Erring on the Side of Caution: Kikwete usiwaapishe mawaziri wasioapishwa kuwa wabunge kwanza!

Mw3anakijiji, hawa jamaa wanataka kutukoroga tu kwa kuweka vitu visivyokuwemo ebu soma ibatra ya 55 na 56 uone zinasemaje. Tena basi bora niiweke hii ya 55 hapa..

Ibara ya 55 kifungu cha:-
4) Mawaziri na Manaibu Mawaziri watateuliwa kutoka miongozi mwa wabunge.

5) Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (1) ikitokea kwamba rais anahitajiwa kumteua waziri au Naibu waziri baada ya bunge kuvunjwa. Basi aweza kumteua mtu yeyote ambaye alikuwa mbunge kabla ya bunge kuvunjwa.

Buuuyaaa!....
Ni msisitizo gani zaidi tunauhitaji hapa jamani?

.

Kwa nini ibara ya bunge kuvunjwa inapewa msisitizo wakati huu? Unajua tofauti ya bunge kuvunjwa na bunge kumaliza kikao mkuu? Unajua tofauti ya kusitishwa kwa mikutano ya bunge na bunge kuvunjwa?

Ibara ya bunge kuvunjwa haihusiki kabisa sasa hivi. Hebu kaangalie ibara ya 90 ujue maana na maainisho ya bunge kuvunjwa. Bunge likivunjwa kinachofuata ni uchaguzi.
 
Kwa nini ibara ya bunge kuvunjwa inapewa msisitizo wakati huu? Unajua tofauti ya bunge kuvunjwa na bunge kumaliza kikao mkuu? Unajua tofauti ya kusitishwa kwa mikutano ya bunge na bunge kuvunjwa?

Ibara ya bunge kuvunjwa haihusiki kabisa sasa hivi. Hebu kaangalie ibara ya 90 ujue maana na maainisho ya bunge kuvunjwa. Bunge likivunjwa kinachofuata ni uchaguzi.
Unataka kusema kitu gani hapa... Bunge likivunjwa kabisa huyo waziri au Naibu unawachagua wa nini tena? utawezaje endelea kuchagua mawaziri na manaibu wengine ikiwa bunge limevunja wabunge wote wanapoteza Ubunge maana unataka uchaguzi mpya au sio?..sasa huyo waziri au Naibu mbunge anayeruhusiwa kumchagua ni mbunge yupi ikiwa hata mawaziri wamepoteza ubunge wao..unataka kusema nini mkuu wangu mbona sikuelewi..
 
Kiranga
,
Tanzania inafuata "presidential system". It is a presidential republic with a full presidential system. I agree, tunatumia predential system & parliment inafuata Westminster style (uk) ambao wao wanatumia parlimentary system. Na hapa ndipo tuna mkorogo maana part of the excutive iko linked na bunge (waziri/naibu waziri ni wabunge).

Ukitaka tafsiri ya katiba fungua kesi mahakamani, mahakama ndiyo ina jukumu la kutafsiri sheria. Kamshtaki JK kwa kuvunja katiba tuone. - Mahakama zipi? Hizi zinawaachia huru waiba kura na hotpot?

Ili uwe waziri unahitaji kuwa mbunge. Walioteuliwa uwaziri wameteuliwa ubunge kwanza. Na hili halikuanza leo, hata Mwinyi alishafanya hivi alipomteua Kikwete. Kufanyika kwa miaka mingi haiminishi ni sahihi.

Kwa sababu uwaziri ni cheo, si shughuli, na kamwe haiwezi kuwa "shughuli ya kibunge". Unaongelea mtu au unaoengelea 'branch' inayohold uwaziri? And how do you separate the two?
 
Je kiapo kina umuhimu gani? Je Mbunge mteule anaweza kufanya shughuli za Mbunge bila kuapishwa? Anaweza kuhudhuria viako vya halmshauri kama diwani (anaapishwa diwani au siyo?) Je anaweza kuingia kwenye vikao vya mfuko wa maendeleo wa jimbo hata bila ya kuapishwa? Kama MBunge anaweza kufanya haya yote kabla ya kuapishwa, kuapishwa ni kwanini basi? Well, jibu ni kwa ajili ya kushiriki shughuli za Bunge!

Sasa kama yeye ni mbunge tayari kiapo kinamuongezea nini ambacho hana? Kwamba akiapa ndio atakuwa mwaminifu zaidi kuliko asipoapa? Lakini kama akiapishwa kiapo cha uaminifu kwa jamhuri kwanini arudie tena kiapo hicho hicho anapokuwa mbunge, siyo redundant hiyo? Lakini zaidini kuwa uwaziri una presume ubunge siyo kinyume chake. Huwezi kuwa waziri hadi uwe mbunge ndio maana Rais asingeweza kumtangaza mtu 'waziri' bila mtu huyo kuwa mbunge kwanza. Kama hili ni kweli, basi rais atatakiwa amuapishe huyo mtu kiapo cha uaminifu kwanza (kutimiza masharti ya Katiba) na kisha kiapo cha uwaziri. Hawezi mtu kuwa waziri bila kiapo cha uaminifu ambacho kinachukuliwa na watumishi wote wa umma wanaotakiwa kukichukua kwa mujibu wa katiba.
Kwani kiapo cha uwaziri siyo kiapo cha uaminifu?
 
Kwani kiapo cha uwaziri siyo kiapo cha uaminifu?
Mimi nijuavyo kiapo cha Bunge ni kiapo cha utumishi kwa wananchi waajiri kwanza kisha unakuja kiapo cha uwaziri pia ni uaminifu kwa rais aliyepo madarakani lakini lazima itangulie kiapo kwa wananchi. Ukianza na cha rais inaonyesha udikteta kwamba waziri ni mwaminifu kwa rais kwanza kabla ya wananchi na Taifa.
 
Kiranga
,
Tanzania inafuata "presidential system". It is a presidential republic with a full presidential system. I agree, tunatumia predential system & parliment inafuata Westminster style (uk) ambao wao wanatumia parlimentary system. Na hapa ndipo tuna mkorogo maana part of the excutive iko linked na bunge (waziri/naibu waziri ni wabunge).

Ukitaka tafsiri ya katiba fungua kesi mahakamani, mahakama ndiyo ina jukumu la kutafsiri sheria. Kamshtaki JK kwa kuvunja katiba tuone. - Mahakama zipi? Hizi zinawaachia huru waiba kura na hotpot?

Kata rufaa mpaka mahakama kuu kabisa ya nchi.

Ili uwe waziri unahitaji kuwa mbunge. Walioteuliwa uwaziri wameteuliwa ubunge kwanza. Na hili halikuanza leo, hata Mwinyi alishafanya hivi alipomteua Kikwete. Kufanyika kwa miaka mingi haiminishi ni sahihi.

Sijabase hili kwenye precedent tu, nimekupa criteria kikatiba. Naona hukubishia criteria, maana yake umekubali.

Kwa sababu uwaziri ni cheo, si shughuli, na kamwe haiwezi kuwa "shughuli ya kibunge". Unaongelea mtu au unaoengelea 'branch' inayohold uwaziri? And how do you separate the two?

Siongelei mtu (ningeongelea mtu ningeandika "waziri" si "uwaziri", uwaziri hauwezi kuwa mtu) na wala siongelei branch inayo hold uwaziri, ningesema executive.

Naongelea cheo cha uwaziri. Cheo cha uwaziri si shughuli, kwa hiyo huwezi kusema hii ni "shughuli ya kibunge" ambayo mbunge hawezi kuifanya mpaka aape kwanza.

Hasha!
 
Mimi nijuavyo kiapo cha Bunge ni kiapo cha utumishi kwa wananchi waajiri kwanza kisha unakuja kiapo cha uwaziri pia ni uaminifu kwa rais aliyepo madarakani lakini lazima itangulie kiapo kwa wananchi. Ukianza na cha rais inaonyesha udikteta kwamba waziri ni mwaminifu kwa rais kwanza kabla ya wananchi na Taifa.

Ujuavyo sivyo.
 
Unataka kusema kitu gani hapa... Bunge likivunjwa kabisa huyo waziri au Naibu unawachagua wa nini tena? utawezaje endelea kuchagua mawaziri na manaibu wengine ikiwa bunge limevunja wabunge wote wanapoteza Ubunge maana unataka uchaguzi mpya au sio?..sasa huyo waziri au Naibu mbunge anayeruhusiwa kumchagua ni mbunge yupi ikiwa hata mawaziri wamepoteza ubunge wao..unataka kusema nini mkuu wangu mbona sikuelewi..

1. Ibara ya bunge kuvunjwa haihusiki kabisa hapa kwa sababu sasa hivi bunge halijavunjwa.
2.Inaelekea unacopy paste ibara bila ya kuzisoma. Soma ibara uliyoileta mwenyewe ya 55(5). Rais akivunja bunge leo, haina maana kwamba hawezi kutaka kubadili mawaziri. Anaweza kuteua watu waliokuwa katika bunge lililovunjwa akawafanya mawaziri. Ila kama bunge limevunjwa hawezi kumteua mtu ubunge na kumfanya waziri, kwa sababu bunge limevunjwa, wabunge wapya watasubiri uchaguzi mpya.

