Dr.Slaa ajiandikisha rasmi kuwa member JF.

Status
Not open for further replies.
Sijui niseme jina langu?Shida hamta niamini.Ila naunga mkono siku moja tuseme majina yetu mtashtuka.Wengine mtapata heart attack.

I know what you mean........... Nilishtuka siku moja nilipoambiwa na mkuu mmoja kuhusu post yangu dakika chache baada ya kupost..... JF inakua na itakua kama jukwaa la watanzania la kutoa maoni yao kwa uhuru kabisa
 
Kama SINCLAIR asingekuwa na ripoti ya madini...Basi hata tusingekuwa na papara za kuulizia.
Lakini kwasababu ni wazi KABURU ANA RIPOTI KABLA YETU...Then sioni kwanini na sisi tusipewe uhondo ili sisi kama wadau wa nchi tuweze kujuwa kuhusu mali zetu.
Tunajua mtu binafsi asiye mtanzania anajuwa kuwa TAIFA letu linatakiwa kuelekea wapi kabla yetu sisi wananchi.
Hilo lenyewe linatosha kutuonea huruma na kuisoma ripoti hiyo maramoja.
 
Heko Dr. Slaa kujiunga na JF! Hapa hakika wanaJF watatoa maoni yao kuhusu ufisadi na udhalimu uliokithiri nchini.
 
wrong.. even the british law is based from Canon Law. Canon Law is the foundation and basis of modern civil law. Unafikiri hicho kilatini cha kwenye sheria kinatoka wapi?

Mwanakijiji,

Mimi sidhani kama CV (hasa elimu) ya Dr. Slaa inatakiwa kujadiliwa sana. Huyu ni mtu aliyesoma vya kutosha. Systems za Elimu ziko tofauti hata kati ya nchi na nchi. Wakatoliki wana syytem yao ambayo ni very strict! Mtu huwezi kupewa PhD kama hustahili! Nadhani tutakubaliana kuwa waseminari (walio wengi) Tanzania huwa wanauwezo mkubwa sana, hata wakija chuo kikuu wakitotokea form six!! Sasa huyu bwana na ma Certificates yote hayo watu bado wanataka awe ameandkiwa BACHELOR, MASTERS, PHD!!!!!!

Wajerumani wana BACHELOR (DIPLOM 4 years) na PhD (3 years)! Wakati Tanzani kuna Bachelor (zingine 4 - 5 years) Masters (zingine 2 or more years) na PhD (at least 3 years). Sijui kama Tanzania ni moja ya nchi zenye elimu bora! Kenya A-level (2 years) hawana!!!!!! Wanatoka form four four straight to university!! Tukubali kwamba reference sio utaratibu wa Tanzania ama commonwealth nk. Kama alivyosema mchangiaji hapo juu, mbona hao wasomi wa Havard, Oxford nk ndio wanaoongoza kwa vituko kwenye uongozi!

Ingawa siungi mkono PhD za akina Mzindakaya, Nchimbi na baadhi ya walimu wa Mzumbe!!
 
I know what you mean........... Nilishtuka siku moja nilipoambiwa na mkuu mmoja kuhusu post yangu dakika chache baada ya kupost..... JF inakua na itakua kama jukwaa la watanzania la kutoa maoni yao kwa uhuru kabisa
zitto,
Karibu ukumbuni asubuhi,Sijaona Tamko lako kuhusu Kusimamishwa kwa Chacha Wangwe.Je huu ulikuwa wakti Muafaka??
 
Ushauri wa kwanza kabisa kwa DK SLAA kama mkichukua nchi.
Mujaribu kuujenga mfumo wa UCHUMI kwa kuangalia mfano KAMA WA TAIFA LA JAPAN.
Ni mfumo wa UCHUMI wenye kuzingatia maslahi ya MJAPAN na si vinginevyo.
Ahsante.

mkuu hiyo imekaa sawa sana,maana hawa mbumbumbu tuliokuwa nao hawajui chochote kuhusu suala la uchumi na ndiyo maana wanamzuia mkulima kuuza hata mazao yake ili ajikwamue kiuchumi,badala ya kumpa ruzuku ili alime zaidi na auze zaidi
 
Naomba niingili hapa mara moja.

a. Hakuna mwanachama ambaye atavushwa hapa kwa kuangalia jina lake au mchango wake mahali kwingine. Akija Kikwete, Salim, hata mmojawapo wa wa mitume watapanda daraja taratibu kama wengine walivyofanya. Hivyo hilo wazo la kurusha watu madaraja sidhani kama lina nafasi katika JF. Njia za kupata daraja ni pamoja na michango ya mtu, kuanzia ya mabandiko yake na ya kuiwezesha JF.

