Habiba Kawawa afariki Dar

Habiba ni mmoja tu ya wanawake maelfu wanaopoteza maisha kutokana na uzazi hapa Tanzania na Africa kwa ujumla,Tanzania ukibeba ujauzito yaani ni riski ya kufa wewe mwenyewe wakati unapotegemea kukipa maisha kiumbe kilichopo tumboni,yaani ni mguu mmoja kaburini.Sijui hili tatizo litaisha lini wenzetu wamefanikiwa kulitatua.
Pumzika kwa amani Habiba.
 
RIP HABIBA!
This is yet another time to reflect on maternal mortality in this country!
MIMI WOS kama mwanamke....najua kabisa kuwa, Mungu alipomuumba mwanamke na kumpa jukumu la kushiriki uumbaji na kuleta viumbe duniani, alimpa adhabu moja tu - kuumwa uchungu wakati wa kuzaa lakini siyo kufa!

Tujiulize- kama kodi zetu zingetumika kwa vipaumbele sahihi, wamama wengi wangezaa salama! Ni aibu kwa nchi yetu kutokushtuka pale wakina mama wanavyozidi kupoteza maisha kwa vile ati wanatekeleza majukumu yao ya kijinsia/jinsi.

Nchi za wenzetu waliondelea, wanawake kufa kwa uzazi ni kitu kisicho cha kawaida.Huku kwetu, mwanamke anapokaribia siku ya kuzaa huona kifo kikimnyemelea..nakumbuka kupitia hofu hii ya kutisha.

Tumwombee ,mwenzetu aliyetangulia mbele ya haki, MUNGU AMPE HURUMA YA PEKEE NA AMSAMEHE MAKOSA YAKE, AMLAZE PEMA PEPONI - AMEN!

WoS ni kweli kabisa katika nchi za wenzetu vifo vya akina mama wajawazito ni vichache mno ukilinganisha na Tanzania. Hata kwetu hali ingeweza kuwa hivyo lakini Serikali zetu zilizo madarakani hasa hizi za miaka ya karibuni hazikuona/hazioni umuhimu wowote wa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito na matokeo yake wengi wataendelea kufa kila mwaka. Miezi michache iliyopita Naomi Campell alipotembelea chumba cha akina mama waliotoka kujifungua aliangusha machozi kutokana na hali ya kusikitisha aliyoiona ya chumba kidogo cha kulala mama mzazi mmoja wamerundikwa (kama magunia ya mkaa) akina mama 20 au zaidi na wengi wakishare kitanda kimoja au tandiko moja kati ya watano au zaidi.
 
Mkuu naona umebadili jina!

Ndugu yangu anambwe mbwe sana SteveD kuwa SteveDII

Huu ni umasikini wa hali ya juu Maternal And Child Mortality ni moja wapo ya ajenda kwenye Millennium Dev Goals kupunguza. Priority zetu ziko kwenye kukuza ufisadi na kusahau mambo ya msingi. I do not know if Tanzania we are progressing in a right way.

Poleni sana wafiwa na Mungu ampumzishe Habiba mahali pema peponi.
 
Poleni wafiwa kwa msiba uliokuja siku chache tu baada ya kumpoteza mzee wetu Simba wa vita! Mungu awe nasi wakati huu mgumu wa maombolezo!
 
Back
Top Bottom