Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 1,914
- 6,033
Marumo Gallants wapo nyumbani kuwaalika Young Africans katika mchezo wa marudiano ya nusu fainali ya CAF Confederation Cup kwanzia saa 1:00 usiku kwa hapa nyumbani Tanzania.
Mechi ya kwanza iliyopigwa juma moja lililopita Yanga waliibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Hivyo matokeo yoyote ya ushindi kwao, au droo yataivusha Yanga na kuipeleka Yanga katika fainali ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza.
Kila la heri kwa Yanga, Taifa zima tupo nyuma yenuπΉπΏπΉπΏπΉπΏπΉπΏ
================================================
Updates:
45' + 1 Mayele anawapa Yanga goli la uongozi
2nd half sasa:
53' Bado Yanga anaongoza na ana miliki mpira kwa utulivu mkubwa
54' Aucho na Katlego wa Marumo wanapata kadi za njano mara baada ya kugombana
56' Musonda akiwa katika nafasi nzuri ya kufunga goli anajikuta akipaisha mpira juu
57' Marumo wanapata goli lakini linakataliwa baada ya mfungaji kuwa katika eneo la kuotea
60' Katlego anaisumbua sana beki ya Yanga, Marumo wanatawala mechi kwa dakika hizi
61' Goallllllllllllllllllll
Kennedy Musonda anawapa Yanga goli la pili baada ya kazi nzuri ya Mayele
63' Yanga wanafanya sub, wanaingia wachezaji watatu Aziz Ki, Moloko na Mzize huku Bangala, Aucho na Musonda wakienda nje
65' Yanga wamerejesha umiliki wa mpira wao
67' Mpira unachezwa kwa kupokezana na kushambuliana kwa zamu
69' Yanga leo wanazuia vizuri mipira ya kona, Marumo walipata kona mbili lakini zimezuiwa vizuri na mabeki wa Yanga
70' Mashabiki wanaishangilia Yanga ambao wengi wao waliojitokeza hapa uwanjani ni Watanzania waishio Afrika Kusini.
71' Zawadi Mauya anaingia kuimarisha ulinzi. Kocha Nabi anaamua kujilinda zaidi baada ya uongozi wa goli 2
75' Mpira umesimama kupisha Mayele atibiwe
76' Edgar Manaka wa Marumo anapata kadi ya njano baada kumchezea rafu Mzize
78' Mayele anatoka huku akichechemea na Farid Mussa anachukua nafasi yake
79' Mawinga wa Marumo wanaamua kuchezea mpira na kupiga chenga baada ya kuona kimahesabu wana mzigo mzito
82' Yanga wanamiliki mpira lakini wanashindwa kutumia nafasi wanazozitengeneza
83' Yanga wanakosa nafasi ya wazi ya kuandika goli la 3
88' Yanga wanapata faulo mara baada ya Moloko kufanyiwa madhambi
89' Yanga wanalishambulia goli la Marumo kwa kasi
90' Marumo wanapata goli ni 1-2
Dakika 4 zimeongezwa
FT' Marumo 1-2 Yanga
Aggregate: 1-4
Yanga wanaingiiiaaaaaa Fainali kwa mara ya kwanza.
Mechi ya kwanza iliyopigwa juma moja lililopita Yanga waliibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Hivyo matokeo yoyote ya ushindi kwao, au droo yataivusha Yanga na kuipeleka Yanga katika fainali ya michuano hiyo kwa mara ya kwanza.
Kila la heri kwa Yanga, Taifa zima tupo nyuma yenuπΉπΏπΉπΏπΉπΏπΉπΏ
================================================
Updates:
45' + 1 Mayele anawapa Yanga goli la uongozi
2nd half sasa:
53' Bado Yanga anaongoza na ana miliki mpira kwa utulivu mkubwa
54' Aucho na Katlego wa Marumo wanapata kadi za njano mara baada ya kugombana
56' Musonda akiwa katika nafasi nzuri ya kufunga goli anajikuta akipaisha mpira juu
57' Marumo wanapata goli lakini linakataliwa baada ya mfungaji kuwa katika eneo la kuotea
60' Katlego anaisumbua sana beki ya Yanga, Marumo wanatawala mechi kwa dakika hizi
61' Goallllllllllllllllllll
Kennedy Musonda anawapa Yanga goli la pili baada ya kazi nzuri ya Mayele
63' Yanga wanafanya sub, wanaingia wachezaji watatu Aziz Ki, Moloko na Mzize huku Bangala, Aucho na Musonda wakienda nje
65' Yanga wamerejesha umiliki wa mpira wao
67' Mpira unachezwa kwa kupokezana na kushambuliana kwa zamu
69' Yanga leo wanazuia vizuri mipira ya kona, Marumo walipata kona mbili lakini zimezuiwa vizuri na mabeki wa Yanga
70' Mashabiki wanaishangilia Yanga ambao wengi wao waliojitokeza hapa uwanjani ni Watanzania waishio Afrika Kusini.
71' Zawadi Mauya anaingia kuimarisha ulinzi. Kocha Nabi anaamua kujilinda zaidi baada ya uongozi wa goli 2
75' Mpira umesimama kupisha Mayele atibiwe
76' Edgar Manaka wa Marumo anapata kadi ya njano baada kumchezea rafu Mzize
78' Mayele anatoka huku akichechemea na Farid Mussa anachukua nafasi yake
79' Mawinga wa Marumo wanaamua kuchezea mpira na kupiga chenga baada ya kuona kimahesabu wana mzigo mzito
82' Yanga wanamiliki mpira lakini wanashindwa kutumia nafasi wanazozitengeneza
83' Yanga wanakosa nafasi ya wazi ya kuandika goli la 3
88' Yanga wanapata faulo mara baada ya Moloko kufanyiwa madhambi
89' Yanga wanalishambulia goli la Marumo kwa kasi
90' Marumo wanapata goli ni 1-2
Dakika 4 zimeongezwa
FT' Marumo 1-2 Yanga
Aggregate: 1-4
Yanga wanaingiiiaaaaaa Fainali kwa mara ya kwanza.