Nyambala
JF-Expert Member
- Oct 10, 2007
- 4,465
- 1,170
Du, kweli sasa naanza kuamini Rostam Aziz ndiye rais wa Tanzania. Yaani miaka yote hii hii kagoda inazungumziwa ndiyo leo DPP anaikumbuka??? Kwa nini asianze na ushahidi kutoka tume ya Mwema na Mwanyika ile ya kuchunguza EPA?
Hapa hakuna ubishi, kinachotafutwa si ushahidi bali kumsafisha RA, baada ya kutajwa kwenye magamba. Hivi kweli TZ tupo siriazi? Namna hii hata miaka 300 hilo linchi halitaendelea. pambaaaaaaaaaffff!
DPP akaribisha ushahidi kuhusu Kagoda
Thursday, 05 May 2011
Patricia Kimelemeta
MKURUGENZI wa Mashtaka Nchini, Eliezer Feleshi, amewataka wananchi wenye ushahidi kuhusu Kampuni ya Kagoda Agricultural Limited, inayodaiwa kuchota Sh40 bilioni za EPA, kuwasilisha katika ofisi yake au polisi, ili ufanyiwe kazi.
Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu jijini Dar es Salaam juzi, Feleshi alisema, ofisi yake inahitaji ushahidi kuhusu kampuni hiyo ili kurahisisha kazi ya upelelezi.Wito huo wa Mkurugenzi, unafuatia madai ya baadhi ya wanasiasa kuwa wana ushahidi kuhusu wamiliki halali wa kampuni hiyo na kwamba serikali ikiwahitaji, watakuwa tayari kutoa ushirikiano.
Alisema ofisi yake anawakaribisha watu wote wenye ushahidi au taarifa kuhusu kampuni hiyo ili iufanyie kazi, itakayowawezesha wamiliki, kufikishwa mahakamani."Nawakaribisha wananchi wenye ushahidi au taarifa kuhusu Kampuni ya Kagoda, kuwasilisha katika ofisi yangu ili tuweze kuufanyia kazi," alisema Feleshi.
Mkurugenzi huyo wa mashtaka pia aliwataka wananchi kuwa na tabia ya kusaidiana na polisi au ofisi yake katika kukabiliana na uhalifu ili kumaliza tatizo hilo.
Alisema haipendezi watu kulalamikia mambo hayo nje ya utaratibu au taasisi zilizowekwa kisheria, kuyashughulikia mambo. Feleshi, alisema serikali ni ya watu wote na sheria zinampa kila mtu nafasi ya kutoa ushahidi kuhusu taarifa mbalimbali,iwe Kagoda au nyingine. "Lengo ni kuisadia serikali kupambana na ufisadi," alisema .
Alisema, kila idara imetengewa majukumu yake na wajibu wa ofisi yake ni kusikiliza ushahidi au taarifa mbalimbali ikiwamo ushahidi kuhusu tuhuma za ufisadi wa Kagoda ili ziweze kufanyia kazi."Jamii inaweza kuwa chanzo kizuri cha taarifa kamili kuliko ofisi yangu, kwa hiyo jamii inapaswa kutoa ushirikiano.
Kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ni miongoni mwa kampuni 22 zinazodaiwa kuchota Sh133 bilioni za EPA.
Imedaiwa kuwa kampuni hiyo inamilikiwa na baadhi ya vigogo wa kisiasa na wafanyabiashara wakubwa. Hata hivyo,Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA),wamedai kuwa, wamiliki wa kampuni hiyo ni John Kyomuhendo na Francis William na kwamba ilisajiliwa Septemba 22 mwaka 2005 na kupata hati yenye namba 54040.
Inadaiwa kuwa ofisi yake iko katika kiwanja namba 87 kilichoko katika eneo la Viwanda la Kipawa, jijini Dar es Salaam.
Hapa hakuna ubishi, kinachotafutwa si ushahidi bali kumsafisha RA, baada ya kutajwa kwenye magamba. Hivi kweli TZ tupo siriazi? Namna hii hata miaka 300 hilo linchi halitaendelea. pambaaaaaaaaaffff!
DPP akaribisha ushahidi kuhusu Kagoda
Thursday, 05 May 2011
Patricia Kimelemeta
MKURUGENZI wa Mashtaka Nchini, Eliezer Feleshi, amewataka wananchi wenye ushahidi kuhusu Kampuni ya Kagoda Agricultural Limited, inayodaiwa kuchota Sh40 bilioni za EPA, kuwasilisha katika ofisi yake au polisi, ili ufanyiwe kazi.
Akizungumza na Mwananchi katika mahojiano maalumu jijini Dar es Salaam juzi, Feleshi alisema, ofisi yake inahitaji ushahidi kuhusu kampuni hiyo ili kurahisisha kazi ya upelelezi.Wito huo wa Mkurugenzi, unafuatia madai ya baadhi ya wanasiasa kuwa wana ushahidi kuhusu wamiliki halali wa kampuni hiyo na kwamba serikali ikiwahitaji, watakuwa tayari kutoa ushirikiano.
Alisema ofisi yake anawakaribisha watu wote wenye ushahidi au taarifa kuhusu kampuni hiyo ili iufanyie kazi, itakayowawezesha wamiliki, kufikishwa mahakamani."Nawakaribisha wananchi wenye ushahidi au taarifa kuhusu Kampuni ya Kagoda, kuwasilisha katika ofisi yangu ili tuweze kuufanyia kazi," alisema Feleshi.
Mkurugenzi huyo wa mashtaka pia aliwataka wananchi kuwa na tabia ya kusaidiana na polisi au ofisi yake katika kukabiliana na uhalifu ili kumaliza tatizo hilo.
Alisema haipendezi watu kulalamikia mambo hayo nje ya utaratibu au taasisi zilizowekwa kisheria, kuyashughulikia mambo. Feleshi, alisema serikali ni ya watu wote na sheria zinampa kila mtu nafasi ya kutoa ushahidi kuhusu taarifa mbalimbali,iwe Kagoda au nyingine. "Lengo ni kuisadia serikali kupambana na ufisadi," alisema .
Alisema, kila idara imetengewa majukumu yake na wajibu wa ofisi yake ni kusikiliza ushahidi au taarifa mbalimbali ikiwamo ushahidi kuhusu tuhuma za ufisadi wa Kagoda ili ziweze kufanyia kazi."Jamii inaweza kuwa chanzo kizuri cha taarifa kamili kuliko ofisi yangu, kwa hiyo jamii inapaswa kutoa ushirikiano.
Kampuni ya Kagoda Agricultural Limited ni miongoni mwa kampuni 22 zinazodaiwa kuchota Sh133 bilioni za EPA.
Imedaiwa kuwa kampuni hiyo inamilikiwa na baadhi ya vigogo wa kisiasa na wafanyabiashara wakubwa. Hata hivyo,Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA),wamedai kuwa, wamiliki wa kampuni hiyo ni John Kyomuhendo na Francis William na kwamba ilisajiliwa Septemba 22 mwaka 2005 na kupata hati yenye namba 54040.
Inadaiwa kuwa ofisi yake iko katika kiwanja namba 87 kilichoko katika eneo la Viwanda la Kipawa, jijini Dar es Salaam.