Fatma Maghimbi huyoooooo!

Bi Fatma Maghimbi na Juma Othman Juma warejea C.C.M 17/10/2010


Wakongwe wawili wa siasa za vyama vingi visiwani Zanzibar Mheshimiwa Fatma Maghimbi na Juma Othman Juma wamerudisha kadi zao za uanachama wa Civic United Front (CUF) na kuchukua za Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo jimboni Kawe, Dar es Salaam na kuahidi wenzao wengi toka CUF watafuata nyayo zao.
6612199.jpg
L-R: Juma Othman Juma na Fatma Maghimbi​
Akielezea sababu zake za kurudi CCM, Juma Othman Juma amesema ameguswa kwa kazi kubwa aliyofanya Mheshimiwa Kikwete Tanzania Bara na Visiwani hususan aliporejesha amani na utulivu visiwani Unguja na Pemba kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka huu.

Alisema tangu historia ya vyama vingi ianze Tanzania, kila wakati wa uchaguzi wananchi wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba hulazimika kukimbia visiwani humo kwa kuhofia hali ya kutokuwa na usalama katika kipindi hicho.

"Lakini sasa napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Kikwete kwa kurudisha heshima ya nchi yetu duniani kwani mwaka huu wa kampeni, hakuna hata mmoja aliyehama visiwani humo kukimbia uchaguzi" alimaliza Juma Othman akishangiliwa na umati mkubwa wa wana CCM waliojitokeza kwenye mkutano huo.

Mama Fatma Maghimbi amewahi kuwa waziri kivuli wa Katiba na Sheria ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kama mbunge wa Chama Cha Wananchi CUF. Naye Juma Othman Juma amewahi kuwa muanzilishi wa Chama Cha Siasa visiwani kabla ya kujiunga na Chama cha Wananchi CUF.





7710032_orig.jpg
Kikwete akielezea mpango wa Serikali wa kujenga Fly-overs jijini Dar kupunguza msongamano wa magari.




1274446_orig.jpg
Kikwete akielezea mpango wa Serikali yake wa kujenga fly-overs Dar kupunguza msongamano wa magari




9405890_orig.jpg
wananchi wa Kawe wakichukua viti ili kukaa wakati wa mkutano wa kampeni za Kikwete/CCM




7905151_orig.jpg
Msanii wa Bongo Fleva Diamond akitumbuiza leo Kawe kwenye mkutano wa kampeni wa Kikwete/CCM




9613886_orig.jpg
Kikwete akimnadi Bw. Othman mgombea udiwani kata ya Kawe




5500086_orig.jpg
Kikwete akimnadi Mama Kizigha, mgombea ubunge wa CCM jimbo la Kawe




from: Bi Fatma Maghimbi na Juma Othman Juma warejea C.C.M -
 
Hana jipya huyo bibi kizee,ameona amechuja CUF,baada ya kukataliwa kwenye kura za maoni!njaa kali kweli kweli!
 
Huyu katanguliza maslahi mbele ndio maana kaamua kurudi CCM. Mamluki wote wanaanza kujionesha .
 
Anafikiri atapata UDC kama JK akipata urais, huyu sio mwanasiasa wa kweli ila ni fisadi wa siasa.
 
Huyu katanguliza maslahi mbele ndio maana kaamua kurudi CCM. Mamluki wote wanaanza kujionesha .

Ndo maana yake..mpiganaji wa kweli haezi kuhama chama ati kisa hakupitishwa kwene 'kula za maoni'..it says a lot about her well-being na intentions zake. Ni kweli kwa umri wake amejidhalilisha utu wake, elimu yake, umri wake, na wamama wote wanaopigana bega kwa bega kuikomboa nchi kutoka kwa makucha ya wahuni wachache..
 
waungwana wasiomjua bi fatma hawakuni kichwa kwani ni mtu alietumia miaka yake kumi na tano ya ubunge wa ke huko pemba kuwaambia wapemba kuwa watu wa bara ni wabaya yeye kaolewa nao na anawajua na alitumia maneno haya kwenye kampeni zake kuwagombanisha watu wa bara na visiwani kwa maslahi yake ya kisiasa , tusubiri sasa ameingia ccm kwani alikua akiwahutubia wana cuf na kuwaambia ccm ni wauwaji wa wapemba na wazanzibari sijui leo vipi bibi huyu anakula matapishi yake na kuingia ccm tusubiri tumsikie .
Yuko flexible jamani!
 
Fatma Maghimbi kachukua kadi ya CCM leo.Any insights???


10/17/2010

Mkutano wa Kampeni Kawe: Mama Fatma Magimbi arejea CCM



Mgombea Urais wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akimpokea Mama Fatma Magimbi, mkongwe wa siasa za visiwani Zanzibar aliyerudi Chama Cha Mapinduzi kutoka Chama Cha Wananchi CUF.
Picha na Campaign Communication Team
- Kaongozana na Juma Othman Juma
- Waiaga CUF na kuchukua kadi za CCM
- Waahidi wengi zaidi wanakuja nyuma yao visiwani humo

Wakongwe wawili wa siasa za vyama vingi visiwani Zanzibar Mheshimiwa Fatma Maghimbi na Juma Othman Juma wamerudisha kadi zao za CUF na kuchukua za CCM leo jimboni Kawe jijini Dar es salaam na kuahidi wenzao wengi watafuata nyayo zao kutoka CUF.


