kibogo
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 9,739
- 4,732
Chocheeni kuni moto uwake ugali uive mnachotaka kitokee
Halikeni mamruki, wakija wangojee, mikeka wawekee
Wanachotaka kitokee
Chochea X 8
Watanzania mwenda kwao siku zote haogopi giza
Acheni nirudi nyumbani safari imenishinda
Nauri zenu ntarudisha
Mtu anatapika nyongo yake anairamba tena anaangaliwa
Ni sawa na tawi kavu linapoanguka watu wakapiga kelele Hayaaaa
Katika misimu minne kwa mwaka tuongeze msimu mwingine wa tano wa kujistusha
Raha ya janvi siku zote ni viraka viraka na dungu linamficha mlinzi wa ndege wakati wa mvua tu.
Eti ooh imenyesha juzi tu maji sio mengi nisubirini kule!
Ilishindikana vipi kuyapima maji kwa mti ndo muwaambie watu wavuke?
Mjomba! Binadamu ni kama ganda la kitabu mpaka umfungue maandishi ndiyo uweze kumuelewa.
Eti lililotokea mbali tufanye limepita na haliwezi kumdhuru mwingine kweli
Inayotaka kunyesha huwa haisubiri mawingu,
Mi sidhani kama kujiponya katika mambo mazito tunahitaji cheti kilichogongwa muhuri wa moto au mtaalamu wa magonjwa ya akili, zaidi ya kutumia neno sahau tu,
Unawaulizaje watu magongo ya nini wakati unasema kuna nyoka?
Mjomba! We si uliwapaka wanja ngoja wao wakupake piripiri harafu kwenye kombolela iwe zamu yako kuzinga.
Mngekuwa mnajua anachokuala nyuki msingethubutu kusema asali ni tamu,
Niwashukuru kwa kufikiri, kwani mmeonyesha ukomavu wa kutoka chini kwenye shingo na sio juu.
Mbona hamkumfikiria aliyekuwa ndani kafungiwa kwa nje usingizi hapati anawaza jinsi ya kutoka?
Nikisema uwezo wa watu kufikiri na mahitaji vinatofautiana mtaanza kusema ninadharau, nina matusi lakini kumbukeni ulimi unauma kuliko meno,
Mnawezaje kumfikiria aliyekuwepo ndani kajifungia mwenyewe, funguo anazo mwenyewe, kalala fofofofo asijue hata idadi ya misumari iliyoshikiria mlango wake?
Kulipamba jeneza kumfanya aliyekufa kufufuka nini
Kama kusema nimekwisha sema sana mwisho wake ntakuwa kama mwanasiasa
Hawajitokezi mpaka kuwe na maafaNTATOA KATON 20 ZA SABUNI YA UNGA aliyekuambia wale ni wachafu nani, kasafisheni kwanza nyoyo zenu ndiyo mrudi kwa wananchi.
Ndugu zangu tawi kavu kuanguka wala sio ajabu
Wakati wao wanatenganisha mavi ya panya kwenye unga nyinyi chocheeni kuni zilizolowa, maji yapate moto ugali usongwe,
Wakiwauliza waambieni huu ni utani, hapa kwetu tuna makabila 120 tunataniana
Waliopo hatuwataki, wanaotaka tuwape hatuwaamini
Maneno siku zote yanauma na yanachefua ukielewa maana yake.
Kwa mfano neno la kitoto kumwambia mtoto tunasema watoto wanacheza
Neno la kitoto kumwambia mkubwa tunasema mtoto anakua
Mtoto akisema baba ile ndege yangu, baba hata kama hana biskeli umwambia ikitua ntakuletea. Lakini maneno ya kitoto mtu mzima kumwambia mtu mzima kunawalakini
Mimi safari imenishinda na sitaki kuulizwa tena kwa nini.
Chocheeni kuni moto uwake ugali uive mnachotaka kitokee
Halikeni mamruki, wakija wangojee, mikeka wawekee
Wanachotaka kitokee
Chochea X 8
Halikeni mamruki, wakija wangojee, mikeka wawekee
Wanachotaka kitokee
Chochea X 8
Watanzania mwenda kwao siku zote haogopi giza
Acheni nirudi nyumbani safari imenishinda
Nauri zenu ntarudisha
Mtu anatapika nyongo yake anairamba tena anaangaliwa
Ni sawa na tawi kavu linapoanguka watu wakapiga kelele Hayaaaa
Katika misimu minne kwa mwaka tuongeze msimu mwingine wa tano wa kujistusha
Raha ya janvi siku zote ni viraka viraka na dungu linamficha mlinzi wa ndege wakati wa mvua tu.
Eti ooh imenyesha juzi tu maji sio mengi nisubirini kule!
Ilishindikana vipi kuyapima maji kwa mti ndo muwaambie watu wavuke?
Mjomba! Binadamu ni kama ganda la kitabu mpaka umfungue maandishi ndiyo uweze kumuelewa.
Eti lililotokea mbali tufanye limepita na haliwezi kumdhuru mwingine kweli
Inayotaka kunyesha huwa haisubiri mawingu,
Mi sidhani kama kujiponya katika mambo mazito tunahitaji cheti kilichogongwa muhuri wa moto au mtaalamu wa magonjwa ya akili, zaidi ya kutumia neno sahau tu,
Unawaulizaje watu magongo ya nini wakati unasema kuna nyoka?
Mjomba! We si uliwapaka wanja ngoja wao wakupake piripiri harafu kwenye kombolela iwe zamu yako kuzinga.
Mngekuwa mnajua anachokuala nyuki msingethubutu kusema asali ni tamu,
Niwashukuru kwa kufikiri, kwani mmeonyesha ukomavu wa kutoka chini kwenye shingo na sio juu.
Mbona hamkumfikiria aliyekuwa ndani kafungiwa kwa nje usingizi hapati anawaza jinsi ya kutoka?
Nikisema uwezo wa watu kufikiri na mahitaji vinatofautiana mtaanza kusema ninadharau, nina matusi lakini kumbukeni ulimi unauma kuliko meno,
Mnawezaje kumfikiria aliyekuwepo ndani kajifungia mwenyewe, funguo anazo mwenyewe, kalala fofofofo asijue hata idadi ya misumari iliyoshikiria mlango wake?
Kulipamba jeneza kumfanya aliyekufa kufufuka nini
Kama kusema nimekwisha sema sana mwisho wake ntakuwa kama mwanasiasa
Hawajitokezi mpaka kuwe na maafaNTATOA KATON 20 ZA SABUNI YA UNGA aliyekuambia wale ni wachafu nani, kasafisheni kwanza nyoyo zenu ndiyo mrudi kwa wananchi.
Ndugu zangu tawi kavu kuanguka wala sio ajabu
Wakati wao wanatenganisha mavi ya panya kwenye unga nyinyi chocheeni kuni zilizolowa, maji yapate moto ugali usongwe,
Wakiwauliza waambieni huu ni utani, hapa kwetu tuna makabila 120 tunataniana
Waliopo hatuwataki, wanaotaka tuwape hatuwaamini
Maneno siku zote yanauma na yanachefua ukielewa maana yake.
Kwa mfano neno la kitoto kumwambia mtoto tunasema watoto wanacheza
Neno la kitoto kumwambia mkubwa tunasema mtoto anakua
Mtoto akisema baba ile ndege yangu, baba hata kama hana biskeli umwambia ikitua ntakuletea. Lakini maneno ya kitoto mtu mzima kumwambia mtu mzima kunawalakini
Mimi safari imenishinda na sitaki kuulizwa tena kwa nini.
Chocheeni kuni moto uwake ugali uive mnachotaka kitokee
Halikeni mamruki, wakija wangojee, mikeka wawekee
Wanachotaka kitokee
Chochea X 8