Tusker Bariiiidi
JF-Expert Member
- Jul 3, 2007
- 5,520
- 2,091
Mkurugenzi wa Kampuni ya Fresho Investment Company (1999) Ltd ya Mjini Shinyanga Fredy Shoo maarufu Fresho amefariki dunia siku ya Jumatano Julai 28,2021 wakati akiendelea kupata matibabu jijini Dar es salaam.
Mwekezaji Mzawa Fredy Shoo ndiye mmiliki wa kiwanda cha kuchambulia pamba , kiwanda cha vifungashio na kiwanda cha kuchakata mafuta ya pamba pamoja na uwanja Mpya wa Kisasa uliopewa jina la ‘Fresho Complex’ uliopo katika eneo la Ugweto kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga,Pia ni kaka mkubwa wa Hillary Shoo mwenye viwanda vya Maji ya HILL,Hill Feeds na Kiwanda cha vifungashio cha Hill...
Na mdogo wao Harold Shoo maarufu HARSHO wa Moshi mwenye kiwanda cha Vifungashio Kwa Sadala Moshi kama HARSHO Packaging maarufu kwa Mifuko ya Super Sokoni.
Mungu Ailaze Mahali Pema Peponi Roho ya Marehemu Fresho. Amina
Pichani: Aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati John Magufuli akikata Utepe kuzindua Kiwanda cha Vifungashio cha FRESHO Shinyanga mwaka 2017 kushoto kwake mwenye Jaketi la Bluu bahari ni Marehemu Fredrick Shoo.
Mwekezaji Mzawa Fredy Shoo ndiye mmiliki wa kiwanda cha kuchambulia pamba , kiwanda cha vifungashio na kiwanda cha kuchakata mafuta ya pamba pamoja na uwanja Mpya wa Kisasa uliopewa jina la ‘Fresho Complex’ uliopo katika eneo la Ugweto kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga,Pia ni kaka mkubwa wa Hillary Shoo mwenye viwanda vya Maji ya HILL,Hill Feeds na Kiwanda cha vifungashio cha Hill...
Na mdogo wao Harold Shoo maarufu HARSHO wa Moshi mwenye kiwanda cha Vifungashio Kwa Sadala Moshi kama HARSHO Packaging maarufu kwa Mifuko ya Super Sokoni.
Mungu Ailaze Mahali Pema Peponi Roho ya Marehemu Fresho. Amina
Pichani: Aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati John Magufuli akikata Utepe kuzindua Kiwanda cha Vifungashio cha FRESHO Shinyanga mwaka 2017 kushoto kwake mwenye Jaketi la Bluu bahari ni Marehemu Fredrick Shoo.