Akielezea sababu zake za kurudi CCM, Juma Othman Juma amesema ameguswa kwa kazi kubwa aliyofanya Mheshimiwa Kikwete Tanzania Bara na Visiwani hususan aliporejesha amani na utulivu visiwani Unguja na Pemba kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka huu.


Alisema tangu historia ya vyama vingi ianze Tanzania, kila wakati wa uchaguzi wananchi wengi wa visiwa vya Unguja na Pemba hulazimika kukimbia visiwani humo kwa kuhofia hali ya kutokuwa na usalama katika kipindi hicho.


"Lakini sasa napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Kikwete kwa kurudisha heshima ya nchi yetu duniani kwani mwaka huu wa kampeni, hakuna hata mmoja aliyehama visiwani humo kukimbia uchaguzi" alimaliza Juma Othman akishangiliwa na umati mkubwa wa wana CCM waliojitokeza kwenye mkutano huo wa kampeni.


Mama Fatma Maghimbi amewahi kuwa waziri kivuli wa Katiba na Sheria ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa kama mbunge wa Chama Cha Wananchi CUF. Naye Juma Othman Juma amewahi kuwa muanzilishi wa Chama Cha Siasa visiwani kabla ya kujiunga na Chama cha Wananchi CUF.

Posted by jakaya2010kikwete at 5:22 PM 0 comments
 
Who doesn't want a stable 'pension fund?' Huu upinzani kweli kiboko...
 
Waungwana wasiomjua Bi Fatma hawakuni kichwa kwani ni mtu alietumia miaka yake kumi na tano ya Ubunge wa ke huko Pemba kuwaambia Wapemba kuwa Watu wa Bara ni wabaya yeye kaolewa nao na anawajua na alitumia maneno haya kwenye kampeni zake kuwagombanisha watu wa bara na visiwani kwa maslahi yake ya kisiasa , tusubiri sasa ameingia CCM kwani alikua akiwahutubia wana CUF na kuwaambia CCM ni wauwaji wa Wapemba na Wazanzibari sijui leo vipi bibi huyu anakula matapishi yake na kuingia CCM tusubiri tumsikie .

Mlekwa siasa ni mchezo mchafu sana tambwe hiza aliishhutubiaga kigamboni kwamba kurudi CCM ni kama kulala na mama yake,sasa hivi yuko CCM ndo mzee wa propaganda, kajilaani mwenyewe!
 
,,,,,,,,,,,,,,Binafsi nitoe angalizo kwa CUF na CHADEMA na hasa CHADEMA kwa maana naona CUF hasa kwa upande wa visiwani wameanza kujirekebisha tena nitoe pongezi za dhati kwa Maalim Seif Sharif Hamad kwa kuona mbali ambapo wengine hawajapaona na bila shaka Mungu atambariki na kumuongoza katika azma yake njema ya kusaini makubaliano ya mwafaka. CHADEMA niwaonye tu kuwa kama kweli wanataka kuwa chama kizuri cha upinzani wajaribu kuacha pupa, watulie chini , waache kulumbanalumbana , wakubali kukosolewa wawe na moyo na bidii ya kujifunza na mwishowe wakatae ushabiki na......................Nova Kambota Is Always A gentle Man Feel Proud To Visit His Site, call 0717-709618 or 0783-610926,email;novakamota@gmail.com
 
Inabidi awatafute akina Msabah na Dr Kabourou.....kama mnawakumbuka....very much silenced...like selling your own vocal abilities
 
Tetetete! Kahama CUF na kwenda CCM? Ukweli ni kwamba kabadili tu Idara! Zamani yale mambo ya Udini wa CUF yalikuwa ni sera nzuri ambayo CCM wameiga na hivyo mama hana haja ya kubakia huko! Tetetetete..kahama Idara tu huyo
 
Waungwana wasiomjua Bi Fatma hawakuni kichwa kwani ni mtu alietumia miaka yake kumi na tano ya Ubunge wa ke huko Pemba kuwaambia Wapemba kuwa Watu wa Bara ni wabaya yeye kaolewa nao na anawajua na alitumia maneno haya kwenye kampeni zake kuwagombanisha watu wa bara na visiwani kwa maslahi yake ya kisiasa , tusubiri sasa ameingia CCM kwani alikua akiwahutubia wana CUF na kuwaambia CCM ni wauwaji wa Wapemba na Wazanzibari sijui leo vipi bibi huyu anakula matapishi yake na kuingia CCM tusubiri tumsikie .
Katika vitu ambavyo sitakaa nifanye katika maisha yangu ni kusema kitu hiki leo tena dunia nzima ikinisikiliza halafu kesho kufanya tofauti kabisa na maneno yangu ya jana. To me this is so embarassing, kweli hata watoto wangu watanishangaa sana. iweje majority ya wanasiasa wanaishi kwa uongo tena uongo mkubwa sana ina maana they have no one from their family to tell them this is not right ama kila mtu huku Tz anaona uongo ni sawa?
 
Back
Top Bottom