Gazeti la Tanzanite: CHADEMA, yajiandaa kwenda Ujerumani na Marekani mwishoni mwa mwaka: Lengo ni kuomba msaada wa kupambana na Serikali

View attachment 849963
Viongozi Waandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wapo katika maandalizi ya kufanya Ziara kabla ya mwishoni mwa mwaka huu 2018 kwenda katika Nchi za Ulaya zikiwemo Ujerumani na Scandinavia, pamoja na Marekani, ikiwemo Bunge la Congress kwa lengo la kuomba msaada dhidi ya masuala ya kisiasa na hali yao dhidi ya Serikali.
Viongozi hao wanakwenda kudai kuwa, wanaonewa, hawana haki dhidi ya Nchi yao, wananchi na wabunge wao. Vilevile, watalalamikia juu ya Ukanda Imani was demokrasia ndani ya Nchi. Aidha, watalalamikia juu ya vitisho na usalama wa uongozi wao, nafasi zao na mwenendo wa uchaguzi kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2020.

Je, CHADEMA wakienda huko watapata nafasi ya kuongea kwenye Bunge la Congress? Endapo wataipata hiyo nafasi, nini athari zake kwa Siasa za Tanzania hasa kuelekea 2020. Je, Marekani atataka kutulima tena kwenye misaada? Je, unadhani Magufuli anaweza kuogopa ghadhabu za Marekani, Ujerumani na Scandinavia (Norway, Sweden, Finland, Denmark na Iceland)? Je, Norway (Statoil/Equinor) na Nchi nyingine yanakotokea Makampuni ya gesi, wanatuvizia baada ya mwenendo wa kobe katika makubaliano ya kujenga LNG nchini?

View attachment 849962
najua kwenye hili mtakuwa kimbelembele kama Mmbwa jike aliona chatu

kabla hamjafanya huu upuuzi wenyu. anzeni kuchunguza nani aliyetoa cctv camera kwenye tukio la kumuua MH TUNDULISU.
Mnatanguliza makalio mbelee kwa vipeperushi vya kipuuzi.
mmepewa msaada wa kuwasaidia kumpata mhalifu na kundi lake mmegoma katakata mpaka mkamalizia kuwa JALADA LA ISHU YA LISU LIMEFUNGWA hii inadhihirisha umafia wenyu ulivyo wa kizamani mnajulikana msiojulikana kwa ujingahuu wa kujifanya hamtaki kuchunguza wala kusaidiwa.
kama kweli mnataka kumjua mhusika na kundi lake hebu waruhusuni SCOTLAND YARD CIA KGB nk waje kuwasaidia mtokwe na hii aibu kujifanya wajuaji kumbe MIZOMBI TU. mfyuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu
 
Hujanielewa, nimesema sio magazeti ya kusomwa na mtu mwenye akili timamu. Kama unayasoma wewe ni sawa.
Uhuru+Tanzanite pamoja Jamvi la habari ni magazeti yenye habari za ukweli na uhakika na simulizi zenye kusisimua.
 
Mungu mbariki Jenerali Mbowe na CHADEMA kwa ujumla. CHADEMA ni kiboko ya CCM.

Karibu nyumbani Rais wetu ajae comrade Tundu Marshal Antipas Lissu uje uwatoe makamasi hawa pimbi
 
Ni upigaji ule ule. Uingereza iliipatiia Tanzania paund milioni 300 miezi michache iliyopita. Hao hao uende kuwaambia kuwa unaonewa kana kwamba kinachoendelea nchini mwako hakijulikani.

Mzungu ndio aliyetengenea google map. Anashindwa vipi kujua yanayoendelea nchini mwetu?.

Kaka wa Hai ni mtoto wa downtown, anajua sana namna ya kupiga fedha ndefu ya maana.
 
Mkuu Mgambilwa ni mntu , with due respect, acha hii tabia ya kutuletea habari kwa njia hii. Kama umenunuliwa scanner ya kutuletea mada zinazokupendeza na kutoka magazeti yanayokupendeza, jua kuwa tupo unaotukwaza. Uwe unaleta hata habari za maendeleo kama uwekezaji na kilimo au hata elimu. Acha kila siku kuleta 'vihabari vya kishabiki'.
umenena mkuu,kutuletea mada za kwenye vijiwe vya kahawa humu ni kuonyesha ni jinsi gani njaa yetu ya matumbo inaweza kutupeleka to the lowest end ya akili zetu;nchi yetu inahitaji chachu ya maendeleo kama sasa kuna fursa ya kufungua biashara na UK(elewa hii nchi inajitoa kutoka EU) ,PM wao yupo Afrika kipindi hiki akitafuta masoko ya kuuza na kununua bidhaa zao ,na uzuri atakuwa hapo Kenya sasa sijui serikali yangu imefanya mipango gani ya kutuma ujumbe wetu wa kibiashara ili kuonana na PM ili nasi tupate fursa ya kuuza bidhaa zetu UK,tuelewe kuwa bila ya kuwa na foreign money itatugharimu mno kununua bidhaa tunazozinunua kwa fedha ya kigeni(oil,medicines etc etc)na tuelewe matunzo ya ndege yetu mpya ni gharama kubwa mno.
 
Uhuru+Tanzanite pamoja Jamvi la habari ni magazeti yenye habari za ukweli na uhakika na simulizi zenye kusisimua.
Kama ni za kweli pitia gazeti la leo la Uhuru uone wanavyoomba kumradhi kwa kuchapisha habari za uongo ambazo wewe kwako ni za kweli na za kusisimua.

Narudia, magazeti ya Uhuru, Tanzanite, jamvi la habari sio magazeti ya kusomwa na mtu mwenye akili timamu
 
Mkuu Mgambilwa ni mntu , with due respect, acha hii tabia ya kutuletea habari kwa njia hii. Kama umenunuliwa scanner ya kutuletea mada zinazokupendeza na kutoka magazeti yanayokupendeza, jua kuwa tupo unaotukwaza. Uwe unaleta hata habari za maendeleo kama uwekezaji na kilimo au hata elimu. Acha kila siku kuleta 'vihabari vya kishabiki'.
Una hakika kila matapishi unayoandika humu JF huwa yanapendeza kila mtu!?
Acha Unafiki. Jifunze kuheshimu mawazo tofauti. Sio kila hoja au jambo likupendeze, kwani Wewe umekuwa mungu mtu!?
Mwanasheria gani usiye na Nidhamu!?
Pathetic Crooked Lawyer!
 
Back
Top Bottom