Dr Slaa na njama ya kukwepa kodi

Status
Not open for further replies.

Ritz

JF-Expert Member
Jan 1, 2011
47,108
32,570
Wanaukumbi.

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema, Dr. Slaa anapenda sana kujinasibisha kwamba yeye ni mzalendo wa kupindukia, anayechukia vitendo vya ufisadi na anayeionea huruma nchi yetu.

Taarifa za uhakika kabisa zinathibitisha kwamba mwishoni wa mwezi Juni, mwaka 2013 Dr.Slaa na Mchumba wake walitembelewa na kundi la Wapani wapatao 20 nyumbani kwao Mbweni, Kinondoni ambapo wote kwa pamoja walikula cha jioni.

Dhumuni la ugeni huo wa Wajapani, ilikuwa ni kuthibitisha kama kweli Chadema kina mpango wa kujenga hospitali kubwa ya kisasa katika eneo la Mlalakuwa Dar es Salaam, Wajapani hao ndiyo walipangwa au kuteuliwa kujenga hospitali hiyo, wameakikishiwa pamoja na mambo mengine ya kimaslahi yao makampuni yao mengine, kwamba msimamizi wa hospitali hiyo ndiyo atakayekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015, kwa maana ya Dr. Slaa.

Mipango yote ya kujenga hospitali hiyo, inaratibiwa na Askofu mmoja anayemiliki Kanisa lake maeneo ya Kawe, Dar es Salaam, Askofu huyo amekuwa akifanya safari za Japani akiwa ameandamana na mchumba wa Dr. Slaa, Josephine, mpango unafanyanyika vifaa vyote vitakavyoingizwa kutoka Japani vipitie mikononi mwa Kanisa ili tu visitozwe kodi na serikali.

Ni Dr.Slaa huyu huyu, ambaye miaka michache iliyopita alitangaza orodha ya aibu ya mafisadi pale Mwembe yanga, leo hii anawakimbia Mamlaka ya Mapato nchini TRA.
59659_451739378204932_322908579_n.jpg


Majibu kutoka kwa Dr. Slaa
Ritz,
Utabwabwaja na propaganda mpaka utachoka. Basi angalau ungelikuwa hata na Taarifa
Sahihi.
  1. Kwanza hoja ya kukutana na Wajapani nyumbani, pamoja na kuwa Dr Slaa hazuiwi na sheria au utaratibu wowote kukutana na yeyote anayetaka nyumbani kwake au mahali popote, siyo ya kweli. Hakuna siku hata mmoja, siyo mwezi Juni tu, wajapani 20 walipofika na kula nyumbani kwangu. Kama ni hivyo, mbona unawake picha za Mama Slaa alipokuwa Japan basi. Isitoshe picha za safari ya Mama Slaa hazikuwa siri zilikuwa kwenye FB yake. Mtihani wa kwanza umefeli vibaya sana. Fanya mwingine tuone.
  2. Ah! Kumbe ujenzi wa Hospitali! Pamoja na kuwa sina mpango huo, labda Kama utakuwepo baadaye tatizo ni nini. Dr. Slaa nimeasisi taasisi ya CCBRT mwaka 1994 na kujenga, pamoja na programs zingine, Hospitali kubwa kuliko zote hasa kwa performance( look at statistics) Afrika South of Sahara inayoshughulikia disagbilities under one roof, ten a katika Ardhi tuliyopewa na Serikali ya JMT. Sasa hivi, tunajenga Hospitali kubwa ya Mama na Mtoto itakayokuwa tayari 2014/15, nayo pia katika nyongeza ya ardhi tuliyopewa na Serikali. hospitali zote ziko exempted. Ukwepaji kodi uko wapi. Kama CCBRT imepata cheti cha TRA, Kama stori yako ungekuwa kweli, si ni utaratibu huo huo ungelifuatwa! Tatizo liko wapi hapo? ritz una akili ya ajabu, ningetaka kufanya biashara ningeshindwa kufanya hivyo kupitia CCBRT. Nadhani mnatafuta pa kushikiza, piga ramble zaidi labda itakusaidia!
 
Asipolipa ushuru sasa ruzuku ya CHADEMA itatoka wapi?
Watu walafi (selfish) huwa hawafikirii kama unavyofikiria wewe. Huoni hata mshahara wa Katibu Mkuu wa CHADEMA alijipangia kwa maslahi yake and his fragmented family.

Kwani unadhani kwa umri wake huu yuko katika siasa kama Samalitan? Thubutu.

Pesa kwanza, wananchi baadaye.
 
Watu walafi (selfish) huwa hawafikirii kama unavyofikiria wewe. Huoni hata mshahara wa Katibu Mkuu wa CHADEMA alijipangia kwa maslahi yake and his fragmented family.

Kwani unadhani kwa umri wake huu yuko katika siasa kama Samalitan? Thubutu.

Pesa kwanza, wananchi baadaye.

Halituhusu....
 
Mara nyingi Dr.Slaa amekuwa anikuu maneno ya Mwalimu Nyerere, juu ya nani ni mzalendo na zaidi kwamba kiongozi wa Watanzania anapaswa kuwa awe mtu muadilifu.
 
Kakojoe ulale! Mbona kwenye thread za mabwana zako za madawa ya kulevya unapiga kimya?

Mtakuja kuelewa tu baada ya kuibiwa saaana na hao akina Silaha na Dj Mbowe! Hawana uzalendo wala nini! Ni wajasiria mali tu! Zindukeni nyie misukule!
 
Dr.slaa ameshasaidia sana watanzania kupitia taasisi yake CCBRT,hivyo ana uzoefu wa kutoa huduma kwa wananchi!JK ana nini?msamaha wa kodi umeruhusiwa na govt ya ccm,hivyo laumu wabunge wa ccm kupitisha wakati mkulo alipojaribu kuifuta
Kamanda hebu acha kupotosha CCBRT siyo taasisi ya Dr.Slaa.

Kwenye vikao vyenu vyama Chadema ndivyo anavyowadanganya.

Muulize tena vizuri.
 
Kamanda hebu acha kupotosha CCBRT siyo taasisi ya Dr.Slaa.

Kwenye vikao vyenu vyama Chadema ndivyo anavyowadanganya.

Muulize tena vizuri.

Nyie mnalikosesha taifa ushuru kwenye biashara ya meno ya tembo na cocaine tunawaangalia tu.
 
Kweli mnahangaika, unaleta story za kuuungaunga wala hueleweki,! Dr Slaa alitaja wezi, sio alidhani wataiba
 
TUWACHE UNAFIKI NA UZINDAKI hili analofanya dk slaa ni jema kwa manufaa ya watanzania wote mambo kama haya ya kimaendeleo ni vyema yakaungwa mkono na serikali kwa nguvu zote
Nadhani hakuna anayepinga ili jambo la kujenga hospitali watu wanachapinga ukwepaji kodi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom