Wadau inakuwaje hii nchi?
Aliyekuwa mkuu wa kitengo cha uwekezaji bw emanuel ole naiko sasa hivi ni mkurugenzi wa masuala ya kiserikali ya kampuni ya african barick gold.
Hii inaingiaje akilini ikizingatiwa kuwa huyu bwana ndiye aliyeipokea hii kamuni akiwa mkurugenzi?
Je hii kampuni inamilikiwa na nani?
Je inalipa kodi kama waliokuwa upande wa serikali sasa hivi ni wakurugenzi wake?
Wadau naombeni mnitoe hapa.
Hapa ndipo tunapokosea kama taifa!
Dalili zilijionyesha tangu mapema, kwa kauli hii nilishahisi kuwa kuna maslahi katika kauli yake - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...imba-madini-kwa-sababu-wanazalisha-umeme.htmlMkuu swali ni: Tufanye nini kama TAIFA, kwa Mataifa ya wenzetu jamaa huyu angehojiwa maswali mengi na kuchukuliwa hatua kali - hata kama amekwisha staafu conflict of INTEREST ziko pale pale.