Dr. Slaa na wengine watapanda chati taratibu kwa kufuata njie ile ile waliyoifuata wengine. Hilo hata hivyo halina maana ya kumshusha hadhi au kumfanya duni bali ni kuonesha kuwa katika JF wanachama wote ni sawa.

Dr. Slaa amekuwa mwanachama hapa kwa muda mrefu na amekuwa akifuatilia kwa kina yanayosemwa hapa na sasa umefika wakati wa kujiunga tena rasmi. Note the word "tena". Alishajiunga hapa lakini alipoteza password yake na leo aliamua tu kujisajili upya.


b. Swali kwamba ni yeye hilo lisiwatie shaka na kuna watu wanaangalie nenno kama "nondo" jamani lugha hii wazee nayo wanayo. Nimewahi kumpigia simu Waziri Mmoja tuliposalimiana akaniambia mambo vipi nikasema "pouwa za huko" akaniambia "Pouwa tu". Sasa enzi zile ningeona anatumia neno la ajabu! Then akaja Bush.. guess aliwasiliamiaje watu "mambo!". Kwa hiyo, ameamua kuingia kwa jina lake ili kusiwe na utata wowote ule. Mojawapo ya vitu ambavyo tumekuwa tukivifanya ni kuona kuwa anapoingia mtu mwenye cheo fulani serikalini kwa jina lake tunacheki moja kwa moja na mtu huyo au wasaidizi wake wa karibu.

Miezi ka miwili iliyopita kuna mtu aliingia hapa na kujiandikisha kwa jina la Kikwete na kutoa speech moja ndefu sana. Mara moja tukazungumza na Ikulu (within minutes) na kukuta Rais alikuwa anauchapa usingizi na msaidizi wake akatuhakikishia kabisa aliyeandika siyo Rais na hakuna mtu aliyeidhinishwa kufanya hivyo. Well tukafuta na jamaa aliyeingia akafungiwa. So, kina invisible wanachukulia haya ya kutumia majina halisi very serious.

c. Kujiunga kwa Dr. Slaa rasmi ni mfano mwingine wa kuthubutu kwa viongozi wetu. JF siyo adui yao lakini ni mahali ambapo yote yanazungumzika. Dr. Slaa anajua kwa kutumia jina lake amejiweka kama swala kwenye mbuga iliyozungukwa na simba! Atapata personal attacks na vurugu mechi za kila aina. Hilo bila ya shaka litakuwa ni wimbi la kwanza na akisurvive basi sidhani kama kuna magumu mengine. Uamuzi wake uwe mfano kwa wabunge wengine kuungana nasi, wakijua wazi kuwa ni bora zaidi kuingia kwa majina ya kupachika kuliko majina halisi (ni distraction kubwa sana) kwani akimfokea mtu barabarani na mwana JF akikuona watakuandika humu! Ukionekana umeshikana mkono na mtu basi jina lako litatangaa. Ndio maana kutumia majina halisi kunapoteza sana hoja muhimu. Hata hivyo mtu akishapima pro and cons kwa upande wake binafsi basi afanye kila anachotaka. Hivyo tunawakaribisha wabunge, wakuu wa mikoa, wakuu waidara n.k kuungana nasi kwani hapa ndiyo Jamii Forums.. where we dare talk openly!!! Hapendwi mtu, haogopwi mtu, na hapendelewi mtu.

Asante Mwanakijiji na wangine kwa mchango wako. Uhuru wa kutoa maoni ni wa kila mtu haina mahusiano na chama chochote wala hayapimwi to degree of prudent. heri kuwa mjinga kwa kutojua kuliko kuwa mfinyu na mvivu wa kifikiri.

Tuachane na haya ya rank hapa JF twende kujenga taifa na tuanzie kwenye family, workplace na kwenye vikao vya jioni then JF inaweza kuwa na maana halisi hata bila kujoin hapa. also let spread our this website to many people as possible who love this country. Tusichoke kuelimisha ipo siku wataelewa tu.

Asante Karibu Dr. Slaa
 
Field Marshal ES,
Thanks a lot. Kimsingi, kinachotusukuma ni uzalendo kwa nchi yetu. Kwangu mimi siasa ya vyama inachukua namba ya mwisho. Kwanza sisi ni Watanzania, na watanzania wawe walalahoi kama wanavyoitwa, au wa ngazi ya juu sana (japo naamini binadamu wote sawa) wote wana mchango katika kuijenga, kuilinda na kuitetea nchi yao. Hakuna mwenye ukiritimba wala hati miliki ya nchi. Hivyo nadhani mchango wa kila mmoja nitauheshimu sana na utaheshimiwa na kila mmoja wetu. Ni kweli JF mimi si mgeni, hivyo kipya ni kujisajili upya. Thanks for the warm welcome.

Welcome great man. They say 'It takes both sunshine and rain to make a rainbow'
Lets all fight for the nation.Mkubwa ,mdogo, excluding mafisadi wote. They have no right to torture us like this.
 
Hapa sasa kila mwana JF naona moyo wake umetakasika baada ya kuona Dr.Slaa amejiunga rasmi hapa.Natambua wengi wetu tumefrahi mno tena sana.
Cha mhimu sasa hapa ni ushirikiano na kumpa support kubwa kwa kushusha NONDO za ukweli kabisa na evidence kisha doctor kama kawaida yake anailipua.
Tunakuomba doctor kama kuna fununu zozote zile unasikia tafadhali usisite kuja hapa na kutumwagia vijana kwa kaka zako hapa JF kisha watu wanaingia kazini kufanya uchunguzi na upembuzi YAKINIFU.
Naombeni wana JF tushirikiane kuwang'oa hawa mafisadi wanao tishia maisha yetu kwa uchoyo na ubinafsi wao.
 
Kuna mtu yeyote ana BIO ya DR Slaa,nataka kumjua huyu mpiganaji maana namsikia tuu!

...Slaa hii mbona unaipita bila jibu? tunataka kujua viongozi wetu!


Do your homework man, unatuangusha sasa!
Ungekuwa umefanya jitihada ya kutafuta mwenyewe ukashindwa wakuu wangekufikiria. Umeuliza swali lako mara ya tatu sasa hakuna anaye-respond, hujishtukii tu?





.
 
Jamani Kumkaribisha Mtu Aliekuwepo Hapa Kwa Dahari Sio Fair .


Halafu Waje Watueleze Sababu Za Kumtimua Wangwe, Au Na Wao Ndio Vibaraka Wa Mbowe Fisadi
 
Karibu sana Dr. Slaa. Nadhani tuwashukuru pia CCM kwa "kukutema" katika michakato yao ya KITAKRIMA. Naamini ungebaki kule usingekuwa hivi ulivyo sasa. Shujaa wa kila anayeitakia mema TZ.
 
Jamani Kumkaribisha Mtu Aliekuwepo Hapa Kwa Dahari Sio Fair .


Halafu Waje Watueleze Sababu Za Kumtimua Wangwe, Au Na Wao Ndio Vibaraka Wa Mbowe Fisadi

MwP,
Tutaishiwa muda. Sidhani kama siasa za chama kimoja kimoja ni muhimu hapa. Siasa za Taifa ndio muhimu. 2010 sio mbali...
 
Nawashukuru kwa sasa najiandaa kwenda Bungeni. Nondo ziwe na ukweli tena ukweli mtupu ili tuweze kuwanusuru vijana hadi vitukuu vyetu.

ila inshu ya wangwe naona itakimega chama chenu ...chadema ilianza kustawi ila naona sasa sisiemu wameanza kutumia njia zile zile walizotumia kwa enisisiara-mageuzi then kwa tielopii japo kafu naona wao wamejitahidi kuweka ustawi wao vyema kwa kiasi flani japo nao wanamatatizo yao.
otherwise mimi binafsi nakupongeza kwa kuwa kazi yako ni njema katika kuwawakilisha wananchi.nadhani tukiwa na wakina slaa 10,wakina nzito 10 na wakina kilango 13 na mwakyembe 15 basi nchi itabadirika hii.
ila mzee hebu tuelezee shutuma za uchagga na ukaskazini ndani ya chadema imekaaje hiyo? nasikia wabunge wa kuteuliwa wa viti maalumu karibu asilimia kubwa ni wa kulekule...!
kama hali ni hivyo basi hii haijakaa njema hata kidogo...
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom