Fumbo: Huko Ndani Kuna Nini?

Ms Judith

JF-Expert Member
Dec 24, 2010
2,563
918
1.
Wapendwa nijuzeni, huko ndani kuna nini?
Tangu zama nilidhani, huko ndiko utamuni,
ni punde nimebaini, si kutamu asilani,
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

2.
Kiumbe huyu makini, hakomi kurandaranda,
Amfumapo mwandani, huparamia kitanda,
Kasiye kama tufani, hutupia mbali mkanda,
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

3.
Na kazi anayo mwenzi, miguno na mashauzi,
Ka’ kufumbata konzi, kiumbe utamuenzi,
kwini ataitwa manzi, kingi ataitwa mwanzi,
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

4.
mwanzi ukitiwa pake, pumzi huenda mrama,
yatisha hayo makeke, vigori hupata homa,
eti imefika mwake, ya nini tena hujuma?
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

5.
Ikishaingia mwake, ndipo huanza hujuma,
Mithili ya mrusha teke, kiumbe hurudi nyuma,
achomoa mwanzi wake, si haki bali dhuluma,
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

6.
ikiwa ndani kutamu, vipi mwanzi usidumu,
Upatemaliza hamu, na kiumbe ajikimu,
faidi hiyo karamu, manzi asijelaumu,
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

7.
Kama ndani kuchungu, kwa nini asibaki nje?
Heri kuchapwa virungu, ndani katu usionje,
Wasikupate machangu, peponi mbuga uchanje,
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

8.
Kuingia na kutoka, ndo mchezo wa kikubwa!
Mwapata vipi mizuka, hata kukacha ubwabwa?
Na mwisho wake mwachoka, hamkomi nyie wakubwa!
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

9.
Naleta kwenu wazo, siku zote mfurahi,
Mtaimaliza mizozo, yale mambo ya kuwahi,
Mtakipata kitulizo, kama wenzenu wa Bahi,
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

10.
Ukiingia ‘sitoke, ukitoka ‘siingie!
Yako ashiki ufyeke, na mwandani uringie,
Vigori wasiteseke,maisha wafurahie!
Huko ndani kuna nini, wapendwa nijuzeni

nawatakia tafakari njema ya fumbo hili na weekend njema

mbarikiwe sana wapendwa,

Glory to God!
 
Ms Judith nakusalim ikiambatana with Love,
haki katu hujatenda kwa hilo hapo above,
Ujuvi mie sina natapa elewa kama ni yale ya Love,
Sote tupate faidi hebu fumbua fumbo above.

BTW Shairi lako la kweli napenda nijifunze Uandishi,
Hatua itafuata kuelewa nini malengo ya Mwandishi,
hapo sasa nasema wana JF watakoma kwa wangu Uandishi,
hahahaha... Miss Judy hope sija baka sheria za Uandishi.
 
Nahisi anashangaa mbona mme habanduki huko ndani, kunani??

Umeshawahi sikia msemo wa 'Men are like rats, always searching for a hole'

I was going to ask the same questio,but i don't think she meant that!
 
Ms Juddy, mara hii unaanza sema kunani?

haha, its not personal, ni vijimambo tu vya weekend vimenipitia kichwani mpendwa!

Asante Miss Judith ..uk ndani kuna fumbo
UKIWEZA TEGUA..

ndo hapo sasa mpendwa!

kama ni kutamu mbona wanatoka nje punde tu wakishaingia? kama kuchungu, mbona wavutia kasi namna ile? nadhani hima waje wenyewe hapa watutegulie.

I was going to ask the same questio,but i don't think she meant that!

haha, dont take it personal!

hii kali eti mwanzi ukitiwa pake.

yap mpendwa,

tusaidie kutegua fumbo basi, please!

Nahisi anashangaa mbona mme habanduki huko ndani, kunani??

Umeshawahi sikia msemo wa 'Men are like rats, always searching for a hole'

haha, hiyo kwenye bold nimeipenda sana, kama kuna ukweli vile!

mwacheni Mungu aitwe Mungu!

mbarikiwe sana wapendwa,

Glory to God!
 
@Ms Juddy, uzuri wa wanamme wanajua kuna wife matirio, wakishawaweka ndani tu wanarudi kwenye kutafuta new holes.

That's how their brain works I guess.
 
Duh

Huko ndani kunani.., kweli ni vigumu kujua... Huenda kwako ndani.., sio sawa na kwangu.

Anyway sometimes tunaweza kuona mlango tukazani tunaingia ndani kumbe tunatoka nje, lakini ukweli ni kwamba hata kule kwenye mazuri mabaya pia yapo, ukipata mazuri zaidi ya mabaya ni kushukuru Mungu.., na kama mpo wawili ndani kwenye furaha (raha uwa zaidi) na kwenye shida (shida hupungua kwa sababu inakuwa shared).

It depends kama umeingia mlango wa ndani au mlango wa choo
 
Ms Judith nakusalim ikiambatana with Love,
haki katu hujatenda kwa hilo hapo above,
Ujuvi mie sina natapa elewa kama ni yale ya Love,
Sote tupate faidi hebu fumbua fumbo above.

