Mgeni wa Jiji
JF-Expert Member
- Jul 27, 2017
- 7,928
- 13,413
Habari wana JF
Leo naomba nigusie maswala machache yanayohusu sheria na utendaji wa makampuni binafsi.
Naamini umewahi kusikia juu ya wito wa kurasimisha biashara na makampuni. Wapo viongozi wa kiserikali na hata binafsi wamekuwa wakihamasisha wafanyabiashara kurasimisha mifumo yao ya biashara ana kwa kusajili biashara au makampuni.
Pengine labsa na wewe una ndoto za kuja kuwq na kampuni yako binafsi au tayari unayo ila unahitaji kufahamu ABCs juu ya sheria za makampuni n namna zinafanya kazi.
Basi leo nitakufahamisha mambo kadhaa ya sheria zinazosimamia makampuni.
Makampuni binafsi Tanzania yanasajiliwa chini ya wakala BRELA kupitia mfumo wa kielectronic unaoitwa ORS (Online Registration System). Kwa leo sitazungumzia mfumo huu ila nimeona nikufahamishe hili kwanza.
Sasa twende kwenye uendeshaji wa makampuni binafsi na sheria zinazosimamia. Sheria kuu ni Sheria ya makampuni yenye marejeo ya 2002, sheria nyingine hutegemea na shughuli kampuni husika inazofanya.
Ifahamike kuwa Kampuni ni mtu kisheria hivyo kama una kampuni basi jua wazi kuwa wewe sio hiyo kampuni bali hiyo kampuni ni mtu anayejitegemea kabisa kisheria hata linapokuja swala la kushitaki au kushitakiwa Mahakamani atakayehusika sio wewe bali ni hiyo kampuni.
Pili ifahamike kuwa kwa Tanzania, kampuni zoteni lazima ziwe na wamiliki kuanzia wawili na umiliki wa kampuni unatokana na hisa hivyo bila kuwa mwanahisa huwezi kuwa mmiliki wa kampuni yoyote Tanzania.
Jambo lingine muhimu kulifahamu ni kuwa mara baada ya kusajili kampuni na kupatiwa cheti, kampuni hiyo inatakiwa kupata leseni kwa mamlaka inayosimamia shughuli inazotaka kuzifanya, mfano kama ni kampuni ya vipodozi basi ni sharti kiwepo kibali cha mamlaka husika, kama ni vinywaji hivyo hivyo pia kwa shughuli za utalii n.k
Kuna kasumba kwa wamiliki wengi wa kampuni kudhani kuwa mara baada ya kufanya usajili BRELA basi wanaweza kuanza shughuli zao na pia ni wazi zipo biashara na kampuni nyingi zinazofanya shughuli kwa mtindo huu ambao ni makosa ambayo huweza kuwa jinai kwa baadhi ya mamlaka.
Jambo lingine muhimu la kisheria kulifahamu ni juu ha Hisa, mara baada ya kusajili kampuni ni sharti la kisheria kufanya kikao cha awali. Katika kikao hichi kunaweza kuwa na ajenda nyingi ila ni muhimu ajenda ya kulipia hisa iwepo mezani na ijulikane idadi ya hisa za kulipiwa.
Ifahamike pia kuwa mtaji wa kampuni unatokana na hisa za kampuni. Na kuwa kampuni haiwezi kuwa n mtaji nje ya hisa zake. Japo huu ndio muongozo wa kesheria lakini hali ni tofauti hapa nchini kwqni kampuni nyingi hazijawahi kuita wala kulipiwa hisa zao na wanahisa wake hivyo kufanya shughuli na biashara zao kwa fedha za watu binafsi, hali hii ni hatari kwani inaweza hadi kuwaingiza kwenye tuhuma za utakatishaji fedha wamiliki wa kampuni husika. Hii ni hatari sana.
Jambo lingine muhimu la kisheria kulifahamu ni kuwa kampuni ni lazima na sharti ifanye mahesabu ya kila mwaka na kutuma ripoti BRELA, na kuchelewesha kufanya hivyo au kutokufanya hivyo ni kosa na husababisha uwepo wa adhabh ya faini.
Mwisho kama unafikiri au tayari umeshasajili kampuni ni vyema sana kutafuta wakili ili akusaidie namna bora ya kuendesha biashara na shughuli za kampuni yako bila kuingia kwenye matatizo na mamlaka mbali mbali nchini.
Ikiwa unahitaji ufafanuzi juu ya jambo lolote ambalo ama nimelielezea hapo juu au sijalielezea hapo juu usisite kuuliza kwenye comment, nitajitahidi kujibu kwa wakati kwani nafahamu kuwa uzi huusiwezi nikawa nimeelezea kila jambo muhimu.
Kila la heri.
Leo naomba nigusie maswala machache yanayohusu sheria na utendaji wa makampuni binafsi.
Naamini umewahi kusikia juu ya wito wa kurasimisha biashara na makampuni. Wapo viongozi wa kiserikali na hata binafsi wamekuwa wakihamasisha wafanyabiashara kurasimisha mifumo yao ya biashara ana kwa kusajili biashara au makampuni.
Pengine labsa na wewe una ndoto za kuja kuwq na kampuni yako binafsi au tayari unayo ila unahitaji kufahamu ABCs juu ya sheria za makampuni n namna zinafanya kazi.
Basi leo nitakufahamisha mambo kadhaa ya sheria zinazosimamia makampuni.
Makampuni binafsi Tanzania yanasajiliwa chini ya wakala BRELA kupitia mfumo wa kielectronic unaoitwa ORS (Online Registration System). Kwa leo sitazungumzia mfumo huu ila nimeona nikufahamishe hili kwanza.
Sasa twende kwenye uendeshaji wa makampuni binafsi na sheria zinazosimamia. Sheria kuu ni Sheria ya makampuni yenye marejeo ya 2002, sheria nyingine hutegemea na shughuli kampuni husika inazofanya.
Ifahamike kuwa Kampuni ni mtu kisheria hivyo kama una kampuni basi jua wazi kuwa wewe sio hiyo kampuni bali hiyo kampuni ni mtu anayejitegemea kabisa kisheria hata linapokuja swala la kushitaki au kushitakiwa Mahakamani atakayehusika sio wewe bali ni hiyo kampuni.
Pili ifahamike kuwa kwa Tanzania, kampuni zoteni lazima ziwe na wamiliki kuanzia wawili na umiliki wa kampuni unatokana na hisa hivyo bila kuwa mwanahisa huwezi kuwa mmiliki wa kampuni yoyote Tanzania.
Jambo lingine muhimu kulifahamu ni kuwa mara baada ya kusajili kampuni na kupatiwa cheti, kampuni hiyo inatakiwa kupata leseni kwa mamlaka inayosimamia shughuli inazotaka kuzifanya, mfano kama ni kampuni ya vipodozi basi ni sharti kiwepo kibali cha mamlaka husika, kama ni vinywaji hivyo hivyo pia kwa shughuli za utalii n.k
Kuna kasumba kwa wamiliki wengi wa kampuni kudhani kuwa mara baada ya kufanya usajili BRELA basi wanaweza kuanza shughuli zao na pia ni wazi zipo biashara na kampuni nyingi zinazofanya shughuli kwa mtindo huu ambao ni makosa ambayo huweza kuwa jinai kwa baadhi ya mamlaka.
Jambo lingine muhimu la kisheria kulifahamu ni juu ha Hisa, mara baada ya kusajili kampuni ni sharti la kisheria kufanya kikao cha awali. Katika kikao hichi kunaweza kuwa na ajenda nyingi ila ni muhimu ajenda ya kulipia hisa iwepo mezani na ijulikane idadi ya hisa za kulipiwa.
Ifahamike pia kuwa mtaji wa kampuni unatokana na hisa za kampuni. Na kuwa kampuni haiwezi kuwa n mtaji nje ya hisa zake. Japo huu ndio muongozo wa kesheria lakini hali ni tofauti hapa nchini kwqni kampuni nyingi hazijawahi kuita wala kulipiwa hisa zao na wanahisa wake hivyo kufanya shughuli na biashara zao kwa fedha za watu binafsi, hali hii ni hatari kwani inaweza hadi kuwaingiza kwenye tuhuma za utakatishaji fedha wamiliki wa kampuni husika. Hii ni hatari sana.
Jambo lingine muhimu la kisheria kulifahamu ni kuwa kampuni ni lazima na sharti ifanye mahesabu ya kila mwaka na kutuma ripoti BRELA, na kuchelewesha kufanya hivyo au kutokufanya hivyo ni kosa na husababisha uwepo wa adhabh ya faini.
Mwisho kama unafikiri au tayari umeshasajili kampuni ni vyema sana kutafuta wakili ili akusaidie namna bora ya kuendesha biashara na shughuli za kampuni yako bila kuingia kwenye matatizo na mamlaka mbali mbali nchini.
Ikiwa unahitaji ufafanuzi juu ya jambo lolote ambalo ama nimelielezea hapo juu au sijalielezea hapo juu usisite kuuliza kwenye comment, nitajitahidi kujibu kwa wakati kwani nafahamu kuwa uzi huusiwezi nikawa nimeelezea kila jambo muhimu.
Kila la heri.