mose
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 284
- 232
Habarini Wote.
Nimepata kufanya Utungaji wenye kufungamana na mawaidha yajayo na mada mbalimbali katika Jukwaa hili Jamii -- kwa faragha.
Mapenzi yangu yamekuwa ni kwamba kama hali bado haijaandaliwa ama umma haujajiandaa, si vema kufunua na kubayanisha mambo ama mashauri fulani juu ya Wanajamii, Mifumo na Dini.
Ninaridhika sasa ya kwamba, ndani ya hili jukwaa kizazi sahihi cha wanamafikara kimeshawasili...
Ninafarijika na kuazimia sasa kushiriki mawaidha ambayo awali niliyafanya kwa ajili watu wenye fikra huru -- japo niliowaandikia hapo nyuma si kuwa niliwategemea hasa kunielewa, ila kuwatumia wale kama vigezo vya kuandaa matanuko wa mashauri, uono na upeo kubayanisha mambo. Kwa kuwa wapendwa wangu hasa ni wale walio ni wadadisi, wachunguzi, wenye kiu ya kuhama kutoka kwenye 'Utumwa wa Kiakili' kuelekea kwenye uwanda wa ahadi--Uhuru katika dimensha zote za mwili, akili na roho...
Kwa wale wote wanaojijua ndani yao kuna ujasiri na wito wa kutoka, safari hii imeshaanza...
Tutaelekezana, kutaamulisha, kupashana, kufundishana, kufundwanishana n.k kusudi hakika ya Taifa Jipya la watu -- watu walio Wapya kwa Mioyo na Dhamira katika kuongozea kuliko bora zaidi iweze kutimia.
Ninawahakikishia uwezo wa kusonga kwenye kheri upo, na mambo makubwa sana yanatungojea safarini... Kwa kuwa safari hii ni safari ya ajabu, maana zawadi yake ni ulimwengu wote kuutwaa... Anga si kikomo...
Niwatake na kuwasihi enyi kizazi cha mitazamo huru na wazi zaidi kwa kheri na jaala njema zaidi, msikatishwe tamaa na lolote kulingana na hapa tulipo kwa kufananisha na kule tunakotamania...
Tuelekezana yote kwa lugha ambayo wote tunaifahamu vizuri -- Kiswahili, tutazungumza yote kuhusu 'Nishati' hadi 'Wakti'... Tutahandisi mambo na mitambo ya kuweza kuyafanya hata makuu--kimawasiliano na uchukuzi... Tufanya namna mpya kuvuna nishati, na tutasafiri hata nje ya sayari yetu ya dunia kwa namna moja hata nyingine... Haijalishi hili litatimia ndani ya miaka 80 - 100 ijayo-- ila ninawahakikishia sehemu ya hizi jitahada zitakuwa hapa hapa kwenye hii ardhi yetu tuuitayo Tanzania kwa leo na Afrika kwa kesho... Kwa kuwa roho ya ushindi huu tayari ipo miongoni mwetu, na kazi ni kwetu...
Msihofu miongoni mwetu ni nani atatuongoza... Zama hizi si zakuongozana. Kwa kuwa tupo katika zama ambazo Uongozi ni Kuchagua na Kujichagulia. Kila mtu kwa nafsi yake yampasa kuamua, ikibidi kuunganisha nguvu zetu kwa ajili ya jambo lolote la kheri ya pamoja, tutajaunda namna ya taasisi zisizoongozwa na 'siasa' za utaratibu ila 'itifaki' sahihi na uelewa kamili juu ya jambo liwalo lolote.
Na sasa nilete kwenu, mashauri anuai -- mapana na marefu juu ya kile ninachokifananisha na kumbukumbu la vitabu vitano vya Musa -- Pentauki, kwa maana ili kufika ustawi na staarabu mpya mambo kama yale yale yaliyosadifiwa kwenye vitabu hivi vya mapokeo yatahusika kwetu sote... Japo huu inakuja kuwa kile ambacho Francis Bacon alikitaja kuwa ni 'Instauration of Knowledge' katika kuielekea 'Atlantisi Mpya'...
Ni wakati wa kuyaupisha mafundisho na maarifa ya zamani...
+++++++++
Kutoka: Mwongozo Hai kuelekea Uhuru Halisi seh. I
5 Septemba 2011 saa 12:15 Asubuhi
Kutoka: Mwongozo Hai kuelekea Uhuru Halisi
(Iliandikwa kwa rafiki kama mchango wa mawazo na kwa uchochezi wa fikra)
Pendo lililobarikiwa dada MwKT,
Siku kadhaa nyuma ulileta habari jukwaani juu ya ‘Kuanzishwa kwa “un-women” – kaeni mkao wa kula’ katika jukwaa la siasa.
Nilipendezwa na habari hii na hasa kwa kuzingatia mapenzi yangu juu ya mabadiliko yenye kuleta kheri katika jamii niishiyo na ulimwengu kwa ujumla. Ni jambo lenye kupendeza kutambua harakati za watu mbali mbali na kujaribu kuunganisha maono ama kufanya fikra tunduizi.
Amko la wanaharakati katika kutunga na kupelekea taasisi kama chombo chenye kuongezea kwenye ushawishi, utendaji chini ya mamlaka, mifumo na utekelezaji wa mipango ama maelekezo; linavutia wote walio na dalili za kuamkia huko kimwelekeo wa fikra na imani lakini pia zaweza kuvuta ukosoaji wa kiudhanifu—yaani juu ya dhahania ya mpango mzima vile kusema, filosofia ama asili ya mwongozo wake na misingi ya ustawishi wa jitihada.
Kwanza kabisa nitambue ‘unene’ na uzito wa michakato uliopo katika vyombo vya kimataifa na utengeneaji wake. Itifaki zake ni namna ya mifano yenye kufafanua mifumo na taratibu katika kuratibu matukio kulingana na makutano ya watu na michakato. Na hivi nitambue msuko wa chombo kama namna ya mipaka na mamlaka juu ya mambo yake na tena kwa muktadha wa kufanyika kwake.
Ujio wa chombo hichi kwako umekusukuma kupenda kuwaatarifu wanajamii wenzako; maana yake: uwezekano wa fursa mbali mbali--ajira, na mipango ya maendeleo. Na vile vile umepata kusema : hivyo havitaweza kuja kwenye sahani ya dhahabu… Kisha ukazungumza juu ya ‘nafasi za juu’… Halafu ukataja mjumuisho wa mataifa na hivi kuonesha kutambua msukumo wa nguvu ya uwezo na ushawishi kulingana na sehemu watu watokayo kmf Amerika ya Kati, Scandinavia na nchi nyingine za Afrika katika ugombeaji wa nafasi za kazi na labda vile vile kumaanisha vyeo vya usimamizi na utendaji pia.
Pia ukazungumza dokezo la kukabiliana na adha ya shughuli kwa kutaja umuhimu wa watarajiaji nafasi kudumu kukesha katika jitihada kwa kufuatilia kwa makini nyenendo za michakato ya uanzilishi.
Nikushukuru kwa angalizo na kushiriki habari na wenzako kama mimi na wengine.
Niliingie neno la leo kwa kutanabaisha jambo kuhusu ulimwengu wa kuona mambo kwa kiini cha usababishaji na matokeo yake.
Tumezoea kuona mipango ikipangwa na jitihada kusukwa na matokeo kuainishwa ili kuelekeza sura ya utendaji na utekelezaji. Binadamu toka zamani hadi hii leo tunaona upangiliaji wa mambo ni kama sanaa inayoweza kufanywa kamilifu ijapokuwa matokeo yake si kwamba daima huwa ni hivyo. Kuna vitu vinaweza kupangilika lakini mara kadha wa kadha mashauri juu ya watu ama jamii si yenye kupangilika na kujitosheleza bila mikingamo ama kadhia ya namna fulani kujitokeza. Labda hii tuseme inatokana na ukweli kwamba binadamu ni kiumbe chenye uwezekano wa fikra binafsi na utashi na hivyo haiwezekana kuwakundisha watu pasipo ridhaa na makubaliano na wao wenyewe kwa wakati.
Basi katika ulimwengu wa makubaliano kuna yale ya juu juu na kuna yale ya ndani. Vivyo hivo kuna kuona mambo kwa sura ya juu juu na kuona mambo katika sura ndani. Naam, vile vile kuchukulia jambo kwa sura ya nje na kuchukulia mambo kwa sura ya ndani. Uhusiano wa mambo ya ndani na yale ya nje ndiyo hujaa kuzaa uthabiti wa makubaliano na labda pia kusema, umadhubuti wa jitihada kulingana ufananikaji wa dhamira. Hata hivyo, kupo kuridhika na mambo ya nje bila kuchunguza misingi yake; na hata tena kwa namna kama hiyo; kutotambua athari za matokeo kwa kutozingatia uasili wa jambo lenyewe kwa uzima wake. Haya mawili hujitokeza hasa katika maisha ya mwanadamu kwa kutoangalia/ujisahau wake wa mashauri yaandamayo dhamira zake kwa wakati hadi wakati.
Na hivi leo ningependa kuzungumzia nafasi ya Tekinokrasia katika ustawi mpya kwa wanadamu katika zama hii mpya.
Nimechagua mchango wako toka jukwaani kujenga usuli wa shauri langu la leo kwako na kwa wadau wengine; kwa kuwa wanawake katika zama hii wanachukua sura takatifu ya michakato ya jamii na ustawi. Na hivi udadavuaji wa utata wa hali ya ustawi wa jamii unachipukia na kuanza kwa kumuelewa mwanamke na sifa ya kike ya uumbaji wote--jambo lililosahaulika katika nidhamu na uelewa wa wanadamu wa leo.
Katika hali ya juu juu shauri lako juu ya uanzishwaji wa baraza la wanawake-umoja wa mataifa, umelenga hasa fursa za ajira na labda kwa upande mwingine usiowazi ni shauku yako ya chombo hiki cha wanawake na kwa ajili ya wanawake. Kuangalia upande wa ajira-- na hapa umewakumbusha hata wanaume pia kutazamia nafasi; kulinikumbusha mashauri juu ya uchumi na siasa—na miye nikapata hamu nije kushiriki na wewe na wengine fikra tunduizi mintarafu vyombo vya jamii na nafasi yake katika kuchochea ama kuleta mabadiliko.
Jambo la kwanza ambalo halinifurahishi na vile kuniacha nikisikitika ni ukweli wa kwamba nafasi za kazi na ajira kugombaniwa na kushindaniwa. Ni ukweli mchungu na ambao mimi siupendi kabisa. Naitekeleza chuki yangu dhidi ya huo kwa kuleta fikra mbadala za jinsi ya kutokomeza sura hiyo ya mambo kwa ghadhabu ya kuwakilisha mawazo ya upeo na maarifa yangu kwa wakati. Lipo tatizo kubwa katika jamii ya leo ambalo ladumu kwa mwendelezeo ama udumishwaji wa dhana ama pia fikra ya kuwa maisha hayanabudi kustahimilishwa kwa urasmi wa ajira za kazi kwa ajili kipato kwa kutumikia chombo fulani na hata kama makusudi mazima ya hicho chombo si yenye kueleweka kwa mtu husika kujihusisha nacho—ama kupimwa/kujipima ikiwa mna dhamira bora kabisa kuwezekana ya utashi ndani ya mtu mwenye kutaka kujihusisha hicho chombo. Hili kwa leo sitazungumza sana kwa maana ni shauri linapelekea kipengele kimoja katika tatu cha kuyaleta mabadiliko kamili ya kijamii katika muktadha wa kufafanua Meritokrasia. Leo nataka kuzungumzia Tekinokrasia kwa mapana.
Dhana ya ushindani kwa lolote lile ni jinsi ya kiume ya mambo. Akili inayofikiria katika minajili hii ni namna ya akili ya kiume. Jamii inayovumilia na kudumisha mashindano ya huyu kupata na yule kukosa, ni yenye jinsia ya kiume na bila shaka inadumisha namna ya mifumo dume katika kusimama kwake.
Mchezo wa ajira ama kutafuta kipato unachezwa katika kiwanja cha uchumi na mabadilishano ya kijamii. Ikiwa mtu hatataka kuusoma uwanja kabla ya mpambano hapana shaka mtu huyu atakuja kutingwa na adha ya ujinga wake kwa kukosa maarifa ya kutosha katika kuungia mchezo. Matokeo yake katika kuuelekea mwisho wa mchezo au kadri mchezo ukiendelea--huenda yakaambatana na dosari nyingi ambazo zitajitokeza kwa sura ya kama mtu kupata hiki kwa gharama ya kukosa kile; ama kupata hili badala ya lile lililotarajiwa ama kutakwa. Basi yampasa mtu kuwa ni mwenye kujitambua ili apate kutambulika katika uwanja wowote wa jitihada chakatuzi. Na hivi aje kuvuna matokeo kwa stahiki ya nia yake katika jitihada sahihi.
Na hili linajenga hoja ya msingi katika filosofia ya Tekinokrasia. Kweli ya kwamba mtu hawezi kuunda bila ya kuwa na ramani; hawezi kuanza safari na hali hajui mapito; hawezi kukatiza kokote eti akafikiri atafika kwa kuwa tu mwenye kutimba maguu… Je, ajijua yeye ni msafiri? Je, ajua uhusiano wa hapo alipo na kule anakokwenda? Je, ajua akiba yake safari na vipindi vya kuitekeleza hiyo safari? Je, ajua jambo la muhimu katika safari ni safari yenyewe? Na je, yu ajua yeye kuwa palipo na nia daima safari hazikomi na hivi penye nia pana njia ? Na basi lilikokuu kuliko yote-- je, yeye yu ajua Nia yake ambayo ni ufunguo wa dhamira yake mwenyewe ?
Kukosa kuelewa Nia zetu hasa daima kutatuacha sisi kama watangajitangaji katika nchi za wageni. Ni kusahau tulikotoka na hivi vile vile kutokujua hasa ni wapi tunakwenda. Pilika za maisha na mahangaiko yanaweza kutia upofu wa tafsiri juu ya maana zetu za kuwa ni wenye kuishi na kuwa hai--binadamu kukosa jicho la kupima uhusiano kati ya mazingira na mambo ya nyakati--katika siti za utu wetu, uzima na busara. Kuangalia chakula, malazi na mavazi kwaweza kumtinga asione maana ipitayo yote yenye kufanyika na yeye kuhifadhika kwamo. Mtu, Dunia, Nyota na Mbingu vinautumikishi wa kimoja kwa mwenzake ; na vivyo hivyo kuonesha dalili ya fumbo la namna ya uhifadhiko kati ya vinavyoonekana basi ndani ya vile visivyoonekana.
Basi natuukague uwanja wa mchezo.
Nia ni mkuki wenye kuleta mwelekeo wa wakati na jitihada. Kutoka na Kufika ni uhifadhiko katika ulimwengu wa madhahirisho. Na hivi wakati si kitu ila tu rajisi ya mabadiliko katika utambuzi wa mtu. Bila nia hakuna badiliko na bila mwili wa madhahiriko hakuna muda wala wakati. Na vile vile pasipo na utambuzi hakuna rajisi ya wakati na wala nia yenyewe. Lakini katika namna yaajabu maisha/uzima ni uhifadhiko wa haya yote katika moja. Itokeapo namna ya utambuzi uliofanyikia katika hiyo moja lakini usijitambue uhifadhiko wake katika moja basi ndipo nia huzaliwa na wakati kuwepo.
Tutatazame mambo ya nyakati na wakati.
Mtu ni kutaniko la uzima wa mwili na karama za yasiyoonekana kwa macho ila tu kutambulika kwa ishara zake. Shani ya utu ni matokeo ya kubebea ndani hadhi ya namna bora za vitu/mambo/matendo kufanyika. Na kuna namna ya kumuona mtu kama mchakato hai miongoni mwa mambo matatu—nia, uwezo na maarifa/busara katika ishara ya sura tuiitayo ‘Uzima’ pale hayo matatu yanapotunukiwa mwili wa madhahirisho wenye kudhihirisha ‘chanzo-sababu / hisia-matendo’ ; kwa kupitia nia na uwezo katika kuhadhikisha kitendo na matokeo yake. Basi haya yakutanapo huzaa sura ya mambo iliyo ni dhana ya Muda na matukio-- vile pia kusema msongo wa wakati kulingana na tafsiri itegemeayo nuru yenye kumulika dhamira ya utambuzi katika siti ya utu wa mtu na akili/kumbukumbu. Na hivi mtu anayonafasi ndani yake yenye kuweza kudadavua mambo ya nyakati na hali pia wakati huo huo anayokurunzi isiyokamatika katika dhana yoyote ya wakati. Kurunzi hii ndiyo mwenge wa busara yake ishindayo tafsiri zote zenye mwanzo na mwisho ; inayomulika na hali yenyewe haimulikwi. Na hivi mengineyo yote kuwa tu ni vina vya tafsiri vya mambo vimvuli kwa ‘Kweli’ ya ‘Moja’ ; kufanya mukabala wa kumbukumbu.
Tutazame vimvuli vya watu na vina vya tafsiri.
Vimvuli haviishi ila tu kwa nguvu ya udhanifu wa mtu ; huhuishwa katika sura ya tafsiri yenye kujaribu kukidhi haja ya kupunguza ama kuondoa mashaka juu ya mashauri ya ustawi wa watu na makabila katika pia kufafanua utambulisho wa mambo yao ambayo kwa ujumla huitwa utamaduni na ustaarabu. Na jinsi hii, watu wa makabila ama utaifa kuwa daima katika kutafuta kujitambulisha kwa jinsi ya kutetea, kudumisha mambo yao yanayowafungamanisha ama pia kuonesha msisitizo wa mapokeo yao juu ya nchi na tawala ; kwa kuyaenzi hayo. Lakini watu pia ni wenye kujua sana dhamira zao za kimakundi zaweza kuharibiwa na hata kuharibika mapema pale zipambanapo uso kwa uso na tamaduni nje ya mizingo yao. Na hivyo binadamu katika sura ya kijamii huwa na namna ya kulinda mila, desturi na mapokeo yao yaliyo ni ishara ya utambulisho wao kwa pumzi ya nguvu ya uwezo wao.
