Freeman Mbowe kuona ni kuamini, achana na siasa za mkia wa mbuzi, jeuri na kiburi sio mtaji kuelekea uchaguzi 2024/2025

Venus Star

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
19,680
59,801
Na;
Hamis Abeid Baruani
UDASA, UDSM.

Kwa masikitiko makubwa leo Mbowe ameushangaza umma kwa kuongea mambo mawili ambayo hadi sasa yamepingwa kila kona ya nchi.

1. Katangaza kususia maridhiano
2. Kaitisha anayoyaita maandamano ya amani.

a) Mhe. Mbowe kabla ya kususia MARIDHIANO unakumbuka lakini majuzi tu 31.12.2023 pale Hai wakati unaongoza Harambee ya kumalizia ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Usharika wa NSHARA MACHAME, Rais Dkt. Samia alichangia Tsh Milioni 150, haya yakiwa ni matunda ya MARIDHIANO ya kisiasa hapa nchini.

b) Mnakumbuka CDM mlikuwa na ziara pamoja na mikutano mikoa mbalimbali na mkafanya kwa amani hakuna mtu alienyooshewa kidole hata mmoja inamaana mmesahau kama hayo ni matunda ya MARIDHIANO

c) Maridhiano haya unayotaka kuyakataa hukumbuki kuwa ndio yamefanya viongozi wa CDM waliokuwa nje ya nchi kurejea nchini kufanya siasa kwa amani bila wasiwasi

d) Hujiulizi hata tukio la leo limefanyika vizuri kwa amani na umepewa ushirikiano wa namna zote kwenye vyombo vya habari kwasababu ya matunda ya MARIDHIANO yaliyoletwa na Rais Dkt. Samia

e) Hata umuhimu wa RUZUKU ambao pengine umepelekea kuhamisha Ofisi toka Kinondoni kwenda Mikocheni nao huoni kama ni matunda ya MARIDHIANO

Tujifunze kuwa waungwana tunapofanyiwa uungwana.

Wakati unafikiria kuandamanisha watu kumbuka wananchi wa sasa sio wa miaka ile, wananchi wanaona mambo makubwa yanayofanywa na Serikali yao, wanaona jitihada za Rais Samia kuwapigania. Ngoja niwakumbushe kidogo:-

1. Januari za miaka ya nyuma Wazazi walikuwa wanateseka kwa michango ya ujenzi wa madarasa na kununua madawati ila sasahivi hakuna mzazi hata mmoja nchini anaesumbuliwa na michango hii, Rais Samia kajenga madarasa mengi nchi nzima lakini pia Serikali kila mwezi inatoa takribani Bilioni 33.3 kugharamia elimu kwa wanafunzi wa ngazi ya awali, msingi na sekondari.

2. Rais Samia amesambaza Vifaa vya Afya Majimbo yote nchini kama ifuatavyo kwa ujumla
a) Vitanda vya wagonjwa 3080
b) Vitanda vya kujifungulia 1000
c) Magodoro 5500
d) Mashuka 36,808
e) Meza za Vitanda 306
f) Pia kasambaza magari ya kubebea wagonjwa (Ambulance) kila kona

Hii inaonesha namna gani ana huruma na wananchi na anajali afya zetu.

3. Takribani asilimia 95% ya Madai ya Watumishi yamefanyiwa kazi ndani ya muda mfupi. (Ulipaji madeni, Ongezeko la Posho, Mikataba ya hali bora, Ajira mpya, Mazingira bora ya Kazi).

4. Wakati wananchi wanajiuliza michango yao mliochangisha CDM kuipeleka Hanang haijulikani imeenda wapi na hakuna jibu kuwa mlikusanya shilingi ngapi,

Rais Samia ametenga ekari 100 kwaajili ya makazi mapya ya wahanga wa Hanang, lakini Serikali itawajengea nyumba 101 ambazo kila moja itakuwa na vyumba vitatu na eneo litawekewa huduma zote za kijamii.

5. Kwa muda mfupi mno wa Rais Samia kuwa madarakani sasahivi kati ya Vijiji 10, Vijiji 9 vina umeme, hii ni hatua kubwa mno.

Hawa wana vijiji huwezi ukawaambia habari za kuandamana wakakuelewa.

6. Ndani ya muda mfupi tu Waalimu takribani 227,263 wamepandishwa madaraja na wanaendelea kuchapa kazi, hawa wataandamana kushukuru na kumpongeza Rais Dkt. Samia.

