Fahamu: Saudi Arabia inafungua duka la Pombe baada ya marufuku ya Miaka zaidi ya 70

Status
Not open for further replies.

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,024
1,617
Saudi Arabia yatangaza kufungua Duka la Kuuza Pombe Mjini Riyadh baada ya Marufuku ya zaidi ya Miaka 70

Wateja watakuwa ni Wafanyakazi wa Kidiplomasia wasio Waislamu , ambao kwa Miaka mingi wamekuwa wakiagiza pombe kwa njia rasmi ifahamikayo kama "Diplomatic Pouches."

Marufuku ya Pombe Nchini humo ilikuwa Sheria tangu Mwaka 1952, baada ya Mtoto wa Mfalme Abdulaziz, Mishari bin Abdulaziz Al Saud kulewa na kumuua kwa risasi Mwanadiplomasia wa Uingereza Cyril Ousman, Novemba 1951

Wateja watapewa Kiwango cha juu cha 240 "alama" za pombe kwa Mwezi, ambapo hawataruhusiwa kununua zaidi ya kiwango hicho. Lita moja ya Pombe Kali itakuwa na thamani ya alama 6, Lita moja ya Mvinyo itakuwa na alama 3, na Lita moja ya Bia itakuwa na alama 1.

Hatua hizi ni sehemu ya mipango inayojulikana kama "Vision 2030" ya kulegeza Sheria za Saudi Arabia chini ya Mwana-Mfalme na Mtawala wa nchi hiyo Mohammed bin Salman

Kulingana na Sheria ya sasa ya Saudi Arabia, adhabu kwa kunywa au kukutwa na pombe inaweza kujumuisha faini, kifungo, kupigwa hadharani, na kufukuzwa nchini kwa wale wasio Raia
 
Saudi Arabia yatangaza kufungua Duka la Kuuza Pombe Mjini Riyadh baada ya Marufuku ya zaidi ya Miaka 70

Wateja watakuwa ni Wafanyakazi wa Kidiplomasia wasio Waislamu , ambao kwa Miaka mingi wamekuwa wakiagiza pombe kwa njia rasmi ifahamikayo kama "Diplomatic Pouches."

Marufuku ya Pombe Nchini humo ilikuwa Sheria tangu Mwaka 1952, baada ya Mtoto wa Mfalme Abdulaziz, Mishari bin Abdulaziz Al Saud kulewa na kumuua kwa risasi Mwanadiplomasia wa Uingereza Cyril Ousman, Novemba 1951

Wateja watapewa Kiwango cha juu cha 240 "alama" za pombe kwa Mwezi, ambapo hawataruhusiwa kununua zaidi ya kiwango hicho. Lita moja ya Pombe Kali itakuwa na thamani ya alama 6, Lita moja ya Mvinyo itakuwa na alama 3, na Lita moja ya Bia itakuwa na alama 1.

Hatua hizi ni sehemu ya mipango inayojulikana kama "Vision 2030" ya kulegeza Sheria za Saudi Arabia chini ya Mwana-Mfalme na Mtawala wa nchi hiyo Mohammed bin Salman

Kulingana na Sheria ya sasa ya Saudi
Arabia, adhabu kwa kunywa au kukutwa na pombe inaweza kujumuisha faini, kifungo, kupigwa hadharani, na kufukuzwa nchini kwa wale wasio Raia
Nilichokiona hapo ni kwamba pombe ilikuwa halali hadi 1952, baada ya mauwaji pombe ikapigwa marufuku. Siyo suala la dini. Sasa kwanini waislam wanakatazwa baada ya mwanamfalme kufanya makosa binafsi?
 
Kama hilo nalo limehalalishwa/limeruhusiwa na mambo mengine yataruhusiwa tuu, ni jambo la muda.
 
Nilichokiona hapo ni kwamba pombe ilikuwa halali hadi 1952, baada ya mauwaji pombe ikapigwa marufuku. Siyo suala la dini. Sasa kwanini waislam wanakatazwa baada ya mwanamfalme kufanya makosa binafsi?
Pombe imeharamishwa ndani ya Quran karne ya sita sasa wewe unaleta historia za Watu eti tumekatazwa pombe na Mwanamfalme ?
 
Diplomats walikua wanaagiza halafu wanauza on black market. Sasa hivi hawatoweza kuagiza tena.
 
Pombe imeharamishwa ndani ya Quran karne ya sita sasa wewe unaleta historia za Watu eti tumekatazwa pombe na Mwanamfalme ?
Kama mleta mada kadanganya kwamba saudi Arabia mwanamfalme alilewa mwaka 1951 na akamuua mwanadiplomasia, na mwaka 1952 pombe ikaharamishwa Saudi Arabia umpinge mleta mada kwanza. Sasa unaacha mada kwanini?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom