Revolutionary
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 456
- 86
Hali ya nchi imekua tete sana siku hizi. Dr Slaa na Chadema wameifumuafumua CCM na serikali yake, wamebaki wanahaha kutwa kuchwa kumtafuta mchawi ni nani wakati wamejoroga wenyewe! CCM nako wanajikanyaga kanyaga tu kujivua gamba hakuwezekani kwani gamba linang'oka na ngozi! Ukiachilia unyoka wa CCM kubaki palepale, sijaona gamba hata moja lililovuliwa, wembe wa CCM ni ule ule UFISADI!
Baada ya DR Slaa kuanza kufumua fumu fumu hadharani ufisadi wa CCM tangu alipokua bungeni na Chadema kuendeleza makali hayo kwa kasi na ari zaidi sasa uchafu wote wa serikali hadharani. Kila mwananchi anajua kila uchafu unaoendelea serikalini.
Kwa miaka kadhaa wananchi tulikua tunafichwa UFISADI wa serikali ya CCM, vigogo walijimegea nchi kwa ari ya ajabu kabisa!
Sasa wananchi tunaona na kuelewa Serikali yetu kwa namna inavyonuka hadi nasikia aibu! Rais baada ya kutajwa fisadi na ufisadi wake wa wazi nae anajikanyaga tu hana meno, hana guts za kumwadhibu yoyote kwa uchafu wake binafsi pia,magamba hayavuki basi tu! Kwa kujikomba komba kwa raia na watu anaishia kuwa msanii sanii na kutoa ahadi za kuclick, za uongo uongo hadi namuonea huruma huyu baba aliyewatoa wakwere kimasomaso, nchi inamshinda kwa kasi na ari ya Chadema ambayo imewashika na watanzania sasa inaivuruga vuruga serikali ya CCM hadi nahisi nchi inakwenda mrama sasa!
Nawaomba Dr Slaa na Chadema kuwa jamani eeh waungwana inatosha tosha sasa, have mercy on our president, kasi yenu inafanya taifa halitawaliki kweli, chama cha magamba kushnei!
Chadema naomba punguzeni spidi!
Baada ya DR Slaa kuanza kufumua fumu fumu hadharani ufisadi wa CCM tangu alipokua bungeni na Chadema kuendeleza makali hayo kwa kasi na ari zaidi sasa uchafu wote wa serikali hadharani. Kila mwananchi anajua kila uchafu unaoendelea serikalini.
Kwa miaka kadhaa wananchi tulikua tunafichwa UFISADI wa serikali ya CCM, vigogo walijimegea nchi kwa ari ya ajabu kabisa!
Sasa wananchi tunaona na kuelewa Serikali yetu kwa namna inavyonuka hadi nasikia aibu! Rais baada ya kutajwa fisadi na ufisadi wake wa wazi nae anajikanyaga tu hana meno, hana guts za kumwadhibu yoyote kwa uchafu wake binafsi pia,magamba hayavuki basi tu! Kwa kujikomba komba kwa raia na watu anaishia kuwa msanii sanii na kutoa ahadi za kuclick, za uongo uongo hadi namuonea huruma huyu baba aliyewatoa wakwere kimasomaso, nchi inamshinda kwa kasi na ari ya Chadema ambayo imewashika na watanzania sasa inaivuruga vuruga serikali ya CCM hadi nahisi nchi inakwenda mrama sasa!
Nawaomba Dr Slaa na Chadema kuwa jamani eeh waungwana inatosha tosha sasa, have mercy on our president, kasi yenu inafanya taifa halitawaliki kweli, chama cha magamba kushnei!
Chadema naomba punguzeni spidi!