Gharama ya nyumba moja ya BoT, yatosheleza madawati 23,000!!

TANURU

Senior Member
Jan 13, 2010
162
6
Naomba kumuuliza Mh. Waziri Mkuu aibu hii ya shule zetu za msingi kukosa madawati na watoto wetu kusoma wakiwa wamekaa chini itakwisha lini?

Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 01/02/2010 ukurasa wa 8 kuna habari isemayo "UKEREWE YAHITAJI MIL. 713/= KUTENGENEZA MADAWATI"

Taarifa hiyo inaendelea kuonyesha kuwa jumla ya shilingi milioni 713.8 zinahitajika kutengeneza madawati 23,700 ili kutosheleza mahitaji katika shule zote za msingi 117 zilizopo wilayani Ukerewe. Habari hiyo inaeleza zaidi kuwa, kati ya wanafunzi wote 78,281 wa shule za msingi wilayani Ukerewe, wanafunzi wapatao 42,400 (53.5%)wanakaa chini. Kwa maneno mengine ni kuwa katika kila wanafunzi 100 wa shule za msingi wilayani ukerewe wanafunzi 54 wanasoma wakiwa wamekaa chini. Natumaini hali ya Ukerewe inawakilisha hali halisi ya shule zetu za msingi hapa nchini. Kwa mantiki hiyo, karibu wanafunzi milioni 5 wanasoma wakiwa wamekaa chini hapa nchini katika shule zetu za msingi.

Mh Waziri Mkuu bajeti ya Ofisi yako kwa mwaka huu wa fedha pekee (2009/2010) ni zaidi ya shilingi trillioni 2.63.

Tunaomba sana aibu hii ifikie mwisho na tuwe wakweli na waungwana katika matumizi yetu na pia tufanye kila njia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuwawezesha watoto wetu kusoma katika mazingira yanayojali utu wa mwanadamu.
 
Tanuru,
Hii hali ya Mtoto/Watoto wa Wakulima na wavuja jasho wengine kufikia mabadiliko ya wao kutambuliwa kuwa wana haki ya HISA katika hiyo Keki/Mkate wa taifa hili, kuwa angalau wanastahili DAWATI NA KITI cha kukali akiwa shule itakuwa ngumu sana sana na tena sana kuifikia kama tutaendelea kuwa na viongzi na watumishi wa serekali, wenye mawazo yanayofanana na yanayokubaliana na yale ya Gavana Ndulu wa BOT ya kutumia BILIONI NA USHEE kwa kajumba kamoja kwa fahari usizoweza kuzipatia kiwango cha malinganisho kama Bwawa la kuogelea!!! Ikiwa mtu mwenye darasa na anejua mambo ya uchmi na mgawanyo wa hesabu zake anashindwa kuelewa, je Mkulima, Waalimu wa watoto wetu, Askari wetu wanaolinda Doria mitaani kutwa kucha na Wadau wengine ambao asilimia kubwa wanaangukia katika kundi hilo la Walalahoi wataweza kuelewa?? Wakati fulani Hayati Mwl. Nyerere alisema "Kupanga ni kuchagua"Yaelekea waliopata Fursa wamchagua kujijenga VIJUMBA VYA FAHARI na kujipangia MABWAWA YA KUOGELEA. Wachilia mbali magari ya kifahari na ubadhirifu wa kila namna na aina ambao umeendelea na kuendelezwa chini ya Serekali ya CCM. JE SISI TUSIO NA FURSA YA YA MAAMUZI JUU YALOLOTE LILE, HATA ILE KURA YANGU IMSHAFANYIWA MAAMUZI!! HISA za KEKI/MKATE wa Taifa hili tutaambulia lini????
 
CCM oyeeeee! Zidumu fikira sahihi za mafisadi.....

Naomba kumuuliza Mh. Waziri Mkuu aibu hii ya shule zetu za msingi kukosa madawati na watoto wetu kusoma wakiwa wamekaa chini itakwisha lini?

Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 01/02/2010 ukurasa wa 8 kuna habari isemayo "UKEREWE YAHITAJI MIL. 713/= KUTENGENEZA MADAWATI"

Taarifa hiyo inaendelea kuonyesha kuwa jumla ya shilingi milioni 713.8 zinahitajika kutengeneza madawati 23,700 ili kutosheleza mahitaji katika shule zote za msingi 117 zilizopo wilayani Ukerewe. Habari hiyo inaeleza zaidi kuwa, kati ya wanafunzi wote 78,281 wa shule za msingi wilayani Ukerewe, wanafunzi wapatao 42,400 (53.5%)wanakaa chini. Kwa maneno mengine ni kuwa katika kila wanafunzi 100 wa shule za msingi wilayani ukerewe wanafunzi 54 wanasoma wakiwa wamekaa chini. Natumaini hali ya Ukerewe inawakilisha hali halisi ya shule zetu za msingi hapa nchini. Kwa mantiki hiyo, karibu wanafunzi milioni 5 wanasoma wakiwa wamekaa chini hapa nchini katika shule zetu za msingi.

Mh Waziri Mkuu bajeti ya Ofisi yako kwa mwaka huu wa fedha pekee (2009/2010) ni zaidi ya shilingi trillioni 2.63.

Tunaomba sana aibu hii ifikie mwisho na tuwe wakweli na waungwana katika matumizi yetu na pia tufanye kila njia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuwawezesha watoto wetu kusoma katika mazingira yanayojali utu wa mwanadamu.
 
Kwako Dr. Slaa,

Kwa kuheshimu mchango wako mkubwa kwa maendeleo ya nchi yetu na ukuaji wa demokrasia, naomba nikuombe katika BUNGE LIJALO uandaye na kuwasilisha HOJA BINAFSI kuhusu KILIO CHETU HICHO HAPO CHINI SISI WATANZANIA.
-----------------------------------------------------------------------

MTOTO WA MKULIMA ( Mh. MKPP) AIBU HII MPAKA LINI???

"""Naomba kumuuliza Mh. Waziri Mkuu aibu hii ya shule zetu za msingi kukosa madawati na watoto wetu kusoma wakiwa wamekaa chini itakwisha lini?

Katika gazeti la Tanzania Daima la leo tarehe 01/02/2010 ukurasa wa 8 kuna habari isemayo "UKEREWE YAHITAJI MIL. 713/= KUTENGENEZA MADAWATI"

Taarifa hiyo inaendelea kuonyesha kuwa jumla ya shilingi milioni 713.8 zinahitajika kutengeneza madawati 23,700 ili kutosheleza mahitaji katika shule zote za msingi 117 zilizopo wilayani Ukerewe. Habari hiyo inaeleza zaidi kuwa, kati ya wanafunzi wote 78,281 wa shule za msingi wilayani Ukerewe, wanafunzi wapatao 42,400 (53.5%)wanakaa chini. Kwa maneno mengine ni kuwa katika kila wanafunzi 100 wa shule za msingi wilayani ukerewe wanafunzi 54 wanasoma wakiwa wamekaa chini. Natumaini hali ya Ukerewe inawakilisha hali halisi ya shule zetu za msingi hapa nchini. Kwa mantiki hiyo, karibu wanafunzi milioni 5 wanasoma wakiwa wamekaa chini hapa nchini katika shule zetu za msingi.

Mh Waziri Mkuu bajeti ya Ofisi yako kwa mwaka huu wa fedha pekee (2009/2010) ni zaidi ya shilingi trillioni 2.63.

Tunaomba sana aibu hii ifikie mwisho na tuwe wakweli na waungwana katika matumizi yetu na pia tufanye kila njia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuwawezesha watoto wetu kusoma katika mazingira yanayojali utu wa mwanadamu."""".

Hatuhitaji zaidi ya shilingi bilioni 75 ili kulimaliza tatizo hili. Fedha hizi ni chini ya asilimia 2.9% ya bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka huu wa fedha wa 2009/2010.
 
Inasikitisha na kutia huruma sana.
mimi ndo maana sichangiagi maendeleo kupitia hizi serikali za mitaa, wanatubebesha mizigo mizito sana wakati wao wananawiri maofisini kwao, aibu sana kwakweli.
 
Haya mambo hata tukisema tunamuachia mungu kama wasemavyo wengi wetu sidhani kama ni jawabu, tunahitaji kutafuta njia mbadala ya kupambana na hili.
 
