Kyela: Dr. Mwakyembe amtolea Uvivu Rostam

Engineer

JF-Expert Member
Jan 5, 2009
265
0
Habari za kutoka hapa Kyela ni kwamba dr. Mwakyembe leo kamvaa Rostam kweli kweli. Kamwita fisadi namba moja, kaiba mali ya Tanzania na ni mbumbumbu, hajui kitu, hata bungeni haongei. Anasema Rostam katumia ufisadi kuiba viwanda viwili alivyoanzisha Nyerere na sasa kafanya godowns zake.

Katika mkutano wake alikuwa ameongozana na waandishi habari kutoka Mbeya baada ya wale wa Kyela kupigwa marufuku kuhudhuria mkutano huo kwa madai kwamba huwa wanamwandika vibaya.

Alitumia muda mwingi kumtukana Rostam.

Pia kasema yeye ni kweli anamiliki shares kwenye hiyo kampuni pamoja na vijana wengine kama 50 wazalendo wa nchi hii na kwamba hiyo kampuni bado haijaanza.

Anasema alipoenda Singida alishangiliwa sana na wananchi wakamwambia kama Kyela hawamtaki basi wao Singida wapo tayari kumpa ubunge.

Kuna mengi mheshimiwa kaongea ambayo mpaka mtu unajikuna kichwa, hivi kweli ni muhimu? Labda ndio siasa zetu zilipofikia sasa. Inaelekea maneno ya Malecela hawajayasikia kabisa.

Wenye taarifa zaidi mnaweza kuongea.
 
Last edited by a moderator:
..CCM sasa itabidi wachague kati ya Mwakyembe na Rostam.

..wakati wa kunyamazisha watu, na kutishana umepita.
 
Mwakyembe ananifurahisha sana. Maana tatizo la nchi yetu ni unafiki mkubwa wa kuwasikiliza watu kama akina Malecela na Chiligati ambao siku zote huweka mbele maslahi ya CCM kwanza badala ya yale ya nchi.

I hope ataendelea kuongea maana tutayajua mengi ambayo tulikuwa hatuyajui. Hongera Mwakyembe Watanzania wengi tuko nyuma yako. Hata hapa jimbo la JF tunaweza kabisa kukupa ubunge maana tumechoshwa na unafiki na ufisadi uliojaa ndani ya nchi yetu.
 
RA jamani ni fitina saana....nasikia hata elimu yake ni fake na ana uraia nchi 3....alianzia kutumwa tumwa deals za watu...hapa mjini nae akapata access a wanene wenye tamaa...wanaomkumbatia shauri yao....hongera Kyembe...
 
Kuna tetesi ambazo nimezisikia hapa, nasema tetesi kwasababu siwaamini wanaozisema. Wanasema Dr. Mwakyembe anatafuta njia ya kuhamia CHADEMA.

Wanasema kwenye mkutano wa leo yule kijana wa CHADEMA aliyewahi kuwekwa ndani wakati ule wa ziara ya JK ndiye alikuwa mbele katika waandaaji. Pia wanataja uhusiano wa Dr. Mwakyembe na Mbowe pamoja na Mengi kama sababu za kuamini hivyo.

Pia inaelekea kuna mpambano mkali unaandaliwa Kyela 2010 kati ya Dr. Mwakyembe na jamaa mmoja nasikia yuko nje ya nchi.

Mimi nilikuwa hapa kwa muda na niliyoyaona leo sina hamu, hii wilaya imegawanyika kweli kweli. Sikuona viongozi wowote wa CCM pale mbele badala yake kulikuwa na wapambe wa mheshimiwa waliokuwa wanamwaga sifa kibao.

Angalieni hili jimbo 2010 inaelekea kutakuwa na vituko.
 
Kuna tetesi ambazo nimezisikia hapa, nasema tetesi kwasababu siwaamini wanaozisema. Wanasema Dr. Mwakyembe anatafuta njia ya kuhamia CHADEMA.

Wanasema kwenye mkutano wa leo yule kijana wa CHADEMA aliyewahi kuwekwa ndani wakati ule wa ziara ya JK ndiye alikuwa mbele katika waandaaji. Pia wanataja uhusiano wa Dr. Mwakyembe na Mbowe pamoja na Mengi kama sababu za kuamini hivyo.

Pia inaelekea kuna mpambano mkali unaandaliwa Kyela 2010 kati ya Dr. Mwakyembe na jamaa mmoja nasikia yuko nje ya nchi.

Mimi nilikuwa hapa kwa muda na niliyoyaona leo sina hamu, hii wilaya imegawanyika kweli kweli. Sikuona viongozi wowote wa CCM pale mbele badala yake kulikuwa na wapambe wa mheshimiwa waliokuwa wanamwaga sifa kibao.

Angalieni hili jimbo 2010 inaelekea kutakuwa na vituko.

Mwakyembe kujiunga na CHADEMA sioni kama ni tatizo, lakini huu si wakati muafaka wa kufanya hivyo kama kweli ana nia ya kujiengua CCM. Kwa maoni yangu Mwakyembe ana nafasi nzuri zaidi ya kubaki CCM na kupambana na mafisadi akiwemo ndani ya chama hicho. Akiamua kuingia CHADEMA wakati huu basi CCM itammaliza kabisa kisiasa maana mashambulizi dhidi yake yatakuwa si ya kawaida lakini hawatakuwa tayari kumshambulia akiwemo ndani ya CCM.
 
Kwa hali hii inaonesha Mwakyembe kaishiwa kisiasa.

Anayesimama na kutetea maslahi ya nchi kaishiwa kisiasa, na yule anayesimama na kuweka maslahi ya CCM mbele badala ya yale ya nchi kama akina Chiligati na Malecela ndiyo wanaonekana wanasiasa wanaokubalika!!! Kazi kweli kweli!!!!
 
Huyu Mwakyembe ange concertrate tu kwenye kueleza ukweli pale ambapo anaona wananchi wamepotoshwa kuhusu yeye then awaachie watu wenyewe ndo wachague mchele toka kwenye pumba, kitendo cha kuendelea kumshambulia Rostam kwa mtazamo wangu kinamfanya aonekane yuko desperate kusafisha jina lake, na alimtuhumu RA kwa kutaka kjisafisha huku akiwachafua wenzie- he is doing exactly the same. Bado nakumbuka kamsemo ka Dr Slaa alikokatoa hapa kwamba "mwendawazimu akichukua nguo zako wakati unaoga mtoni na kukimbia, ukimkimbiza wote mtaishia kuonekana wendawazimu".
 
Habari za kutoka hapa Kyela ni kwamba dr. Mwakyembe leo kamvaa Rostam kweli kweli. Kamwita fisadi namba moja, kaiba mali ya Tanzania na ni mbumbumbu, hajui kitu, hata bungeni haongei. Anasema Rostam katumia ufisadi kuiba viwanda viwili alivyoanzisha Nyerere na sasa kafanya godowns zake.

Katika mkutano wake alikuwa ameongozana na waandishi habari kutoka Mbeya baada ya wale wa Kyela kupigwa marufuku kuhudhuria mkutano huo kwa madai kwamba huwa wanamwandika vibaya.

Alitumia muda mwingi kumtukana Rostam.

Pia kasema yeye ni kweli anamiliki shares kwenye hiyo kampuni pamoja na vijana wengine kama 50 wazalendo wa nchi hii na kwamba hiyo kampuni bado haijaanza.

Anasema alipoenda Singida alishangiliwa sana na wananchi wakamwambia kama Kyela hawamtaki basi wao Singida wapo tayari kumpa ubunge.

Kuna mengi mheshimiwa kaongea ambayo mpaka mtu unajikuna kichwa, hivi kweli ni muhimu? Labda ndio siasa zetu zilipofikia sasa. Inaelekea maneno ya Malecela hawajayasikia kabisa.

Wenye taarifa zaidi mnaweza kuongea.

Maneno ya Malecela hayana mpango.

Alichofanya Mwakyembe, that's what's up.

Whether yuko wrong or right, unajua anaposimama.Sio mambo ya kupeleka issues into our sissy parliament ambako yule bureaucrat Samwel Sitta ataya filter na kuya censor mpaka watu waitiwe kikao cha chama na kuamulia issue behind closed doors ambako hata muandishi wa habari hataruhusiwa.Tushachoka hayo, so 1989!.

Mwakyembe ana michemsho fulani fulani hivi, mambo ya conflict of interest and all, lakini in the grand scheme of things Rostam ni fisadi kweli na Mwakyembe yuko sawa tu kum blast.

Ningependa kuona mtu msafi zaidi ya Mwakyembe anam blast Rostam, lakini sasa hivi inaonekana mtu pekee mwenye balls ni huyu Mwakyembe.

Mwacheni amblast Rostam tu.

Halafu zaidi ya hapo, Mwakyembe anatoa statement kwa Malecela, mzee wewe ni old school, kaa pembeni, watu tunapaka tu hatujali vikao vya CCM wala bunge.

Saafi sana.
 
Kuna tetesi ambazo nimezisikia hapa, nasema tetesi kwasababu siwaamini wanaozisema. Wanasema Dr. Mwakyembe anatafuta njia ya kuhamia CHADEMA.

Wanasema kwenye mkutano wa leo yule kijana wa CHADEMA aliyewahi kuwekwa ndani wakati ule wa ziara ya JK ndiye alikuwa mbele katika waandaaji. Pia wanataja uhusiano wa Dr. Mwakyembe na Mbowe pamoja na Mengi kama sababu za kuamini hivyo.

Pia inaelekea kuna mpambano mkali unaandaliwa Kyela 2010 kati ya Dr. Mwakyembe na jamaa mmoja nasikia yuko nje ya nchi.

Mimi nilikuwa hapa kwa muda na niliyoyaona leo sina hamu, hii wilaya imegawanyika kweli kweli. Sikuona viongozi wowote wa CCM pale mbele badala yake kulikuwa na wapambe wa mheshimiwa waliokuwa wanamwaga sifa kibao.

Angalieni hili jimbo 2010 inaelekea kutakuwa na vituko.

Nani anayemwandaa huyu jamaa ama jamaa anajiandaa mwenyewe
 
Mwakyembe kujiunga na CHADEMA sioni kama ni tatizo, lakini huu si wakati muafaka wa kufanya hivyo kama kweli ana nia ya kujiengua CCM. Kwa maoni yangu Mwakyembe ana nafasi nzuri zaidi ya kubaki CCM na kupambana na mafisadi akiwemo ndani ya chama hicho. Akiamua kuingia CHADEMA wakati huu basi CCM itammaliza kabisa kisiasa maana mashambulizi dhidi yake yatakuwa si ya kawaida lakini hawatakuwa tayari kumshambulia akiwemo ndani ya CCM.

Sidhani kama atahama CCM sasa, kinachosemwa ni kwamba akishindwa 2010 huko jimboni kwake atahamia CHADEMA kwa kisingizio kwamba mafisadi wamefanya mipango ili yeye aangushwe. Hiyo ndio strategy ya Dr. Mwakyembe kwasasa. Na jinsi leo alivyokuwa anaongea, napata hisia kwamba huenda mtaji wa Dr. kwa mwaka 2010 ni vita dhidi ya ufisadi.

Tatizo linaweza kutokea pale atakapokuja mtu mwingine ambaye hana uhusiano na mafisadi. Kuna mfanyabiashara mmoja aliashaanza kujitangaza kugombea, nasikia ana uhusiano na akina Lowassa na pia hana elimu kubwa. Alikuwa amefit vizuri kwenye huo mtego wa Dr. Mwakyembe. Ghafla upepo umebadilika, sasa kuna watu wengine wanatajwa wakiwemo ambao walimwunga mkono Dr. hiyo 2005. Hapo ndipo kazi inaanza kuwa ngumu na pressure kupanda.

Hawa CCM watamalizana kweli 2010.
 
Sidhani kama atahama CCM sasa, kinachosemwa ni kwamba akishindwa 2010 huko jimboni kwake atahamia CHADEMA kwa kisingizio kwamba mafisadi wamefanya mipango ili yeye aangushwe. Hiyo ndio strategy ya Dr. Mwakyembe kwasasa. Na jinsi leo alivyokuwa anaongea, napata hisia kwamba huenda mtaji wa Dr. kwa mwaka 2010 ni vita dhidi ya ufisadi.

Tatizo linaweza kutokea pale atakapokuja mtu mwingine ambaye hana uhusiano na mafisadi. Kuna mfanyabiashara mmoja aliashaanza kujitangaza kugombea, nasikia ana uhusiano na akina Lowassa na pia hana elimu kubwa. Alikuwa amefit vizuri kwenye huo mtego wa Dr. Mwakyembe. Ghafla upepo umebadilika, sasa kuna watu wengine wanatajwa wakiwemo ambao walimwunga mkono Dr. hiyo 2005. Hapo ndipo kazi inaanza kuwa ngumu na pressure kupanda.

Hawa CCM watamalizana kweli 2010.

Mbona huyo jamaa hajawahi kufanya kazi bongo sasa Mwakyembe mchecheto wa nini?
 
Kana -Ka-Nsugu,
Mkuu wangu katika siasa siku zote ni Offense tu usitake kujisafisha hata siku moja mahala ambapo huna ulazima kwa sababu watu wanakufahamu vizuri zaidi ya unavyofikiria..DUkiwa defensive mara nyingi unaacha mwanya wa watu kukushambulia na mara nyingi unaweza fanya kosa ambalo hukulitegemea litatafsirika vibaya... ikitoka imetoka mkuu wangu.
Mwakyembe kwa kila hali mgonvi wake ni Rostam na kisiasa inatakiwa amvurugevuruge hadi wananchi waamini kile anachowakilisha. hayupo pale kujiwakilisha/kujisafisha yeye bali kulinda maslahi ya wananchi na jinsi gani wananchi wajihadhari na watu kama Rostam..
Nimefurahi sana kuona usiri wa huyu Rostam unaanza kutoka kwani watu wengi wanampa heshima na kumwogopa wakifikiria ni Kichwa fulani hivi.. huyu kajaliwa tu Mifedha na Personality ambayo kwa namna fulani ni tishio la walalahoi..
 
Sio popcorn tena sasa inabidi kupata kikombe cha kahawa tena Cappuccino maana ngoma ishaanza kunoga. Tusubiri RA kama sio wapambe wake sasa. Lazima watarusha kombora tu!

Whistling!!!
 
Mwakyembe na apumzike tu.. hana haja ya kumblast zaidi RA. Sote tunajua kuwa Rostam ni fisadi namba wani Tanzania.There is an Engish saying 'never argue with a fool' cause people might not notice the difference.

Sasa anapaswa kutueleza yale ambayo hakuyasema kwenye kamati ya Bunge ya Richmond. Ya Rostam tunayajua Mh. Mwakyembe
 
Back
Top Bottom