Dr Slaa na Chadema sasa basi, inatosha!

Revolutionary

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
456
86
Hali ya nchi imekua tete sana siku hizi. Dr Slaa na Chadema wameifumuafumua CCM na serikali yake, wamebaki wanahaha kutwa kuchwa kumtafuta mchawi ni nani wakati wamejoroga wenyewe! CCM nako wanajikanyaga kanyaga tu kujivua gamba hakuwezekani kwani gamba linang'oka na ngozi! Ukiachilia unyoka wa CCM kubaki palepale, sijaona gamba hata moja lililovuliwa, wembe wa CCM ni ule ule UFISADI!

Baada ya DR Slaa kuanza kufumua fumu fumu hadharani ufisadi wa CCM tangu alipokua bungeni na Chadema kuendeleza makali hayo kwa kasi na ari zaidi sasa uchafu wote wa serikali hadharani. Kila mwananchi anajua kila uchafu unaoendelea serikalini.

Kwa miaka kadhaa wananchi tulikua tunafichwa UFISADI wa serikali ya CCM, vigogo walijimegea nchi kwa ari ya ajabu kabisa!

Sasa wananchi tunaona na kuelewa Serikali yetu kwa namna inavyonuka hadi nasikia aibu! Rais baada ya kutajwa fisadi na ufisadi wake wa wazi nae anajikanyaga tu hana meno, hana guts za kumwadhibu yoyote kwa uchafu wake binafsi pia,magamba hayavuki basi tu! Kwa kujikomba komba kwa raia na watu anaishia kuwa msanii sanii na kutoa ahadi za kuclick, za uongo uongo hadi namuonea huruma huyu baba aliyewatoa wakwere kimasomaso, nchi inamshinda kwa kasi na ari ya Chadema ambayo imewashika na watanzania sasa inaivuruga vuruga serikali ya CCM hadi nahisi nchi inakwenda mrama sasa!

Nawaomba Dr Slaa na Chadema kuwa jamani eeh waungwana inatosha tosha sasa, have mercy on our president, kasi yenu inafanya taifa halitawaliki kweli, chama cha magamba kushnei!
Chadema naomba punguzeni spidi!
 
aagh mkuu...umeanza vizuri lakini swala la kusema wapunguze kasi,nalipinga,kwa CCm 1 mistake 7 goals, huu moto ndo ushaanza hivyo na unaendelea,hadi kukipambazuka ...2015 hiyooo!! Bado pande za kusini Mtwara na Lindi hawajaenda!!watu wana hamu kweli ya mabadiliko kule ,sema basi tu hakuna muhamasishaji...!!
 
Ni kweli dr Slaa kafichua ufisadi lakini nadhani siyo peke yake. Tofauti tu ni kwamba yeye alizua moto bungeni na kwenye mikutano ya hadhara. Ukisoma magazeti, ukinukuu thread nyingi hapa JF hasa za MM utakubali kwamba siyo dr Slaa peke yake. Wote wapewe sifa
 
Hali ya nchi imekua tete sana siku hizi. Dr Slaa na Chadema wameifumuafumua CCM na serikali yake, wamebaki wanahaha kutwa kuchwa kumtafuta mchawi ni nani wakati wamejoroga wenyewe! CCM nako wanajikanyaga kanyaga tu kujivua gamba hakuwezekani kwani gamba linang'oka na ngozi! Ukiachilia unyoka wa CCM kubaki palepale, sijaona gamba hata moja lililovuliwa, wembe wa CCM ni ule ule UFISADI!

Baada ya DR Slaa kuanza kufumua fumu fumu hadharani ufisadi wa CCM tangu alipokua bungeni na Chadema kuendeleza makali hayo kwa kasi na ari zaidi sasa uchafu wote wa serikali hadharani. Kila mwananchi anajua kila uchafu unaoendelea serikalini.

Kwa miaka kadhaa wananchi tulikua tunafichwa UFISADI wa serikali ya CCM, vigogo walijimegea nchi kwa ari ya ajabu kabisa!

Sasa wananchi tunaona na kuelewa Serikali yetu kwa namna inavyonuka hadi nasikia aibu! Rais baada ya kutajwa fisadi na ufisadi wake wa wazi nae anajikanyaga tu hana meno, hana guts za kumwadhibu yoyote kwa uchafu wake binafsi pia,magamba hayavuki basi tu! Kwa kujikomba komba kwa raia na watu anaishia kuwa msanii sanii na kutoa ahadi za kuclick, za uongo uongo hadi namuonea huruma huyu baba aliyewatoa wakwere kimasomaso, nchi inamshinda kwa kasi na ari ya Chadema ambayo imewashika na watanzania sasa inaivuruga vuruga serikali ya CCM hadi nahisi nchi inakwenda mrama sasa!

Nawaomba Dr Slaa na Chadema kuwa jamani eeh waungwana inatosha tosha sasa, have mercy on our president, kasi yenu inafanya taifa halitawaliki kweli, chama cha magamba kushnei!
Chadema naomba punguzeni spidi!


Mkuu nakubaliana nawe kabisa kwa yote; ila hapo kwenye nyekundu "sikubaliani nawe". Katika nchi za kiafrika ili tuendelee tunahitaji matumizi mazuri ya rasilimali za taifa. Na ili hili liwezekane, inabidi kukomesha ufisadi wa aina zote. Kukomesha ufisadi si jambo rahisi sana, ni mpaka wananchi waliowengi waamke (awareness) kujua namna viongozi wao wanavyowaibia na wawe na uwezo wa kujua namna ya kuwazuia wasiibe. Kwa msingi huo, elimu inayotolewa sasa na CDM inatakiwa iwafikie kila mtanzania hadi vijijini; na hapo ndo rasilimali za nchi hazitabakwa ki-urahisi na hivyo kutumika kwa maendeleo ya waliowengi-watanzania. Hivyo CDM ongezeni spidi kwenda hadi vijijini kuliko na watu wengi ambao hawajajua vema-na ambao hutumika kama mtaji wa watawala kuudanganya umma.
 
aagh mkuu...umeanza vizuri lakini swala la kusema wapunguze kasi,nalipinga,kwa CCm 1 mistake 7 goals, huu moto ndo ushaanza hivyo na unaendelea,hadi kukipambazuka ...2015 hiyooo!! Bado pande za kusini Mtwara na Lindi hawajaenda!!watu wana hamu kweli ya mabadiliko kule ,sema basi tu hakuna muhamasishaji...!!

Mkuu kwa kweli hapo kusema wapunguze spidi ni kwamba namuonea tu huruma rais wetu! Sijawahi ona serikali iliyokosa mwelekeo kama hii!

Halafu Chadema wana potential kubwa sana ukiacha hulo kusini ambako hawajaenda huku mjini tu kuna watu wangependa kuwa wanachama hata leo lakini ndo kama hivyo muihamasishaji hakuna!
 
Ni kweli dr Slaa kafichua ufisadi lakini nadhani siyo peke yake. Tofauti tu ni kwamba yeye alizua moto bungeni na kwenye mikutano ya hadhara. Ukisoma magazeti, ukinukuu thread nyingi hapa JF hasa za MM utakubali kwamba siyo dr Slaa peke yake. Wote wapewe sifa

Muhosni umejieleza vizuri sana, wote waliochokoza mijadala na kufichua ufisadi wapewe sifa, ujasiri wao umetukuka, haswa Dr Slaa!
 
[/COLOR]
Mkuu nakubaliana nawe kabisa kwa yote; ila hapo kwenye nyekundu "sikubaliani nawe". Katika nchi za kiafrika ili tuendelee tunahitaji matumizi mazuri ya rasilimali za taifa. Na ili hili liwezekane, inabidi kukomesha ufisadi wa aina zote. Kukomesha ufisadi si jambo rahisi sana, ni mpaka wananchi waliowengi waamke (awareness) kujua namna viongozi wao wanavyowaibia na wawe na uwezo wa kujua namna ya kuwazuia wasiibe. Kwa msingi huo, elimu inayotolewa sasa na CDM inatakiwa iwafikie kila mtanzania hadi vijijini; na hapo ndo rasilimali za nchi hazitabakwa ki-urahisi na hivyo kutumika kwa maendeleo ya waliowengi-watanzania. Hivyo CDM ongezeni spidi kwenda hadi vijijini kuliko na watu wengi ambao hawajajua vema-na ambao hutumika kama mtaji wa watawala kuudanganya umma.

Nsimba hapo nimeongea kwa huruma tu! Hali ni mbaya! Ona hadi mbunge anarushiwa mawe aiseee!
Mori wa Chadema sasa imewaingia wananchi! Najiuliza wakizidisha itakuaje! JK anaweza kurushiwa mawe pia! Si litakuwa balaa hilo!
 
wote yani watanzania kwa ujumla wake sasa tumekubali kwamba chadema inakubalika. na hasa baada ya chadema kufahamu udhaifu wao ulikua wapi.
tunajua kwamba baadhi ya weakness ilikua.
1. migogoro iliyosababisha (mfano) kigoma ambayo kwa upande wangu ilikuwa ndiyo ngome ya upinzani kupoteza majimbo manne kwa nccr ambapo leo hiki chama kingekuwa marehemu.
2.kutokuwekeza vijijini.
asilimia karibia tisini ya majimbo na kata zote yako vijijini lakini hadi uchaguzi wa mwaka jana ni maeneo machache sana ya vijijini yalikua yamefikiwa na hii weakness ccm waliitumia vizuri.

maoni yangu.
1.ni vizuri chadema wakawekeza sasa kuanzia kwenye matawi kwa mbinu yoyote ile itakayonekana inafaa.
2.wasielekeze nguvu tuu kwenye yale maeneo wanayofiri kwamba wanakubalika bali ni wakati wa kufika kwenye yale maeneo ambayo hayafikiki na kufungua matawi.
na mwisho kabisa alama za nyakati zinaonyesha kwamba 2015 ikulu ni ya cdm, wanataka kuniambia kwamba wataingia ikulu bila ya kuwa na wabunge na madiwani kutoka mtwara na lindi?, ninaomba kufahamishwa ratiba ya huko.
 
Ni kweli dr Slaa kafichua ufisadi lakini nadhani siyo peke yake. Tofauti tu ni kwamba yeye alizua moto bungeni na kwenye mikutano ya hadhara. Ukisoma magazeti, ukinukuu thread nyingi hapa JF hasa za MM utakubali kwamba siyo dr Slaa peke yake. Wote wapewe sifa

hata Bob Marley hakuanzisha reggae, ila ndiyo LEGEND
 
lakini hali haitakuwa nzuri kwa CDM kupiga kimya ila kwa serikali kuwajibika. JK bado anao muda na uwezo mkubwa wa kuwanyamazisha CDM na Dr. Slaa kwa kuyashughulikia yale ambayo yanawafanya cdm wazunguke na kuyadai, baadhi ya hayo mambo ni kama:-
Kuboresha hali za wafanyakazi kwa kupunguza kodi na kupandisha kima cha chini cha mishahara, kupunguza ugumu wa maisha kwa kupunguza kodi nyingi ktk bidhaa muhimu kama mafuta.
Kupunguza matumizi ya anasa ya serikali ikiwa pamoja na mishahara mikbwa na marupurupu ya viongozi kama wabunge kuwepo na uwiano kati ya mishahara na kiwango cha elimu na unyeti wa kazi yenyewe.
Kuheshimu na kufata utawala wa sheria watu wahukumiwe ktk muda muafaka maamuzi ya siasa yasibind maamuzi ya mahakama.
Kusimamia maadili ya viongozi kwa ukaribu na athubutu kuwaadhibu na kuwafikisha mahakamani wtuhumiwa wakuu wa ufisadi ikibidi kuwafunga hata kama ni marafiki zake.
Kupitia upya mikataba yoote ya rasilimali za taifa na iandikwe kwa manufaa ya wananchi, pamoja na transparency ktk uendeshaji wa nchi, kupunguza ukubwa wa serikali.
Hayo ni baadhi tu ila kuna mambo mengi mengi ambayo CDM na watz wengi yanawaboa akiweza kubadilisha mbona cdm watacease coz watakuwa hawana la kuishtaki ccm kwa wananchi otherwise this movement is unstopable yaani hata Cdm na Dr wakinyamaza kwa hali ya sasa hata mawe yatapiga kelele
 
Mkuu kwa kweli hapo kusema wapunguze spidi ni kwamba namuonea tu huruma rais wetu! Sijawahi ona serikali iliyokosa mwelekeo kama hii!

Halafu Chadema wana potential kubwa sana ukiacha hulo kusini ambako hawajaenda huku mjini tu kuna watu wangependa kuwa wanachama hata leo lakini ndo kama hivyo muihamasishaji hakuna!

Dawa katika mazingira kama haya si kwa Chadema kupunguza mwendo, isipokuwa wale walioshindwa waachie ngazi ili Chadema wandeshe nchi inavyotakiwa
 
lakini hali haitakuwa nzuri kwa CDM kupiga kimya ila kwa serikali kuwajibika. JK bado anao muda na uwezo mkubwa wa kuwanyamazisha CDM na Dr. Slaa kwa kuyashughulikia yale ambayo yanawafanya cdm wazunguke na kuyadai, baadhi ya hayo mambo ni kama:-
Kuboresha hali za wafanyakazi kwa kupunguza kodi na kupandisha kima cha chini cha mishahara, kupunguza ugumu wa maisha kwa kupunguza kodi nyingi ktk bidhaa muhimu kama mafuta.
Kupunguza matumizi ya anasa ya serikali ikiwa pamoja na mishahara mikbwa na marupurupu ya viongozi kama wabunge kuwepo na uwiano kati ya mishahara na kiwango cha elimu na unyeti wa kazi yenyewe.
Kuheshimu na kufata utawala wa sheria watu wahukumiwe ktk muda muafaka maamuzi ya siasa yasibind maamuzi ya mahakama.
Kusimamia maadili ya viongozi kwa ukaribu na athubutu kuwaadhibu na kuwafikisha mahakamani wtuhumiwa wakuu wa ufisadi ikibidi kuwafunga hata kama ni marafiki zake.
Kupitia upya mikataba yoote ya rasilimali za taifa na iandikwe kwa manufaa ya wananchi, pamoja na transparency ktk uendeshaji wa nchi, kupunguza ukubwa wa serikali.
Hayo ni baadhi tu ila kuna mambo mengi mengi ambayo CDM na watz wengi yanawaboa akiweza kubadilisha mbona cdm watacease coz watakuwa hawana la kuishtaki ccm kwa wananchi otherwise this movement is unstopable yaani hata Cdm na Dr wakinyamaza kwa hali ya sasa hata mawe yatapiga kelele

Aisee umenifurahisha hapo mwishooo uliposema "this movement is unstopable yaani hata Cdm na Dr wakinyamaza kwa hali ya sasa hata mawe yatapiga kelele"
 
Mkuu kwa kweli hapo kusema wapunguze spidi ni kwamba namuonea tu huruma rais wetu! Sijawahi ona serikali iliyokosa mwelekeo kama hii!

Halafu Chadema wana potential kubwa sana ukiacha hulo kusini ambako hawajaenda huku mjini tu kuna watu wangependa kuwa wanachama hata leo lakini ndo kama hivyo muihamasishaji hakuna!
Yani pamoja na matatizo yote tuliyonayo chini ya uongozi wa magamba bila kusahau potential wanayoionyesha CDM bado watu wanahitaji kuhamasishwa???Kweli waTanzania wameridhika......
 
Nimekubaliana na wewe ila kwenye kupunguza kasi sijaafiki kabisa,Chadema mwendo mdundo 120 ileile.
 
Slaa amefanya nini zaidi ya kuimba wimbo wa UFISADI? Imebaki atoe wimbo wa Taarab aupe jina FISADI. Alete mambo mapya sio kukalia tatizo moja kila siku. Kila kipanda kwenye jukwaa anatoa list ya watu. Tunataka kusikia chama chake kina fanya nini bungeni? Uchaguzi umepita sasa wabunge wake wafanye kazi yao bungeni, na hii tabia ya kidemu ya kususa waache.
 
Slaa amefanya nini zaidi ya kuimba wimbo wa UFISADI? Imebaki atoe wimbo wa Taarab aupe jina FISADI. Alete mambo mapya sio kukalia tatizo moja kila siku. Kila kipanda kwenye jukwaa anatoa list ya watu. Tunataka kusikia chama chake kina fanya nini bungeni? Uchaguzi umepita sasa wabunge wake wafanye kazi yao bungeni, na hii tabia ya kidemu ya kususa
waache.[/QUOTE

Umechangia kisiasa,kihisia pia sidhani Kama utakuwa unaelewa chochote.Kuwa mkweli usiwe mnafiki Ktk hili uliloandiaka
 
Tunajua wazi kuwa ukisema ukweli juu ya ubovu wa Slaa basi unaitwa mnafiki. Endeleeni kumtukuza na siku akiwaharia ndio mtajua kwamba yeye ni mwanasiasa na wala sio malaika kama mnavyo amini..
 
Back
Top Bottom