7. Kwenye kuongeza mapato makubwa hivi karibuni Serikali inatatajia kuanza kuchimba MAKAA YA MAWE katika mradi wa MCHUCHUMA, Tani karibia 315,000 zitachimbwa.

8. Wakulima wanafurahia Ruzuku kwenye Pembejeo za Kilimo ambazo zimefanya hali ya kilimo kuwa vizuri.

9. Ndani ya muda mfupi fedha za kigeni zimeongezeka baada ya kuongeza biashara nje ya nchi.

Mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi yameongezeka kwa asilimia 17.8
  • Novemba 2022 tuliuza Trilioni 29.8
  • Novemba 2023 tuliuza Trilioni 35.1

Mfano; Desemba 2022 hadi Desemba 2023 tumeuza NYAMA Tani 20,500 nje ya nchi, takribani mara mbili ya mauzo ya mwaka uliopita.

Hii inaonyesha ni namna gani Serikali inapambana kuleta maendeleo.

10. Miradi ya Maji nchi nzima inaendelea ili lengo la kumtua Mama Ndoo Kichwani litimie, mfano kwa Wilaya ya Ubungo kuna Miradi mikubwa miwili a) Tegeta A na b) Mshikamano
Ambayo itamaliza kabisa tatizo la maji.

Hawa wananchi hawahitaji maandamano bali wanahitaji kutoa pongezi kwa kazi kubwa inayofanywa.

Ni mengi yaliyofanyika na yote yana lengo la kumfaidisha Mwananchi ili aendelee kuwa na imani na Serikali yake.

Tusikubali kuyumbishwa na SIASA ZA MKIA WA MBUZI.

Kila Chama kijipange tukutane kwenye DEBE muda ukifika.

Ahsanteni.
 
Kuna kitu anakiogopa Mbowe

1705161885085.png
 
Na;
Hamis Abeid Baruani
UDASA, UDSM.

Kwa masikitiko makubwa leo Mhe. Mbowe ameushangaza umma kwa kuongea mambo mawili ambayo hadi sasa yamepingwa kila kona ya nchi.

1. Katangaza kususia maridhiano
2. Kaitisha anayoyaita maandamano ya amani.

a) Mhe. Mbowe kabla ya kususia MARIDHIANO unakumbuka lakini majuzi tu 31.12.2023 pale Hai wakati unaongoza Harambee ya kumalizia ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Usharika wa NSHARA MACHAME, Rais Dkt. Samia alichangia Tsh Milioni 150, haya yakiwa ni matunda ya MARIDHIANO ya kisiasa hapa nchini.

b) Mnakumbuka CDM mlikuwa na ziara pamoja na mikutano mikoa mbalimbali na mkafanya kwa amani hakuna mtu alienyooshewa kidole hata mmoja inamaana mmesahau kama hayo ni matunda ya MARIDHIANO

c) Maridhiano haya unayotaka kuyakataa hukumbuki kuwa ndio yamefanya viongozi wa CDM waliokuwa nje ya nchi kurejea nchini kufanya siasa kwa amani bila wasiwasi

d) Hujiulizi hata tukio la leo limefanyika vizuri kwa amani na umepewa ushirikiano wa namna zote kwenye vyombo vya habari kwasababu ya matunda ya MARIDHIANO yaliyoletwa na Rais Dkt. Samia

e) Hata umuhimu wa RUZUKU ambao pengine umepelekea kuhamisha Ofisi toka Kinondoni kwenda Mikocheni nao huoni kama ni matunda ya MARIDHIANO

Tujifunze kuwa waungwana tunapofanyiwa uungwana.

Wakati unafikiria kuandamanisha watu kumbuka wananchi wa sasa sio wa miaka ile, wananchi wanaona mambo makubwa yanayofanywa na Serikali yao, wanaona jitihada za Rais Samia kuwapigania. Ngoja niwakumbushe kidogo:-

1. Januari za miaka ya nyuma Wazazi walikuwa wanateseka kwa michango ya ujenzi wa madarasa na kununua madawati ila sasahivi hakuna mzazi hata mmoja nchini anaesumbuliwa na michango hii, Rais Samia kajenga madarasa mengi nchi nzima lakini pia Serikali kila mwezi inatoa takribani Bilioni 33.3 kugharamia elimu kwa wanafunzi wa ngazi ya awali, msingi na sekondari.

2. Rais Samia amesambaza Vifaa vya Afya Majimbo yote nchini kama ifuatavyo kwa ujumla
a) Vitanda vya wagonjwa 3080
b) Vitanda vya kujifungulia 1000
c) Magodoro 5500
d) Mashuka 36,808
e) Meza za Vitanda 306
f) Pia kasambaza magari ya kubebea wagonjwa (Ambulance) kila kona

Hii inaonesha namna gani ana huruma na wananchi na anajali afya zetu.

3. Takribani asilimia 95% ya Madai ya Watumishi yamefanyiwa kazi ndani ya muda mfupi. (Ulipaji madeni, Ongezeko la Posho, Mikataba ya hali bora, Ajira mpya, Mazingira bora ya Kazi).

4. Wakati wananchi wanajiuliza michango yao mliochangisha CDM kuipeleka Hanang haijulikani imeenda wapi na hakuna jibu kuwa mlikusanya shilingi ngapi,

Rais Samia ametenga ekari 100 kwaajili ya makazi mapya ya wahanga wa Hanang, lakini Serikali itawajengea nyumba 101 ambazo kila moja itakuwa na vyumba vitatu na eneo litawekewa huduma zote za kijamii.

5. Kwa muda mfupi mno wa Rais Samia kuwa madarakani sasahivi kati ya Vijiji 10, Vijiji 9 vina umeme, hii ni hatua kubwa mno.

Hawa wana vijiji huwezi ukawaambia habari za kuandamana wakakuelewa.

6. Ndani ya muda mfupi tu Waalimu takribani 227,263 wamepandishwa madaraja na wanaendelea kuchapa kazi, hawa wataandamana kushukuru na kumpongeza Rais Dkt. Samia.

7. Kwenye kuongeza mapato makubwa hivi karibuni Serikali inatatajia kuanza kuchimba MAKAA YA MAWE katika mradi wa MCHUCHUMA, Tani karibia 315,000 zitachimbwa.

8. Wakulima wanafurahia Ruzuku kwenye Pembejeo za Kilimo ambazo zimefanya hali ya kilimo kuwa vizuri.

9. Ndani ya muda mfupi fedha za kigeni zimeongezeka baada ya kuongeza biashara nje ya nchi.

Mauzo ya bidhaa na huduma nje ya nchi yameongezeka kwa asilimia 17.8
  • Novemba 2022 tuliuza Trilioni 29.8
  • Novemba 2023 tuliuza Trilioni 35.1

Mfano; Desemba 2022 hadi Desemba 2023 tumeuza NYAMA Tani 20,500 nje ya nchi, takribani mara mbili ya mauzo ya mwaka uliopita.

Hii inaonyesha ni namna gani Serikali inapambana kuleta maendeleo.

10. Miradi ya Maji nchi nzima inaendelea ili lengo la kumtua Mama Ndoo Kichwani litimie, mfano kwa Wilaya ya Ubungo kuna Miradi mikubwa miwili a) Tegeta A na b) Mshikamano
Ambayo itamaliza kabisa tatizo la maji.

Hawa wananchi hawahitaji maandamano bali wanahitaji kutoa pongezi kwa kazi kubwa inayofanywa.

Ni mengi yaliyofanyika na yote yana lengo la kumfaidisha Mwananchi ili aendelee kuwa na imani na Serikali yake.

Tusikubali kuyumbishwa na SIASA ZA MKIA WA MBUZI.

Kila Chama kijipange tukutane kwenye DEBE muda ukifika.

Ahsanteni.
Kama hizi ndo akili za UDASA basi mzee wetu Ulimwengu ana haki ya kuiita UDSM kwa namna alivyoiita
 
Hahahaaaa...
Nimepoteza muda wangu wa kunyonya VAT 69 kwa kusoma upupu.

Mlisema na mkaandika sana kwamba Mbowe ni mtoa taarifa.

Leo mmeangushiwa na kitu kizito mnaanza kuandika upupu.

Ni wananchi wepi hao wanaomshangaa Mbowe kwa hayo aliyoyaongea!!??

UDSM ya sasa ni "chawa in the making" tofauti na ile ya kwetu ya miaka ya 80 na 90.
 
Hahahaaaa...
Nimepoteza muda wangu wa kunyonya VAT 69 kwa kusoma upupu.

Mlisema na mkaandika sana kwamba Mbowe ni mtoa taarifa.

