DPP: Ushahidi Kagoda unakaribishwa

Nyambala

JF-Expert Member
Oct 10, 2007
4,465
1,170
Du, kweli sasa naanza kuamini Rostam Aziz ndiye rais wa Tanzania. Yaani miaka yote hii hii kagoda inazungumziwa ndiyo leo DPP anaikumbuka??? Kwa nini asianze na ushahidi kutoka tume ya Mwema na Mwanyika ile ya kuchunguza EPA?

Hapa hakuna ubishi, kinachotafutwa si ushahidi bali kumsafisha RA, baada ya kutajwa kwenye magamba. Hivi kweli TZ tupo siriazi? Namna hii hata miaka 300 hilo linchi halitaendelea. pambaaaaaaaaaffff!

DPP akaribisha ushahidi kuhusu Kagoda

Thursday, 05 May 2011
Patricia Kimelemeta


MKURUGENZI wa Mashtaka Nchini, Eliezer Feleshi, amewataka wananchi wenye ushahidi kuhusu Kampuni ya Kagoda Agricultural Limited, inayodaiwa kuchota Sh40 bilioni za EPA, kuwasilisha katika ofisi yake au polisi, ili ufanyiwe kazi.

Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu jijini Dar es Salaam juzi, Feleshi alisema, ofisi yake inahitaji ushahidi kuhusu kampuni hiyo ili kurahisisha kazi ya upelelezi.Wito huo wa Mkurugenzi, unafuatia madai ya baadhi ya wanasiasa kuwa wana ushahidi kuhusu wamiliki halali wa kampuni hiyo na kwamba serikali ikiwahitaji, watakuwa tayari kutoa ushirikiano.

Alisema ofisi yake anawakaribisha watu wote wenye ushahidi au taarifa kuhusu kampuni hiyo ili iufanyie kazi, itakayowawezesha wamiliki, kufikishwa mahakamani."Nawakaribisha wananchi wenye ushahidi au taarifa kuhusu Kampuni ya Kagoda, kuwasilisha katika ofisi yangu ili tuweze kuufanyia kazi," alisema Feleshi.

Mkurugenzi huyo wa mashtaka pia aliwataka wananchi kuwa na tabia ya kusaidiana na polisi au ofisi yake katika kukabiliana na uhalifu ili kumaliza tatizo hilo.

Alisema haipendezi watu kulalamikia mambo hayo nje ya utaratibu au taasisi zilizowekwa kisheria, kuyashughulikia mambo. Feleshi, alisema serikali ni ya watu wote na sheria zinampa kila mtu nafasi ya kutoa ushahidi kuhusu taarifa mbalimbali,iwe Kagoda au nyingine.
"Lengo ni kuisadia serikali kupambana na ufisadi," alisema .

Alisema, kila idara imetengewa majukumu yake na wajibu wa ofisi yake ni kusikiliza ushahidi au taarifa mbalimbali ikiwamo ushahidi kuhusu tuhuma za ufisadi wa Kagoda ili ziweze kufanyia kazi."Jamii inaweza kuwa chanzo kizuri cha taarifa kamili kuliko ofisi yangu, kwa hiyo jamii inapaswa kutoa ushirikiano.

Kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ni miongoni mwa kampuni 22 zinazodaiwa kuchota Sh133 bilioni za EPA.

Imedaiwa kuwa kampuni hiyo inamilikiwa na baadhi ya vigogo wa kisiasa na wafanyabiashara wakubwa. Hata hivyo,Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA),wamedai kuwa, wamiliki wa kampuni hiyo ni John Kyomuhendo na Francis William na kwamba ilisajiliwa Septemba 22 mwaka 2005 na kupata hati yenye namba 54040.

Inadaiwa kuwa ofisi yake iko katika kiwanja namba 87 kilichoko katika eneo la Viwanda la Kipawa, jijini Dar es Salaam.

