nzalendo
JF-Expert Member
- May 26, 2009
- 10,684
- 9,862
Things do change...Habari wapendwa. Ni wazi dunia inapigana kuhakikisha gari za umeme ndio zinatawala kwa hoja ya kuwa rafiki na mazingira. Licha ya yote bado hizi gari ni changamoto hasa inapopata damage.
Tuchukue mfano kesi ya hivi karibuni huko Vancouver, mmiliki wa Hyundai Ioniq 5 ya mwaka 2022 alipata ajali iliyopelekea cover plate ya battery pack kubonyea na kuharibu battery lakini body haikuwa hata na mchubuko. Gari hii thamani yake ni $41,245 mpaka $55,745 ikiwa mpya lakini Bill ya kubadilisha betrii alipewa $60,000. Aliporipoti katika shirika la bima la ICBC(Insurance Corporation of British Columbia) waliiandika gari kama haitengenezeki kwa sababu matengenezo yamezidi thamani ya gari.
Professor mmoja huko Marekani anasema, " hizi gari watu wanazinunua bila kujua ukweki lakini thamani ya battery pekee ni 30% ya bei ya gari, kwamba kama utatoa milioni 100 basi battery ikifa andaa milioni 30+ au zaidi kwani huenda ukaambiwa ubadili na battery management system. Watu mliowahi kununua injini za gari za mafuta nazani mtaelewa hapa kwenye battery na engine kipi nafuu.
Tukiangalia Tesla Cyber truck baytery yake inauzwa $20,000 lakini bado kuna battery la $16000 linajulikana kama range extender au reserve. Jumla ya battery pekee ni $36,000 zaidi ya milioni 80 za kitanzania na unatakiwa baada ya miaka 10 hadi 20 ubadili battery kulingana na matumizi yako.
Hitimisho: Hizi gari sizioni Afrika leo wala kesho kutwa.
Hata simu za mkononi zilipoingia zilikuwa aghali.....
Ngoja tumsubiri Mchina