Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Nimejaribu kufuatilia suala la credit cards za Exim na kupewa utaratibu wao kwa muhtasari. Ingawa wamejitahidi sana kutoa hiyo huduma, bado nadhani kuna vitu ambavyo wanatakiwa kutuelimisha. Kwa sasa ningeomba wenye uzoefu watusaidie ili tupanue ufahamu wetu na tuweze kuchangamkia hii huduma.
- Wanatoa kadi za aina mbili (Silver na Gold)
- Ili uweze kupata Silver, lazima uweke fixed deposit ya Tshs 1m (or $1000) na unaweza kutumia kwenye credit card yako hadi 80% ya hizo pesa ulizoweka kwenye fixed deposit. Kwa upande wa Gold, fixed deposit ni 5m ($5000). Pia unaweza kutumia hadi 80%.
- Kuna gharama ya kujiunga (kama sijakosea ni 25000) na kuna gharama nyingine nimesahau. Pia unatakiwa kulipa 50,000/- kwa mwaka.
- Ukitumia kununa vitu hakuna gharama ila ukichukua pesa kwenye ATM au cash machine yoyote unalipishwa 3%.
- Utaletewa muhtasari wa matumizi kwa mwezi na ukichelewa kulipa utalipishwa penalty ya Tsh 2500/- kila siku.