kichenchele
JF-Expert Member
- Jun 28, 2010
- 539
- 176
Kupitia TBC1 nikiwa naangalia taarifa ya habari ya saa 2 usiku, niliweza kuona Jk akimnadi kwa wapiga kura waliopauka na kuonekana wamechoka na naweza diriki kusema wanamatumaini kidogo sana juu ya kesho yao, Lowassa na kikwete wakiwa wameng'aa na kunawili. Hoja yangu hapa mimi naomba kuuliza usafi wa lowassa ambao kikwete alikuwa anaupigia mistari kila mara ni upi? nukuu: Huyu ni mgombea safi, mchapakazi,na mtu wa watu mpeni kura, yaliyopita si ndwele-tugange yajayo. ni baadhi ya maneno ya JK, sasa mimi nashangaa, kikwete ndiye aliye mwambia Lowassa apime uzito wa kashifa za Richmond na mwisho wake akaachia ngazi, ripoti ile ilikuwa ikimtaja Lowassa ushiriki wake ktk mikataba ile mibovu kwa kutoa maagizo au kwa kushinikiza kusainiwa kwa mikataba hii,sasa hii ripoti chini ya mwenyekiti wake Dr.Mwakyembe inatakiwa ifanyiwe editing kwa kufuta vipengele vinavyomtaja Lowassa maana mkuu wa nchi ameshamsafisha kuwa yeye ni mtu safi.