CAPO DELGADO
JF-Expert Member
- Aug 31, 2020
- 7,621
- 16,700
Friends of Simba wamerudi kazini
TAJIRI na kipenzi cha mashabiki wa Simba, Mohammed Dewji ameteua wajumbe 21 wa Baraza la Ushauri ambao kati yao 13 ni kutoka kwenye kundi lenye nguvu la Friends of Simba.
Duru za ndani ya Simba zinasema kuwa uteuzi huo ambao vigogo saba waliwahi kuwa viongozi wa klabu hiyo, unalenga zaidi kuongeza nguvu kwenye mechi dhidi ya Yanga Jumapili, ligi Kuu, FA pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika.
Simba iliyoivua ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Zamaleki ya Misri mwaka 2003, asilimia kubwa ya wajumbe hao ndio waliohusika chini ya kundi hilo lililoanzishwa mwaka 1999.
Vigogo hao waliibeba Simba katika nyakati zote ingawa mchakato wa mfumo wa uendesha ulipoanza miaka mitano nyuma kundi hilo lilipoteza nguvu, hii huenda ni mfumo huo ulipoanza kufanya kazi chini ya Mohammed Dewji ‘Mo Dewji’ ambaye ni mwekezaji wa Simba.
Baada ya mchakato huo kuanza na kufanyika uchaguzi wa klabu mambo yalibadilika, Simba inaendeshwa na Bodi ya Wakurugenzi ambayo awali ilikuwa chini ya Mwenyekiti Mo Dewji ingawa kwasasa inaongozwa na Salim Abdallah ‘Try Again’.
Mo Dewji ambaye ni Rais wa Heshima ameteua wajumbe hao na kueleza kuwa pamoja na kupiga hatua lakini bado hawajafikia malengo yao hivyo kuongeza baraza hilo anaamini watafikia malengo. MO Dewji amekiri kuwa mojawapo ya majukumu yake kama Rais wa Heshima ni kuhakikisha Uongozi na Utawala bora kila wakati.
Kazi kubwa ya Baraza hilo ni kuishauri Bodi ya Wakurugenzi juu ya maendeleo ya Klabu, Uongozi na Utawala bora
Wajumbe walioteuliwa kutoka Friends ni Thomas Mihayo, Evans Aveva, Kassim Dewji, Musleh Al-Ruweh, Mohamed Nassor, Mulamu Ng’ambi, Prof Janabi, Hassan Kipusi, Geofrey Nyange, Gerald Yambi, Moses Kaluwa, Crescentius Magori na Juma Pinto.
Wengine ambao waliwahi kuwa viongozi wa klabu hiyo ni Hassan Dalali, Ismail Aden Rage, Swedi Mkwabi ambao hawa waliwahi kushika nafasi ya Mwenyekiti kwa nyakati tofauti, Faroukh Baghoza, Azim Dewji, Octavian Mshiu, Mwina Kaduguda na Idd Kajuna.
Ukiangalia majina yalioitwa asilimia kubwa ni wanachama waandamizi wa Simba na wengi waliwahi kuwa viongozi.
Hawa wazee watakuwa na maamuzi makubwa , Watapiga sana pesa. Na hakuna timu itafanikiwa dhidi simba mbaka uchaguzi ujao.
Tuseme tu ukweli simba ikiwa pamoja hakuna timu inaweza ikapata hata sare kwa mkapa.
Alhly na Raja
Ogopa sana kauli mbiu ya nguvu moja
Mo ameona matokeo si mazuri ndani na nje ya Klub mambo hayaendi kabisa (kukosa ubingwa kwa miaka miwili
Haya majeraha ya mala kwa mala ya wachezaji muhimu Manula Inonga, phiri aubin Kramo si kitu cha kawaida (gizani).
Sajili mbovu na kufungwa giza kwa Baadhi ya wachezaji.
Ayoub,Kramo,Saido,Miqui nk.
Baadhi ya wazee wanavyoamini wao wanasema wamepeleka mpira wa simba jangwanj kwasababu ya majeraha ya vyeo na makovu ya chaguzi.
Kama hawa wazee wote walioteuliwa wakikubaliana
Kila kitu simba kitakwenda sawa yatarudi yale ya Ubingwa mala 4 mfululizo.
Itarudi simba ya Biriani na lunyasi.
NGUVU MOYA
TAJIRI na kipenzi cha mashabiki wa Simba, Mohammed Dewji ameteua wajumbe 21 wa Baraza la Ushauri ambao kati yao 13 ni kutoka kwenye kundi lenye nguvu la Friends of Simba.
Duru za ndani ya Simba zinasema kuwa uteuzi huo ambao vigogo saba waliwahi kuwa viongozi wa klabu hiyo, unalenga zaidi kuongeza nguvu kwenye mechi dhidi ya Yanga Jumapili, ligi Kuu, FA pamoja na Ligi ya Mabingwa Afrika.
Simba iliyoivua ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Zamaleki ya Misri mwaka 2003, asilimia kubwa ya wajumbe hao ndio waliohusika chini ya kundi hilo lililoanzishwa mwaka 1999.
Vigogo hao waliibeba Simba katika nyakati zote ingawa mchakato wa mfumo wa uendesha ulipoanza miaka mitano nyuma kundi hilo lilipoteza nguvu, hii huenda ni mfumo huo ulipoanza kufanya kazi chini ya Mohammed Dewji ‘Mo Dewji’ ambaye ni mwekezaji wa Simba.
Baada ya mchakato huo kuanza na kufanyika uchaguzi wa klabu mambo yalibadilika, Simba inaendeshwa na Bodi ya Wakurugenzi ambayo awali ilikuwa chini ya Mwenyekiti Mo Dewji ingawa kwasasa inaongozwa na Salim Abdallah ‘Try Again’.
Mo Dewji ambaye ni Rais wa Heshima ameteua wajumbe hao na kueleza kuwa pamoja na kupiga hatua lakini bado hawajafikia malengo yao hivyo kuongeza baraza hilo anaamini watafikia malengo. MO Dewji amekiri kuwa mojawapo ya majukumu yake kama Rais wa Heshima ni kuhakikisha Uongozi na Utawala bora kila wakati.
Kazi kubwa ya Baraza hilo ni kuishauri Bodi ya Wakurugenzi juu ya maendeleo ya Klabu, Uongozi na Utawala bora
Wajumbe walioteuliwa kutoka Friends ni Thomas Mihayo, Evans Aveva, Kassim Dewji, Musleh Al-Ruweh, Mohamed Nassor, Mulamu Ng’ambi, Prof Janabi, Hassan Kipusi, Geofrey Nyange, Gerald Yambi, Moses Kaluwa, Crescentius Magori na Juma Pinto.
Wengine ambao waliwahi kuwa viongozi wa klabu hiyo ni Hassan Dalali, Ismail Aden Rage, Swedi Mkwabi ambao hawa waliwahi kushika nafasi ya Mwenyekiti kwa nyakati tofauti, Faroukh Baghoza, Azim Dewji, Octavian Mshiu, Mwina Kaduguda na Idd Kajuna.
Ukiangalia majina yalioitwa asilimia kubwa ni wanachama waandamizi wa Simba na wengi waliwahi kuwa viongozi.
Hawa wazee watakuwa na maamuzi makubwa , Watapiga sana pesa. Na hakuna timu itafanikiwa dhidi simba mbaka uchaguzi ujao.
Tuseme tu ukweli simba ikiwa pamoja hakuna timu inaweza ikapata hata sare kwa mkapa.
Alhly na Raja
Ogopa sana kauli mbiu ya nguvu moja
Mo ameona matokeo si mazuri ndani na nje ya Klub mambo hayaendi kabisa (kukosa ubingwa kwa miaka miwili
Haya majeraha ya mala kwa mala ya wachezaji muhimu Manula Inonga, phiri aubin Kramo si kitu cha kawaida (gizani).
Sajili mbovu na kufungwa giza kwa Baadhi ya wachezaji.
Ayoub,Kramo,Saido,Miqui nk.
Baadhi ya wazee wanavyoamini wao wanasema wamepeleka mpira wa simba jangwanj kwasababu ya majeraha ya vyeo na makovu ya chaguzi.
Kama hawa wazee wote walioteuliwa wakikubaliana
Kila kitu simba kitakwenda sawa yatarudi yale ya Ubingwa mala 4 mfululizo.
Itarudi simba ya Biriani na lunyasi.
NGUVU MOYA