 
DPP asitufanye mafala Watz! Aende katika benki ya Dr Kimei (CRDB) na akahoji wahusika na kuomba kumbukumbu kuhusu nani au akina nani waliyokwenda kuchukua hela hiyo kutoka akaunti sita zilizofunguliwa ktk matawi ya benki hiyo na Kagoda. Akaunti hizo zilikuwa zimepokea hela kutoka BoT.

Hakika CRDB wanazo kumbukumbu ni akina nani walizichukuwa hela hizo kutoka CRDB! Narudia DPP na Hosea pia wasitufanye siye mafala kwani mwanachi wa kawaida hawezi akafanya hiyo kazi ya kukusanya ushahidi huo kutoka CRDB, ni wao (DPP/Hosea) ndiyo chini ya sheria wana uwezo wa kufanya hivyo!

Jamani, tunazungushwa hadi lini?
 
Yaani nimekasirikaaaa hadi unajiuliza hawa watu hata kufanya maigizo ya kwenye movie hawawezi? Anataka tumpatie vipengele vya sheria vinavyompa yeye madaraka ya kufanya kazi ya Mwerndesha Mashtaka Mkuu wa Taifa hili? gademu!! Halafu utasikia keshokutwa "Rais amwagia sifa DPP"!!!
 
Stori za namna hii itabidi nibuni mbinu mpya ya kuzikwepa kuzisoma, ya zamani naona haifanyi kazi tena... :(
 
Feleshi aidha ni maamuma au mbumbumbu wa sheria pamoja na kwamba kakalia kiti cha mtu anayepashwa kubobea ktk sheria.
Kufungua akaunti ya biashara pale CRDB uahitaji mdhamini - lazima kuna kumbukumbu benki.
Kuna kesi ya madai imefunguliwa mahakamani kati ya Kagoda na makampuni ya Quality Group yanayomilikiwa na Manji (wamedhulumiana.....?). Huyu DPP Feleshi naye ni swahiba, rafiki au shoga wa mafisadi?
 
can somebody fire this mxxxxyyyyffjckjer!!! what the @##$$K!!!
Anyone who doesn't take truth seriously in small matters cannot be trusted in large ones either. Hapa DPP anamaanisha kwamba yeye hana ushahidi wa kumpeleka huko mnakotaka. Magamba ni magumu kuliko ya kobe wa nchi kavu!.

 
Hata mimi na sisitiza kuwa RA ndo Rais wa hii nchi tupende tusipende. Huyu dpp ni mtu mdogo sana kwa RA, hawezi kufanya kitu pasipo mkuu wake kujua anataka kufanya nini.
Hivi office kama ya dpp haiwezi kuwa a completely independent organ ambayo inaweza kufanya kazi yake bila kuwa chini ya serikali? Inaonyesha hii office inafanya kile ambacho Raisi anataka.
Tuliona hata ile geresha ya kuwapeleka akina Mramba tumeona ni wazi kabisa hii kitu ilikuwa planned tu ili kutupiga changa la macho wakati wa uchaguzi.
Hakuna nia ya serikali ya kushughulikia issue za Epa na dowans maana wakubwa ndo wahusika wakubwa.

Dawa ipo moja tu ni NGUVU YA UMMA kuingilia kati kunusuri hii hali. Sheria ni nzuri kwa nchi zilizoendelea maana haki hutendeka, ila kwa nchi maskini sidhani kama tunahitaji kusbiri sheria zitutendee haki.

We will wait until we are all gone! Kama tuna mapenzi mema na hii nchi wananchi ndiyo tunahitaji kuchukua hatua siyo vyombo vya sheria maana hatutafika tunakotaka kufika kwa mtindo huu PERIOD
 
Jamani mods watu kama DDP na Hosea, mimi nitakuwa nawatukana matusi ya nguoni na wazazi wao live . Gari tan 50 haliwezi kufaulisha mzigo tan 50 kwenye pick up. Hawana busara, kila kitu wanacho wao.
 
DPP asitufanye mafala Watz! Aende katika benki ya Dr Kimei (CRDB) na akahoji wahusika na kuomba kumbukumbu kuhusu nani au akina nani waliyokwenda kuchukua hela hiyo kutoka akaunti sita zilizofunguliwa ktk matawi ya benki hiyo na Kagoda. Akaunti hizo zilikuwa zimepokea hela kutoka BoT.

Hakika CRDB wanazo kumbukumbu ni akina nani walizichukuwa hela hizo kutoka CRDB! Narudia DPP na Hosea pia wasitufanye siye mafala kwani mwanachi wa kawaida hawezi akafanya hiyo kazi ya kukusanya ushahidi huo kutoka CRDB, ni wao (DPP/Hosea) ndiyo chini ya sheria wana uwezo wa kufanya hivyo!

Jamani, tunazungushwa hadi lini?

Ni kweli mkuu. DPP na Hosea wanaonesha utoto sana, kuwagilibu watanzania kuwa hawana akili. Mtu baki kama mimi nina ushahidi ndo uutegemee, wakati ukweli uko wazi kwenye ma-banki fedha zilikoingia toka BOT na kutolewa na wajanja!!! Huu ji ujinga wa hali ya juu, taasisis za serikali kufanyia kazi mafisadi. Hata ukiwapa data halisi wataziharibu!!!!!!!!!!!!!!!!!pambaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaf!
 
can somebody fire this mxxxxyyyyffjckjer!!! what the @##$$K!!!
MMK naona machungu yanazidi japo hujanifikia, si bora angekaa kimya!!!!???? ....wenzetu ndio wanasema "common sense is not common"!!!! Fikiria, mbali na mshahara kutokana na nguvu zetu atalipwa na pension! Nimemuona Dr. A. Lwaitama jana kwenye TV show akisema "amkeni na kukataa mateso haya"
 
Ni bora kukaa kimya watu wakakudhania kuwa u mpumbav kuliko kuongea watu wakathibitisha kuwa u mpumbavu, DPP ni taasisi ya mashtaka nt investigatory organ, nlikuwa napita tu anyway.
 
Yaani nimekasirikaaaa hadi unajiuliza hawa watu hata kufanya maigizo ya kwenye movie hawawezi? Anataka tumpatie vipengele vya sheria vinavyompa yeye madaraka ya kufanya kazi ya Mwerndesha Mashtaka Mkuu wa Taifa hili? gademu!! Halafu utasikia keshokutwa "Rais amwagia sifa DPP"!!!


sababu ni Mot&*((*)er Fu)^**$%R mwenzake
 
Kama ameshindwa kupata ushahidi na anasubiri sisi wananchi tumletee basi hafai kuwa kwenye hiyo ofisi. Atupishe sisi tuje tukae hapo aone kama hata itachukua siku 3 kukushanya evidence zote muhimu. Yaani anatuona sisi wajinga kiasi hicho. Evidence tumpelekee yeye!!! He must do his homework well and not wait to copy from us. Kama yeye na mamlaka aliyonayo kisheria anajidai hana evidence anataka sisi raia wa kawaida tuzipate wapi. Na tukimpelekea kesi inageuzwa kwetu kuwa tumezigushi hizo documents. Kama watu wamemtafuta Osama na kumpata yeye anashindwa vipi kuzipata evidence na watu kila sehemu zinakopatikana ziko wazi kabisa.
 
Ndo maana nawaambia kazi imewashinda,msubiri dr Slaa awaelekeze maana siku izi mnasubiri kila kitu aseme kwanza. Kama hamna ushaidi iweje mzuie peoples power isiwatawale? Pia Nimesikia chama kipya cha siasa TRA (Tanzania revenue authority) kwenye gazeti la mwananchi wakisema eti kwa kuwa afsa wao Luoga alienda shule basi hawezi kuleta hasara serikalini. Kweli taifa limekwisha kama na TRA imeanza kuleta ngonjera!!
 
Back
Top Bottom