Dr Slaa na Chadema sasa basi, inatosha!

Yani pamoja na matatizo yote tuliyonayo chini ya uongozi wa magamba bila kusahau potential wanayoionyesha CDM bado watu wanahitaji kuhamasishwa???Kweli waTanzania wameridhika......

Lizzy kipenzi...kuhamasishwa ni muhimu tofauti na unavyofikiria...wazee wengi hata kama hali ni ngumu huwa hawapendi mabadiliko, wengi wanachojali siku imeanza ,siku imeisha..na wengi wanafikiria nchi ikiongozwa na chama kingine tofauti na CCm basi patatokea vita kubwa na nyie mnaoishi daslama mtapanda ndege na kukimbilia huko mbali...mkiwaacha wazee wanakufa huku. Hii ndio theory iliyokuwepo kwa wakazi/wazee/vibibi wengi wa pande za kusini mtwara na lindi. Bila kuhamasishwa dizain hii ya watu, ule kalaghabao!!
 
^ wewe sema hao wazee hawana imani na hiki chama usilete hadithi ya vita. Ni vijana wenye mawazo ya kimaskini ndio washabiki.
 
Slaa amefanya nini zaidi ya kuimba wimbo wa UFISADI? Imebaki atoe wimbo wa Taarab aupe jina FISADI. Alete mambo mapya sio kukalia tatizo moja kila siku. Kila kipanda kwenye jukwaa anatoa list ya watu. Tunataka kusikia chama chake kina fanya nini bungeni? Uchaguzi umepita sasa wabunge wake wafanye kazi yao bungeni, na hii tabia ya kidemu ya kususa waache.

Haya maneno akiyaona Msekwa na Nape watfurahi sana mpaka gego zitaonekana
 
lakini hali haitakuwa nzuri kwa CDM kupiga kimya ila kwa serikali kuwajibika. JK bado anao muda na uwezo mkubwa wa kuwanyamazisha CDM na Dr. Slaa kwa kuyashughulikia yale ambayo yanawafanya cdm wazunguke na kuyadai, baadhi ya hayo mambo ni kama:-
Kuboresha hali za wafanyakazi kwa kupunguza kodi na kupandisha kima cha chini cha mishahara, kupunguza ugumu wa maisha kwa kupunguza kodi nyingi ktk bidhaa muhimu kama mafuta.
Kupunguza matumizi ya anasa ya serikali ikiwa pamoja na mishahara mikbwa na marupurupu ya viongozi kama wabunge kuwepo na uwiano kati ya mishahara na kiwango cha elimu na unyeti wa kazi yenyewe.
Kuheshimu na kufata utawala wa sheria watu wahukumiwe ktk muda muafaka maamuzi ya siasa yasibind maamuzi ya mahakama.
Kusimamia maadili ya viongozi kwa ukaribu na athubutu kuwaadhibu na kuwafikisha mahakamani wtuhumiwa wakuu wa ufisadi ikibidi kuwafunga hata kama ni marafiki zake.
Kupitia upya mikataba yoote ya rasilimali za taifa na iandikwe kwa manufaa ya wananchi, pamoja na transparency ktk uendeshaji wa nchi, kupunguza ukubwa wa serikali.
Hayo ni baadhi tu ila kuna mambo mengi mengi ambayo CDM na watz wengi yanawaboa akiweza kubadilisha mbona cdm watacease coz watakuwa hawana la kuishtaki ccm kwa wananchi otherwise this movement is unstopable yaani hata Cdm na Dr wakinyamaza kwa hali ya sasa hata mawe yatapiga kelele

Ndugu umeainisha vizuri sana,
Ila ukifikiri zaidi utagundua msingi wa yote hayo ni MFUMO WA UTAWALA!
Kitu ambacho kilifumwa na serikali za ccm toka mwanzo!
Si JK wala yeyote wa ccm kwa kutumia mfumo tulionao (walioufuma) atafanya chochote zaidi ya danganya toto!
Ila nakubaliana na wewe kwamba, kwasasa ni lazima harakati ziendelee kuelekea mfumo mpya wa maisha.
 
Hali ya nchi imekua tete sana siku hizi. Dr Slaa na Chadema wameifumuafumua CCM na serikali yake, wamebaki wanahaha kutwa kuchwa kumtafuta mchawi ni nani wakati wamejoroga wenyewe! CCM nako wanajikanyaga kanyaga tu kujivua gamba hakuwezekani kwani gamba linang'oka na ngozi! Ukiachilia unyoka wa CCM kubaki palepale, sijaona gamba hata moja lililovuliwa, wembe wa CCM ni ule ule UFISADI!

Baada ya DR Slaa kuanza kufumua fumu fumu hadharani ufisadi wa CCM tangu alipokua bungeni na Chadema kuendeleza makali hayo kwa kasi na ari zaidi sasa uchafu wote wa serikali hadharani. Kila mwananchi anajua kila uchafu unaoendelea serikalini.

Kwa miaka kadhaa wananchi tulikua tunafichwa UFISADI wa serikali ya CCM, vigogo walijimegea nchi kwa ari ya ajabu kabisa!

Sasa wananchi tunaona na kuelewa Serikali yetu kwa namna inavyonuka hadi nasikia aibu! Rais baada ya kutajwa fisadi na ufisadi wake wa wazi nae anajikanyaga tu hana meno, hana guts za kumwadhibu yoyote kwa uchafu wake binafsi pia,magamba hayavuki basi tu! Kwa kujikomba komba kwa raia na watu anaishia kuwa msanii sanii na kutoa ahadi za kuclick, za uongo uongo hadi namuonea huruma huyu baba aliyewatoa wakwere kimasomaso, nchi inamshinda kwa kasi na ari ya Chadema ambayo imewashika na watanzania sasa inaivuruga vuruga serikali ya CCM hadi nahisi nchi inakwenda mrama sasa!

Nawaomba Dr Slaa na Chadema kuwa jamani eeh waungwana inatosha tosha sasa, have mercy on our president, kasi yenu inafanya taifa halitawaliki kweli, chama cha magamba kushnei!
Chadema naomba punguzeni spidi!

Hayo ni mawazo yako tu! Sioni spidi yoyote ya CDM zaid ya kupoteza muda wao na fedha za ruzuku
 
lakini hali haitakuwa nzuri kwa CDM kupiga kimya ila kwa serikali kuwajibika. JK bado anao muda na uwezo mkubwa wa kuwanyamazisha CDM na Dr. Slaa kwa kuyashughulikia yale ambayo yanawafanya cdm wazunguke na kuyadai, baadhi ya hayo mambo ni kama:-
Kuboresha hali za wafanyakazi kwa kupunguza kodi na kupandisha kima cha chini cha mishahara, kupunguza ugumu wa maisha kwa kupunguza kodi nyingi ktk bidhaa muhimu kama mafuta.
Kupunguza matumizi ya anasa ya serikali ikiwa pamoja na mishahara mikbwa na marupurupu ya viongozi kama wabunge kuwepo na uwiano kati ya mishahara na kiwango cha elimu na unyeti wa kazi yenyewe.
Kuheshimu na kufata utawala wa sheria watu wahukumiwe ktk muda muafaka maamuzi ya siasa yasibind maamuzi ya mahakama.
Kusimamia maadili ya viongozi kwa ukaribu na athubutu kuwaadhibu na kuwafikisha mahakamani wtuhumiwa wakuu wa ufisadi ikibidi kuwafunga hata kama ni marafiki zake.
Kupitia upya mikataba yoote ya rasilimali za taifa na iandikwe kwa manufaa ya wananchi, pamoja na transparency ktk uendeshaji wa nchi, kupunguza ukubwa wa serikali.
Hayo ni baadhi tu ila kuna mambo mengi mengi ambayo CDM na watz wengi yanawaboa akiweza kubadilisha mbona cdm watacease coz watakuwa hawana la kuishtaki ccm kwa wananchi otherwise this movement is unstopable yaani hata Cdm na Dr wakinyamaza kwa hali ya sasa hata mawe yatapiga kelele

Mngejua hali ilivyo mbaya kwa CCM mbele ya wananchi ni balaa nini uhakika asilimia milion 10 kwamba CCM ndo mwisho na ndo mwanzo wa kuwashitaki hawa mafedhuli na mwisho wao ni uhamishoni au behind the bars ninaomba iyo siku ifike maana kila lona CCM haitakiwi
 
Yani pamoja na matatizo yote tuliyonayo chini ya uongozi wa magamba bila kusahau potential wanayoionyesha CDM bado watu wanahitaji kuhamasishwa???Kweli waTanzania wameridhika......

Lizzy, waTz washahamasika, sasa Chadema watumie vizuri hii opportunity kutap wanachama na wapiga kura!
Si unajua mapenzi yanaponoga watu ndo hutangaza ndoa!
 
Lizzy kipenzi...kuhamasishwa ni muhimu tofauti na unavyofikiria...wazee wengi hata kama hali ni ngumu huwa hawapendi mabadiliko, wengi wanachojali siku imeanza ,siku imeisha..na wengi wanafikiria nchi ikiongozwa na chama kingine tofauti na CCm basi patatokea vita kubwa na nyie mnaoishi daslama mtapanda ndege na kukimbilia huko mbali...mkiwaacha wazee wanakufa huku. Hii ndio theory iliyokuwepo kwa wakazi/wazee/vibibi wengi wa pande za kusini mtwara na lindi. Bila kuhamasishwa dizain hii ya watu, ule kalaghabao!!

Mkuu umenena vyema, natumani Lizzy kaelewa somo! Nashukuru binafsi amehamasika!
 
Slaa amefanya nini zaidi ya kuimba wimbo wa UFISADI? Imebaki atoe wimbo wa Taarab aupe jina FISADI. Alete mambo mapya sio kukalia tatizo moja kila siku. Kila kipanda kwenye jukwaa anatoa list ya watu. Tunataka kusikia chama chake kina fanya nini bungeni? Uchaguzi umepita sasa wabunge wake wafanye kazi yao bungeni, na hii tabia ya kidemu ya kususa waache.

kati ya mazumbukuku ndo wewe yani slaa akaimbe taarab na huyo mwenyekiti wa magamba taimba nini? Amefanya ikulu kama gheto anaingiza wasanii ikulu sijawahi ona hata UGANDA na ujinga wao hawako ivo
 
Mngejua hali ilivyo mbaya kwa CCM mbele ya wananchi ni balaa nini uhakika asilimia milion 10 kwamba CCM ndo mwisho na ndo mwanzo wa kuwashitaki hawa mafedhuli na mwisho wao ni uhamishoni au behind the bars ninaomba iyo siku ifike maana kila lona CCM haitakiwi

Nafurahi kina mama wamehamasika pia, Juzi juzi mama yangu mkubwa na rafiki yake walikua wanasema Yaani hawampendi Kikwete, kiasi kwamba akimuona anaongea kwenye TV anaizima!
 
Mimi nilikuwa mwanachama wa CCM lakini sasa nimebaki njiapanda, kwa uchungu wa nchi yangu inavyoangamia kwa uvivu na ufisadi lakini hasa hao waliokalia madaraka kutokuwa na nia ya kweli ya kuwakomboa kwa haraka Watanzania basi mimi nakubali Moto wa Dr. Slaa uendelee mpaka kieleweke, iwe kwa vyovyote ile, kwani mpaka sasa na utulivu wetu pamoja na shida je tuna faida gani? kama ni unyanyasaji wa polisi ni vitu vya kawaida, mabomu uzembe yalipuka kila siku? style ya kitunisia ya Maandamano mi naikubali, na nakiri mimi ni CCM, japo kwa sasa sijui, simlaumu JK peke yake, kwa uozo uko popote Tanzania, mimi ningeshauri kuokoa nchi Dr Slaa apewe ukuu wa serikali, yaani Waziri Mkuu, badala ya mkulima wa kulia lia akiona tatizo badala ya kutoa amri
 
Mimi nilikuwa mwanachama wa CCM lakini sasa nimebaki njiapanda, kwa uchungu wa nchi yangu inavyoangamia kwa uvivu na ufisadi lakini hasa hao waliokalia madaraka kutokuwa na nia ya kweli ya kuwakomboa kwa haraka Watanzania basi mimi nakubali Moto wa Dr. Slaa uendelee mpaka kieleweke, iwe kwa vyovyote ile, kwani mpaka sasa na utulivu wetu pamoja na shida je tuna faida gani? kama ni unyanyasaji wa polisi ni vitu vya kawaida, mabomu uzembe yalipuka kila siku? style ya kitunisia ya Maandamano mi naikubali, na nakiri mimi ni CCM, japo kwa sasa sijui, simlaumu JK peke yake, kwa uozo uko popote Tanzania, mimi ningeshauri kuokoa nchi Dr Slaa apewe ukuu wa serikali, yaani Waziri Mkuu, badala ya mkulima wa kulia lia akiona tatizo badala ya kutoa amri

Nakupongea kwa kuusemea moyo wako vyema. Miaka kadhaa iliyopita watu tulikua tukiipenda CCM unconditionally kumbee kumbeee tulikua hatuijui!

Slaa akichua uwaziri mkuu hapata noga! Aingie mjengoni kabisa pale magogono street!
 
Kinachofanya CDM na Dr. wasiache kupambana na ufisadi ni kutokana na watawala kuzoea kuishi kwa kutegemea hela za ufisadi kwa hiyo inakuwa vigumu kwao kuacha kukwapua rasilimali za taifa. Ninachopenda kuwaambia watanzania ni kwamba dawa ya ufisadi ni kubabadili mfumo wa utawala kwani utawala wa ccm hauwezi kusogeza taifa hili mbele hata ipate viongozi wa namna yoyote ile. Simnamuona JK tulimwamini mwaka 2005, pamoja na kuonesha utashi wa kubadili maisha ya watanzania amefanya nini? Mambo ya gamba ni uzushi mtupu na njia ya kuwaadaa watz. Ufisadi upo hadi kwa wafanyakazi nani atawakemea wakati na viongozi ni watuhumiwa WA UFISADI.
 
Sina kadi ya chama chochote lakini CDM wananikuna kichwa ile mbaya ,ila ilijukumu ni kubwa tusiwaachie baadhi ya watu kuliendesha tuungane wote ili tuweze kulifikisha hapo tunapotaka ,"if you don't want change,change will change you"
 
Tunajua wazi kuwa ukisema ukweli juu ya ubovu wa Slaa basi unaitwa mnafiki. Endeleeni kumtukuza na siku akiwaharia ndio mtajua kwamba yeye ni mwanasiasa na wala sio malaika kama mnavyo amini..

Naomba unatajie uzuri wa JK!
Sio uzuri wa sura na tabasamu
 
moto wa ukombozi huwa haupunguzwi. ukishaleta ukombozi moto huo hutumika kuleta maendeleo na taifa bora zaidi. hakuna kupunguza spidi bali inapaswa kuongezwa. wanaoshindwa kutawala wajitoe waje wawezao kutawala. nao wakishindwa wanatolewa. hawekwi mtu madarakani kwa personal liking yake bali kwa uwezo na upo wake wa kuongoza watu. kama hawezi hapewi nafasi ya uongozi. hiyo ndo kanuni ijayo
 
Mwacheni JK na watu wake wapate dozi, kwani nchi imewashinda.

Mfano; JK anasema kwenye sherehe za meimosi kuwa hawezi kukubali mtanzania kuwa mtumwa kwa mwajiri wake ndani ya nchi yake (yaani TZ), hivi kweli anajua anachokisema huyu mkuu wetu? Kuna viwanda vingapi vya wageni/wanyonyaji (wao wanawaita wawekezaji) mfanyakazi kibarua miaka nenda rudi, hakuna mkataba, hana medical insurance, mafao ya uzeeni na mwajiri anakufukuza siku yeyote akijisikia. Kuna kiwanda kimoja maeneo ya Vingunguti kibarua wa miaka rukuki alikufa kwa ajali akiwa kazini ikabidi mwajiri wake amwajiri siku ile baada ya kufa ili kukwepa taabu ya kisheria iliyokuwa mbele yake!

Mwacheni Dr. Slaa na Chadema wafanye kazi yao. CCM nchi imewashinda na hawana jipya leo, kesho wala keshokutwa.
 
Back
Top Bottom