Leo mmeangushiwa na kitu kizito mnaanza kuandika upupu.

Ni wananchi wepi hao wanaomshangaa Mbowe kwa hayo aliyoyaongea!!??

UDSM ya sasa ni "chawa in the making" tofauti na ile ya kwetu ya miaka ya 80 na 90.
Wewe ulisom chuo gani?
 
Sipendi maandamano na kashi kashi za kisiasa ila maridhiano ilikuwa njia muafaka ya kuleta maendeleo ktk nchi yetu.

Siasa hizi ambazo zinataka kuanza zinaweza zikaaribu kabisa twaswira ya nchi yetu hapa ilipofikia na ikafifisha hatua xa maendeleo tuliyopiga kwa kipindi hiki cha Mama samia. maandamano yataambana na kamata kamata na vipigo kwa wananchi na kiwango cha uhasama na chuki baina ya watu na serkali inazidi kupandishwa kila kona, Mitandaoni, mikutano ya hadhara na maongezi baina ya mtu na mtu.

Niseme kuwa Serikali ya CCM ilifanya vizuri sana kuhakikisha inapata maoni ya wadau ili kuweza kuleta uchaguzi ulio huru na haki lakini maoni hayo hayajazingatiwa vilivyo na watu bado wana machungu ya kile walichofanyiwa 2019 na 2020 hii inaweza ikasababisha kuibua rabsha rabsha ambazo si muafaka ktk kipindi hiki ambacho ndiyo kwanz tunachemea kujenga uchumi wetu kutokana na majanga mbali mbali yaliyo ikumba Dunia.

CDM ni chama cha siasa kinafanya taratibu za kisiasa mimi ninachogopa ni pale yatakapo tokea makundi ya kigaidi na kufanya vitendi vya gigaidi kwa visingizio vya kisiasa. Mungu ibariki Tanzania na watu wake
 
Sipendi maandamano na kashi kashi za kisiasa ila maridhiano ilikuwa njia muafaka ya kuleta maendeleo ktk nchi yetu. Siasa hizi ambazo zinataka kuanza zinaweza zikaaribu kabisa twaswira ya nchi yetu hapa ilipofikia na ikafifisha hatua xa maendeleo tuliyopiga kwa kipindi hiki cha Mama samia...
Waambie.
 
Umepotea mdaa wote huo kuandikia ugoro kiasi hiki. Inawezekani hatujui maumivu ya watanzania tunao pitia. Mbowe Kawa pole Sana kwa maumivu haya wapo watu wako tayari kuingia Hat mistuni. maumivu haya
 
Umepotea mdaa wote huo kuandikia ugoro kiasi hiki. Inawezekani hatujui maumivu ya watanzania tunao pitia. Mbowe Kawa pole Sana kwa maumivu haya wapo watu wako tayari kuingia Hat mistuni. maumivu haya
Unaongelea nini kuhusu Mbowe kuwa mwenyekiti wa milele?
 
Sipendi maandamano na kashi kashi za kisiasa ila maridhiano ilikuwa njia muafaka ya kuleta maendeleo ktk nchi yetu. Siasa hizi ambazo zinataka kuanza zinaweza zikaaribu kabisa twaswira ya nchi yetu hapa ilipofikia na ikafifisha hatua xa maendeleo tuliyopiga kwa kipindi hiki cha Mama samia. maandamano yataambana na kamata...
Kwan kati ya Ccm na CDM nani anashida na kwa nini ccm wao wawafanye watu kama wajinga, unapoita maridhiano lazima hoja za kila pande zitiliwe mkazo kati ya vitu 10 basi unaweza kutekeleza hata 3 au 4 ili kuleta Imani kwa wananchi na pia wapinzani wako Sasa je ccm ametekeleza nini kati ya hayo waliozungumza huko ? Au waliita maridhiano tu kama propaganda Wakati ukweli hauko hivyo
 
Kwan kati ya Ccm na CDM nani anashida na kwa nini ccm wao wawafanye watu kama wajinga, unapoita maridhiano lazima hoja za kila pande zitiliwe mkazo kati ya vitu 10 basi unaweza kutekeleza hata 3 au 4 ili kuleta Imani kwa wananchi na pia wapinzani wako Sasa je ccm ametekeleza nini kati ya hayo waliozungumza huko ? Au waliita maridhiano tu kama propaganda Wakati ukweli hauko hivyo
Tuitumie vizuri 4R
 
Back
Top Bottom