BTW Shairi lako la kweli napenda nijifunze Uandishi,
Hatua itafuata kuelewa nini malengo ya Mwandishi,
hapo sasa nasema wana JF watakoma kwa wangu Uandishi,
hahahaha... Miss Judy hope sija baka sheria za Uandishi.

subalkheir ADii, na love ndilo kusudi,
nimekusoma kwa bidii, beti zako za stadi,
fumbo mie sirudii, kusoma usikaidi,
saizi yako hilo ADii, shamsham ka zawadi

swali langu li bayana, kiumbe kantatiza,
ndani na nje ka laana, hasa kukiwapo kiza,
pumzize zinapobana, hawezi hata puliza,
saizi yako hilo ADii, shamsham ka zawadi
 
Duh

Huko ndani kunani.., kweli ni vigumu kujua... Huenda kwako ndani.., sio sawa na kwangu.

Anyway sometimes tunaweza kuona mlango tukazani tunaingia ndani kumbe tunatoka nje, lakini ukweli ni kwamba hata kule kwenye mazuri mabaya pia yapo, ukipata mazuri zaidi ya mabaya ni kushukuru Mungu.., na kama mpo wawili ndani kwenye furaha (raha uwa zaidi) na kwenye shida (shida hupungua kwa sababu inakuwa shared).

It depends kama umeingia mlango wa ndani au mlango wa choo


Sun mimi naamini kila entrance ina mazuri na mabaya.... Pale penye mazuri ina maana kuna alie weka hayo mazingira ya Mazuri kuwepo hadi ikakurahisishia mhusika. Na pale penye mabaya you have an obligation ya kujaribu badilisha na boresha mazingira yawe mazuri.... Hivo naweza sema at the end of the day.... Ndani kuna kila kitu mabaya na mazuri.... Ni jinsi wewe tu mhusika utavoamua, dedicate kuhakikisha mazuri yakukimbilia wewe na sio mabaya tu.
 
@Ms Juddy, uzuri wa wanamme wanajua kuna wife matirio, wakishawaweka ndani tu wanarudi kwenye kutafuta new holes.

That's how their brain works I guess.

Hiyo wife material unavyoikazania hebu tupe darasa ndo wapoje hao wasije kuwa waloimbwa na ace hood.
@mis jud
ntarud ngoja nkaumize ndonga ila always home sweet home na our homes is where our heart is and always kwa wanaume our heart is somewhere between legs. MWANZI PAHALA PAKE LOH.
 
subalkheir ADii, na love ndilo kusudi,
nimekusoma kwa bidii, beti zako za stadi,
fumbo mie sirudii, kusoma usikaidi,
saizi yako hilo ADii, shamsham ka zawadi

swali langu li bayana, kiumbe kantatiza,
ndani na nje ka laana, hasa kukiwapo kiza,
pumzize zinapobana, hawezi hata puliza,
saizi yako hilo ADii, shamsham ka zawadi


Ukitaka faulu Ms J, tambua love sio kusudi,
Ukitaka jibu kamili, elewa ngono ndio kusudi,
ndani nje kama laana, ukute wala sio lake kusudi,
ila tu zake tamaa, yamfanya onekana na kusudi.

Kiumbe majibu hana, bure utajikondesha,
waweza mjua hasa, na bado akakuendesha,
kama ndani arudi, basi tambua wamkosha,
kama nje atabaki, huna budi ni kujiondosha.
 
Sun mimi naamini kila entrance ina mazuri na mabaya.... Pale penye mazuri ina maana kuna alie weka hayo mazingira ya Mazuri kuwepo hadi ikakurahisishia mhusika. Na pale penye mabaya you have an obligation ya kujaribu badilisha na boresha mazingira yawe mazuri.... Hivo naweza sema at the end of the day.... Ndani kuna kila kitu mabaya na mazuri.... Ni jinsi wewe tu mhusika utavoamua, dedicate kuhakikisha mazuri yakukimbilia wewe na sio mabaya tu.

Kweli kabisa ni jukumu la wote wawili kuhakikisha mazuri yanakuwa mengi kuliko mabaya..., lakini mara nyingine kama ni mmoja tu ndio anajaribu hupelekea shughuli kuwa ngumu (au almost impossible), uvumilivu ni muhimu.., sababu huko ndani kuna milima na mabonde sio plain surface. (huko ndani kunani..., :) )

Kwahio cha muhimu ni wote kujaribu kufanya all you can kufanya shida na matatizo kuvumilika.., na kama mmoja hafanyi wajibu wake, ni wajibu wa mwingine kujaribu kila linalowezekana and hope mwenza atakuwa na busara na kuona umuhimu wa kuishi kwa amani na uzuri.

After all a problem shared is half a problem na what is the use of FURAHA (Happiness) if it cant be shared
 
Wife matirio wanatofautiana kati ya mtu na mtu.
Ni matarajio ya mtu kwa mkewe.

Hiyo wife material unavyoikazania hebu tupe darasa ndo wapoje hao wasije kuwa waloimbwa na ace hood.
@mis jud
ntarud ngoja nkaumize ndonga ila always home sweet home na our homes is where our heart is and always kwa wanaume our heart is somewhere between legs. MWANZI PAHALA PAKE LOH.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom