Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,361
- 2,734
Kwa muda mrefu sasa Jamii Forums imeshajulikana na sifa kemkem imepata. Lakini kwa kiasi kikubwa inajulikana sana kwa wasomi na wachache wenye uelewa wa masuala ya internet.
Kwa utafiti nilioufanya japo sio rasmi, nimegundua kuwa tunapokaa sehemu na kuanza kuongea mambo mbalimbali, tunaombwa source, na kila tunapotaja Jamii Forums, wengi na ambao tunawapigania hushangaa na wengine hutaka waione hiyo jamii forum wakidhani kuwa ni gazeti. Sasa ndo nikapata wazo kuwa kazi nzuri tunayoifanya kuipigania nchi yetu, si vibaya na walengwa wakalijua hili. Hivyo mawazo yangu ni kuwa viranja waandae Business Plan nzuri ikiwa na lengo la kuanzisha gazeti. Baadae tukijua gharama za kuanzisha hilo gazeti, kila mwana JF mwenye moyo atajua achangie kiasi gani kwa ajili ya kufanya kitu fulani.
Gazeti hili la Jamii Forums litasomwa kwanza na sisi wadau na ndio itakuwa njia mojawapo ya kuichangia JF kwa njia rahisi. Sio mbaya gazeti hili hata likitoka mara moja kwa wiki. Wananchi watajua ukweli na harakati zote tunazozifanya. Hii kwa mawazo yangu najua itasaidia sana. Mapambano tunayoyafanya humu yanaonwa na wachache ukisema uanzishe movement wenye taarifa ni wachache.
Naomba niwasilishe kwa wadau na mniambie imekaaje hii. Nasubiri comments.
Kwa utafiti nilioufanya japo sio rasmi, nimegundua kuwa tunapokaa sehemu na kuanza kuongea mambo mbalimbali, tunaombwa source, na kila tunapotaja Jamii Forums, wengi na ambao tunawapigania hushangaa na wengine hutaka waione hiyo jamii forum wakidhani kuwa ni gazeti. Sasa ndo nikapata wazo kuwa kazi nzuri tunayoifanya kuipigania nchi yetu, si vibaya na walengwa wakalijua hili. Hivyo mawazo yangu ni kuwa viranja waandae Business Plan nzuri ikiwa na lengo la kuanzisha gazeti. Baadae tukijua gharama za kuanzisha hilo gazeti, kila mwana JF mwenye moyo atajua achangie kiasi gani kwa ajili ya kufanya kitu fulani.
Gazeti hili la Jamii Forums litasomwa kwanza na sisi wadau na ndio itakuwa njia mojawapo ya kuichangia JF kwa njia rahisi. Sio mbaya gazeti hili hata likitoka mara moja kwa wiki. Wananchi watajua ukweli na harakati zote tunazozifanya. Hii kwa mawazo yangu najua itasaidia sana. Mapambano tunayoyafanya humu yanaonwa na wachache ukisema uanzishe movement wenye taarifa ni wachache.
Naomba niwasilishe kwa wadau na mniambie imekaaje hii. Nasubiri comments.