Gharama za kuagiza gari, kodi za TRA, usajili hadi kumfikia mtumiaji

merckme

New Member
Mar 29, 2024
2
3
Habari za mida hii wanajf.
Kama kichwa kinavyosomeka.

Kuna jambo huwa najiuliza kwenye suala zima la kuagiza gari kwa kutumia beforward, tcv, sbt, n.k. Nikipitia kwenye websites zao unakuta kwenye bei ya gari ni Tsh. 5,000,000/- na kwenye bei ya jumla sehemu ya Clearing & forwarding kwa port ya Dar ni 11,000,000/- au 12,000,000/- na ni RORO.

Maswali yangu ya ufahamu ni je,
1. Hiyo 11,000,000 au 12,000,000 ya kwenye C&F ndiyo bei ya mpaka gari inafika mikononi mwa mhusika pamoja na kodi zote?

2. Kama siyo kwenye namba 1 je, range ya kodi au gharama zote ikoje kwenye kuagiza lolote kwa kutumia hiyo price ya kununua na hiyo ya c&f).

Naomba kufahamishwa kwa wenye uzoefu kwenye hili. Nimetafuta calculator ya TRA naona kama haifanyi kazi.

Mfano wa gari na bei ni kama inavyooneka kwenye picha. Hii nimetumia kama mfano tu wa gari ya 2013
CX 5.jpg
CX 5_2.jpg
 

Attachments

  • CX 5.jpg
    CX 5.jpg
    456.9 KB · Views: 8
Hiyo Mazda CX-5 ambayo CIF( kwenye hiyo pesa itaenda kwenye manununuzi ,ukaguzi,usafirishaji)
Kimbembe kitakuja kwenye kulipia ushuru huku bongo ni zaidi ya milioni 8-9
 
Link ya TRA inafanya kazi vyema tu sema sometimes huwa inakuwa down

Ila usiikatie tamaa ukijaribuida mwengine inakubali

Cha msingi unahifadhi taarifa kama hivyo kisha unafanya yako
 
Habari za mida hii wanajf.
Kama kichwa kinavyosomeka.

Kuna jambo huwa najiuliza kwenye suala zima la kuagiza gari kwa kutumia beforward, tcv, sbt, n.k. Nikipitia kwenye websites zao unakuta kwenye bei ya gari ni Tsh. 5,000,000/- na kwenye bei ya jumla sehemu ya Clearing & forwarding kwa port ya Dar ni 11,000,000/- au 12,000,000/- na ni RORO.

Maswali yangu ya ufahamu ni je,
1. Hiyo 11,000,000 au 12,000,000 ya kwenye C&F ndiyo bei ya mpaka gari inafika mikononi mwa mhusika pamoja na kodi zote?

2. Kama siyo kwenye namba 1 je, range ya kodi au gharama zote ikoje kwenye kuagiza lolote kwa kutumia hiyo price ya kununua na hiyo ya c&f).

Naomba kufahamishwa kwa wenye uzoefu kwenye hili. Nimetafuta calculator ya TRA naona kama haifanyi kazi.

Mfano wa gari na bei ni kama inavyooneka kwenye picha. Hii nimetumia kama mfano tu wa gari ya 2013
View attachment 2948267View attachment 2948268
Kwa kifupi tu ni kwamba hiyo gharama ya wewe kuiagiza gari toka japani mpaka dar bandarini. Hesabu rahisi sana kujua kodi ya gari yako chukuwa hiyo milioni 11 x2 = 20 hivo mpaka gari kukufikia mkononi itakuwa milioni 20
 
Kama hutaki kuingia TRA kucheki we zidisha mara 2 hiyo CIF. Ukija baadae kuangalia hutakuwa mbali sana na uhalisia.
 
Back
Top Bottom