mi_mdau
JF-Expert Member
- Oct 29, 2010
- 1,104
- 1,476
wadau mi si mzoefu sana wa mapenzi lakini nimegundua kitu ambacho labda na wengine ambao pengine ni wazoefu linaweza kuwasaidia, hata walio kwenye ndoa.
Tulipoanza mahusiano ya kimapenzi na rafiki yangu wa kike, kwa hakika tulihisi kupendana na muda mwingi tulikuwa na furaha. Shida moja kubwa ilikuwa ni kugombana na kubishana kila baada ya muda mfupi sana. Kitu kidogo kinaweza kuwakosesha raha mliyokuwa nayo kutwa nzima na mkalala na maumivu. Baada ya muda na siku kadhaa nikaja kugundua kuwa hata ikiwa ni ugomvi mdogo, bila kujali nani ana makosa wote tulikuwa tukipanda juu na kila mmoja anajifanya ndo mwenye sauti, hakuna aliyetaka kujishusha.
Baada ya siku kadhaa tulikaa chini na kujiuliza kuwa labda kuna 'mdudu' na anatokea wapi. Kwa sababu mimi nilijua nampenda kwa dhati sasa kwa nn nagombana naye, na yeye kwa wakati wake akawa ananiambia kitu kama hicho. Niliwaza na kumwambia kuwa tuendelee kuishi maisha yetu ya kawaida bila kuigiza ila tu, mmoja anapokasirishwa, hata kitu kikubwa, since hataki kunipoteza kirahisi, aulize kwa upole tu. mfano "mpenzi, mbona nimekupigia simu, nimekutumia message, hujajibu?" badala ya "wewe mi napiga, nakutumia sms, hujibu? unaniringia kwa kuwa nakupenda au? ulikuwa unaongea na NANI?".
Tukagundua kuwa si mara zote mtu anafanya makosa kwa kukusudia, kwa hiyo ukimuuliza kwa ukali unasababisha aone unamwonea na yeye anapandisha hasira, na hakuna kuelewana. Lakini hata kama amekosa kwa kukusudia, ukimuuliza kwa upole, atajutia kosa lake (kama anakupenda) na atajirudi kwa upesi. Tangu hapo suala la ugomvi kati yetu limekuwa la nadra sana (halikwepeki kwa asilimia 100) na mapenzi ni raha zaidi.
TUJARIBU KUJISHUSHA, KUHESHIMIANA NA UAMINIFU
Tulipoanza mahusiano ya kimapenzi na rafiki yangu wa kike, kwa hakika tulihisi kupendana na muda mwingi tulikuwa na furaha. Shida moja kubwa ilikuwa ni kugombana na kubishana kila baada ya muda mfupi sana. Kitu kidogo kinaweza kuwakosesha raha mliyokuwa nayo kutwa nzima na mkalala na maumivu. Baada ya muda na siku kadhaa nikaja kugundua kuwa hata ikiwa ni ugomvi mdogo, bila kujali nani ana makosa wote tulikuwa tukipanda juu na kila mmoja anajifanya ndo mwenye sauti, hakuna aliyetaka kujishusha.
Baada ya siku kadhaa tulikaa chini na kujiuliza kuwa labda kuna 'mdudu' na anatokea wapi. Kwa sababu mimi nilijua nampenda kwa dhati sasa kwa nn nagombana naye, na yeye kwa wakati wake akawa ananiambia kitu kama hicho. Niliwaza na kumwambia kuwa tuendelee kuishi maisha yetu ya kawaida bila kuigiza ila tu, mmoja anapokasirishwa, hata kitu kikubwa, since hataki kunipoteza kirahisi, aulize kwa upole tu. mfano "mpenzi, mbona nimekupigia simu, nimekutumia message, hujajibu?" badala ya "wewe mi napiga, nakutumia sms, hujibu? unaniringia kwa kuwa nakupenda au? ulikuwa unaongea na NANI?".
Tukagundua kuwa si mara zote mtu anafanya makosa kwa kukusudia, kwa hiyo ukimuuliza kwa ukali unasababisha aone unamwonea na yeye anapandisha hasira, na hakuna kuelewana. Lakini hata kama amekosa kwa kukusudia, ukimuuliza kwa upole, atajutia kosa lake (kama anakupenda) na atajirudi kwa upesi. Tangu hapo suala la ugomvi kati yetu limekuwa la nadra sana (halikwepeki kwa asilimia 100) na mapenzi ni raha zaidi.
TUJARIBU KUJISHUSHA, KUHESHIMIANA NA UAMINIFU