Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,407
- 31,392
- Thread starter
- #161
HILI LA CCM DODOMA LIMETIA DOA
KUENDELEA KULITETEA NI KUHARIBU ZAIDI
Bandiko 121 tulizungumzia kauli ya 'walk the talk' kwa maana ya kuishi katika kauli.
Katika siku za karibuni kumekuwa na mvutano 'tension' kuhusu 'marufuku ya mikutano ya siasa
Mvutano huo umeletwa na uwepo wa mkutano wa CCM Dodoma tofauti na marufuku yaliyopo.
Wengi wamejiuliza, tangazo la kupiga mikutano marufuku lilihusu akina nani au kundi gani la jamii?
Tatizo kubwa ni pale utetezi wa uwepo wa mkutano huo unapopinga kila uchao.
Msajili wa vyama vya siasa alisema ' Wapinzani hawakumwelewa Rais, na wala hakupiga marufuku bali kuwakaribisha katika siasa za kuendeleza nchi na kuacha siasa za ukandamizaji'
Msajili hakueleza nani anafanya siasa za ukandamizaji au siasa za ukandamizaji ni kitu gani.
Tukasikia jeshi la Polisi likisema, taarifa yake ya June ilipotoshwa. Marufuku ya mikutano na maandamano hayahusu shughuli za kiutendaji za vyama vya siasa.
Na kwamba marufku hayo yalitokana na hali ya usalama kutokuwa nzuri.
Kauli ya hali ya usalama haikuwahi kusemwa na wasemaji wa awali kama Rais au msajili wa vyama
Rais alisema, alihitaji nafasi ya kutekeleza ahadi zake za uchaguzi na kwamba siasa zifanywe katika maeneo ya uwakilishi kna madiwani au wabunge.
Tumesikia viongozi wengine nao wakidai marufuku ya mikutano maeneo yao.
Sababu zinazotolewa ni kutoa nafasi ya shughuli za maendeleo.
Huko nyuma waziri mkuu alishawahi kutoa maagizo kama hayo kwa kuruhusu 'walioshinda' na siyo walioshindwa. Ilisemwa pia uchaguzi umekwisha sasa ni muda wa watu kufanya kazi.
Mtiririko mzima unazua maswali mengi kuliko majibu
1. Je, kuzuia mikutano ilikuwa kuwaalika wapinzani kama alivyosema msajili wa vyama?
2. Je, kuzuia mikutano ni kutokana na hali ya usalama isiyoridhisha kama alivyosema Polisi?
4. Je, zuio ni la mikutano ya nje pekee au linahusu ya ndani?
5. Je, kuzuia mikutano ni kutoa nafasi za watu kufanya kazi ?
6. Je, kuzuia mikutano ni katika kuisaidia serikali kukamilisha ahadi zake za ilani ya uchaguzi?
Inaendelea...
KUENDELEA KULITETEA NI KUHARIBU ZAIDI
Bandiko 121 tulizungumzia kauli ya 'walk the talk' kwa maana ya kuishi katika kauli.
Katika siku za karibuni kumekuwa na mvutano 'tension' kuhusu 'marufuku ya mikutano ya siasa
Mvutano huo umeletwa na uwepo wa mkutano wa CCM Dodoma tofauti na marufuku yaliyopo.
Wengi wamejiuliza, tangazo la kupiga mikutano marufuku lilihusu akina nani au kundi gani la jamii?
Tatizo kubwa ni pale utetezi wa uwepo wa mkutano huo unapopinga kila uchao.
Msajili wa vyama vya siasa alisema ' Wapinzani hawakumwelewa Rais, na wala hakupiga marufuku bali kuwakaribisha katika siasa za kuendeleza nchi na kuacha siasa za ukandamizaji'
Msajili hakueleza nani anafanya siasa za ukandamizaji au siasa za ukandamizaji ni kitu gani.
Tukasikia jeshi la Polisi likisema, taarifa yake ya June ilipotoshwa. Marufuku ya mikutano na maandamano hayahusu shughuli za kiutendaji za vyama vya siasa.
Na kwamba marufku hayo yalitokana na hali ya usalama kutokuwa nzuri.
Kauli ya hali ya usalama haikuwahi kusemwa na wasemaji wa awali kama Rais au msajili wa vyama
Rais alisema, alihitaji nafasi ya kutekeleza ahadi zake za uchaguzi na kwamba siasa zifanywe katika maeneo ya uwakilishi kna madiwani au wabunge.
Tumesikia viongozi wengine nao wakidai marufuku ya mikutano maeneo yao.
Sababu zinazotolewa ni kutoa nafasi ya shughuli za maendeleo.
Huko nyuma waziri mkuu alishawahi kutoa maagizo kama hayo kwa kuruhusu 'walioshinda' na siyo walioshindwa. Ilisemwa pia uchaguzi umekwisha sasa ni muda wa watu kufanya kazi.
Mtiririko mzima unazua maswali mengi kuliko majibu
1. Je, kuzuia mikutano ilikuwa kuwaalika wapinzani kama alivyosema msajili wa vyama?
2. Je, kuzuia mikutano ni kutokana na hali ya usalama isiyoridhisha kama alivyosema Polisi?
4. Je, zuio ni la mikutano ya nje pekee au linahusu ya ndani?
5. Je, kuzuia mikutano ni kutoa nafasi za watu kufanya kazi ?
6. Je, kuzuia mikutano ni katika kuisaidia serikali kukamilisha ahadi zake za ilani ya uchaguzi?
Inaendelea...