Again, sasa hivi bunge halijavunjwa kwa hiyo sielewi hata relevance ya hii ibara ya bunge kuvunjwa ni ipi katika discussion hii.
 
1. Ibara ya bunge kuvunjwa haihusiki kabisa hapa kwa sababu sasa hivi bunge halijavunjwa.
2.Inaelekea unacopy paste ibara bila ya kuzisoma. Soma ibara uliyoileta mwenyewe ya 55(5). Rais akivunja bunge leo, haina maana kwamba hawezi kutaka kubadili mawaziri. Anaweza kuteua watu waliokuwa katika bunge lililovunjwa akawafanya mawaziri. Ila kama bunge limevunjwa hawezi kumteua mtu ubunge na kumfanya waziri, kwa sababu bunge limevunjwa, wabunge wapya watasubiri uchaguzi mpya.

Again, sasa hivi bunge halijavunjwa kwa hiyo sielewi hata relevance ya hii ibara ya bunge kuvunjwa ni ipi katika discussion hii.
Ok ulosema ndivyo ilivyo kulingana na katiba na kweli niliposoma kifungu hicho nilielewa vibaya, wala siku copy na ku paste isipokuwa nilichofahamu mimi ni kwamba rais hawezi kumchagua waziri wala Naibu kama sio mbunge hata kama bunge limevunjwa, Hivyo ndio maana imesisitizwa bunge lililopita na sii kumchagua mtu yeyote toka nje ampe ubunge na kisha kumwapisha kama waziri. Nimechukulia hili kama ni msisitizo wa kutomchagua waziri au naibu toka nje ya wabunge waliokuwepo.

Halafu nimeisoma vizuri katiba sehemu hii ya bunge inaonyesha kwamba rais na makamu wake ni sehemu ya bunge lakini wanakosa vikao kibao bila kuhudhuria na bado wakawa part ya Bunge lakini in reality inaonesha sio lazima wawepo bungeni - yaani hata sielewi kitu. Pamoja na yote hili la kumchagua mtu nje ya bunge laweza kuwa sio mbaya sana kama angeapishwa kama mbunge halafu ndio kuapishwa kwa rais. Kwani taabu ya kufuata utaratibu huo ni ipi haswa?
 
Mimi nijuavyo kiapo cha Bunge ni kiapo cha utumishi kwa wananchi waajiri kwanza kisha unakuja kiapo cha uwaziri pia ni uaminifu kwa rais aliyepo madarakani lakini lazima itangulie kiapo kwa wananchi. Ukianza na cha rais inaonyesha udikteta kwamba waziri ni mwaminifu kwa rais kwanza kabla ya wananchi na Taifa.
Na makatibu wakuu siyo waaminifu kwa wananchi?
 
Ok ulosema ndivyo ilivyo kulingana na katiba na kweli niliposoma kifungu hicho nilielewa vibaya, wala siku copy na ku paste isipokuwa nilichofahamu mimi ni kwamba rais hawezi kumchagua waziri wala Naibu kama sio mbunge hata kama bunge limevunjwa, Hivyo ndio maana imesisitizwa bunge lililopita na sii kumchagua mtu yeyote toka nje ampe ubunge na kisha kumwapisha kama waziri. Nimechukulia hili kama ni msisitizo wa kutomchagua waziri au naibu toka nje ya wabunge waliokuwepo.

Halafu nimeisoma vizuri katiba sehemu hii ya bunge inaonyesha kwamba rais na makamu wake ni sehemu ya bunge lakini wanakosa vikao kibao bila kuhudhuria na bado wakawa part ya Bunge lakini in reality inaonesha sio lazima wawepo bungeni - yaani hata sielewi kitu. Pamoja na yote hili la kumchagua mtu nje ya bunge laweza kuwa sio mbaya sana kama angeapishwa kama mbunge halafu ndio kuapishwa kwa rais. Kwani taabu ya kufuata utaratibu huo ni ipi haswa?

Umuapishe mtu ubunge wakati bunge haliko in session, huyu si mbunge mwenye jimbo fulani kusema ataenda jimboni mwake, uwahi kumuapisha ubunge ili iweje? Akisubiri kuapishwa bunge lijalo kitapungua nini?
 
Back
Top Bottom