iringa walitumia masaa matatu pekee

“mh!! Huku napo kijijini kweli huyo nae sijui ni mgonjwa sasa usiku huu atapata wapi lifti ya gari” mama Reshmail alimwambia dereva wake alipoona watu wawili wakisimamisha gari

“ah!! Ndo maisha ya Tanzania yalivyo” alijibu dereva huku akiongeza zaidi mwendo wa gari hadi wakaifikia ngome ya vigogo waliyokuwa wakiifuata


** ** *****

Magari makubwa ya mizigo yatokayo Morogoro kwenda Zambia na Malawi ndiyo yaliyotoa msaada kwa Bite na Adam ambapo Bite alijitambulisha kama mke wa Adam na kwamba wamevamiwa na majambazi na mumewe (Adam) amepigwa risasi. Laiti kama madereva wangekuwa watanzania kwa jinsi walivyo waoga katu wasingewapandisha wawili hawa lakini wakongomani wale ambao vita kwao ni jambo la kawaida waliwachukua Adam na Bite hadi Iringa mjini walipowaacha jirani kabisa na hospitali ya rufaa.

“bila RB hatupokei mgonjwa wa aina hii” alisema muuguzi wa kike wa hospitali ile wakati Bite anajieleza.ni kweli yule muuguzi(nesi) alikuwa na haki zote za kupingana na ujio ule kwani hali aliyokuwa nayo Adam ilihitaji taarifa za polisi kwanza

“haa!!! Mama Christian,ni wewe hata siamini au nakufananisha?” wakati Bite akijiegemeza kwenye ukuta huku akiwa amekata tama alishangaa kutambulika kwake na nesi yule

“Mungu wangu mama wawili jamani!!!” baada ya kumkazia macho naye Bite akamtambua yule nesi kuwa waliwahi kufanya nae biashara katika soko la Uyole Mbeya na pia alikuwa jirani yake pale alipokuwa anaishi,ulikuwa mshangao mkubwa sana

“ehe!! Kulikoni tena ndugu yangu yamekukuta yapi tena mwenzangu?” alihoji nesi huku akiwa amechangamka sana safari hii

“ni makubwa sana,lakini ningeupata msaada wako kwanza kwa mume wangu ndio tungeongea vizuri shoga” alijibu Bite akiwa na matumaini tele

“ondoa shaka shoga huduma mnaipata sasa hivi tena huduma bora,daktari tunaheshimiana naye sana na pia ni shemeji yangu” nesi aliongea hayo huku wakisaidiana kumwingiza Adam ndani ya chumba cha wagonjwa,hapakuwa na maswali mengi,undugu ulitawala pale. Adam akafanyiwa upasuaji mdogo wa kuondoa risasi katika ambao haukuchukua hata hata nusu saa damu na maji pia vikaongezwa katika mwili wake uliokuwa dhaifu sana.kufikia majira ya saa kumi na moja alfajiri Adam alikuwa amepata nafuu kubwa na aliweza kutembea japo kwa kuchechemea

“shoga nikueleze wazi tu kwamba sisi pa kufikia hapa Iringa mimi na mume wangu hatuna! Tangu niondoke ghafla niliacha sijalipa kodi nina uhakika chumba sio changu tena kwa hiyo pa kwenda hatujui” Bite alimweleza hayo mama wawili baada ya kuwa amemsogeza pembeni ili mtu mwingine asiweze kusikia

“ondoa shaka Bite miim kwangu pana nyumba kubwa tu!! Nimejengewa na mnyakyusa mmoja,nimemweka kwenye kiganja kwangu mimi hasikii,haoni wala hasemi,ni kaka yake na huyu daktari we mwenyewe si umeona alivyowashughulikia haraka” kwa sauti ya chini kabisa nesi alijibu

Wote watatu katika teksi wakaongozana hadi nyumbani kwa nesi ni kweli nesi hakuwa na chembe ya utani hata kidogo nyumba ile ilikuwa kubwa sana na haikuwa haki kukaliwa na watu wawili pekee vilikuwa ni vyumba sita pamoja na sebule

“karibuni! Karibuni sana! Nesi aliwakaribisha walipofika nyumbani kwake.

“asante sana ndugu yangu ama kweli ishi na watu uvae viatu” alisema Bite kwa upole sana

“usijali Bite tumeishi vizuri,hatukuwahi kugombana hata siku moja,tumetwishana matenga ya nyanya kwa nini sasa nishindwe kukutendea wema!!!” nesi alimtoa hofu Bite

Chumba walichopewa kilikuwa kikubwa cha kuwatosha kabisa,kitanda cha tano kwa sita kilikuwa saizi yao kabisa. Adam alishangazwa sana na wema huo wa nesi lakini mshango wake uliongezeka maradufu baada ya kukutana na mume wa nesi siku ambayo walikuwa wakitambulishwa kwake kama shemeji zake yaani ndugu zake Bite.mzee huyu wa kinyakyusa aliyeitwa Gwakisa ni kama heshima ilipitiliza na kuwa kama anawanyenyekea wawili hawa. Adam alihudumiwa na yule daktari kana kwamba alikuwa ni mgonjwa wa kisukari au alikuwa ni mtoto wa mfalme,Adam alipata farijiko kubwa sana kuishi pale

Bite kama kawaida alikuwa mwanamke wa kujituma sana,ndani ya wiki moja tayari alikuwa amepata kazi ya ndani katika nyumba nzuri waliyoishi wanafamilia watatu,mwanaume na mke pamoja na mtoto wa kama miaka mitatu wa kike aliyekuwa anasoma shule ya awali


***** ****** ****** ******

“bite mama!!”

“bee mama”

“mpeleke mtoto shule halafu baadaye mpeleke pale zahanati akapimwe jana usiku amekohoa sana” ilikuwa sauti ya Eveline akimpa maelekezo Bite ambaye alikuwa mfanyakazi wake mpya na wa kwanza wa ndani ya nyumba yake na mchumba wake. Ratiba ya Bite ilikuwa ni kazi kuanzia asubuhi ya saa mbili ambapo alikuwa akimpeleka Loyce {mtoto wa kaka yake Benny} shuleni na kisha akirejea anaandaa chakula cha mchana kwa siku ambayo Benny hurudi nyumbani mchana na baada ya hapo humfuata Loyce shuleni,kisha maandalizi ya chakula cha jioni na majira ya saa kumi na mbili huaga na kuondoka,ilikuwa kazi ambayo haikumtoa jasho Bite na malipo ya shilingi laki moja kila mwezi yalimtosheleza kabisa kupanga chumba kidogo walicholipia shilingi 15000 kwa mwezi

“tunashukuru sana kwa ukarimu wenu bwana na bibi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom