Dr. Nchimbi na urais 2015

Tunajua Bw. Nchimbi ana haki yake ya msingi ya kugombea nafasi yoyote nchini na kupigiwa kura. Lakini mmh kwenye hili la Urais kweli anahitaji kuwa serious kidogo. Ikulu walishazoea mafyoso tu kama wanavyopata hizo Ph.D za mafyoso. Ndo maana anaona ni rahisi kuwa na mawazo kama hayo ya kugombea urais wa JMT. Sasa kama elimu tu kapiga mafyoso, yaliyobaki yatakuwaje??
 
Naomba Mungu atuepushie hizi balaa nyingine. Kuongoza nchi kwa mbali inaonekana ni kitu rahisi.Yanayotokea sasa yanaonyesha wazi kuwa kukimbilia tu kuwa rais haitoshi kama huna uwezo wa delivering
 
5

nadhani wa kuhama ..bora mjiandae kuhama ..maana hakuna anayeijuwa kesho..na siasa hazitabiriki!!..kwani hapa mmewataja vijana wengi....kwa nini nchimbi peke yake ndie awe hoja...hii ina maana ana weight...!!...na amekomaa kisiasa...

nadhani ni mapema mno kuanza kampeni za 2015.....lolote hapa kati linaweza tokea na kubadili upepo wa kisiasa....ila pamoja na hayo mimi projection zangu ni kuwa rais wa tanzania mwaka 2015 atakuwa kijana yeyote mwenye miaka 38 hadi 45...leo,.........wote ambao wametajwa wanaozidi miaka niliyoweka hapo wasahau nafasi ya urais.....,na vijana wenye miaka 38 hadi 45 ..ambao wanautaka urais basi wapange vema karata zao,wapate uzoefu,wajenge network....na walinde afya zao kama mboni ya jicho lao....!!!

Kusema kweli habari hizi mimi binafsi sijazichukulia serious hata kidogo. Kama mkifuatilia kwa makini habari (headline news ) za Tanzania Daima Jumapili huwa ni za kubuni buni (speculative) hivi. Ni mara chake Tanzania Daima Jumapili kuwa na headline news ambazo zinahusu matukio halisi (factual news). Nadhani editorial policy ya TZ Daima Jumapili inalenga zaidi katika uchambuzi wa siasa (analysis) ndio maana headline news karibu zote (Jumapili) zinajikita katika kuchambua aidha serikali ya JK au CCM.

Ukisoma uchambuzi huu (reading between the lines) kwa makini utagundua kwamba habari hizi ni za hisia ya mwandishi mmoja ambaye hajafanya utafiti wa kina ila anajaribu kunukuu vyanzo vya habari ambavyo kusema kweli havipo! Ni mapema mno kujua nani atagombea Urais CCM 2015 kwa vile wote tunajua kwamba uchaguzi wa Urais ndani ya CCM 2010 ni dhahiri (foregone conclusion) hasa baada ya EL kuweka msimamo wake wazi.

Kwa mfano kuna utafiti gani katika kusema Lowasa, Mwandosya, Sumaye wanategemewa kuchukua fomu 2015? Kwa nini hasiwemo Kigoda? Au nini jipya katika kusema Membe na Dr. Gama nao wanaunyemela Urais 2015? Ni dhahiri hawa wametajwa na Mwandishi kwa vile walikuwa vinara wa mtandao 2015. Mimi binafsi aniingii akilini kwamba 2015 Pombe Magufuli atakaa pembeni katika kinyanganyiro cha Urais ndani ya CCM ndio maana alikuwa mtu wa kwanza kushambuliwa na Gazeti la Rai mwanzoni wa utawala wa awamu ya nne. Hakufungua kinywa hata kidogo. Si bure.
 
jamani acheni mzaha,huyu nchimbi asije akafikiri naye ni mmoja wa wale wanaoweza kushika uraisi...abaki kule kule kwenye ukada wake na PHd yake fake na kazi yake ya kuiba kura ili mafisadi washinde,Ikulu hatumtaki na hatopata!
 
jamani acheni mzaha,huyu nchimbi asije akafikiri naye ni mmoja wa wale wanaoweza kushika uraisi...abaki kule kule kwenye ukada wake na PHd yake fake na kazi yake ya kuiba kura ili mafisadi washinde,Ikulu hatumtaki na hatopata!

Tell him,tell him!!
 
siamini kama kweli lowasa anaushawishi kama mwandishi anavyosema.......ila ni mkurupukaji tu na mpenda sifa na hafai kuwa katika uongozi kama kweli watz mnamuenzi mwalimu nyere
 
Wana JF kwa nini kujadii Urais 2015 kama vile 2010 hakuna uchaguzi au kuna mtu tayari kesha shinda huo uchaguzi?
Nawahakikishia taswira wengi waliyonayo ya 2015 itabadilika baada ya uchaguzi wa mwaka 2010. Uchaguzi ujao majeraha yatakayoipata CCM ndiyo yatakayotoa picha ya 2015 na msambaratiko wa Lichama kongwe kabisa.
Mwakani hata kama CCM ni wezi wazoefu wa kura, hali ni tofauti na siku za nyuma na hawataweza kutawanyika nchi nzima na kufanya hujuma kila mahali kama awali.
 
urais ni hot cake.....na tunakoelekea watatoana majicho........yetu macho ila tunaomba zisimwagwe pesa chafu..............
 
Nonono!!!! hiyo post aliyonayo sasa sijui kwanini watu hawamwambii jamaa amtoe tu hapo mara moja.upuuzi mtupu!

Muungwana hana ubavu wa kumtoa Nchimbi hapo alipo kwasababu ni mtu wake wa karibu sana na siri zake za ndani anazijua!! Masangoma wote wa mkwere yeye ndio hubeba mikoba kwahiyo kumtema si rahisi bali ngojeni msikie akipandishwa cheo na kupewa wizara yake!! Hii ndio DANGANYIKA na ukweli ndio huo!!
 
Naomba kuuliza swali. Hivi Nchimbi kafanya kosa gani au ufisadi gani hadi akose kuwa na sifa za kuwa rais?
 
Naomba kuuliza swali. Hivi Nchimbi kafanya kosa gani au ufisadi gani hadi akose kuwa na sifa za kuwa rais?

Alidanganya elimu yake ya PhD,kama ingekuwa nchi yenye kufuata sheria sasa hivi Nchimbi angekuwa anapumzika huko Ukonga;Rejea kwenye tovuti ya Bunge uone madudu aliyoyaweka huko kuelezea elimu yake!

Je hilo tu halitoshi kumfanya jamaa huyu awe disqualified MgonjwawaUkimwi?
 
blank.gif
logo2.gif
• Malecela, Dk. Salim, Prof. Mwandosya wajeruhiwa

na Mwandishi Wetu


amka2.gif

NAFASI ya kuwania kiti cha urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) hivi sasa inaonekana kuzusha balaa yenye kuogopwa na wagombea mbalimbali, kutokana na kuzingirwa na mbinu chafu zenye kudhalilisha kwa kila mwenye kuiwania.

Uchunguzi wa Tanzania Daima Jumapili unaonyesha kwamba, baadhi ya hoja nzito za hivi sasa zinazohusisha baadhi ya wanasiasa na harakati za kugombea urais ndani ya CCM ama 2010 au 2015, zinatoa mwelekeo ule ule wa kuchaguana na kuchafuana kama ilivyokuwa mwaka 2005.

Majeruhi wa kwanza wa siasa hizo safari hii ni aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ambaye jina lake limekuwa likihusishwa na harakati hizo kutaka urais.

Lowassa mwenyewe katika mahojiano aliyofanya na gazeti dada la hili, alihusisha hoja hizo juu yake kuwa sehemu ya mkakati wa watu ambao hakuwataja, wa kumkosanisha na Rais Kikwete.

Wachambuzi wengine wa mambo wanasema kwamba kusukwasukwa kwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta nako kunahusishwa kwa namna moja au nyingine na harakati za urais ndani na nje ya chama hicho.

Ingawa wana CCM wamekuwa wakikubaliana kuwa mwaka 2010, Rais Kikwete ndiye anayepewa nafasi kubwa ya kuendelea kugombea kwa tiketi ya chama chake, hali inaonekana kuwa tofauti na kinyang’anyiro cha mwaka 2015, ambapo majina kadhaa makubwa yamekuwa yakitajwa.

Miongoni mwa wanaohusishwa na kusaka urais mwaka 2015 ni pamoja na Lowassa, Sitta, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dk. Asha - Rose Migiro na Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Emmanuel Nchimbi.

Hofu hiyo pia imewakumba baadhi ya vigogo waliowania kiti hicho mwaka 2005, ambao sasa wameonekana kuwa kimya zaidi huku wakisisitiza kutotaka kusikia au kukumbushwa yale yaliyowakuta katika mchakato huo uliowafanya wachafuke katika jamii kiasi cha kusababisha makovu yasiyofutika.

“Bwana mdogo nisingependa uniulize kuhusu kuwania urais, kilichonipata mwaka 2005 siwezi kukisahau, urais ni tishio, sitaki kujihusisha nao tena,” alisema mmoja wa aliyewahi kugombea nafasi hiyo alipokuwa akizungumza na Tanzania Daima Jumapili.

Baadhi ya wanachama wa CCM waliozungumza na gazeti hili wamebainisha matukio ya udhalilishaji na vitisho walivyofanyiwa wagombea waliowahi kujitokeza kuwania kiti hicho, ndiyo yanayowafanya waione nafasi hiyo mwiba.

Hofu hiyo inachagizwa zaidi na mambo yaliyofanyika katika Uchaguzi Mkuu uliopita, ambapo Dk. Salim Ahmed Salim, aliyekuwa mmoja wa waliokuwa wakiwania nafasi hiyo alipozushiwa mambo kadhaa, ikiwamo kuhusishwa na kifo cha aliyekuwa Rais wa Zanzibar, hayati Abeid Aman Karume.

Dk. Salim pia aliambiwa si raia wa Tanzania (Mwarabu), pamoja na kuwa mwanachama wa Chama cha Hizbu ambacho kilikuwa kikiutambua utawala wa sultani visiwani Zanzibar, hivyo kuhusishwa moja kwa moja na Waarabu.

Kashfa hizo kwa kiasi kikubwa zilichangia kuharibu sifa ya Dk. Salim ndani na nje ya CCM, hivyo kujikuta akikosa kutimiza ndoto yake ya kuwania kiti hicho ambacho kwa wakati huo kilikuwa na upinzani mkubwa ndani ya CCM.

Baada ya kukumbwa na tuhuma hizo, Dk. Salim aliweka bayana wazi kuumia kwake na kutoridhishwa na mbinu chafu zilizokuwa zikitumiwa na washindani wake, hasa kundi la wanamtandao, kwa kumzushia mambo yenye kumhatarishia maisha yake, pamoja na kupandikiza chuki kwa Wazanzibari na familia ya Karume.

Mgombea mwingine ambaye alionja adha ya kuwania urais ni aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, ambaye naye kupitia vyombo vya habari alianikwa kumiliki akaunti yenye zaidi ya sh trilioni tano nje ya nchi.

Sumaye alionekana kushtushwa na habari hizo pasipo kujua ni mkakati kabambe wa kumchafulia jina lake ili asiweze kupitishwa na vikao vya juu vya chama hicho kuwa mgombea urais.

Kiongozi huyo pia alishutumiwa kumiliki mashamba makubwa kwa njia zinazotiliwa shaka katika Kijiji cha Kibaigwa, wilayani Mpwapwa, mkoani Dodoma.

Tuhuma hizo zilimfanya kiongozi huyo mstaafu kukwaa kisiki katika mchakato huo huku akiendelea kuugulia majereha aliyoachiwa na wanamtandao waliodhamiria kumuingiza Rais Jakya Kikwete, Ikulu pasipo kuangalia madhara ya mbinu zisizofaa walizokuwa wakizitumia.
John Samwel Malecela, ni miongoni mwa majeruhi wa wanamtandao katika kinyang’anyiro cha urais, ambapo katika pilikapilika hizo alizushiwa maneno kadhaa, ikiwamo uhusiano wake na nchi za Kiarabu, ambazo zilikuwa zikimsaidia kifedha.

Katika lengo hilo hilo la kumchafua Malecela, alihusishwa kutokuwa na uwezo wa kukikalia kiti hicho kutokana na umri wake kuwa mkubwa, tofauti na Kikwete ambaye alipambwa kwa nyimbo za kuwa ni kijana na mwenye kufanya kazi kwa ari mpya, nguvu mpya na kasi mpya.

Wakati propaganda hizo na mambo mengine yakiendelea, Malecela alijitokeza na kudai kuwa mbinu zinazotumika si za kiungwana, huku akiwaponda wale wanamuona mzee huyo hafai kuongoza, kwa kuwaambia kuwa kiti cha urais si kwa watu wenye nguvu za kubeba zege, bali huhitaji busara, utulivu wa mhusika pamoja na kuzungukwa na watendaji imara.
Wachambuzi wa masuala ya siasa waliziona mbinu za wanamtandao zilikuwa mbaya na zisizofaa katika medani ya siasa, kwa kuwa zililenga kuchafua majina ya watu na kupandikiza chuki ambazo mwisho wake ni kukigawa chama na wananchi.

Wakati wanasiasa waliojitokeza kuwania urais wakishughulikiwa kwa stahili hizo mwaka 2005, Lowassa anatajwa kuwa na ushawishi mkubwa ndani na nje ya CCM iwapo atasimama kugombea nafasi hiyo mwaka 2015.

Pamoja na ushawishi huo unaoelezwa kuwa anao Lawassa, bado atakabiliana na wakati mgumu dhidi ya Membe ambaye ameshaanza kupigiwa chapuo ya kuwania kiti hicho Dk. Asha -Rose Migiro naye anaweza kutoa changamoto kubwa katika kinyang’anyiro hicho hasa kutokana na uwezo wake wa kuongoza Umoja wa Mataifa.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanabashiri Migiro anaweza kupata wakati mzuri kwa kuwa baadhi ya watu hivi sasa wangependa kuona mageuzi kwa nchi kuongozwa na rais wa kike mwanamke kama ilivyo Liberia. Wachambuzi hao pia wanaonya kwamba kama vigogo wa CCM hawataacha matumizi ya kampeni chafu katika kuwania kiti hicho, makundi ndani ya chama hicho yatakimaliza na kuna hatari uhusiano baina ya wanachama ukazidi kudorora kadiri siku zinavyozidi kusonga mbele.


h.sep3.gif


blank.gif

Hii nyuuzi inatisha!
 
Alidanganya elimu yake ya PhD,kama ingekuwa nchi yenye kufuata sheria sasa hivi Nchimbi angekuwa anapumzika huko Ukonga;Rejea kwenye tovuti ya Bunge uone madudu aliyoyaweka huko kuelezea elimu yake!

Je hilo tu halitoshi kumfanya jamaa huyu awe disqualified MgonjwawaUkimwi?

Malafyale, point nzito na nimekuelewa. Sasa yeye kadanganya elimu bila kuliibia taifa na anashambuliwa kiasi hiki, je wezi watukutu kama EL, RA, V-g-chenji, na wengine wote waliosababisha umasikini wetu mbona hawashambuliwi kiasi hiki?
 
Alidanganya elimu yake ya PhD,kama ingekuwa nchi yenye kufuata sheria sasa hivi Nchimbi angekuwa anapumzika huko Ukonga;Rejea kwenye tovuti ya Bunge uone madudu aliyoyaweka huko kuelezea elimu yake!

Je hilo tu halitoshi kumfanya jamaa huyu awe disqualified MgonjwawaUkimwi?

Good! we can tolarate so many things but when it comes to education we are serious men! He better opts other things than this one!
 
Wanabodi,

Nimetafakari kidogo bila majibu kwa nini Serikali, baadhi ya Usalama wa Taifa na baadhi ya Wakuu ndani ya CCM wanakuwa wanafiki kiasi hiki juu ya wagombea watarajiwa ambao tayari wamepanga timu zao za maandalizi.

Kwa walio karibu na "corridor of power" hakuna asiyejua state inavyomuandaa John Emmanuel Nchimbi kama mteule mpya wa Mkuu wa Kaya kumrithi pale Magogoni. Mipango yake na harakati zote zinaratibiwa na State. Lowassa anajua, Pinda anajua, Membe anajua na wengine tumepata kujua. Sasa kwa nini kila kukicha wapambe wameng'ang'ana na Lowassa tu kama vile wengine hawafanyi?

Binafsi simaini kama kuna mtu anatarajia kufanikisha jambo lolote maishani bila maandalizi, mikakati na jitihada. Hawa wanaowaandaliawengine ufalme kwa nini hawataki kuona wala kusikia wengine wenye Uwezo wa kujiandalia wakifanya hivyo? Miujiza huonekana kama vitu vitokeavyo bila kutarajiwa lakini nayo ili mtu imtokee lazima afanye maandalizi i.e kutubu, kujitakasa, na kusali kwa imani. Kwa nini hawa "wenye mteule wao mfukoni" hawataki kusikia wenye uwezo wakijiandaa?

Kuanzia sasa nami natangaza kujiunga na timu Lowassa ili nikajue kwa nini anahofiwa kuliko wengine wote.
 
Mwaka huu ukija kuisha wengi mtakuwa Mirembe,sasa eti naye Nchimbi ana timu ya kusaka uraisi alafu anamtuma huyu ----
amsemee aone JF ina maoni gani. Mwambie hauziki na lile jimbo la Songea Prof.J ndo atakalogombea kwa hiyo atakuwa raia wa kawaida
 
Usishangae sana. Ngoma ikivuma sana mwishowe hupasuka. Hata hawa wanaovuma sasa soon watapotea na kuibuka wengine
 
Back
Top Bottom