Gaddaffi na Kashfa

Exaud J. Makyao

JF-Expert Member
Nov 30, 2008
1,518
22
Inasemekana kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Rais Gaddaffi, amekumbwa na kashfa ya mahusiano ya kimapenzi na mama mmoja wa ukoo wa kifalme huko Uganda.Habari hizi ni kwa madai ya gazeti liitwalo Red Paper huko Uganda.
Wana JF fuatilieni tetesi hizi na kuweka wazi kinachojiri.
 
ni Red Pepper, pilipili kali!kesi imefikishwa mahakamani, Red Pepper walipewa 24 kuomba radhi wakagoma.

jamaa wanadai wana ushahidi wa kutosha, Gadaffi awasubiri mahakamani.
 
Inasemekana kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Rais Gaddaffi, amekumbwa na kashfa ya mahusiano ya kimapenzi na mama mmoja wa ukoo wa kifalme huko Uganda.Habari hizi ni kwa madai ya gazeti liitwalo Red Paper huko Uganda.
Wana JF fuatilieni tetesi hizi na kuweka wazi kinachojiri.

Samahani,
Ni gazeti la RED PEPPER.
 
Gadaffi atamweza wapi mwanamke wa Kiganda jinsi wanavyojua mapenzi???

Naona babu huyu atulie tu huko Libya na waschana wakiarabu!

Mambo ya kiganda hayawazi!
 
Huenda hizi ni njama za Museven za kumchafulia jina uhusiano wao sio mzuri kwa sasa.Bw.Habib Kagimu ana more influence than president in Uganda and Mr.president is not happy about that.The fact is he can not even push Mr.Kagimu out of his circle so he use a newspaper.

SAHIBA.
 
I guess the dude has 'true' liking to Buganda blood... isn't he the only one who helped Idi Amin fight Tanzania?
 
Hii habari niliisoma mwanzo wa mwaka jana, wanamzungumzia Kemigisha wa Tooro royal family kama sikosei.
 
Wakuu,

Mimi nafikiri jibu zuri juu ya kashfa hii, kama ni kweli, ni lile alilotoa Rais Obama wa Marekani. Alipoulizwa, mbona wengi katika wale uliowateua wana kashfa za kodi na/au mambo mengine?

Akasema, "nikitafuta kuwateua wasiokuwa na kashfa ya aina yoyote, nitakuwa sina wa kumteua."

Kila mwanamume mwenye afya njema haachi kummezea mate mwanamke aliyekuwa halali yake. Kuwa alimwendea au hakumwendea haya ni msuala nyeti, si lazima wote wajue. Wanasema, "usilolijua ni usiku wa kiza."
 
Back
Top Bottom