Historia inaonesha jitihada zote za wanadamu katika muktadha huu zimezaa kuinuka na kuanguka kwa mataifa ya makabila na vipindi vya utawala kwa wale waliokamia hilo; kwa kukutana uso kwa uso na wale waliothubutu kuleta mpishano katika kupanda na kuporomoka kwa mataifa/makabila hasimu. Basi nia za chini za wanadamu zenye kutawala matendo yao ni zenye namna ya kukosa utangamano miongoni mwa mataifa na makabila na daima hutoa ahadi kubwa kubwa kwa makundi ya watu na hali katika kupita kwa wakati huleta pia majonzi, vilio, maasi na mambo yote yote yaliyokosa ubarikika.
Basi binadamu kwa jinsi hii ana nafsi mbili ; ya chini na ya juu. Ya chini ni ile yenye kuzaa makusudio yenye kuharibika upesi na hivi ni kimvuli tu cha nafsi ya kweli isiyoweza kuharibiwa wala kunajisiwa na mashauri ya mwili wa nyama wenye maradhi ya kuridhi ya kupenda kujipendezesha nafsi na kujihifadhi kwa mahodhi ya mali ama starehe za nchi/dunia na hivi mwili wa madhahirisho.
Nafsi ya juu ya mtu ni hazina kwa yale yote yasiyodhahirika na ni kioo kwa utambuzi wa mawezekano yaliyoko katika nyakati zote na fumbo kuu la imani kwa mtu. Ikiwa 'Mungu' ni dhana yenye kuwakilisha moja na moja na moja katika moja ; basi ndani ya mtu kuna daraja-mbegu ambalo ni lenye kuweza kusemwa mtu na mungu ni moja pia katika muktadha wake. Na nuru ya ufahamu wa mtu ndiyo muujiza mkuu kuliko wote wa dhahirisho la Uzima katika ‘mwili wa madhahirisho’ na ‘pasipo udhahirisho’ vile vile. Lakini mwanadamu akiwa ni mwenye kulewa sana na mvinyo wa fahari za mwili wenye kuharibika ; huishi kupenda kudumisha kimvuli cha nafsi yenye kufa na kutotambua namna ya fahari yake isiyojua mauti wala kuzaliwa—Ukweli juu ya ‘uzima wa milele’. Na hivi anguko la mwanadamu ni dhana ya mwanadamu kujitambulisha na mwili wenye kufuata sheria ya mauti na adha zake zote na hivyo kuuona ulimwengu katika jicho la namna hiyo. Na ndiyo katika kisomo cha leo tunaita namna hii ya jambo—‘dainetenia’ ya utambuzi ; mtu hutaka kuona kile anachopenda kuona kudumisha kile anachokidhania na kuwa kipofu wa vinginevyo vyote.
Nilipata kudokeza ya kwamba kazi niliyofanya kusanifu USANISI WA UJASIRIAMALI WA KIJAMII, Oganam ya karne ya 21 juu ya njia ya tatu-- ni mkamilisho wa kujumuisha kazi za Pythagoras, Yesu na Buddha katika kuwakilisha sura halisi ya mabadiliko ya kiustaarabu tunayoyaingia. Basi kwa jinsi hii Pythagoras ni kiungo kati ya Ufahamu kwa mujibu wa Yesu kuelekeza mafundisho; na kujaribu kwake kuwasilisha namna ya uelewa wa maumbile ; yeye pia ni kiungo katika kukutanisha maelekezo ya Yesu na yale ya Buddha ambayo yote kwa pamoja ndiyo mhimili wa fahari ya zama hizi katika ustawi na neema. Na hili halina budi kufafanuliwa kwa maelezo zaidi. Na tena si katika mrengo wa kiordhodoksi ila sayansi halisi ya ukweli wa mambo. Kwa kuwa mimi si muumin wa dini yoyote ya kimapokeo na wala sipendekezi kwa mtu yeyote usadikifu wowote iwe wa 'Mungu' ama mambo yajayo/yaliyopita/yaendeleyo kwa jicho la upofu wa fikra ya udhanifu na hofu. Usadikifu ni kasumba na hadhi ya sifa dumazi--haimtii binadamu heshima ya ‘kweli’ ya utu ila tu kimvuli chake.
Kwa kuwa kutokana na Pythagoras ninazungumza mambo ya nyakati na utangamano wa vitu/mambo kihadhi na pia ukiasi wa namna yake katika msuko ya yote yanayoonekana na yale yasiyoonekana. Na hivi Pythagoras anawakilisha Wakati na mshahibiano wake na mtiririko wa madhahirisho, Yesu anawakilisha Tekinokrasia na Buddha anawakilisha Meritokrasia ; lakini mwenye kuvitanganamisha vyote hivi ni Pythagoras.
Na sasa basi nimtambulishe Yesu kama mtu aliyeyajua haya kwa kutangulia na kujaribu kuleta msogezo wa dhana na pia fikra miaka kadhaa iliyopita ; takribani kipindi cha zama moja toka leo—kadri tuzisomapo tabia za mabadiliko ya watu kimakundi na mnyambuliko wa hadhi na ustaarabu wao ; twazigawanya hizo katika vipindi tuvitajavyo kama zama.
Basi Yesu alijua dhahiri jitihada zake zilikuwa ni kipindi cha matayarisho lakini matunda yake halisi ama kusema musimu wa kuchanua ni zama moja mbele katika mwendo wa hatua za mabadiliko ya kiustaarabu na hadhi ya utabia kwa wanadamu. Lakini tena katika utambuzi ndani ya daraja-mbegu ; fahari yake kamili yeye alipata kuiita ni ‘Ufalme wa Mbingu’, ni vile kutamka bayana kuwa upo karibu na hapa na vile pia kusema upo ndani ya mtu na labda tu akizaliwa mara ya pili si kwa jinsi ya mwili wala kiakili na wala kihisia za mwili bali kwa jinsi ya ‘roho wa uzima’-- huwa moja na huo na hivyo kuwa ni ‘Mfalme’. Kwa kuwa wakati si kitu katika roho wa uzima ijapohali hili ni shauri gumu kuenea katika uelewa wa kawaida wa mtu asiyetaamulika, aiishiye katika uwanda wa nchi ya vimvuli, ila tu kuelekezwa yeye kwa namna ya picha za vielezi vyenye funguo za kuleta ishara ya ukweli wenyewe ulivyo.
Basi kabla ya kuyadadavua mashauri ya ontolojia kwa mujibu wa Yesu tuikague kazi yake kulingana na kumbukumbu zilizopo na mapokeo. Yeye ni mtu mwenye kukumbukwa kwa kulingania ‘Ufalme Mpya’, pia kusihi umma kuwa tayari kuupokea ‘Ufalme’. Alikuwa ni muasi wa sheria na desturi na huku akisisitiza kuzikamilisha hizo kwa Sheria Mpya. Alipata kukiri kiulaini tu kuwa yeye ni ‘mwana wa mungu’ na vile kusisitiza pia kuwa mtu yeyote kwenye kuzaliwa tena kwa jinsi ya roho hufanyika ‘mwana wa mungu’. Pia alitamka bayana kwa kukumbushia, kusema binadamu ni ‘miungu’; wana wa aliye Juu (katika Mbingu). Aliponda dhana ya watu kutaka ishara ili kujiridhisha usadikifu juu ya karama za kimamlaka ya wadhifa/ukiongozi mkuu kutarajiwa ama unabii mkubwa--akikwepa kuridhisha watu na siasa zao. Lakini hapo hapo ikitaarifika kufanya ‘miujiza’ ya wenye kuwa ‘viziwi’ kusikia, wenye ‘upofu’ kuona, walio ‘bubu’ kuzungumza, Kuzungumza na ‘vipepo’ vyenye kuendesha Pepo na dhoruba za mawimbi ya bahari nahivyo ‘vipepo’ kumsikia na kuitika kwa kutuliza tafrani… Yote hayo kukimbia sifa za kiuanadamu ila tu kuitikia hitaji la wakati.
Shughuli ya Yesu ilikuwa na mwanzo wa upacha na binamu yake aliyeitwa Yohana. Machache hujulikana kuhusu Yohana katika mapokeo ya vitabu kama vile pia kukosekana kwa simulizi la maisha ya Yesu kati ya miaka 12 na mpaka kuja kukutana na Yohana akiwa na umri wa kama miaka 28 katika ile shughuli isiyofafanuliwa kinagaubaga ya ‘Kubatiza’ ambayo alikuwa akitenda binamu yake huyo katika ukingo wa mto Yordani.
Labda ikiwa shughuli ya Yohana ingehifadhika kwa kina katika kumbukumbu za simulizi za kimaandishi, ‘ukweli wa ishara’ ya tendo lenyewe la ubatizo ingeng’amuliwa vema na uhusiano wa shughuli za hao wote wawili mbele za umma kufahamika vema.
Basi kulingana na simulizi mbadala toka kwenye kumbukumbu la matendo yote ndani ya nyakati inatupasa kutafuta majibu. Upo ujuzi wa kuona matukio katika ‘kitabu cha uzima’ na ambapo yeyote aweza kuzisoma kumbukumbu za mambo yaliyotangulia kwa vipeo vyote vya taarifa: picha, maneno, harufu, hisia n.k… Basi nitumie msaada wa Levi Dowling , aliyepenyezea kiufahamu ndani penye ‘Akasha’—mahala pa kumbu kumbu zote, kuwakilisha ujaziliazi wa simulizi kosekanifu.
Nimepata kutafsiri kazi ya Levi na hii hapa ni nukuu nyakuzi:
SURA 7
Arkelausi atawala mamlaka. Mariamu na Elizabeti pamoja na wana wao wapo Soani na wafundishwa na Elihu na Salome. Somo la Utangulizi la Elihu. Asimulia juu ya mfasiri.
Mwana wa Herode, Arkelausi, alitawala mamlaka yote katika Yerusalemu. Alikuwa ni mbinafsi, Mfalme mkatili, aliwaua wale wote wasiompa heshima yeye. 2 Aliita barazani wote wenye hekima zaidi juu ya watu na kuwauliza kuhusu mtoto mchanga mwenye kudaiwa kustahiki kiti cha ufalme wake. 3 Baraza likasema kwamba wote wawili Yohana na Yesu walikuwa wameshakufa; basi na yeye akaridhishwa. 4 Sasa Yosefu, Maria na Wana wao walikuwa chini katika Soani, na Yohana alikuwa na mama yake katika vilima vya Yudea. 5 Elihu na Salome wakawatuma wajumbe kuharakisha kuwatafuta Elizabeti na Yohana. Waliwapata nao wakawaleta wao Soani. 6 Sasa, Mariamu na Elizabeti walikuwa wakistaajabia sana kwa sababu ya kukombolewa kwao. 7 Elihu akasema, si ajabu, hakuna matokeo tu; kanuni hutawala kuendesha matukio yote. 8 Kutokea nyakati za nyuma sana ilishapangwa kwamba mtalikuja kuwa nasi, na katika shule hii yenye kutunzwa kusudio safi ili kufundishwa. 9 Elihu na Salome wakawachukua Mariamu na Elizabeti nje kwenye ua takatifu karibu na pale ambako wao walikuwa na desturi kufundisha. 10 Elihu akawaambia Mariamu na Elizabeti, mwaweza kujionelea furaha ninyi wenyewe mmebarikiwa mara tatu, kwa kuwa ninyi ni mama wateule wa wana walioahadiwa kipindi kirefu, 11 Wao ambao ilivyopangwa kuwekewa mkono kuja kuweka mwamba mgumu imara msingi jiwe wa uhakika ambao juu yake hekalu la mtu kamilifu litasimama--hekalu ambalo halitaweza kamwe kubomolewa. 12 Twauhesabu wakati kwa mizunguko ya zama za vipindi, na lango kwa kila zama twasema akilini ya kuwa ni jiwe la maili katika safari ya kundi la watu wa sifa ya namna moja. 13 Zama zimepita; lango kuelekea kwenye zama ingine lafunguka wazi katika kugusa kwa wakati. Hii ni zama ya maandalizi ya nafsi roho, ufalme wa Imanueli, wa Mungu katika mtu; 14 Na hawa, wana wenu, watakuwa ni wa kwanza kueleza habari, na kuhubiri injili ya mapenzi mema kwa watu, na amani duniani. 15 Kazi kubwa ni yao; kwa kuwa watu wa miili ya nyama hawataki Nuru, wao walipenda giza, na pale ambapo nuru yang'ara gizani wao hawaitambui. 16 Twawaita hawa wana, Wafunuaji wa mwanga; lakini inawapasa kuwa na nuru kabla ya wao kuweza kufunua nuru. 17 Na yawalazimu kuwafundisha wana wenu, na kuzitia moto nafsi-roho zao kwa upendo na msisimko mtakatifu, na kuwafanya wao kuwa macho fahamuni na mpango wao mahsusi kwa wana za watu. 18 Wafundisheni kwamba Mungu na Mwanadamu ni moja; ila kwamba kupitia mawazo ya mwili wa nyama na maneno na matendo, mwanadamu hujirarua mwenyewe mbali na Mungu; kujishusha hadhi yeye mwenyewe. 19 Fundisheni ya kwamba Pumzi Takatifu italiwafanya wao moja tena, kurejesha hali ya kwenda kwa utangamano; 20 Kwamba hakuna chochote chenye kuweza kuwafanya moja ila Upendo; kwamba Mungu ameupenda sana ulimwengu hata kumvika mwana wake katika nyama ili kwamba mwanadamu aweze kutambua. 21 Mwokozi pekee wa ulimwengu ni upendo, na Yesu, mwana wa Mariamu, aja kudhahirisha pendo hilo kwa watu. 22 Sasa, pendo haliwezi kudhahirika mpaka njia yake iandaliwe, na hakuna chochote chenye kuweza kuivunjilia mbali miamba na kuangusha chini vilima vilivyo kwea juu sana na kujazia juu mabonde, na hivyo kutayarisha njia, ila usafi wa moyo. 23 Lakini usafi wa moyo katika maisha wanadamu hawatambui; na hivyo, huo, pia, waja katika mwili wa nyama. 24 Nawe Elizabeti, umebarikiwa kwa kuwa mwana wako ni Usafi wa moyo kufanyika nyama, na yeye ataifanya njia kwa Pendo. 25 Zama hii itatambua ila kidogo tu juu ya kazi ya Usafi wa Moyo na Upendo; lakini hakuna neno limepotea, kwa kuwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Mungu ingizo lafanyika kwa kila wazo, na neno, na tendo; 26 Na pale ambapo ulimwengu u tayari kupokea, lo, Mungu atamtuma mjumbe kufungua kitabu na kunakili kutoka kwenye kurasa zake zilizohifadhika patakatifu ujumbe wote wa Usafi wa Moyo na Upendo. 27 Na kisha tena kila mtu wa juu ya nchi atayasoma maneno ya uhai katika lugha ya nchi yake ya kuzaliwa, na wanadamu wataiona nuru, kutembea katika nuru na kuwa nuru. 28 Na mwanadamu tena atakuwa mmoja na Mungu.
Zama inayokwisha ni zama za ya ‘Maandalizi’ na hivi kwa imani binadamu amepata shauri la kuogelea katika ‘bahari’ ya kweli ya uzima wote akiwa kama samaki asiyebudi kuwa na kiu. Kwani lugha ya ishara na vielelezi aliyotumia Yesu ni ufundi wa kufungua pazia la mkingamo wa udhanifu dhidi ya ‘Kweli’ na uchukuliaji wa hadhi ya matendo katika kumwandaa mtu na upokeaji wa ‘busara’ ya ‘roho wa uzima’ kama Yesu alivyoijua na yeye kujulikana katika hiyo. Na hivi kila mtu aweza kufunguka kwa kadri ya stahiki yake kwa wakati na hali kielelezi kikiwa vilele. Na vile vile kuthibitisha jinsi binadamu awezavyo kujifunza kwa kushirikisha ubongo wenye kutenda kazi kwa kutumia picha za mfano na mashauri yenye mantiki/changanuzi; na Yesu alikuwa muepesishaji wa mawasiliano ya ndani ya mtu katika kuchochea utambuzi wa kiroho.
Mapokeo ya mafundisho ya Yesu yameleta mkondo wa imani na taasisi za dini. Ni ushawishi na msukumo wa vitendo ndivyo vilivyozaa mwongozo katika sura ya dini na mtapanyiko wake wa madhehebu. Kwa kuwa fikra na hisia-kutenda zikinogeshwa kwa itikadi huweza kusimamisha utaasisi wa watu na msukumo wa ushawishi. Na hivi twaweza kutazama finomena ya dini kama Ukristo ulivyo kuwa ni kama chombo tu chenye mfano wa utumikivu wa mwanadamu katika kufanikisha kazi fulani. Lakini la msingi ni kuelewa utaasisi ni kitu gani na ‘Kweli Halisi’ ni kitu gani. Taasisi ni ubunifu wa mwanadamu ; ‘Kweli’ haina ushirika wa moja kwa moja na utaasisi ingawaje utaasisi waweza kutengeneza mazingira ya ‘Kweli’ kumea katika wanataasisi husika. Hili hutazamwa na kupimwa kwa ‘matunda’ ya taasisi yenyewe.
Taasisi ni kifungo cha kufungamanisha na itikadi na ushawishi; Kweli haina mipaka na ni hadhi ya mbegu ya yote yenye kufanyika na kudhahirika. Dhana vile vile ni kitu chenye sura ya ukikomo na hivi haewezi kuwa ‘Kweli’. Dhana ni chembe katika mwili wa ufikirifu katika daraja la mawasiliano, ubunifu na uchukuliaji wa tambuko akilini. Lakini dhana si stawishi la yote na kwa jinsi ya mote katika uchukuaji wa nafasi. Dhana, mawazo na fikra vyaweza kuandikwa na kuwasilishwa lakini daima vitafaa kwa akili na utambuzi wa namna yake. Na hivi hakuna neno la maandishi ama maandiko linaloweza kuwa 'Kweli' ila tu kimvuli cha tafsiri. Ni tafsiri ya mwanadamu na kwa jinsi ya mwanadamu. Kweli haikamatiki kwa mawasiliano na ndio maana hata kama miujiza ilitendwa na Yesu, ‘Kweli’ ilibaki ni fumbo la Imani kwa watu wenyewe. Na hadi hii leo ‘Kweli’ ipo karibu sana na mwanadamu lakini yeye haitambui na hivi yeye kutafuta maana ya maisha yake kwa kufukuzia kimvuli cha muuakisiko wa hofu zake yeye mwenyewe na ujinga wa kukosa utambuzi wa kiroho na hivyo kuamini katika mamlaka ya wale wenye ushawishi wa namna za ishara za nje. Kwa kuwa ‘Kweli’ hujulikana kwa jinsi ya ‘Rohoni’.
Basi nilete maneno ya Paulo wa Tarso kama ‘msikirifu’--mystic wa namna yake katika mkondo wa mapokeo ya mafundisho ya Yesu na ndiye busara yake inaunganisha ‘Tertium Organum’ ya PD Ouspensky na Oganam ya karne ya 21 juu ya njia ya Tatu ninayoitayarisha mimi. Nayeye anataarifika kupata kusema hivi :
Walakini iko hekima tusemayo kati ya wakamilifu; ila si hekima ya dunia hii, wala ya hao wanaoitawala dunia hii wanaobatilika; bali wanena hekima ya mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu; ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangalijua, wasingalimsulubisha Bwana wa utukufu; lakini, kama iliyoandikwa,
Mambo ambayo jicho halikuyaona wala masikio halikuyasikia,
(Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,)
Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.
Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyondani yake? Vivyo hivyo mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena si kwa maneno yanayoyanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya roho. Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yanajulikana kwa jinsi ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote na wala yeye hatambuliwi na mtu. Maana, Ni nani aliyefahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.
Tafsiri hii kwa Kiswahili ni yenye kujaribu sana kwani kuna maneno yalikosa tafsiri ya moja kwa moja. Na hivi nilete ya kiingereza cha zamani kukoreza maana; ile iliyokuwa kabla ya hisani ya Mfalme James wa Uingereza katika kufadhili kazi tafsiri na uhakiki na nakala za kiingereza zilizotangulia katika jitihada zake za kuhifadhi mapokeo ya vitabu vya dini ya kikristo:
We speak the hidden mystical Wisdom of God, which God ordained before the World unto our Glory; Which none of the Princes of this World knew; For had they known it, they would not have crucified the Lord of Glory. But, as it is written, Eye hath not seen, nor Ear heard, neither hath it entered into the Heart of man to conceive the Things which God hath prepared for them that Love him. But God hath revealed them unto us by His Spirit: For the Spirit searcheth all Things, yea, the deep Things of God. For what Man knoweth the Things of a Man, save the Spirit of a Man which is in him? Even so the Things of God knoweth no Man, but the Spirit of God. Now we have received, not the Spirit of this World, but the Spirit which is of God; that we might know the Things that are freely given us of God. Which Things also we speak, not in the Words which Man's Wisdom teacheth, but which the Holy Ghost teacheth; comparing Spiritual Things with Spiritual. But the natural Man receiveth not the Things of the Spirit of God: For they are Foolishness unto him; neither can he know them, because they are Spiritually discerned. But he that is Spiritual judgeth, or discerneth all Things. “For who knowth the mind of the Lord so as to instruct him?” But we have the mind of Christ.
Nimependa kutumia nukuu nyakuzi iliyopata kutumika katika siku za Jacob Boehm wa Ujerumani miaka ya karne ya 16 na 17 kwa kuwa na yeye alikuwa ni msikirifu wa siku za karibuni aliyepata kufumbua kwa watu siri za mambo ya kiroho, naam kama ilivyopata kuwa na Dionysius, askofu wa kwanza wa jimbo la Athens-- maarufu kwa kazi yake ya Theologia Mystica, siku za nyuma zaidi; na meister Eckhart wa Ujerumani katika karne ya 14.
Shauri la ‘Jinsi ya rohoni’ ni kuzungumzia ginosia ya nafsi, ya kuwa mtu ‘hujua’ si kwa kutaarifiwa bali kwa ‘uzoefu’ wa kupitia hali ya utambuzi wa 'Moja' kati ya nafsi yake ya chini na nafsi yake ya juu. Nimeongeza neno katika msamiati wa Kiswahili ‘Usikirifu’ kukidhi tafsiri ya moja kwa moja ya neno ‘Mysticism’. Katika hali ya kawaida binadamu huwa wamependelea mambo ya mitaala ya ‘usadikifu’ na imani na hivi kusema mambo ya kiordhodoksi. Lakini mambo ya kiordhodoksi hufaa kwa watu wasiotambua shauri lipitalo unafsi wa kawaida wa mtu na wao kupendelea uhifadhina wa fikra na mawazo katika muktadha wa Theolojia na matendo ya kimapokeo. Na ndiyo hayo huja kuleta madhehebu na mgawanyiko wa taasisi za kiimani kwa mirengo ya kiitikadi za kutukuza na kuendeleza utaratibu wao.
Paulo alikuwa anajua umuhimu wa kuunganisha nguvu katika pilika na jitihada za kusambaza mafunzo ya imani na ujuzi wa kufungamanisha watu. Hii ni moja azma ya zama inayokwisha katika kuchochea watu kukaa pamoja katika namna za imani. Na hivi Paulo alijua fika Yesu ni kielelezo cha kuwaunganisha watu katika mashauri ya itikadi na hivi ndio maana alikuwa anaweza kuzungumza kuhusu uhusiano wa wanataasisi na Yesu ama ghafla akahamia kwenye elekezo mbadala la Kristo kama ‘Kweli’ ya ‘Roho wa Uzima’ katika Nia ya kudharihisha fahari ya Mbingu katika maisha ya Watu. Na ndivyo hivi kwa nini alikuwa mjuzi wa kubomoa hoja za mapokeo ya kiordhodoksi kama vile dhana ya kutokuwa na hukumu dhidi ya watu wenye ‘kuishi’ katika Kristo, maelekezi ya kushinda ‘mauti’ na ‘dhambi—uasi wa sheria za staha ya kiroho na dhana ya dosari ya moja kwa moja’ haya mawili katika muktadha wa kutambua Ufahamu wa Kristo ndani ya mtu mwenyewe. Kwa kuwa Paulo alikuwa ni msikirifu na tena mwenye kukiri uwezo na Ufahamu ndani yake wenye kupita fahamu za mwili kwa jinsi ya kiroho—mwili wa Kristo.
Na hivi kuna mahali anasema hivi:
Hata imekuwa, sisi tumemtambua Kristo kwa jinsi ya mwili, lakini sasa hatumtambui hivi tena. Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya kristo amekuwa kiumbe kipya ; ya kale yamepita ; tazama ! yamekuwa mapya. Lakini vyote pia vyatoka na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake katika Kristo ; naye alitupa huduma ya upatanisho ; yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao ; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.
Neno la upatanisho ndivyo Pythagoras alipata kufundisha miaka mingi kabla ya Yesu juu ya uhusiano kati ulimwengu wa LOGOS na NECESSITY ; ulimwengu wa Neno lenye Nguvu na ulimwengu wa Utumikishi wa Mwili wa madhahiriko. Na hivi dhana ya Kristo ni yenye kufafanisha maana mbadala kati ya ‘Kristo’ na ‘Neno la Uzima’. Kinyume na ulimwengu wa kiordhodoksi, watu huchukulia maandishi ama maandiko kama ndiyo ‘neno la uzima’... Hii ni tafsiri ya vimvuli vya unafsi wao wenyewe.
Lakini jinsi ambayo Neno la Uzima huhifadhi na kustahimilisha yote ndiyo safari ya haja ya Pythagoras kutafuta kueleza ‘Muziki’ wa utangamano wa yote yaliyopata kudhahirika. Kristo—Neno la Uzima, ni ramani na uweza wa nguvu utaokutanisha ulimwengu uliodhahirika na upasipo dhahiriko katika kutaniko liitwalo WAKATI. Na hivi Pythagoras aliliita Neno hili ni SHERIA. Kwani kila kitu hufanyika ndani ya kanuni zake. Kutokujua daraja la kanuni ni kuishi katika dhambi na mpotoko lakini kuzaliwa katika Kristo ni kukomboka na kuishi zaidi kuzidia mbali ulimwengu wa vipimo iwe vya nyakati, umbali, upana wa uso, na hata ujazo. Na kwa hivi kufaa kusema neno liko kote na pote ; hakuna palipo na dhahiriko pasipo neno—vitu vyote vimefanyika katika neno. Mbingu huhifadhi vyote vilivyodhahirika lakini yenyewe hahihifadhiki na kitu chochote cha mfano. Na hivi Neno ni kiungo cha upatanishi wa mambo ya ulimwengu wa madhahirisho-Mtu, Dunia, Nyota na Mbingu. Naye Paulo huyazungumza haya anapomulika juu ya fahari ya mwili wa nyama, fahari ya miili ya nyota—uharibika na usipouharibika. Dhana ya Mauti na Ufufuko ambayo ni ontolojia ya Kristo katika Yesu pia.
Na hivi tutazame alichofundisha Yesu kwa msaada wa kumbu kumbu ya Levi :
Sura 115
Yesu afundisha kando ya Bahari. Asimulia kielezi cha mpanzi. Asema ni kwanini yeye afundisha kwa vielezi. Aelezea kwa mapana kielezi cha mpanzi. Asimulia kielelezi cha ngano na magugu nyasi.
NA Yesu akasimama kando ya bahari na kufundisha; makundi ya watu wakabanana naye na yeye akaenda katika mtumbwi ulio karibu na kusogea mbali kidogo na ukingo wa maji, na halafu akazungumza katika lugha ya vielezi; yeye akasema, 2 Tazameni, mpanzi alichukua mbegu na kwenda shambani kupanda. 3 Kwa mikono yenye kutoa kwa moyo alizitapanya mbegu na nyingine zikaangukia kwenye udongo mgumu ambao watu wamefanya, 4 Na muda si mrefu zilikanyagwa chini na miguu ya watu wengine; na ndege wakaja chini na kuzibeba na kuruka nazo mbali. 5 Mbegu nyingine zikaangukia katia ardhi yenye mwamba ambako kulikuwa na udongo kidogo; zikakua na muda si mrefu majani yakajitokeza na kuonesha dalili njema; 6 lakini basi hakukuwa na kina katika udongo, na hakuna nafasi ya kulishwa toka mizizini, na katika joto la mchana yakanyauka na kufa. 7 Nyingine zilianguka kwenye vichaka vya majani, na kukosa udongo wa kukulia nazo zikawa zimepotea; 8 Lakini mbegu nyingine zilipata makazi katika udongo mzuri na wenye rutuba na kukua haraka, na katika kipindi cha mavuno ikakutwa kwamba mingine ilizaa na kuleta mara mia, mingine sitini, mingine thelathini. 9 Wale wenye masikio ya kusikia waweza kusikia; na wale wenye mioyo ya kuelewa waweza kuelewa. 10 Sasa, wafuasi wake walikuwa kando yake ndani ya mtumbwi, na Tomaso akauliza, ni kwanini wazungumza katika lugha ya vielezi? 11 Na Yesu akasema, maneno yangu, kama maneno ya kila mkuu, ni yenye maana mbili kwa wakati mmoja. 12 Kwa nyie wenye kujua lugha ya nafsi-roho, maneno yangu yana maana iliyo ya kuzama ndani sana kwa watu wengine kumaizi. 13 Maana ingine ya kile nikisemacho ni kile makundi yote ya watu waweza kuelewa; maneno haya ni chakula kwao; mafikara ya ndani ni chakula kwa ajili yenu. 14 Acheni kila mmoja wenu kuunyosha mkono na kuchukua chakula ambacho yu tayari kukipokea. 15 Na halafu alizungumza ili kwamba wote waweze kusikia; yeye akasema, sikieni maana ya kielezi: 16 Watu wasikia maneno yangu na kutoyaelewa, na halafu nafsi yao ya kimwili yakwapua mbali mbegu, na wala dalili ya roho ya uzima kutokea. 17 Hii ni mbegu ambayo yaanguka ndani ya mapito ya watu. 18 Na wengine wayasikia maneno ya uzima, na kwa uchangamfu wa jazba kuyapokea yote; waonekana kumaizi kweli na dalili njema; 19 Lakini matatizo yaja; kuvunjika moyo kuinuka; hakuna kina katika mafikara; dhamira zao njema zakauka na kufa. 20 Hizi ni mbegu ambazo zilianguka kwenye ardhi ngumu. 21 Na wengine wasikia maneno ya ukweli na kuonekana kujua thamani ya kustahili kwake; lakini kupenda starehe, heshima, utajiri wa mali na umaarufu wa jina kuijaza ardhi yote; mbegu hazipaji mahitaji yake nazo zapotea. 22 Hizi ni mbegu ambazo zilianguka katikati ya vichaka vya majani na miiba. 23 Lakini wengine wasikia maneno ya ukweli na kumaizi vema; wao wazama vizuri katika nafsi-roho zao; waishi maisha matakatifu na ulimwengu wote wabarikiwa. 24 Hizi ni mbegu ambazo ziliangukia kwenye udongo wenye rutuba, ambayo ilileta matunda kwa ujazi. 25 Enyi watu wa Galilaya, mpate kuangalia jinsi msikiavyo na jinsi mpandavyo mashamba yenu; kwani ikiwa mwapuuzia matoleo ya siku hii, mpanzi aweza asije tena kwenu katika zama hii ama katika zama ingine ijayo. 26 Halafu Yesu asema kielezi; yeye akasema: 27 Basi ufalme nauweza kuufananisha na shamba ambalo mtu alipanda mbegu bora; 28 Lakini wakati amelala muovu akaenda na kupanda kujaza kote mbegu za magugu; halafu akaenda zake. 29 Udongo ulikuwa ni mzuri, na hivyo ngano na magugu nyasi vikakua; na watumishi alipoona magugu miongoni mwa ngano, walimpata mmiliki wa shamba na kusema, Mtu mwovu mmoja amepanda mbegu za magugu nyasi. 32 Watumishi wakasema, Je, tuende na kung'oa hadi mizizi manyasi ya magugu na kuyachoma motoni? 33 Mmiliki akasema, Hapana, hivyo haitakuwa vyema. Ngano na magugu nyasi vyakua karibu karibu pamoja udongoni, na wakati mkivuta manyasi mtaiharibu ngano. 34 Hivyo tutaziacha zote kukua pamoja mpaka wakati wa mavuno. Halafu kwa wavunaji nitasema, 35 Enendeni na kukusanya magugu na kuyafungia pamoja na kuyachoma motoni, na mkusanye ngano yote katika maghala yangu. 36 Aliposema haya, akaondoka kwenye mtubwi na kwenda juu kwenye nyumba, na wafuasi wake wakamfuata.
Sura 116
Wakristuni wapo nyumbani kwa Filipo. Yesu atafsiri kielezi cha ngano na magugu nyasi. Aelezea kwa mapana ufunukaji wa ufalme kwa vielezi: mbegu bora; kukua kwa mti; chachu; hazina iliyofichika. Aenda mlimani kusali.
Wakristuni walikuwapo nyumbani kwa Filipo na Petro akasema kwa Yesu, Bwana, utatuelezea maana ya vielezi ulivyotuambia leo? Na hasa kile kuhusu ngano na magugu nyasi? 2 Na Yesu akasema, Ufalme wa Mungu ni umbili; una namna ya sura ya nje na ile ya ndani. 3 Kama vile uonekanavyo kwa watu hufanyika kwa namna ya watu, ya wale ambao wamefanya ukirifu katika jina la Kristu. 4 Kwa sababu mbali mbali watu mbali mbali wajazana kuubana ufalme huu wa nnje wa Mungu wetu. 5 Ufalme wa ndani ni ufalme wa roho-nafsi, ufalme wa waliosafi katika moyo. 6 Ufalme wa nje naweza kuelezea vema kwa mapana katika vielezi. Tazameni, kwani nimewaona ninyi mkizitupa nyavu zenu baharini, 7 Na wakati mlipozivutia ndani, lo, zilikuwa zimejaa kwa kila namna ya samaki, wengine wazuri, wengine wabaya, wengine wakubwa, wengine wadogo; na nimewaona ninyi mkiwabakiza wazuri na kuwatupa mbali wabaya. 8 Ufalme huu wa nje ni nyavu, na kila namna ya mwanadamu hushikwa; lakini katika siku ya kuchagua wabaya wote watatupwa, na wazuri kutuzwa. 9 Sikieni, basi, maana ya kielezi cha ngano na magugu nyasi: 10 Mpanzi ni mwana wa mtu; shamba ni ulimwengu; mbegu nzuri ni watoto wa nuru; magugu nyasi, watoto wa giza; adui ni nafsi ya kimwili; siku ya mavuno, ni mwishoni mwa kufunga zama; mvunaji ni mjumbe wa Mungu. 11 siku ya malipo*[Pia siku ya hukumu] itakuja kwa kila mtu; halafu kutakuwa na magugu nyasi kukusanyika pamoja, na kutupiwa katika moto na kuchomwa. 12 Halafu wema kung'aa kuwaka mbele kama majua katika ufalme wa roho-nafsi. 13 Na Filipo akasema, Je, yawabidi wanaume kwa wanawake kuteswa katika moto kwa sababu hawakuipata njia ya uzima? 14 Na Yesu akasema, Moto wasafisha. Wakimiya*[Watu washughuliakao na kubadili sifa za tabia za vitu kwa kanuni za uelewa wake] hutupa motoni malighafi ya chuma chuma na kushikilia kuichuja kila namna ya mabaki ya yasiyotakiwa. 15 Mali ghafi ya chuma chuma yenye kuonekana kutokuwa na manufaa kuwa imetafunwa na moto; lakini si hata chembe ya dhahabu yapotea. 16 Hakuna mtu ambaye ndani yake hana dhahabu ambayo haiwezi kuharibikika. Vitu viovu vya watu vyote vyatafunwa katika moto; dhahabu yabakia. 17 Ufalme wa kindani wa roho-nafsi naweza kuuelezea katika vielezi: 18 Mwana wa mtu aenda mbele na kutawanya mbegu za kweli; Mungu azimwagia vizuri udongo maji; mbegu yaonesha uhai na kukua; kwanza yaja majani, na halafu mashuke; na halafu masikio, na halafu ngano tupu katika masikio. 19 Mavuno yaja na lo, mvunaji abeba mavuno yaliyoiva hadi katika maghala ya Bwana. 20 Tena, ufalme wa roho-nafsi ni kama mbegu ndogo ambayo watu waweza kupanda katika udongo wenye rutuba. 21 ( Maelfu yake kwa kiasi pungufu tu kwa uzito wa shekeli moja.) 22 Mbegu ndogo yaanza kukua; yasukuma kupenya katika udongo, na baada ya miaka ya kukua kwake waja kuwa ni mti mkubwa na ndege watulia katika matawi yake yenye majani na watuwapata hifadhi katika kimvuli kukingwa na Jua na matufani. 23 Tena, ile kweli, hali ya roho ya ufalme wa roho-nafsi, ni kama vipande vya unga wa kukandwa uliotiwa chachu ambayo mwanamke huufunikia katika kipimo, tatu, na katika muda kidogo wote waumuka. 24 Tena, ufalme wa roho-nafsi ni kama hazina iliyofichwa shambani ambako mtu huipata, na moja kwa moja aenda njia yake na kuuza vyote alivyonavyo na kununua lile shamba. 25 Yesu aliposema yote hivi alikwenda peke yake katikati ya vilima palipo ni karibu na kusali.
Sura 120
Nikodemasi yupo kalamuni. Amuuliza Yesu, Je, dini ya kristuni haiwezi kuletwa mbele kwa mafanikio zaidi kwa kutengeneza upya huduma ya Kiyahudi? Yesu ajibu katika namna ya kinyume na atoa sababu. Yesu amponya mwanamke mwenye matatizo ya kuvuja damu. Amponya binti Yairo. Apotea watu wanapolitaka kumuabudu.
SASA, Nikodemasi, ambaye hapo mwanzo alikuja kwa Yesu wakati wa usiku kujifunza njia ya uzima, alikuwa ni miongoni mwa wageni. 2 Na kusimama mbele yeye akasema, Raboni, ni kweli kwamba Kanuni za sheria za Kiyahudi na matendo ya Kiyahudi haviendani. 3 Ukuhani wahitaji kufanyiwa matengenezo upya; watawala yawapasa kuwa na rehema zaidi na huruma; wanasheria yawapasa kuwa na haki zaidi; watu wa wakawaida yawapasa kutokubeba mizigo kama hiyo. 4 Lakini Je, huwezi kuongezea humo ndani yake kwa matengenezo mapya na pasipo kuharibu huduma za Kiyahudi? 5 Je, huwezi kufanya kazi zako kubwa ziendane sambamba na zile za Mafarisayo na waandishi? Je, ukuhani huewezi kunufaika na filosofia yako manani? 6 Lakini Yesu akasema, Hauwezi kuutia mvinyo mpya katika vifuko vya kale, kwani utakapojisafisha kuwa bora, lo, watanuka; vifuko vya kale haviwezi kumudu nguvu ya mtanuko; hivyo hupasuka, na mvinyo wote wapotea. 7 Watu hawatii viraka nguo iliyochakaa kwa kipande cha nguo mpya, ambayo haiwezi kustahimili msokoto wa nyuzi, mdhaifu kwa uzee, na halafu mtatuko mkubwa zaidi watokea. 8 Mvinyo wa zamani waweza kuhifadhiwa katika vifuko vya zamani; lakini mvinyo mpya wavitaka vyombo vipya vya kuhifadhia. 9 Hii kweli-ya-roho niiletayo kwa kizazi hiki ni mpya, na ikiwa tutaiweka katika vifuko vya zamani vya namna za Kiyahudi, lo, utapotea. 10 Ni lazima utanuke; vibebeo vya zamani haviwezi kustahimili na hivyo vingalipasuka. 11 Tazameni ufalme wa Kristu! Ni wenye umri sawa na Mungu mwenyewe, na wakati ni mpya kama vile jua la asubuhi; wenyewe tu ndio uwezao kubeba ndani yake kweli ya Mungu. 12 Na alivyokuwa akizungumza mtawala wa sinagogu, Yairo kwa jina, akaingia na kuinamisha kichwa miguuni pa Yesu na kusema, 13 Mkuu wangu, sikia ombi langu! Mwanangu ni mgonjwa sana, ninahofu atakufa; lakini hili nalijua ya kwamba ikiwa utakuja na kuzungumza Neno mwana wangu ataishi. 14 (Alikuwa ni mtoto wake wa pekee, binti wa miaka kumi na miwili.) 15 Na Yesu hakungoja; alitoka na yule mtu, na watu wengi wakawafuata wao. 16 Na walipokuwa wakienda mwanamke aliyekuwa akiugua ugonjwa wa kuvuja damu kwa miaka mingi, amekuwa akijaribiwa kutibiwa na waganga toka mbali na karibu, na wote walikuwa wamesema, hawezi kuishi, akainuka kutoka kitandani mwake na kukimbia njiani Yesu alivyokuwa akipita. 17 Na yeye alisema ndani, ikiwa nitagusa vazi lake, basi najua nitakuwa ni mzima. 19 Na Yesu akasikia kama vile nguvu za uponyoji zimemtoka, na kuzungumza kwa makundi, yeye akasema, 20 Ni nani amegusa koti langu? 21 Na Petro akasema, Hakuna mtu anayeweza kusema; makundi yamekubana bana; idadi ya watu waweza kuwa wamekugusa koti lako. 22 Lakini Yesu akasema, Mtu mmoja kwa imani, kwa fikara la kuponya, amegusa koti langu, kwani kipawa cha uweza wa uponyaji kimetoka toka kwangu. 23 Na mwanamke akajua ya kwamba alichokifanya kimejulikana, yeye akaja na kupiga magoti miguuni pa Yesu na kusema yote. 24 Na Yesu akasema, Imani yako imekufanya uwe mzima, enenda zako kwa amani. 25 Sasa, alipokuwa akizungumza, matumishi kutoka nyumba ya Yairo akaja na kusema, Mkuu wangu, Yairo, usimsumbue Bwana kuja; mtoto wako kafariki. 26 Lakini Yesu akasema, Yairo, mtu wa imani, usiruhusu imani yako kutetereka katika wasaa huu wa majaribu. 27 Hicho ni kitu gani ambacho mtumishi kakisema? Eti, mtoto kafariki? Lo, kifo ni nini? 28 Ni kuondoka kwa nafsi-roho kutoka katika nyumba ya mwili wa nyama. 29 Mtu ni mkuu wa nafsi-roho na wa nyumba yake. Mtu anapoinuka toka kwenye mashaka na hofu, lo, yeye aweza kuitakasa nyumba yake tupu na kuwarejesha wapangaji tena. 30 Basi akimchukua pamoja naye Petro, James na Yohana, Yairo na mama wa mtoto, alikwenda kwenye chumba cha aliyekufa. 31 Na milango ilipowafungia makundi nje, yeye akazungumza maneno ambayo nafsi-roho yaweza kuelewa, na halafu alimchukua mwanamwali mikononi na kusema, 32 Talith cumi, mtoto, inuka juu! Nafsi-roho ya mwanamwali ikarudi na yeye akainuka na kuomba chakula. 33 Na watu wote wa mji wakastaajabu, na wengi wangalitaka kumuabudu Yesu kama Mungu. 34 Lakini, kama vile jinamizi la usiku, yeye alipotea na kwenda zake.
Yesu alitumia vielelezi vyenye kufananisha utaratibu wa maisha na mazingira katika kufafanua shauri lake la Kristo na Ufalme. Maisha kama milki ya fahari ya Kristo katika mpinduko wa sura ; toka umilele na kuwa umuda ; yeye alizungumza kupambanua Mambo ya Nyakati na Msuko wa hali na Hadhi.
Kwake yeye maisha ya mwanadamu ni makutano ya jinsi ya kanuni za mwili wa nyama na hivi ndivyo kusema himaya nzima ya ulimwengu wa madhahiriko ; na vile pia, chembe mbegu ya ufahamu kwa ukweli wenye kupita yote yenye ukomo wa hali—pale mwanadamu ahusishwavyo kiuzima wake na utambuzi. Katika hali ya kawaida huweza kusemwa kwamba binadamu ana macho mawili ; moja ni lenye kuona mambo kwa kanuni za vipimo, kadri, ukiasi na kupelekea ujengaji wa hoja/fikra ; na hali jingine ni lenye kutazama hadhi ya mambo kwa wakati pasipo kujenga hoja. Basi husemwa pia jicho moja lenye kuona kwa hoja za tafsiri ndilo mkingamo wa kutambua Ufalme wa Mbingu uliopo hapa na sasa. Na ndivyo hivi kwa nini--lugha ya picha ama vielezi ni ufundi wa kuzunguka hoja na hali vile vile kuonesha hadhi ya mchukuo wa sura kwa jinsi yake na hata namna ya hali endelevu ya jambo. Na hivi pia kusema binadamu hataingia katika ‘Ufalme wa Mbingu’ hadi tu Macho yake mawili yawe Moja—kusudi apate kukirimika kwa ‘Busara’ ya Roho wa Uzima na hivi kujua hata mambo ya Kina katika ile Moja. Kuachana la lile moja jicho lenye kumponza kutoufikia ‘Ufalme’ angali likimpatia yeye namna ya utumikivu baina yake na viumbe vya dunia na mazingira yake kulingana na hisia zake na fikra za utanabaishaji... Na hivi tena Kristu ndiyo ile Njia, na Kweli, na Uzima—Neno la Uzima wote na namna ya kuipata ile Nia ya kung’amua mashauri ama maarifa juu ya yote na kote. Hakuna mwenye kuweza kuingia Ufalme wa Mbingu ila tu kwa kufanyika moja na Kristu. Kristu--jicho lenye kuona kote na kutambua yote na hali hilo halitambuliwi na mtu ila tu katika yule mtu aliyezaliwa mara ya pili katika Nuru iingaziayo kote ; kumfanya huyo mtu kuwa mwana wa Nuru. Asiyekuwa katika hii nuru kuwa ni mwana wa giza na mtu aiishiye katika nchi ya kimvuli na vina vya tafsiri kwa jinsi ya fahamu za mwili wa nyama na kwa hekima ya mambo ya kimwili.
Na hapa ndipo penye hekima ya Neno lenyewe, aliye na macho na aone, aliye na masikio naasikiye.
Oganam ya Karne ya 21 juu ya Njia ya Tatu inajengwa juu ya shauri lenye kuelekea katika Jicho lenye kuona kote na kwa nia yake ya ung’amuzi.
Jitihada za mtu kuitafuta ‘Kweli’ kusudi aje kuisimamisha heshima ya utu wake ndiyo hasa hutajwa ni ‘Kuuleta Ufalme’. Ufalme huletwa kwa matendo yenye kheri kwa kadri ya Nia ya mtu aliyekirimika kuyajua yaliyo katika hazina ya Mbingu. Mwanadamu si mkamilifu wa kutunukiwa shani ya ubora usioharibika mpaka apate kufahamu ufundi wa kujenga hekalu lake ambamo ajifunza staha ya ‘kuabudu katika roho na Kweli’.
Basi lipo jiwe liliokataliwa na Waashi wa Dunia hii ya nchi ya watu wenye kuishi kwenye vimvuli na hali ndilo jiwe kuu la pembezoni kukamilisha Hekalu lisilobomokeka na kile hasa kitovu cha ‘Ufalme’ ulio ni ule uhuru wenye kumweka mtu huru kweli kweli. Na Jicho la Tatu ndilo jicho ambamo ‘mbili hufanyika moja’ kwa wakati wowote na mtu kufanyika Moja na ‘Kweli’ ili kuuendea ustawi na ustaarabu mpya—mpangiko wa ulimwengu mpya.
Tekinokrasia ni ujenzi ; ni ujenzi kwa mujibu kwa picha na kanuni zenye kukirimika kheri. Yesu alionesha hizo ramani za ‘Mpango Mzima’ lakini matokeo ya shughuli yake yalibashirika hata kwa wenye busara wa siku hizo ; kuwa zama yake itatambua japo kidogo tu shauri lake juu ya huduma yake kuu na mshughuliko wake. Kwa kuwa kizingiti kikuu ni mlemeo wa ujinga wa fahamu za mwili na mazoea ya mapokeo na kiutamaduni wa kufikiwa. Kosekano la usafi wa dhamira katika moyo wa wanadamu wenye kuruhusu maarifa yenye kubatilisha utaasisi na mapokeo ya kale na kusimamisha mambo mapya.
Zama yake Yesu inakatikia na hii hapa sasa zama mpya ikisogea karibu kabisa. Wanadamu wote wa siku ya leo wanataharuki migogoro mikubwa ya kiustawi na mapokeo ; vile vile mitafaruku ya kisiasa, machafuko na hata mapigano. Mahodhi ya kiuchumi kwa mataifa na udororaji wa ‘ukuaji’ wake. Na katika kutazama Utaasisi wa taaluma za mambo ya sayansi na pia mawasiliano na usambazaji habari ; haya mawili kuchukua nafasi ya kuonekana kana vile ndiyo shani ya ‘ukuhani mkuu’ na ‘utowashi wake’ katika kipindi hiki katika kushawishi mwelekeo wa ukubali wa watu kuamini kitu gani juu ya maisha ama wachukuliaje taarifa—kila siku. Vile vile itikadi za kiutawala zenye kufanya mamlaka katika serikali za watu hali ni zenye kupwaya shauri kuu juu uhusishaji na vile vile maridhiano kwa raia wake wote katika sura ya mikakati ya kupanga na pia katika kutekeleza mipango ya ustawi ndani ya mipaka yao.
Mihimili ya mapokeo ya dini zote zenye idadi kubwa ya watu inaanza kukosolewa na kuumbuliwa juu ya mashauri ya uchukuliaji wake wa maadili. Ukasisi wa kusisitiza utaratibu wenye kuonekana kama ni sahihi katika macho ya wanadamu na kumbe ni njia ya mauti yenye kujishindilia aibu ya unajisi wa makusudi wa nguvu za uzazi. Uimamu unaojaza fikra za uharibifu kwa minajili ya chuki-- kwa umma wa waumin wake ili kujitoa muhanga kwa mauaji ya kukusudia na hali wao wenye siyo wenye kuonesha mfano wa kufa kwanza ikiwa mashauri hayo ni yenye kujitosheleza ukweli. Haya yote kuonesha jinsi kiu ya haja ya ushawishi huweza hata kumsukuma mwanadamu kutenda upumbafu na kuhatarisha amani na maridhiano—na hilo hatimaye kumtafuna mwanadamu mwenyewe na ustawi wake.
Maelekezo yote ya wenye kheri yaliyoleta dini na ukundiko wa kiimani sasa hayanabudi kutathminiwa matunda yake na hukumu kupitishwa. Baraza la kutoa hukumu ni utashi wenye kuinukia kwenye jicho lenye kuona kote na tena la Muamuzi mmoja kwa kila mtu mwenyewe—si tena andiko lolote wala shauri la nje nje juu ya watu kwa ujumla.
Oganam ya karne ya 21 juu ya Njia ya Tatu ni kazi ya udadavuaji kwa mwanadamu mwenye kutafuta sura ya mfananio wa utatuzi kwa mambo yaonekanayo ni magumu kutafutia majawabu katika wakati huu wa mpito kuianza rasmi zama mpya.
Oganam ni chombo chenye kutumikika katika mchakato wa kazi, na hasa pale ukwamuzi unapohitajika kwa tatizo lililojitokeza. Lakini vile vile kwa jinsi yake ni wavu wenye kuchuja yatakiwayo na yasiyotakiwa kutoka baharini.
Kupokelewa kwa kazi hii ya Oganam katika jamii ya watu wote duniani ni mashauri kuwasilishwa katika siti ya Muamuzi na matokeo yake ya kufikia hukumu juu ya mashauri ni kunawa ama kujisafisha ili kuingia Zama Mpya—na hivi ni Mavuno ; kipindi cha kutaharuki pumba na uwele vikitenganika kwa pumzi ya upepo unaovuma...
...... Inaendelea....
Nimepata kufanya Utungaji wenye kufungamana na mawaidha yajayo na mada mbalimbali katika Jukwaa hili Jamii -- kwa faragha.
Mapenzi yangu yamekuwa ni kwamba kama hali bado haijaandaliwa ama umma haujajiandaa, si vema kufunua na kubayanisha mambo ama mashauri fulani juu ya Wanajamii, Mifumo na Dini.
Ninaridhika sasa ya kwamba, ndani ya hili jukwaa kizazi sahihi cha wanamafikara kimeshawasili...
Ninafarijika na kuazimia sasa kushiriki mawaidha ambayo awali niliyafanya kwa ajili watu wenye fikra huru -- japo niliowaandikia hapo nyuma si kuwa niliwategemea hasa kunielewa, ila kuwatumia wale kama vigezo vya kuandaa matanuko wa mashauri, uono na upeo kubayanisha mambo. Kwa kuwa wapendwa wangu hasa ni wale walio ni wadadisi, wachunguzi, wenye kiu ya kuhama kutoka kwenye 'Utumwa wa Kiakili' kuelekea kwenye uwanda wa ahadi--Uhuru katika dimensha zote za mwili, akili na roho...
Kwa wale wote wanaojijua ndani yao kuna ujasiri na wito wa kutoka, safari hii imeshaanza...
Tutaelekezana, kutaamulisha, kupashana, kufundishana, kufundwanishana n.k kusudi hakika ya Taifa Jipya la watu -- watu walio Wapya kwa Mioyo na Dhamira katika kuongozea kuliko bora zaidi iweze kutimia.
Ninawahakikishia uwezo wa kusonga kwenye kheri upo, na mambo makubwa sana yanatungojea safarini... Kwa kuwa safari hii ni safari ya ajabu, maana zawadi yake ni ulimwengu wote kuutwaa... Anga si kikomo...
Niwatake na kuwasihi enyi kizazi cha mitazamo huru na wazi zaidi kwa kheri na jaala njema zaidi, msikatishwe tamaa na lolote kulingana na hapa tulipo kwa kufananisha na kule tunakotamania...
Tuelekezana yote kwa lugha ambayo wote tunaifahamu vizuri -- Kiswahili, tutazungumza yote kuhusu 'Nishati' hadi 'Wakti'... Tutahandisi mambo na mitambo ya kuweza kuyafanya hata makuu--kimawasiliano na uchukuzi... Tufanya namna mpya kuvuna nishati, na tutasafiri hata nje ya sayari yetu ya dunia kwa namna moja hata nyingine... Haijalishi hili litatimia ndani ya miaka 80 - 100 ijayo-- ila ninawahakikishia sehemu ya hizi jitahada zitakuwa hapa hapa kwenye hii ardhi yetu tuuitayo Tanzania kwa leo na Afrika kwa kesho... Kwa kuwa roho ya ushindi huu tayari ipo miongoni mwetu, na kazi ni kwetu...
Msihofu miongoni mwetu ni nani atatuongoza... Zama hizi si zakuongozana. Kwa kuwa tupo katika zama ambazo Uongozi ni Kuchagua na Kujichagulia. Kila mtu kwa nafsi yake yampasa kuamua, ikibidi kuunganisha nguvu zetu kwa ajili ya jambo lolote la kheri ya pamoja, tutajaunda namna ya taasisi zisizoongozwa na 'siasa' za utaratibu ila 'itifaki' sahihi na uelewa kamili juu ya jambo liwalo lolote.
Na sasa nilete kwenu, mashauri anuai -- mapana na marefu juu ya kile ninachokifananisha na kumbukumbu la vitabu vitano vya Musa -- Pentauki, kwa maana ili kufika ustawi na staarabu mpya mambo kama yale yale yaliyosadifiwa kwenye vitabu hivi vya mapokeo yatahusika kwetu sote... Japo huu inakuja kuwa kile ambacho Francis Bacon alikitaja kuwa ni 'Instauration of Knowledge' katika kuielekea 'Atlantisi Mpya'...
Ni wakati wa kuyaupisha mafundisho na maarifa ya zamani...
+++++++++
Kutoka: Mwongozo Hai kuelekea Uhuru Halisi seh. I
5 Septemba 2011 saa 12:15 Asubuhi
Kutoka: Mwongozo Hai kuelekea Uhuru Halisi
(Iliandikwa kwa rafiki kama mchango wa mawazo na kwa uchochezi wa fikra)
Pendo lililobarikiwa dada MwKT,
Siku kadhaa nyuma ulileta habari jukwaani juu ya ‘Kuanzishwa kwa “un-women” – kaeni mkao wa kula’ katika jukwaa la siasa.
Nilipendezwa na habari hii na hasa kwa kuzingatia mapenzi yangu juu ya mabadiliko yenye kuleta kheri katika jamii niishiyo na ulimwengu kwa ujumla. Ni jambo lenye kupendeza kutambua harakati za watu mbali mbali na kujaribu kuunganisha maono ama kufanya fikra tunduizi.
Amko la wanaharakati katika kutunga na kupelekea taasisi kama chombo chenye kuongezea kwenye ushawishi, utendaji chini ya mamlaka, mifumo na utekelezaji wa mipango ama maelekezo; linavutia wote walio na dalili za kuamkia huko kimwelekeo wa fikra na imani lakini pia zaweza kuvuta ukosoaji wa kiudhanifu—yaani juu ya dhahania ya mpango mzima vile kusema, filosofia ama asili ya mwongozo wake na misingi ya ustawishi wa jitihada.
Kwanza kabisa nitambue ‘unene’ na uzito wa michakato uliopo katika vyombo vya kimataifa na utengeneaji wake. Itifaki zake ni namna ya mifano yenye kufafanua mifumo na taratibu katika kuratibu matukio kulingana na makutano ya watu na michakato. Na hivi nitambue msuko wa chombo kama namna ya mipaka na mamlaka juu ya mambo yake na tena kwa muktadha wa kufanyika kwake.
Ujio wa chombo hichi kwako umekusukuma kupenda kuwaatarifu wanajamii wenzako; maana yake: uwezekano wa fursa mbali mbali--ajira, na mipango ya maendeleo. Na vile vile umepata kusema : hivyo havitaweza kuja kwenye sahani ya dhahabu… Kisha ukazungumza juu ya ‘nafasi za juu’… Halafu ukataja mjumuisho wa mataifa na hivi kuonesha kutambua msukumo wa nguvu ya uwezo na ushawishi kulingana na sehemu watu watokayo kmf Amerika ya Kati, Scandinavia na nchi nyingine za Afrika katika ugombeaji wa nafasi za kazi na labda vile vile kumaanisha vyeo vya usimamizi na utendaji pia.
Pia ukazungumza dokezo la kukabiliana na adha ya shughuli kwa kutaja umuhimu wa watarajiaji nafasi kudumu kukesha katika jitihada kwa kufuatilia kwa makini nyenendo za michakato ya uanzilishi.
Nikushukuru kwa angalizo na kushiriki habari na wenzako kama mimi na wengine.
Niliingie neno la leo kwa kutanabaisha jambo kuhusu ulimwengu wa kuona mambo kwa kiini cha usababishaji na matokeo yake.
Tumezoea kuona mipango ikipangwa na jitihada kusukwa na matokeo kuainishwa ili kuelekeza sura ya utendaji na utekelezaji. Binadamu toka zamani hadi hii leo tunaona upangiliaji wa mambo ni kama sanaa inayoweza kufanywa kamilifu ijapokuwa matokeo yake si kwamba daima huwa ni hivyo. Kuna vitu vinaweza kupangilika lakini mara kadha wa kadha mashauri juu ya watu ama jamii si yenye kupangilika na kujitosheleza bila mikingamo ama kadhia ya namna fulani kujitokeza. Labda hii tuseme inatokana na ukweli kwamba binadamu ni kiumbe chenye uwezekano wa fikra binafsi na utashi na hivyo haiwezekana kuwakundisha watu pasipo ridhaa na makubaliano na wao wenyewe kwa wakati.
Basi katika ulimwengu wa makubaliano kuna yale ya juu juu na kuna yale ya ndani. Vivyo hivo kuna kuona mambo kwa sura ya juu juu na kuona mambo katika sura ndani. Naam, vile vile kuchukulia jambo kwa sura ya nje na kuchukulia mambo kwa sura ya ndani. Uhusiano wa mambo ya ndani na yale ya nje ndiyo hujaa kuzaa uthabiti wa makubaliano na labda pia kusema, umadhubuti wa jitihada kulingana ufananikaji wa dhamira. Hata hivyo, kupo kuridhika na mambo ya nje bila kuchunguza misingi yake; na hata tena kwa namna kama hiyo; kutotambua athari za matokeo kwa kutozingatia uasili wa jambo lenyewe kwa uzima wake. Haya mawili hujitokeza hasa katika maisha ya mwanadamu kwa kutoangalia/ujisahau wake wa mashauri yaandamayo dhamira zake kwa wakati hadi wakati.
Na hivi leo ningependa kuzungumzia nafasi ya Tekinokrasia katika ustawi mpya kwa wanadamu katika zama hii mpya.
Nimechagua mchango wako toka jukwaani kujenga usuli wa shauri langu la leo kwako na kwa wadau wengine; kwa kuwa wanawake katika zama hii wanachukua sura takatifu ya michakato ya jamii na ustawi. Na hivi udadavuaji wa utata wa hali ya ustawi wa jamii unachipukia na kuanza kwa kumuelewa mwanamke na sifa ya kike ya uumbaji wote--jambo lililosahaulika katika nidhamu na uelewa wa wanadamu wa leo.
Katika hali ya juu juu shauri lako juu ya uanzishwaji wa baraza la wanawake-umoja wa mataifa, umelenga hasa fursa za ajira na labda kwa upande mwingine usiowazi ni shauku yako ya chombo hiki cha wanawake na kwa ajili ya wanawake. Kuangalia upande wa ajira-- na hapa umewakumbusha hata wanaume pia kutazamia nafasi; kulinikumbusha mashauri juu ya uchumi na siasa—na miye nikapata hamu nije kushiriki na wewe na wengine fikra tunduizi mintarafu vyombo vya jamii na nafasi yake katika kuchochea ama kuleta mabadiliko.
Jambo la kwanza ambalo halinifurahishi na vile kuniacha nikisikitika ni ukweli wa kwamba nafasi za kazi na ajira kugombaniwa na kushindaniwa. Ni ukweli mchungu na ambao mimi siupendi kabisa. Naitekeleza chuki yangu dhidi ya huo kwa kuleta fikra mbadala za jinsi ya kutokomeza sura hiyo ya mambo kwa ghadhabu ya kuwakilisha mawazo ya upeo na maarifa yangu kwa wakati. Lipo tatizo kubwa katika jamii ya leo ambalo ladumu kwa mwendelezeo ama udumishwaji wa dhana ama pia fikra ya kuwa maisha hayanabudi kustahimilishwa kwa urasmi wa ajira za kazi kwa ajili kipato kwa kutumikia chombo fulani na hata kama makusudi mazima ya hicho chombo si yenye kueleweka kwa mtu husika kujihusisha nacho—ama kupimwa/kujipima ikiwa mna dhamira bora kabisa kuwezekana ya utashi ndani ya mtu mwenye kutaka kujihusisha hicho chombo. Hili kwa leo sitazungumza sana kwa maana ni shauri linapelekea kipengele kimoja katika tatu cha kuyaleta mabadiliko kamili ya kijamii katika muktadha wa kufafanua Meritokrasia. Leo nataka kuzungumzia Tekinokrasia kwa mapana.
Dhana ya ushindani kwa lolote lile ni jinsi ya kiume ya mambo. Akili inayofikiria katika minajili hii ni namna ya akili ya kiume. Jamii inayovumilia na kudumisha mashindano ya huyu kupata na yule kukosa, ni yenye jinsia ya kiume na bila shaka inadumisha namna ya mifumo dume katika kusimama kwake.
Mchezo wa ajira ama kutafuta kipato unachezwa katika kiwanja cha uchumi na mabadilishano ya kijamii. Ikiwa mtu hatataka kuusoma uwanja kabla ya mpambano hapana shaka mtu huyu atakuja kutingwa na adha ya ujinga wake kwa kukosa maarifa ya kutosha katika kuungia mchezo. Matokeo yake katika kuuelekea mwisho wa mchezo au kadri mchezo ukiendelea--huenda yakaambatana na dosari nyingi ambazo zitajitokeza kwa sura ya kama mtu kupata hiki kwa gharama ya kukosa kile; ama kupata hili badala ya lile lililotarajiwa ama kutakwa. Basi yampasa mtu kuwa ni mwenye kujitambua ili apate kutambulika katika uwanja wowote wa jitihada chakatuzi. Na hivi aje kuvuna matokeo kwa stahiki ya nia yake katika jitihada sahihi.
Na hili linajenga hoja ya msingi katika filosofia ya Tekinokrasia. Kweli ya kwamba mtu hawezi kuunda bila ya kuwa na ramani; hawezi kuanza safari na hali hajui mapito; hawezi kukatiza kokote eti akafikiri atafika kwa kuwa tu mwenye kutimba maguu… Je, ajijua yeye ni msafiri? Je, ajua uhusiano wa hapo alipo na kule anakokwenda? Je, ajua akiba yake safari na vipindi vya kuitekeleza hiyo safari? Je, ajua jambo la muhimu katika safari ni safari yenyewe? Na je, yu ajua yeye kuwa palipo na nia daima safari hazikomi na hivi penye nia pana njia ? Na basi lilikokuu kuliko yote-- je, yeye yu ajua Nia yake ambayo ni ufunguo wa dhamira yake mwenyewe ?
Kukosa kuelewa Nia zetu hasa daima kutatuacha sisi kama watangajitangaji katika nchi za wageni. Ni kusahau tulikotoka na hivi vile vile kutokujua hasa ni wapi tunakwenda. Pilika za maisha na mahangaiko yanaweza kutia upofu wa tafsiri juu ya maana zetu za kuwa ni wenye kuishi na kuwa hai--binadamu kukosa jicho la kupima uhusiano kati ya mazingira na mambo ya nyakati--katika siti za utu wetu, uzima na busara. Kuangalia chakula, malazi na mavazi kwaweza kumtinga asione maana ipitayo yote yenye kufanyika na yeye kuhifadhika kwamo. Mtu, Dunia, Nyota na Mbingu vinautumikishi wa kimoja kwa mwenzake ; na vivyo hivyo kuonesha dalili ya fumbo la namna ya uhifadhiko kati ya vinavyoonekana basi ndani ya vile visivyoonekana.
Basi natuukague uwanja wa mchezo.
Nia ni mkuki wenye kuleta mwelekeo wa wakati na jitihada. Kutoka na Kufika ni uhifadhiko katika ulimwengu wa madhahirisho. Na hivi wakati si kitu ila tu rajisi ya mabadiliko katika utambuzi wa mtu. Bila nia hakuna badiliko na bila mwili wa madhahiriko hakuna muda wala wakati. Na vile vile pasipo na utambuzi hakuna rajisi ya wakati na wala nia yenyewe. Lakini katika namna yaajabu maisha/uzima ni uhifadhiko wa haya yote katika moja. Itokeapo namna ya utambuzi uliofanyikia katika hiyo moja lakini usijitambue uhifadhiko wake katika moja basi ndipo nia huzaliwa na wakati kuwepo.
Tutatazame mambo ya nyakati na wakati.
Mtu ni kutaniko la uzima wa mwili na karama za yasiyoonekana kwa macho ila tu kutambulika kwa ishara zake. Shani ya utu ni matokeo ya kubebea ndani hadhi ya namna bora za vitu/mambo/matendo kufanyika. Na kuna namna ya kumuona mtu kama mchakato hai miongoni mwa mambo matatu—nia, uwezo na maarifa/busara katika ishara ya sura tuiitayo ‘Uzima’ pale hayo matatu yanapotunukiwa mwili wa madhahirisho wenye kudhihirisha ‘chanzo-sababu / hisia-matendo’ ; kwa kupitia nia na uwezo katika kuhadhikisha kitendo na matokeo yake. Basi haya yakutanapo huzaa sura ya mambo iliyo ni dhana ya Muda na matukio-- vile pia kusema msongo wa wakati kulingana na tafsiri itegemeayo nuru yenye kumulika dhamira ya utambuzi katika siti ya utu wa mtu na akili/kumbukumbu. Na hivi mtu anayonafasi ndani yake yenye kuweza kudadavua mambo ya nyakati na hali pia wakati huo huo anayokurunzi isiyokamatika katika dhana yoyote ya wakati. Kurunzi hii ndiyo mwenge wa busara yake ishindayo tafsiri zote zenye mwanzo na mwisho ; inayomulika na hali yenyewe haimulikwi. Na hivi mengineyo yote kuwa tu ni vina vya tafsiri vya mambo vimvuli kwa ‘Kweli’ ya ‘Moja’ ; kufanya mukabala wa kumbukumbu.
Tutazame vimvuli vya watu na vina vya tafsiri.
Vimvuli haviishi ila tu kwa nguvu ya udhanifu wa mtu ; huhuishwa katika sura ya tafsiri yenye kujaribu kukidhi haja ya kupunguza ama kuondoa mashaka juu ya mashauri ya ustawi wa watu na makabila katika pia kufafanua utambulisho wa mambo yao ambayo kwa ujumla huitwa utamaduni na ustaarabu. Na jinsi hii, watu wa makabila ama utaifa kuwa daima katika kutafuta kujitambulisha kwa jinsi ya kutetea, kudumisha mambo yao yanayowafungamanisha ama pia kuonesha msisitizo wa mapokeo yao juu ya nchi na tawala ; kwa kuyaenzi hayo. Lakini watu pia ni wenye kujua sana dhamira zao za kimakundi zaweza kuharibiwa na hata kuharibika mapema pale zipambanapo uso kwa uso na tamaduni nje ya mizingo yao. Na hivyo binadamu katika sura ya kijamii huwa na namna ya kulinda mila, desturi na mapokeo yao yaliyo ni ishara ya utambulisho wao kwa pumzi ya nguvu ya uwezo wao.
Historia inaonesha jitihada zote za wanadamu katika muktadha huu zimezaa kuinuka na kuanguka kwa mataifa ya makabila na vipindi vya utawala kwa wale waliokamia hilo; kwa kukutana uso kwa uso na wale waliothubutu kuleta mpishano katika kupanda na kuporomoka kwa mataifa/makabila hasimu. Basi nia za chini za wanadamu zenye kutawala matendo yao ni zenye namna ya kukosa utangamano miongoni mwa mataifa na makabila na daima hutoa ahadi kubwa kubwa kwa makundi ya watu na hali katika kupita kwa wakati huleta pia majonzi, vilio, maasi na mambo yote yote yaliyokosa ubarikika.
Basi binadamu kwa jinsi hii ana nafsi mbili ; ya chini na ya juu. Ya chini ni ile yenye kuzaa makusudio yenye kuharibika upesi na hivi ni kimvuli tu cha nafsi ya kweli isiyoweza kuharibiwa wala kunajisiwa na mashauri ya mwili wa nyama wenye maradhi ya kuridhi ya kupenda kujipendezesha nafsi na kujihifadhi kwa mahodhi ya mali ama starehe za nchi/dunia na hivi mwili wa madhahirisho.
Nafsi ya juu ya mtu ni hazina kwa yale yote yasiyodhahirika na ni kioo kwa utambuzi wa mawezekano yaliyoko katika nyakati zote na fumbo kuu la imani kwa mtu. Ikiwa 'Mungu' ni dhana yenye kuwakilisha moja na moja na moja katika moja ; basi ndani ya mtu kuna daraja-mbegu ambalo ni lenye kuweza kusemwa mtu na mungu ni moja pia katika muktadha wake. Na nuru ya ufahamu wa mtu ndiyo muujiza mkuu kuliko wote wa dhahirisho la Uzima katika ‘mwili wa madhahirisho’ na ‘pasipo udhahirisho’ vile vile. Lakini mwanadamu akiwa ni mwenye kulewa sana na mvinyo wa fahari za mwili wenye kuharibika ; huishi kupenda kudumisha kimvuli cha nafsi yenye kufa na kutotambua namna ya fahari yake isiyojua mauti wala kuzaliwa—Ukweli juu ya ‘uzima wa milele’. Na hivi anguko la mwanadamu ni dhana ya mwanadamu kujitambulisha na mwili wenye kufuata sheria ya mauti na adha zake zote na hivyo kuuona ulimwengu katika jicho la namna hiyo. Na ndiyo katika kisomo cha leo tunaita namna hii ya jambo—‘dainetenia’ ya utambuzi ; mtu hutaka kuona kile anachopenda kuona kudumisha kile anachokidhania na kuwa kipofu wa vinginevyo vyote.
Nilipata kudokeza ya kwamba kazi niliyofanya kusanifu USANISI WA UJASIRIAMALI WA KIJAMII, Oganam ya karne ya 21 juu ya njia ya tatu-- ni mkamilisho wa kujumuisha kazi za Pythagoras, Yesu na Buddha katika kuwakilisha sura halisi ya mabadiliko ya kiustaarabu tunayoyaingia. Basi kwa jinsi hii Pythagoras ni kiungo kati ya Ufahamu kwa mujibu wa Yesu kuelekeza mafundisho; na kujaribu kwake kuwasilisha namna ya uelewa wa maumbile ; yeye pia ni kiungo katika kukutanisha maelekezo ya Yesu na yale ya Buddha ambayo yote kwa pamoja ndiyo mhimili wa fahari ya zama hizi katika ustawi na neema. Na hili halina budi kufafanuliwa kwa maelezo zaidi. Na tena si katika mrengo wa kiordhodoksi ila sayansi halisi ya ukweli wa mambo. Kwa kuwa mimi si muumin wa dini yoyote ya kimapokeo na wala sipendekezi kwa mtu yeyote usadikifu wowote iwe wa 'Mungu' ama mambo yajayo/yaliyopita/yaendeleyo kwa jicho la upofu wa fikra ya udhanifu na hofu. Usadikifu ni kasumba na hadhi ya sifa dumazi--haimtii binadamu heshima ya ‘kweli’ ya utu ila tu kimvuli chake.
Kwa kuwa kutokana na Pythagoras ninazungumza mambo ya nyakati na utangamano wa vitu/mambo kihadhi na pia ukiasi wa namna yake katika msuko ya yote yanayoonekana na yale yasiyoonekana. Na hivi Pythagoras anawakilisha Wakati na mshahibiano wake na mtiririko wa madhahirisho, Yesu anawakilisha Tekinokrasia na Buddha anawakilisha Meritokrasia ; lakini mwenye kuvitanganamisha vyote hivi ni Pythagoras.
Na sasa basi nimtambulishe Yesu kama mtu aliyeyajua haya kwa kutangulia na kujaribu kuleta msogezo wa dhana na pia fikra miaka kadhaa iliyopita ; takribani kipindi cha zama moja toka leo—kadri tuzisomapo tabia za mabadiliko ya watu kimakundi na mnyambuliko wa hadhi na ustaarabu wao ; twazigawanya hizo katika vipindi tuvitajavyo kama zama.
Basi Yesu alijua dhahiri jitihada zake zilikuwa ni kipindi cha matayarisho lakini matunda yake halisi ama kusema musimu wa kuchanua ni zama moja mbele katika mwendo wa hatua za mabadiliko ya kiustaarabu na hadhi ya utabia kwa wanadamu. Lakini tena katika utambuzi ndani ya daraja-mbegu ; fahari yake kamili yeye alipata kuiita ni ‘Ufalme wa Mbingu’, ni vile kutamka bayana kuwa upo karibu na hapa na vile pia kusema upo ndani ya mtu na labda tu akizaliwa mara ya pili si kwa jinsi ya mwili wala kiakili na wala kihisia za mwili bali kwa jinsi ya ‘roho wa uzima’-- huwa moja na huo na hivyo kuwa ni ‘Mfalme’. Kwa kuwa wakati si kitu katika roho wa uzima ijapohali hili ni shauri gumu kuenea katika uelewa wa kawaida wa mtu asiyetaamulika, aiishiye katika uwanda wa nchi ya vimvuli, ila tu kuelekezwa yeye kwa namna ya picha za vielezi vyenye funguo za kuleta ishara ya ukweli wenyewe ulivyo.
Basi kabla ya kuyadadavua mashauri ya ontolojia kwa mujibu wa Yesu tuikague kazi yake kulingana na kumbukumbu zilizopo na mapokeo. Yeye ni mtu mwenye kukumbukwa kwa kulingania ‘Ufalme Mpya’, pia kusihi umma kuwa tayari kuupokea ‘Ufalme’. Alikuwa ni muasi wa sheria na desturi na huku akisisitiza kuzikamilisha hizo kwa Sheria Mpya. Alipata kukiri kiulaini tu kuwa yeye ni ‘mwana wa mungu’ na vile kusisitiza pia kuwa mtu yeyote kwenye kuzaliwa tena kwa jinsi ya roho hufanyika ‘mwana wa mungu’. Pia alitamka bayana kwa kukumbushia, kusema binadamu ni ‘miungu’; wana wa aliye Juu (katika Mbingu). Aliponda dhana ya watu kutaka ishara ili kujiridhisha usadikifu juu ya karama za kimamlaka ya wadhifa/ukiongozi mkuu kutarajiwa ama unabii mkubwa--akikwepa kuridhisha watu na siasa zao. Lakini hapo hapo ikitaarifika kufanya ‘miujiza’ ya wenye kuwa ‘viziwi’ kusikia, wenye ‘upofu’ kuona, walio ‘bubu’ kuzungumza, Kuzungumza na ‘vipepo’ vyenye kuendesha Pepo na dhoruba za mawimbi ya bahari nahivyo ‘vipepo’ kumsikia na kuitika kwa kutuliza tafrani… Yote hayo kukimbia sifa za kiuanadamu ila tu kuitikia hitaji la wakati.
Shughuli ya Yesu ilikuwa na mwanzo wa upacha na binamu yake aliyeitwa Yohana. Machache hujulikana kuhusu Yohana katika mapokeo ya vitabu kama vile pia kukosekana kwa simulizi la maisha ya Yesu kati ya miaka 12 na mpaka kuja kukutana na Yohana akiwa na umri wa kama miaka 28 katika ile shughuli isiyofafanuliwa kinagaubaga ya ‘Kubatiza’ ambayo alikuwa akitenda binamu yake huyo katika ukingo wa mto Yordani.
Labda ikiwa shughuli ya Yohana ingehifadhika kwa kina katika kumbukumbu za simulizi za kimaandishi, ‘ukweli wa ishara’ ya tendo lenyewe la ubatizo ingeng’amuliwa vema na uhusiano wa shughuli za hao wote wawili mbele za umma kufahamika vema.
Basi kulingana na simulizi mbadala toka kwenye kumbukumbu la matendo yote ndani ya nyakati inatupasa kutafuta majibu. Upo ujuzi wa kuona matukio katika ‘kitabu cha uzima’ na ambapo yeyote aweza kuzisoma kumbukumbu za mambo yaliyotangulia kwa vipeo vyote vya taarifa: picha, maneno, harufu, hisia n.k… Basi nitumie msaada wa Levi Dowling , aliyepenyezea kiufahamu ndani penye ‘Akasha’—mahala pa kumbu kumbu zote, kuwakilisha ujaziliazi wa simulizi kosekanifu.
Nimepata kutafsiri kazi ya Levi na hii hapa ni nukuu nyakuzi:
SURA 7
Arkelausi atawala mamlaka. Mariamu na Elizabeti pamoja na wana wao wapo Soani na wafundishwa na Elihu na Salome. Somo la Utangulizi la Elihu. Asimulia juu ya mfasiri.
Mwana wa Herode, Arkelausi, alitawala mamlaka yote katika Yerusalemu. Alikuwa ni mbinafsi, Mfalme mkatili, aliwaua wale wote wasiompa heshima yeye. 2 Aliita barazani wote wenye hekima zaidi juu ya watu na kuwauliza kuhusu mtoto mchanga mwenye kudaiwa kustahiki kiti cha ufalme wake. 3 Baraza likasema kwamba wote wawili Yohana na Yesu walikuwa wameshakufa; basi na yeye akaridhishwa. 4 Sasa Yosefu, Maria na Wana wao walikuwa chini katika Soani, na Yohana alikuwa na mama yake katika vilima vya Yudea. 5 Elihu na Salome wakawatuma wajumbe kuharakisha kuwatafuta Elizabeti na Yohana. Waliwapata nao wakawaleta wao Soani. 6 Sasa, Mariamu na Elizabeti walikuwa wakistaajabia sana kwa sababu ya kukombolewa kwao. 7 Elihu akasema, si ajabu, hakuna matokeo tu; kanuni hutawala kuendesha matukio yote. 8 Kutokea nyakati za nyuma sana ilishapangwa kwamba mtalikuja kuwa nasi, na katika shule hii yenye kutunzwa kusudio safi ili kufundishwa. 9 Elihu na Salome wakawachukua Mariamu na Elizabeti nje kwenye ua takatifu karibu na pale ambako wao walikuwa na desturi kufundisha. 10 Elihu akawaambia Mariamu na Elizabeti, mwaweza kujionelea furaha ninyi wenyewe mmebarikiwa mara tatu, kwa kuwa ninyi ni mama wateule wa wana walioahadiwa kipindi kirefu, 11 Wao ambao ilivyopangwa kuwekewa mkono kuja kuweka mwamba mgumu imara msingi jiwe wa uhakika ambao juu yake hekalu la mtu kamilifu litasimama--hekalu ambalo halitaweza kamwe kubomolewa. 12 Twauhesabu wakati kwa mizunguko ya zama za vipindi, na lango kwa kila zama twasema akilini ya kuwa ni jiwe la maili katika safari ya kundi la watu wa sifa ya namna moja. 13 Zama zimepita; lango kuelekea kwenye zama ingine lafunguka wazi katika kugusa kwa wakati. Hii ni zama ya maandalizi ya nafsi roho, ufalme wa Imanueli, wa Mungu katika mtu; 14 Na hawa, wana wenu, watakuwa ni wa kwanza kueleza habari, na kuhubiri injili ya mapenzi mema kwa watu, na amani duniani. 15 Kazi kubwa ni yao; kwa kuwa watu wa miili ya nyama hawataki Nuru, wao walipenda giza, na pale ambapo nuru yang'ara gizani wao hawaitambui. 16 Twawaita hawa wana, Wafunuaji wa mwanga; lakini inawapasa kuwa na nuru kabla ya wao kuweza kufunua nuru. 17 Na yawalazimu kuwafundisha wana wenu, na kuzitia moto nafsi-roho zao kwa upendo na msisimko mtakatifu, na kuwafanya wao kuwa macho fahamuni na mpango wao mahsusi kwa wana za watu. 18 Wafundisheni kwamba Mungu na Mwanadamu ni moja; ila kwamba kupitia mawazo ya mwili wa nyama na maneno na matendo, mwanadamu hujirarua mwenyewe mbali na Mungu; kujishusha hadhi yeye mwenyewe. 19 Fundisheni ya kwamba Pumzi Takatifu italiwafanya wao moja tena, kurejesha hali ya kwenda kwa utangamano; 20 Kwamba hakuna chochote chenye kuweza kuwafanya moja ila Upendo; kwamba Mungu ameupenda sana ulimwengu hata kumvika mwana wake katika nyama ili kwamba mwanadamu aweze kutambua. 21 Mwokozi pekee wa ulimwengu ni upendo, na Yesu, mwana wa Mariamu, aja kudhahirisha pendo hilo kwa watu. 22 Sasa, pendo haliwezi kudhahirika mpaka njia yake iandaliwe, na hakuna chochote chenye kuweza kuivunjilia mbali miamba na kuangusha chini vilima vilivyo kwea juu sana na kujazia juu mabonde, na hivyo kutayarisha njia, ila usafi wa moyo. 23 Lakini usafi wa moyo katika maisha wanadamu hawatambui; na hivyo, huo, pia, waja katika mwili wa nyama. 24 Nawe Elizabeti, umebarikiwa kwa kuwa mwana wako ni Usafi wa moyo kufanyika nyama, na yeye ataifanya njia kwa Pendo. 25 Zama hii itatambua ila kidogo tu juu ya kazi ya Usafi wa Moyo na Upendo; lakini hakuna neno limepotea, kwa kuwa katika kitabu cha kumbukumbu cha Mungu ingizo lafanyika kwa kila wazo, na neno, na tendo; 26 Na pale ambapo ulimwengu u tayari kupokea, lo, Mungu atamtuma mjumbe kufungua kitabu na kunakili kutoka kwenye kurasa zake zilizohifadhika patakatifu ujumbe wote wa Usafi wa Moyo na Upendo. 27 Na kisha tena kila mtu wa juu ya nchi atayasoma maneno ya uhai katika lugha ya nchi yake ya kuzaliwa, na wanadamu wataiona nuru, kutembea katika nuru na kuwa nuru. 28 Na mwanadamu tena atakuwa mmoja na Mungu.
Zama inayokwisha ni zama za ya ‘Maandalizi’ na hivi kwa imani binadamu amepata shauri la kuogelea katika ‘bahari’ ya kweli ya uzima wote akiwa kama samaki asiyebudi kuwa na kiu. Kwani lugha ya ishara na vielelezi aliyotumia Yesu ni ufundi wa kufungua pazia la mkingamo wa udhanifu dhidi ya ‘Kweli’ na uchukuliaji wa hadhi ya matendo katika kumwandaa mtu na upokeaji wa ‘busara’ ya ‘roho wa uzima’ kama Yesu alivyoijua na yeye kujulikana katika hiyo. Na hivi kila mtu aweza kufunguka kwa kadri ya stahiki yake kwa wakati na hali kielelezi kikiwa vilele. Na vile vile kuthibitisha jinsi binadamu awezavyo kujifunza kwa kushirikisha ubongo wenye kutenda kazi kwa kutumia picha za mfano na mashauri yenye mantiki/changanuzi; na Yesu alikuwa muepesishaji wa mawasiliano ya ndani ya mtu katika kuchochea utambuzi wa kiroho.
Mapokeo ya mafundisho ya Yesu yameleta mkondo wa imani na taasisi za dini. Ni ushawishi na msukumo wa vitendo ndivyo vilivyozaa mwongozo katika sura ya dini na mtapanyiko wake wa madhehebu. Kwa kuwa fikra na hisia-kutenda zikinogeshwa kwa itikadi huweza kusimamisha utaasisi wa watu na msukumo wa ushawishi. Na hivi twaweza kutazama finomena ya dini kama Ukristo ulivyo kuwa ni kama chombo tu chenye mfano wa utumikivu wa mwanadamu katika kufanikisha kazi fulani. Lakini la msingi ni kuelewa utaasisi ni kitu gani na ‘Kweli Halisi’ ni kitu gani. Taasisi ni ubunifu wa mwanadamu ; ‘Kweli’ haina ushirika wa moja kwa moja na utaasisi ingawaje utaasisi waweza kutengeneza mazingira ya ‘Kweli’ kumea katika wanataasisi husika. Hili hutazamwa na kupimwa kwa ‘matunda’ ya taasisi yenyewe.
