Eti mume gani? Ulikuwa wapi siku zote?

Huyo mama ameongea vibaya kwa kweli. maneno ya namna hii ndiyo yanawafanya baadhi ya wanaume kujinyonga au kunywa sumu. Kamdhalilisha sana, hasa kudharau uwanaume wake. Ni kitendo kibaya. Hata kama jamaa akujaliwa sana ilibidi amheshimu kwani Bwana wa upendo ndiye aliyempatia.

Kweli kama ulivyosema ni Bwana wa Upendo ndiye aliyempatia.
Hakuna kitendo kiovu kama mwanamke au hata mwanaume kumkashifu mzazi mwenzie mbele ya watoto licha ya watu baki.Ni nani asiyeona mzazi wake kama ndiyo zaidi ya mtu mwingine hapa duniani?
Mama unapomdhalilisha baba wa watoto wako namna ile... ni sawasawa na kuwatusi wanao! Tena watoto kama ni wakubwa watakushangaa iweje hukuchagua mwanaume bora kwa ajili ya ubaba wa watoto wako?Tujisahihishe jamani.
Tukirudi upande wa pili kwa akina baba, ni mara ngapi tunasikia au hata kushuhudia wababa wakipiga wake zao tena wakati mwingine kuwaacha uchi wa mnyama bila kujali kuwa huyo mama ndiye aliyekufanya ukaonekana mwanaume mbele za watu kwa kukuheshimu na kukuzalia watoto?
Acheni hizo wakina baba.
 
wanasema panapofuka moshi pana moto.hivi kweli hasira tu itamfanya atamke yote hayo?
 
Hayo ndiyo maneno ambayo huwezi kuyafuta. Yakishatoka kinywani mwako ndio imetoka hiyo.
 
Mimi naona talaka zinanukia.hata kama mama alikuwa anapeana mavi2z kama fainali ya kombe la dunia naamini ataenda tu.haha.
 
Mimi naona talaka zinanukia.hata kama mama alikuwa anapeana mavi2z kama fainali ya kombe la dunia naamini ataenda tu.haha.

Hiyo ni verbal abuse na itakuwa bora huyo baba akimtaliki huyo mkewe.

nyani nakubaliana nawe hapo.ingekuwa mie tayari ningekuwa niko kwa kadhi.doh!

Waungwana,
Hivi kweli hapo mnaona kuna kitu kinachoitwa ndoa kinachosubiri talaka?
Tena kama ndio hao wanaofikiria kuandikiana talaka kwenye karatasi basi huyo bwana wala asijisumbue kuandika... huyo bibie tayari ana lake jambo.Mwanamke akishafikia hatua hiyo ya kukutukana na kukuadhiri ujue she dont care! Tena ukimwandikia talaka ndo umemrahisishia misheni zake.Kawaida mwanamke anayempenda mumewe atamlinda kwa gharama yeyote kumpa hadhi mbele za watu na siyo kumdhalilisha.
 
Hiyo ni verbal abuse na itakuwa bora huyo baba akimtaliki huyo mkewe.

Ngabu, uko sawa kabisa maana madhara ya domo lake kubwatuka maneno
mazito kama hayo mbele ya kadamnasi huwa ni ngumu sana kufutika
kichwani mwa mwanamme..

Hapo hata kama jamaa alikuwa anaheshimu ndoa ndo basi tena lazima ataanza
kuwa kicheche atafute wa kumpa maneno ya kumliwaza.
 
Mimi naona kuna kitu cha muda mrefu UGOMVI kilikuwa 'endelevu'!sema ilifika muda wamekinzana kwa muda mrefu huyo mama kaamua kusema hadharani sasa,kwa hasira kali

Pia huyo mwanamke naona ni HASIRA TU!kuyatamka aliyoyatamka baada ya uzao mara tatu HAINIINGII AKILINI KABISA!labda aje aweke wazi pia wale watoto sio wa huyu mume

Kwa ninavyowaelewa mimi wanawake.................!huyo mwanaume angetafuta reconcilliation kuitetea na kuilinda ndoa yake kwa nguvu zake zote.Kwa sababu alichokitamka mwanamke SIO VALID,NOR PRACTICAL.
 
Mimi naona kuna kitu cha muda mrefu UGOMVI kilikuwa 'endelevu'!sema ilifika muda wamekinzana kwa muda mrefu huyo mama kaamua kusema hadharani sasa,kwa hasira kali

Pia huyo mwanamke naona ni HASIRA TU!kuyatamka aliyoyatamka baada ya uzao mara tatu HAINIINGII AKILINI KABISA!labda aje aweke wazi pia wale watoto sio wa huyu mume

Kwa ninavyowaelewa mimi wanawake.................!huyo mwanaume angetafuta reconcilliation kuitetea na kuilinda ndoa yake kwa nguvu zake zote.Kwa sababu alichokitamka mwanamke SIO VALID,NOR PRACTICAL.
Aaa! mwanamke hakusema kwamba wale watoto si wa yule mumewe wala hajasema jamaa hajiwezi. Kwake hili siyo tatizo. Yeye kadharau "mwili" wa jamaa, kwamba maumbile yake ni madogo hayamfikishi popote mwanamke, yaani haridhiki katika tendo la ndoa. Amemdharau kwa hilo. Hivyo watoto wanaweza kuwa bado ni wake lakini si mahiri katika chumba cha ndoa. Uko hapo? Ndo mana mi nasema maneno haya ni maneno ambayo wanaume huwahawapendi kuyasikia. yanaweza kumfanya ajimalize maana ameguswa kwenye nafsi yake ya ndani. Mbaya bana!
 
Mtowa maoni ni yakweli hayo au yamekukuta binafsi mwenzio amekwambia hakimtoshi hicho kifrut chako (KIWI)anahitaji bilinganyi?
 
hajatukanwa ameambiwa ukweli
Sawa dada amemwambia ukweli lakini style aliyotumia ni mbaya...yakupayuka! ili ampe faida nani, kama mumeo anamatatizo tafuta muda muafaka mueleze taratibu hata kumpa mawazo ya jinsi ya kulimaliza.
Hapo mwanamke kachemsha...
 
Back
Top Bottom