Ukiwauliza wakuu wa CCM NA SERIKALI watakwambia bado tunajipanga na tuko katika mchakato.....HII MICHAKATO IFIKIE MWISHO NA NAFASI YAKE ICHUKULIWE NA VITENDO.
 
Mkuu TANURU, kwa joto, munkari na vugu vugu la maendeleo ulilo nalo WEWE emechangia madawati mangapi katika sehemu wewe unayotoka?
Watoto ni wale wale na usiwe a mere lip server!!
 
Mkuu TANURU, kwa joto, munkari na vugu vugu la maendeleo ulilo nalo WEWE emechangia madawati mangapi katika sehemu wewe unayotoka?
Watoto ni wale wale na usiwe a mere lip server!!

Lole Gwakisa,


Jana na leo asubuhi mimi na rafiki yangu mmoja, ambaye nilifanikiwa kumshawishi siku ya Jumapili, tumechangia jumla ya shilingi 120,000 kwa ajili ya shule moja ya msingi. Fedha hizi ni kwa ajili ya mifuko 10 ya cement kwa ajili ya kuweka sakafu katika moja ya madarasa hapo shuleni.


Lengo langu ni kuichangia hiyo shule angalau shilingi elfu 50 kila mwezi kwa ajili ya maendeleo ya taaluma. Pia nimeanzisha mpango wa kuwaomba rafiki zangu waniunge mkono kadri ya uwezo wao. Nategemea kukusanya angalau shilingi laki tatu kila robo mwaka toka kwa marafiki zangu kwa ajili ya maendeleo ya taaluma katika hiyo shule, hasa kwa masomo ya Hisabati, Sayansi na Kingereza.
 
Lole Gwakisa,


Jana na leo asubuhi mimi na rafiki yangu mmoja, ambaye nilifanikiwa kumshawishi siku ya Jumapili, tumechangia jumla ya shilingi 120,000 kwa ajili ya shule moja ya msingi. Fedha hizi ni kwa ajili ya mifuko 10 ya cement kwa ajili ya kuweka sakafu katika moja ya madarasa hapo shuleni.


Lengo langu ni kuichangia hiyo shule angalau shilingi elfu 50 kila mwezi kwa ajili ya maendeleo ya taaluma. Pia nimeanzisha mpango wa kuwaomba rafiki zangu waniunge mkono kadri ya uwezo wao. Nategemea kukusanya angalau shilingi laki tatu kila robo mwaka toka kwa marafiki zangu kwa ajili ya maendeleo ya taaluma katika hiyo shule, hasa kwa masomo ya Hisabati, Sayansi na Kingereza.

haya ndiyo maneno; naomba tuwasiliane aisee naweza kukuunga mkono vile vile kwa kadiri niwezavyo.
 
Ukiwauliza wakuu wa CCM NA SERIKALI watakwambia bado tunajipanga na tuko katika mchakato.....HII MICHAKATO IFIKIE MWISHO NA NAFASI YAKE ICHUKULIWE NA VITENDO.

Haiwezekani kufikia mwisho kwa uongozi huu wa sisiem labda ziraele awachukue wote hao kwa mkupuo.
 
Lole Gwakisa,


Jana na leo asubuhi mimi na rafiki yangu mmoja, ambaye nilifanikiwa kumshawishi siku ya Jumapili, tumechangia jumla ya shilingi 120,000 kwa ajili ya shule moja ya msingi. Fedha hizi ni kwa ajili ya mifuko 10 ya cement kwa ajili ya kuweka sakafu katika moja ya madarasa hapo shuleni.


Lengo langu ni kuichangia hiyo shule angalau shilingi elfu 50 kila mwezi kwa ajili ya maendeleo ya taaluma. Pia nimeanzisha mpango wa kuwaomba rafiki zangu waniunge mkono kadri ya uwezo wao. Nategemea kukusanya angalau shilingi laki tatu kila robo mwaka toka kwa marafiki zangu kwa ajili ya maendeleo ya taaluma katika hiyo shule, hasa kwa masomo ya Hisabati, Sayansi na Kingereza.

Mkuu jinsi ulivyolichukulia suala hili naona kweli una uchungu na nji hii.
 
Back
Top Bottom