Taasisi ni kifungo cha kufungamanisha na itikadi na ushawishi; Kweli haina mipaka na ni hadhi ya mbegu ya yote yenye kufanyika na kudhahirika. Dhana vile vile ni kitu chenye sura ya ukikomo na hivi haewezi kuwa ‘Kweli’. Dhana ni chembe katika mwili wa ufikirifu katika daraja la mawasiliano, ubunifu na uchukuliaji wa tambuko akilini. Lakini dhana si stawishi la yote na kwa jinsi ya mote katika uchukuaji wa nafasi. Dhana, mawazo na fikra vyaweza kuandikwa na kuwasilishwa lakini daima vitafaa kwa akili na utambuzi wa namna yake. Na hivi hakuna neno la maandishi ama maandiko linaloweza kuwa 'Kweli' ila tu kimvuli cha tafsiri. Ni tafsiri ya mwanadamu na kwa jinsi ya mwanadamu. Kweli haikamatiki kwa mawasiliano na ndio maana hata kama miujiza ilitendwa na Yesu, ‘Kweli’ ilibaki ni fumbo la Imani kwa watu wenyewe. Na hadi hii leo ‘Kweli’ ipo karibu sana na mwanadamu lakini yeye haitambui na hivi yeye kutafuta maana ya maisha yake kwa kufukuzia kimvuli cha muuakisiko wa hofu zake yeye mwenyewe na ujinga wa kukosa utambuzi wa kiroho na hivyo kuamini katika mamlaka ya wale wenye ushawishi wa namna za ishara za nje. Kwa kuwa ‘Kweli’ hujulikana kwa jinsi ya ‘Rohoni’.
Basi nilete maneno ya Paulo wa Tarso kama ‘msikirifu’--mystic wa namna yake katika mkondo wa mapokeo ya mafundisho ya Yesu na ndiye busara yake inaunganisha ‘Tertium Organum’ ya PD Ouspensky na Oganam ya karne ya 21 juu ya njia ya Tatu ninayoitayarisha mimi. Nayeye anataarifika kupata kusema hivi :
Walakini iko hekima tusemayo kati ya wakamilifu; ila si hekima ya dunia hii, wala ya hao wanaoitawala dunia hii wanaobatilika; bali wanena hekima ya mungu katika siri, ile hekima iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu; ambayo wenye kuitawala dunia hii hawaijui hata mmoja; maana kama wangalijua, wasingalimsulubisha Bwana wa utukufu; lakini, kama iliyoandikwa,
Mambo ambayo jicho halikuyaona wala masikio halikuyasikia,
(Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,)
Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao.
Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu. Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyondani yake? Vivyo hivyo mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu. Nayo twayanena si kwa maneno yanayoyanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya roho. Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yanajulikana kwa jinsi ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote na wala yeye hatambuliwi na mtu. Maana, Ni nani aliyefahamu nia ya Bwana, amwelimishe? Lakini sisi tunayo nia ya Kristo.
Tafsiri hii kwa Kiswahili ni yenye kujaribu sana kwani kuna maneno yalikosa tafsiri ya moja kwa moja. Na hivi nilete ya kiingereza cha zamani kukoreza maana; ile iliyokuwa kabla ya hisani ya Mfalme James wa Uingereza katika kufadhili kazi tafsiri na uhakiki na nakala za kiingereza zilizotangulia katika jitihada zake za kuhifadhi mapokeo ya vitabu vya dini ya kikristo:
We speak the hidden mystical Wisdom of God, which God ordained before the World unto our Glory; Which none of the Princes of this World knew; For had they known it, they would not have crucified the Lord of Glory. But, as it is written, Eye hath not seen, nor Ear heard, neither hath it entered into the Heart of man to conceive the Things which God hath prepared for them that Love him. But God hath revealed them unto us by His Spirit: For the Spirit searcheth all Things, yea, the deep Things of God. For what Man knoweth the Things of a Man, save the Spirit of a Man which is in him? Even so the Things of God knoweth no Man, but the Spirit of God. Now we have received, not the Spirit of this World, but the Spirit which is of God; that we might know the Things that are freely given us of God. Which Things also we speak, not in the Words which Man's Wisdom teacheth, but which the Holy Ghost teacheth; comparing Spiritual Things with Spiritual. But the natural Man receiveth not the Things of the Spirit of God: For they are Foolishness unto him; neither can he know them, because they are Spiritually discerned. But he that is Spiritual judgeth, or discerneth all Things. “For who knowth the mind of the Lord so as to instruct him?” But we have the mind of Christ.
Nimependa kutumia nukuu nyakuzi iliyopata kutumika katika siku za Jacob Boehm wa Ujerumani miaka ya karne ya 16 na 17 kwa kuwa na yeye alikuwa ni msikirifu wa siku za karibuni aliyepata kufumbua kwa watu siri za mambo ya kiroho, naam kama ilivyopata kuwa na Dionysius, askofu wa kwanza wa jimbo la Athens-- maarufu kwa kazi yake ya Theologia Mystica, siku za nyuma zaidi; na meister Eckhart wa Ujerumani katika karne ya 14.
Shauri la ‘Jinsi ya rohoni’ ni kuzungumzia ginosia ya nafsi, ya kuwa mtu ‘hujua’ si kwa kutaarifiwa bali kwa ‘uzoefu’ wa kupitia hali ya utambuzi wa 'Moja' kati ya nafsi yake ya chini na nafsi yake ya juu. Nimeongeza neno katika msamiati wa Kiswahili ‘Usikirifu’ kukidhi tafsiri ya moja kwa moja ya neno ‘Mysticism’. Katika hali ya kawaida binadamu huwa wamependelea mambo ya mitaala ya ‘usadikifu’ na imani na hivi kusema mambo ya kiordhodoksi. Lakini mambo ya kiordhodoksi hufaa kwa watu wasiotambua shauri lipitalo unafsi wa kawaida wa mtu na wao kupendelea uhifadhina wa fikra na mawazo katika muktadha wa Theolojia na matendo ya kimapokeo. Na ndiyo hayo huja kuleta madhehebu na mgawanyiko wa taasisi za kiimani kwa mirengo ya kiitikadi za kutukuza na kuendeleza utaratibu wao.
Paulo alikuwa anajua umuhimu wa kuunganisha nguvu katika pilika na jitihada za kusambaza mafunzo ya imani na ujuzi wa kufungamanisha watu. Hii ni moja azma ya zama inayokwisha katika kuchochea watu kukaa pamoja katika namna za imani. Na hivi Paulo alijua fika Yesu ni kielelezo cha kuwaunganisha watu katika mashauri ya itikadi na hivi ndio maana alikuwa anaweza kuzungumza kuhusu uhusiano wa wanataasisi na Yesu ama ghafla akahamia kwenye elekezo mbadala la Kristo kama ‘Kweli’ ya ‘Roho wa Uzima’ katika Nia ya kudharihisha fahari ya Mbingu katika maisha ya Watu. Na ndivyo hivi kwa nini alikuwa mjuzi wa kubomoa hoja za mapokeo ya kiordhodoksi kama vile dhana ya kutokuwa na hukumu dhidi ya watu wenye ‘kuishi’ katika Kristo, maelekezi ya kushinda ‘mauti’ na ‘dhambi—uasi wa sheria za staha ya kiroho na dhana ya dosari ya moja kwa moja’ haya mawili katika muktadha wa kutambua Ufahamu wa Kristo ndani ya mtu mwenyewe. Kwa kuwa Paulo alikuwa ni msikirifu na tena mwenye kukiri uwezo na Ufahamu ndani yake wenye kupita fahamu za mwili kwa jinsi ya kiroho—mwili wa Kristo.
Na hivi kuna mahali anasema hivi:
Hata imekuwa, sisi tumemtambua Kristo kwa jinsi ya mwili, lakini sasa hatumtambui hivi tena. Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya kristo amekuwa kiumbe kipya ; ya kale yamepita ; tazama ! yamekuwa mapya. Lakini vyote pia vyatoka na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake katika Kristo ; naye alitupa huduma ya upatanisho ; yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao ; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho.
Neno la upatanisho ndivyo Pythagoras alipata kufundisha miaka mingi kabla ya Yesu juu ya uhusiano kati ulimwengu wa LOGOS na NECESSITY ; ulimwengu wa Neno lenye Nguvu na ulimwengu wa Utumikishi wa Mwili wa madhahiriko. Na hivi dhana ya Kristo ni yenye kufafanisha maana mbadala kati ya ‘Kristo’ na ‘Neno la Uzima’. Kinyume na ulimwengu wa kiordhodoksi, watu huchukulia maandishi ama maandiko kama ndiyo ‘neno la uzima’... Hii ni tafsiri ya vimvuli vya unafsi wao wenyewe.
Lakini jinsi ambayo Neno la Uzima huhifadhi na kustahimilisha yote ndiyo safari ya haja ya Pythagoras kutafuta kueleza ‘Muziki’ wa utangamano wa yote yaliyopata kudhahirika. Kristo—Neno la Uzima, ni ramani na uweza wa nguvu utaokutanisha ulimwengu uliodhahirika na upasipo dhahiriko katika kutaniko liitwalo WAKATI. Na hivi Pythagoras aliliita Neno hili ni SHERIA. Kwani kila kitu hufanyika ndani ya kanuni zake. Kutokujua daraja la kanuni ni kuishi katika dhambi na mpotoko lakini kuzaliwa katika Kristo ni kukomboka na kuishi zaidi kuzidia mbali ulimwengu wa vipimo iwe vya nyakati, umbali, upana wa uso, na hata ujazo. Na kwa hivi kufaa kusema neno liko kote na pote ; hakuna palipo na dhahiriko pasipo neno—vitu vyote vimefanyika katika neno. Mbingu huhifadhi vyote vilivyodhahirika lakini yenyewe hahihifadhiki na kitu chochote cha mfano. Na hivi Neno ni kiungo cha upatanishi wa mambo ya ulimwengu wa madhahirisho-Mtu, Dunia, Nyota na Mbingu. Naye Paulo huyazungumza haya anapomulika juu ya fahari ya mwili wa nyama, fahari ya miili ya nyota—uharibika na usipouharibika. Dhana ya Mauti na Ufufuko ambayo ni ontolojia ya Kristo katika Yesu pia.
Na hivi tutazame alichofundisha Yesu kwa msaada wa kumbu kumbu ya Levi :
Sura 115
Yesu afundisha kando ya Bahari. Asimulia kielezi cha mpanzi. Asema ni kwanini yeye afundisha kwa vielezi. Aelezea kwa mapana kielezi cha mpanzi. Asimulia kielelezi cha ngano na magugu nyasi.
NA Yesu akasimama kando ya bahari na kufundisha; makundi ya watu wakabanana naye na yeye akaenda katika mtumbwi ulio karibu na kusogea mbali kidogo na ukingo wa maji, na halafu akazungumza katika lugha ya vielezi; yeye akasema, 2 Tazameni, mpanzi alichukua mbegu na kwenda shambani kupanda. 3 Kwa mikono yenye kutoa kwa moyo alizitapanya mbegu na nyingine zikaangukia kwenye udongo mgumu ambao watu wamefanya, 4 Na muda si mrefu zilikanyagwa chini na miguu ya watu wengine; na ndege wakaja chini na kuzibeba na kuruka nazo mbali. 5 Mbegu nyingine zikaangukia katia ardhi yenye mwamba ambako kulikuwa na udongo kidogo; zikakua na muda si mrefu majani yakajitokeza na kuonesha dalili njema; 6 lakini basi hakukuwa na kina katika udongo, na hakuna nafasi ya kulishwa toka mizizini, na katika joto la mchana yakanyauka na kufa. 7 Nyingine zilianguka kwenye vichaka vya majani, na kukosa udongo wa kukulia nazo zikawa zimepotea; 8 Lakini mbegu nyingine zilipata makazi katika udongo mzuri na wenye rutuba na kukua haraka, na katika kipindi cha mavuno ikakutwa kwamba mingine ilizaa na kuleta mara mia, mingine sitini, mingine thelathini. 9 Wale wenye masikio ya kusikia waweza kusikia; na wale wenye mioyo ya kuelewa waweza kuelewa. 10 Sasa, wafuasi wake walikuwa kando yake ndani ya mtumbwi, na Tomaso akauliza, ni kwanini wazungumza katika lugha ya vielezi? 11 Na Yesu akasema, maneno yangu, kama maneno ya kila mkuu, ni yenye maana mbili kwa wakati mmoja. 12 Kwa nyie wenye kujua lugha ya nafsi-roho, maneno yangu yana maana iliyo ya kuzama ndani sana kwa watu wengine kumaizi. 13 Maana ingine ya kile nikisemacho ni kile makundi yote ya watu waweza kuelewa; maneno haya ni chakula kwao; mafikara ya ndani ni chakula kwa ajili yenu. 14 Acheni kila mmoja wenu kuunyosha mkono na kuchukua chakula ambacho yu tayari kukipokea. 15 Na halafu alizungumza ili kwamba wote waweze kusikia; yeye akasema, sikieni maana ya kielezi: 16 Watu wasikia maneno yangu na kutoyaelewa, na halafu nafsi yao ya kimwili yakwapua mbali mbegu, na wala dalili ya roho ya uzima kutokea. 17 Hii ni mbegu ambayo yaanguka ndani ya mapito ya watu. 18 Na wengine wayasikia maneno ya uzima, na kwa uchangamfu wa jazba kuyapokea yote; waonekana kumaizi kweli na dalili njema; 19 Lakini matatizo yaja; kuvunjika moyo kuinuka; hakuna kina katika mafikara; dhamira zao njema zakauka na kufa. 20 Hizi ni mbegu ambazo zilianguka kwenye ardhi ngumu. 21 Na wengine wasikia maneno ya ukweli na kuonekana kujua thamani ya kustahili kwake; lakini kupenda starehe, heshima, utajiri wa mali na umaarufu wa jina kuijaza ardhi yote; mbegu hazipaji mahitaji yake nazo zapotea. 22 Hizi ni mbegu ambazo zilianguka katikati ya vichaka vya majani na miiba. 23 Lakini wengine wasikia maneno ya ukweli na kumaizi vema; wao wazama vizuri katika nafsi-roho zao; waishi maisha matakatifu na ulimwengu wote wabarikiwa. 24 Hizi ni mbegu ambazo ziliangukia kwenye udongo wenye rutuba, ambayo ilileta matunda kwa ujazi. 25 Enyi watu wa Galilaya, mpate kuangalia jinsi msikiavyo na jinsi mpandavyo mashamba yenu; kwani ikiwa mwapuuzia matoleo ya siku hii, mpanzi aweza asije tena kwenu katika zama hii ama katika zama ingine ijayo. 26 Halafu Yesu asema kielezi; yeye akasema: 27 Basi ufalme nauweza kuufananisha na shamba ambalo mtu alipanda mbegu bora; 28 Lakini wakati amelala muovu akaenda na kupanda kujaza kote mbegu za magugu; halafu akaenda zake. 29 Udongo ulikuwa ni mzuri, na hivyo ngano na magugu nyasi vikakua; na watumishi alipoona magugu miongoni mwa ngano, walimpata mmiliki wa shamba na kusema, Mtu mwovu mmoja amepanda mbegu za magugu nyasi. 32 Watumishi wakasema, Je, tuende na kung'oa hadi mizizi manyasi ya magugu na kuyachoma motoni? 33 Mmiliki akasema, Hapana, hivyo haitakuwa vyema. Ngano na magugu nyasi vyakua karibu karibu pamoja udongoni, na wakati mkivuta manyasi mtaiharibu ngano. 34 Hivyo tutaziacha zote kukua pamoja mpaka wakati wa mavuno. Halafu kwa wavunaji nitasema, 35 Enendeni na kukusanya magugu na kuyafungia pamoja na kuyachoma motoni, na mkusanye ngano yote katika maghala yangu. 36 Aliposema haya, akaondoka kwenye mtubwi na kwenda juu kwenye nyumba, na wafuasi wake wakamfuata.
Sura 116
Wakristuni wapo nyumbani kwa Filipo. Yesu atafsiri kielezi cha ngano na magugu nyasi. Aelezea kwa mapana ufunukaji wa ufalme kwa vielezi: mbegu bora; kukua kwa mti; chachu; hazina iliyofichika. Aenda mlimani kusali.
Wakristuni walikuwapo nyumbani kwa Filipo na Petro akasema kwa Yesu, Bwana, utatuelezea maana ya vielezi ulivyotuambia leo? Na hasa kile kuhusu ngano na magugu nyasi? 2 Na Yesu akasema, Ufalme wa Mungu ni umbili; una namna ya sura ya nje na ile ya ndani. 3 Kama vile uonekanavyo kwa watu hufanyika kwa namna ya watu, ya wale ambao wamefanya ukirifu katika jina la Kristu. 4 Kwa sababu mbali mbali watu mbali mbali wajazana kuubana ufalme huu wa nnje wa Mungu wetu. 5 Ufalme wa ndani ni ufalme wa roho-nafsi, ufalme wa waliosafi katika moyo. 6 Ufalme wa nje naweza kuelezea vema kwa mapana katika vielezi. Tazameni, kwani nimewaona ninyi mkizitupa nyavu zenu baharini, 7 Na wakati mlipozivutia ndani, lo, zilikuwa zimejaa kwa kila namna ya samaki, wengine wazuri, wengine wabaya, wengine wakubwa, wengine wadogo; na nimewaona ninyi mkiwabakiza wazuri na kuwatupa mbali wabaya. 8 Ufalme huu wa nje ni nyavu, na kila namna ya mwanadamu hushikwa; lakini katika siku ya kuchagua wabaya wote watatupwa, na wazuri kutuzwa. 9 Sikieni, basi, maana ya kielezi cha ngano na magugu nyasi: 10 Mpanzi ni mwana wa mtu; shamba ni ulimwengu; mbegu nzuri ni watoto wa nuru; magugu nyasi, watoto wa giza; adui ni nafsi ya kimwili; siku ya mavuno, ni mwishoni mwa kufunga zama; mvunaji ni mjumbe wa Mungu. 11 siku ya malipo*[Pia siku ya hukumu] itakuja kwa kila mtu; halafu kutakuwa na magugu nyasi kukusanyika pamoja, na kutupiwa katika moto na kuchomwa. 12 Halafu wema kung'aa kuwaka mbele kama majua katika ufalme wa roho-nafsi. 13 Na Filipo akasema, Je, yawabidi wanaume kwa wanawake kuteswa katika moto kwa sababu hawakuipata njia ya uzima? 14 Na Yesu akasema, Moto wasafisha. Wakimiya*[Watu washughuliakao na kubadili sifa za tabia za vitu kwa kanuni za uelewa wake] hutupa motoni malighafi ya chuma chuma na kushikilia kuichuja kila namna ya mabaki ya yasiyotakiwa. 15 Mali ghafi ya chuma chuma yenye kuonekana kutokuwa na manufaa kuwa imetafunwa na moto; lakini si hata chembe ya dhahabu yapotea. 16 Hakuna mtu ambaye ndani yake hana dhahabu ambayo haiwezi kuharibikika. Vitu viovu vya watu vyote vyatafunwa katika moto; dhahabu yabakia. 17 Ufalme wa kindani wa roho-nafsi naweza kuuelezea katika vielezi: 18 Mwana wa mtu aenda mbele na kutawanya mbegu za kweli; Mungu azimwagia vizuri udongo maji; mbegu yaonesha uhai na kukua; kwanza yaja majani, na halafu mashuke; na halafu masikio, na halafu ngano tupu katika masikio. 19 Mavuno yaja na lo, mvunaji abeba mavuno yaliyoiva hadi katika maghala ya Bwana. 20 Tena, ufalme wa roho-nafsi ni kama mbegu ndogo ambayo watu waweza kupanda katika udongo wenye rutuba. 21 ( Maelfu yake kwa kiasi pungufu tu kwa uzito wa shekeli moja.) 22 Mbegu ndogo yaanza kukua; yasukuma kupenya katika udongo, na baada ya miaka ya kukua kwake waja kuwa ni mti mkubwa na ndege watulia katika matawi yake yenye majani na watuwapata hifadhi katika kimvuli kukingwa na Jua na matufani. 23 Tena, ile kweli, hali ya roho ya ufalme wa roho-nafsi, ni kama vipande vya unga wa kukandwa uliotiwa chachu ambayo mwanamke huufunikia katika kipimo, tatu, na katika muda kidogo wote waumuka. 24 Tena, ufalme wa roho-nafsi ni kama hazina iliyofichwa shambani ambako mtu huipata, na moja kwa moja aenda njia yake na kuuza vyote alivyonavyo na kununua lile shamba. 25 Yesu aliposema yote hivi alikwenda peke yake katikati ya vilima palipo ni karibu na kusali.
Sura 120
Nikodemasi yupo kalamuni. Amuuliza Yesu, Je, dini ya kristuni haiwezi kuletwa mbele kwa mafanikio zaidi kwa kutengeneza upya huduma ya Kiyahudi? Yesu ajibu katika namna ya kinyume na atoa sababu. Yesu amponya mwanamke mwenye matatizo ya kuvuja damu. Amponya binti Yairo. Apotea watu wanapolitaka kumuabudu.
SASA, Nikodemasi, ambaye hapo mwanzo alikuja kwa Yesu wakati wa usiku kujifunza njia ya uzima, alikuwa ni miongoni mwa wageni. 2 Na kusimama mbele yeye akasema, Raboni, ni kweli kwamba Kanuni za sheria za Kiyahudi na matendo ya Kiyahudi haviendani. 3 Ukuhani wahitaji kufanyiwa matengenezo upya; watawala yawapasa kuwa na rehema zaidi na huruma; wanasheria yawapasa kuwa na haki zaidi; watu wa wakawaida yawapasa kutokubeba mizigo kama hiyo. 4 Lakini Je, huwezi kuongezea humo ndani yake kwa matengenezo mapya na pasipo kuharibu huduma za Kiyahudi? 5 Je, huwezi kufanya kazi zako kubwa ziendane sambamba na zile za Mafarisayo na waandishi? Je, ukuhani huewezi kunufaika na filosofia yako manani? 6 Lakini Yesu akasema, Hauwezi kuutia mvinyo mpya katika vifuko vya kale, kwani utakapojisafisha kuwa bora, lo, watanuka; vifuko vya kale haviwezi kumudu nguvu ya mtanuko; hivyo hupasuka, na mvinyo wote wapotea. 7 Watu hawatii viraka nguo iliyochakaa kwa kipande cha nguo mpya, ambayo haiwezi kustahimili msokoto wa nyuzi, mdhaifu kwa uzee, na halafu mtatuko mkubwa zaidi watokea. 8 Mvinyo wa zamani waweza kuhifadhiwa katika vifuko vya zamani; lakini mvinyo mpya wavitaka vyombo vipya vya kuhifadhia. 9 Hii kweli-ya-roho niiletayo kwa kizazi hiki ni mpya, na ikiwa tutaiweka katika vifuko vya zamani vya namna za Kiyahudi, lo, utapotea. 10 Ni lazima utanuke; vibebeo vya zamani haviwezi kustahimili na hivyo vingalipasuka. 11 Tazameni ufalme wa Kristu! Ni wenye umri sawa na Mungu mwenyewe, na wakati ni mpya kama vile jua la asubuhi; wenyewe tu ndio uwezao kubeba ndani yake kweli ya Mungu. 12 Na alivyokuwa akizungumza mtawala wa sinagogu, Yairo kwa jina, akaingia na kuinamisha kichwa miguuni pa Yesu na kusema, 13 Mkuu wangu, sikia ombi langu! Mwanangu ni mgonjwa sana, ninahofu atakufa; lakini hili nalijua ya kwamba ikiwa utakuja na kuzungumza Neno mwana wangu ataishi. 14 (Alikuwa ni mtoto wake wa pekee, binti wa miaka kumi na miwili.) 15 Na Yesu hakungoja; alitoka na yule mtu, na watu wengi wakawafuata wao. 16 Na walipokuwa wakienda mwanamke aliyekuwa akiugua ugonjwa wa kuvuja damu kwa miaka mingi, amekuwa akijaribiwa kutibiwa na waganga toka mbali na karibu, na wote walikuwa wamesema, hawezi kuishi, akainuka kutoka kitandani mwake na kukimbia njiani Yesu alivyokuwa akipita. 17 Na yeye alisema ndani, ikiwa nitagusa vazi lake, basi najua nitakuwa ni mzima. 19 Na Yesu akasikia kama vile nguvu za uponyoji zimemtoka, na kuzungumza kwa makundi, yeye akasema, 20 Ni nani amegusa koti langu? 21 Na Petro akasema, Hakuna mtu anayeweza kusema; makundi yamekubana bana; idadi ya watu waweza kuwa wamekugusa koti lako. 22 Lakini Yesu akasema, Mtu mmoja kwa imani, kwa fikara la kuponya, amegusa koti langu, kwani kipawa cha uweza wa uponyaji kimetoka toka kwangu. 23 Na mwanamke akajua ya kwamba alichokifanya kimejulikana, yeye akaja na kupiga magoti miguuni pa Yesu na kusema yote. 24 Na Yesu akasema, Imani yako imekufanya uwe mzima, enenda zako kwa amani. 25 Sasa, alipokuwa akizungumza, matumishi kutoka nyumba ya Yairo akaja na kusema, Mkuu wangu, Yairo, usimsumbue Bwana kuja; mtoto wako kafariki. 26 Lakini Yesu akasema, Yairo, mtu wa imani, usiruhusu imani yako kutetereka katika wasaa huu wa majaribu. 27 Hicho ni kitu gani ambacho mtumishi kakisema? Eti, mtoto kafariki? Lo, kifo ni nini? 28 Ni kuondoka kwa nafsi-roho kutoka katika nyumba ya mwili wa nyama. 29 Mtu ni mkuu wa nafsi-roho na wa nyumba yake. Mtu anapoinuka toka kwenye mashaka na hofu, lo, yeye aweza kuitakasa nyumba yake tupu na kuwarejesha wapangaji tena. 30 Basi akimchukua pamoja naye Petro, James na Yohana, Yairo na mama wa mtoto, alikwenda kwenye chumba cha aliyekufa. 31 Na milango ilipowafungia makundi nje, yeye akazungumza maneno ambayo nafsi-roho yaweza kuelewa, na halafu alimchukua mwanamwali mikononi na kusema, 32 Talith cumi, mtoto, inuka juu! Nafsi-roho ya mwanamwali ikarudi na yeye akainuka na kuomba chakula. 33 Na watu wote wa mji wakastaajabu, na wengi wangalitaka kumuabudu Yesu kama Mungu. 34 Lakini, kama vile jinamizi la usiku, yeye alipotea na kwenda zake.
Yesu alitumia vielelezi vyenye kufananisha utaratibu wa maisha na mazingira katika kufafanua shauri lake la Kristo na Ufalme. Maisha kama milki ya fahari ya Kristo katika mpinduko wa sura ; toka umilele na kuwa umuda ; yeye alizungumza kupambanua Mambo ya Nyakati na Msuko wa hali na Hadhi.
Kwake yeye maisha ya mwanadamu ni makutano ya jinsi ya kanuni za mwili wa nyama na hivi ndivyo kusema himaya nzima ya ulimwengu wa madhahiriko ; na vile pia, chembe mbegu ya ufahamu kwa ukweli wenye kupita yote yenye ukomo wa hali—pale mwanadamu ahusishwavyo kiuzima wake na utambuzi. Katika hali ya kawaida huweza kusemwa kwamba binadamu ana macho mawili ; moja ni lenye kuona mambo kwa kanuni za vipimo, kadri, ukiasi na kupelekea ujengaji wa hoja/fikra ; na hali jingine ni lenye kutazama hadhi ya mambo kwa wakati pasipo kujenga hoja. Basi husemwa pia jicho moja lenye kuona kwa hoja za tafsiri ndilo mkingamo wa kutambua Ufalme wa Mbingu uliopo hapa na sasa. Na ndivyo hivi kwa nini--lugha ya picha ama vielezi ni ufundi wa kuzunguka hoja na hali vile vile kuonesha hadhi ya mchukuo wa sura kwa jinsi yake na hata namna ya hali endelevu ya jambo. Na hivi pia kusema binadamu hataingia katika ‘Ufalme wa Mbingu’ hadi tu Macho yake mawili yawe Moja—kusudi apate kukirimika kwa ‘Busara’ ya Roho wa Uzima na hivi kujua hata mambo ya Kina katika ile Moja. Kuachana la lile moja jicho lenye kumponza kutoufikia ‘Ufalme’ angali likimpatia yeye namna ya utumikivu baina yake na viumbe vya dunia na mazingira yake kulingana na hisia zake na fikra za utanabaishaji... Na hivi tena Kristu ndiyo ile Njia, na Kweli, na Uzima—Neno la Uzima wote na namna ya kuipata ile Nia ya kung’amua mashauri ama maarifa juu ya yote na kote. Hakuna mwenye kuweza kuingia Ufalme wa Mbingu ila tu kwa kufanyika moja na Kristu. Kristu--jicho lenye kuona kote na kutambua yote na hali hilo halitambuliwi na mtu ila tu katika yule mtu aliyezaliwa mara ya pili katika Nuru iingaziayo kote ; kumfanya huyo mtu kuwa mwana wa Nuru. Asiyekuwa katika hii nuru kuwa ni mwana wa giza na mtu aiishiye katika nchi ya kimvuli na vina vya tafsiri kwa jinsi ya fahamu za mwili wa nyama na kwa hekima ya mambo ya kimwili.
Na hapa ndipo penye hekima ya Neno lenyewe, aliye na macho na aone, aliye na masikio naasikiye.
Oganam ya Karne ya 21 juu ya Njia ya Tatu inajengwa juu ya shauri lenye kuelekea katika Jicho lenye kuona kote na kwa nia yake ya ung’amuzi.
Jitihada za mtu kuitafuta ‘Kweli’ kusudi aje kuisimamisha heshima ya utu wake ndiyo hasa hutajwa ni ‘Kuuleta Ufalme’. Ufalme huletwa kwa matendo yenye kheri kwa kadri ya Nia ya mtu aliyekirimika kuyajua yaliyo katika hazina ya Mbingu. Mwanadamu si mkamilifu wa kutunukiwa shani ya ubora usioharibika mpaka apate kufahamu ufundi wa kujenga hekalu lake ambamo ajifunza staha ya ‘kuabudu katika roho na Kweli’.
Basi lipo jiwe liliokataliwa na Waashi wa Dunia hii ya nchi ya watu wenye kuishi kwenye vimvuli na hali ndilo jiwe kuu la pembezoni kukamilisha Hekalu lisilobomokeka na kile hasa kitovu cha ‘Ufalme’ ulio ni ule uhuru wenye kumweka mtu huru kweli kweli. Na Jicho la Tatu ndilo jicho ambamo ‘mbili hufanyika moja’ kwa wakati wowote na mtu kufanyika Moja na ‘Kweli’ ili kuuendea ustawi na ustaarabu mpya—mpangiko wa ulimwengu mpya.
Tekinokrasia ni ujenzi ; ni ujenzi kwa mujibu kwa picha na kanuni zenye kukirimika kheri. Yesu alionesha hizo ramani za ‘Mpango Mzima’ lakini matokeo ya shughuli yake yalibashirika hata kwa wenye busara wa siku hizo ; kuwa zama yake itatambua japo kidogo tu shauri lake juu ya huduma yake kuu na mshughuliko wake. Kwa kuwa kizingiti kikuu ni mlemeo wa ujinga wa fahamu za mwili na mazoea ya mapokeo na kiutamaduni wa kufikiwa. Kosekano la usafi wa dhamira katika moyo wa wanadamu wenye kuruhusu maarifa yenye kubatilisha utaasisi na mapokeo ya kale na kusimamisha mambo mapya.
Zama yake Yesu inakatikia na hii hapa sasa zama mpya ikisogea karibu kabisa. Wanadamu wote wa siku ya leo wanataharuki migogoro mikubwa ya kiustawi na mapokeo ; vile vile mitafaruku ya kisiasa, machafuko na hata mapigano. Mahodhi ya kiuchumi kwa mataifa na udororaji wa ‘ukuaji’ wake. Na katika kutazama Utaasisi wa taaluma za mambo ya sayansi na pia mawasiliano na usambazaji habari ; haya mawili kuchukua nafasi ya kuonekana kana vile ndiyo shani ya ‘ukuhani mkuu’ na ‘utowashi wake’ katika kipindi hiki katika kushawishi mwelekeo wa ukubali wa watu kuamini kitu gani juu ya maisha ama wachukuliaje taarifa—kila siku. Vile vile itikadi za kiutawala zenye kufanya mamlaka katika serikali za watu hali ni zenye kupwaya shauri kuu juu uhusishaji na vile vile maridhiano kwa raia wake wote katika sura ya mikakati ya kupanga na pia katika kutekeleza mipango ya ustawi ndani ya mipaka yao.
Mihimili ya mapokeo ya dini zote zenye idadi kubwa ya watu inaanza kukosolewa na kuumbuliwa juu ya mashauri ya uchukuliaji wake wa maadili. Ukasisi wa kusisitiza utaratibu wenye kuonekana kama ni sahihi katika macho ya wanadamu na kumbe ni njia ya mauti yenye kujishindilia aibu ya unajisi wa makusudi wa nguvu za uzazi. Uimamu unaojaza fikra za uharibifu kwa minajili ya chuki-- kwa umma wa waumin wake ili kujitoa muhanga kwa mauaji ya kukusudia na hali wao wenye siyo wenye kuonesha mfano wa kufa kwanza ikiwa mashauri hayo ni yenye kujitosheleza ukweli. Haya yote kuonesha jinsi kiu ya haja ya ushawishi huweza hata kumsukuma mwanadamu kutenda upumbafu na kuhatarisha amani na maridhiano—na hilo hatimaye kumtafuna mwanadamu mwenyewe na ustawi wake.
Maelekezo yote ya wenye kheri yaliyoleta dini na ukundiko wa kiimani sasa hayanabudi kutathminiwa matunda yake na hukumu kupitishwa. Baraza la kutoa hukumu ni utashi wenye kuinukia kwenye jicho lenye kuona kote na tena la Muamuzi mmoja kwa kila mtu mwenyewe—si tena andiko lolote wala shauri la nje nje juu ya watu kwa ujumla.
Oganam ya karne ya 21 juu ya Njia ya Tatu ni kazi ya udadavuaji kwa mwanadamu mwenye kutafuta sura ya mfananio wa utatuzi kwa mambo yaonekanayo ni magumu kutafutia majawabu katika wakati huu wa mpito kuianza rasmi zama mpya.
Oganam ni chombo chenye kutumikika katika mchakato wa kazi, na hasa pale ukwamuzi unapohitajika kwa tatizo lililojitokeza. Lakini vile vile kwa jinsi yake ni wavu wenye kuchuja yatakiwayo na yasiyotakiwa kutoka baharini.
Kupokelewa kwa kazi hii ya Oganam katika jamii ya watu wote duniani ni mashauri kuwasilishwa katika siti ya Muamuzi na matokeo yake ya kufikia hukumu juu ya mashauri ni kunawa ama kujisafisha ili kuingia Zama Mpya—na hivi ni Mavuno ; kipindi cha kutaharuki pumba na uwele vikitenganika kwa pumzi ya upepo unaovuma...
...... Inaendelea....