Sizinga
Platinum Member
- Oct 30, 2007
- 9,101
- 6,027
Yani pamoja na matatizo yote tuliyonayo chini ya uongozi wa magamba bila kusahau potential wanayoionyesha CDM bado watu wanahitaji kuhamasishwa???Kweli waTanzania wameridhika......
Lizzy kipenzi...kuhamasishwa ni muhimu tofauti na unavyofikiria...wazee wengi hata kama hali ni ngumu huwa hawapendi mabadiliko, wengi wanachojali siku imeanza ,siku imeisha..na wengi wanafikiria nchi ikiongozwa na chama kingine tofauti na CCm basi patatokea vita kubwa na nyie mnaoishi daslama mtapanda ndege na kukimbilia huko mbali...mkiwaacha wazee wanakufa huku. Hii ndio theory iliyokuwepo kwa wakazi/wazee/vibibi wengi wa pande za kusini mtwara na lindi. Bila kuhamasishwa dizain hii ya watu, ule kalaghabao!!