EXIM Credit Cards-MasterCard

Dark City

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
16,253
11,598
Nimejaribu kufuatilia suala la credit cards za Exim na kupewa utaratibu wao kwa muhtasari. Ingawa wamejitahidi sana kutoa hiyo huduma, bado nadhani kuna vitu ambavyo wanatakiwa kutuelimisha. Kwa sasa ningeomba wenye uzoefu watusaidie ili tupanue ufahamu wetu na tuweze kuchangamkia hii huduma.

  1. Wanatoa kadi za aina mbili (Silver na Gold)
  2. Ili uweze kupata Silver, lazima uweke fixed deposit ya Tshs 1m (or $1000) na unaweza kutumia kwenye credit card yako hadi 80% ya hizo pesa ulizoweka kwenye fixed deposit. Kwa upande wa Gold, fixed deposit ni 5m ($5000). Pia unaweza kutumia hadi 80%.
  3. Kuna gharama ya kujiunga (kama sijakosea ni 25000) na kuna gharama nyingine nimesahau. Pia unatakiwa kulipa 50,000/- kwa mwaka.
  4. Ukitumia kununa vitu hakuna gharama ila ukichukua pesa kwenye ATM au cash machine yoyote unalipishwa 3%.
  5. Utaletewa muhtasari wa matumizi kwa mwezi na ukichelewa kulipa utalipishwa penalty ya Tsh 2500/- kila siku.
Inawezekana kuna taarifa nyingine lakini hizo ndizo nimekumbuka. Naomba kupata michango yenu wadau.
 
Hii naona ni Debit Card inayojifanya ni Credit Card. Kwa sababu unaweza kutumia hela zilizopo kwenye account tu.
Tena labda ni mbaya kuliko Debit Card kwa sababu inabidi uwe na hiyo minimum ya 1m au 5m kwenye account.
 
This is a direction this country must use!

NMB, CRDB, NBC mko wapi??
Service hii ya Exim ni ya siku nyingi...

Wala si Credit Card, ni Debit Card.

Niliwahi kutumia Gold na niliumia vibaya (more than a year ago), card zinakuwa rejected sehemu nyingi!

CRDB wao nasikia inafanya kazi vizuri, tatizo usi-deal na branches za nje ya Jiji la Dar es Salaam kama una-apply, nenda Premier Branch (Benjamin Towers) na wambie unachotaka kufanya, wao watakupa maelekezo ambayo naamini yatakusaidia kwa urahisi. Tatizo matawi ya mabenki yetu ni kuwa na customer service isiyojali wateja, wengine hata services hizi hawajui kama zipo na hata kuzielezea hawawezi.

You can read this topic:

Using PayPal and MoneyBookers with CRDB VISA Card
 
Service hii ya Exim ni ya siku nyingi...

Wala si Credit Card, ni Debit Card.

Niliwahi kutumia Gold na niliumia vibaya (more than a year ago), card zinakuwa rejected sehemu nyingi!

CRDB wao nasikia inafanya kazi vizuri, tatizo usi-deal na branches za nje ya Jiji la Dar es Salaam kama una-apply, nenda Premier Branch (Benjamin Towers) na wambie unachotaka kufanya, wao watakupa maelekezo ambayo naamini yatakusaidia kwa urahisi. Tatizo matawi ya mabenki yetu ni kuwa na customer service isiyojali wateja, wengine hata services hizi hawajui kama zipo na hata kuzielezea hawawezi.

You can read this topic:

Using PayPal and MoneyBookers with CRDB VISA Card

Ahsante sana mkuu kwa hii taarifa.

Hilo likuwa swali langu la kwanza kwao na wakadai wanafanya hivyo kwa sababu sisi (Watanzania) hatuna utamaduni wa kulipa mikopo na pia hatuna anwani! Kwa hiyo wanaweka hiyo kitu kama dhamana.

Nilipotaka kujua kwa nini wasitafute dhamana ya aina nyingine eg. mwajiri au mali zisizohamishika wakaruka na kusema kuwa hiyo haina uhakika kama kukalia pesa zako kwenye fixed deposit. Hilo limenitatiza sana kwani kama ninazo 5m kwa nini nitafute credit zao zenye gharama zaidi?
 
Nimejaribu kufuatilia suala la credit cards za Exim na kupewa utaratibu wao kwa muhtasari. Ingawa wamejitahidi sana kutoa hiyo huduma, bado nadhani kuna vitu ambavyo wanatakiwa kutuelimisha. Kwa sasa ningeomba wenye uzoefu watusaidie ili tupanue ufahamu wetu na tuweze kuchangamkia hii huduma.

  1. Wanatoa kadi za aina mbili (Silver na Gold)
  2. Ili uweze kupata Silver, lazima uweke fixed deposit ya Tshs 1m (or $1000) na unaweza kutumia kwenye credit card yako hadi 80% ya hizo pesa ulizoweka kwenye fixed deposit. Kwa upande wa Gold, fixed deposit ni 5m ($5000). Pia unaweza kutumia hadi 80%.
  3. Kuna gharama ya kujiunga (kama sijakosea ni 25000) na kuna gharama nyingine nimesahau. Pia unatakiwa kulipa 50,000/- kwa mwaka.
  4. Ukitumia kununa vitu hakuna gharama ila ukichukua pesa kwenye ATM au cash machine yoyote unalipishwa 3%.
  5. Utaletewa muhtasari wa matumizi kwa mwezi na ukichelewa kulipa utalipishwa penalty ya Tsh 2500/- kila siku.
Inawezekana kuna taarifa nyingine lakini hizo ndizo nimekumbuka. Naomba kupata michango yenu wadau.

Wizi mtupu. Unakopa hela yako tu. CRDB Visa card is the best.
 
wakuu ninaomba ushauri jinsi ya kupata crdb visa card au kama kuna benki nyingine yenye utaratibu kama huo
 
Service hii ya Exim ni ya siku nyingi...

Wala si Credit Card, ni Debit Card.

Niliwahi kutumia Gold na niliumia vibaya (more than a year ago), card zinakuwa rejected sehemu nyingi!

CRDB wao nasikia inafanya kazi vizuri, tatizo usi-deal na branches za nje ya Jiji la Dar es Salaam kama una-apply, nenda Premier Branch (Benjamin Towers) na wambie unachotaka kufanya, wao watakupa maelekezo ambayo naamini yatakusaidia kwa urahisi. Tatizo matawi ya mabenki yetu ni kuwa na customer service isiyojali wateja, wengine hata services hizi hawajui kama zipo na hata kuzielezea hawawezi.
https://www.jamiiforums.com/busines...pal-and-moneybookers-with-crdb-visa-card.html

Kiongozi ni kweli.

Ni majuzi tu hapa nimeenda tawi la CRDB la Mlimani City kuulizia kuhusu upatikanaji wa credit card mhusika anayehusika na kadi akanambia eti huduma ya credit card haipo CRDB! Nikapoteza appetite ya kuwa mteja wao. Naamini bongo kila kona wamejaa watu incompetent.
 
Mimi naunga mkono kauli ya Invisible kuwa hio ni Credit Card. Ukiwa na hio kadi unapewa kiasi fulani cha fwedha ili utumie ikiwa ni mkopo wa dharura, sasa inategemea na kipato chako cha kila mwezi katika current account yako.

Pia katika nchi zilizoendelea watu wa benki hupenda kushauri wateja wenye kutumia akaunti mara kwa mara kwa kuwa na fwedha za kutosha kuchukua credit cards ili ziwasadie kwa matumizi mbalimbali ya dharura ambayo mengi yanakuwa yanahitaji kulipa kwa credit card.

Kwa hio unapopewa kadi hizo kunakuwa na limit na ukitumia ama iwe ndani ya nchi au nje basi kunakuwa na charge na ndio naona Exim wanatandika 3%.

Ila mtu huna haja ya kutaka credit cards ikiwa una uwezo wa kutumia debit card na pia kuwa na overdraft ya nguvu ambayo pia ni mtindo kama wa credit cards.
 
Kiongozi ni kweli.

Ni majuzi tu hapa nimeenda tawi la CRDB la Mlimani City kuulizia kuhusu upatikanaji wa credit card mhusika anayehusika na kadi akanambia eti huduma ya credit card haipo CRDB! Nikapoteza appetite ya kuwa mteja wao. Naamini bongo kila kona wamejaa watu incompetent.

Ya CRDB sio credid card, ni Visa Debit card.
 
exim sasa hivi wametoa huduma mpya ya faida acc nimeifwatilia sijapata detail sana ila ina visa na credit card ila ni debit na unafungua kwa kuanzia elfu 5000 na inakuwa na insurence ya millioni moja aina makato unapochukua na unatumia kwenye mashine yoyote ndani na nje ya nchi
 
mimi nina kadi ya Exim Silver na Visa ya CRDB. Zote zinafanya kazi. Lakini nimekuwa napata shida kidogo na kadi ya Exim nyakati nyingine nikiwa nataka kununua kitu on line. Kadi inakuwa rejected. Ila kwa kutumia Visa card ya CRDB sijawahi kupata tatizo hilo.
 
Back
Top Bottom