3squere
JF-Expert Member
- Aug 2, 2011
- 925
- 181
[h=3]DOKII SASA AKIMBILIA KUIMBA SIASA[/h]
Msanii wa maigizo nchini Dokiiiamesema kwa sasa ameamua kujikita zaidi katika kuimba muziki wa siasa katika kampeni mbalimbaki za Chama cha Mapinduzi (CCM) ili kumuunga mkono mama yake ambaye ni Mwanachama wa Chama hicho.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam Dokii alisema muziki wa bongo fleva ameuweka pembeni na kwamba atakuwa akiimba zaidi muziki wa siasa na kuigiza filamu mbalimbali.
Kwa sasa nimeweka muziki pembeni unajua tena mama yangu ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa(Nec) nimeona nimuunge mkono kuimba nyimbo za kampeni na zinazohusu CCM,alisema.
Pamoja na kuimba nyimbo za siasa alisema nia yake sio kuja kugombea Ubunge baadaye bali amevutiwa mwenyewe na Chama hicho kwani atakuwa anatumia kipaji chake cha uimbaji kuelimisha jamii masuala ya siasa.
Alisema pia pamoja na kuimba muziki wa siasa pia anaendelea na harakati za kuigiza katika filamu na sasa tayari wameshatoa filamu mbili zinazoitwa sista duu na machepele.
Alisema baada ya siku mbili filamu hizo zitakuwa sokoni hivyo mashabiki wake wasikate tamaa wataendelea kumuona katika filamu mbalimbali na kuomba wamuunge mkono kwa kununua kazi hizo.
Msanii wa maigizo nchini Dokiiiamesema kwa sasa ameamua kujikita zaidi katika kuimba muziki wa siasa katika kampeni mbalimbaki za Chama cha Mapinduzi (CCM) ili kumuunga mkono mama yake ambaye ni Mwanachama wa Chama hicho.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam Dokii alisema muziki wa bongo fleva ameuweka pembeni na kwamba atakuwa akiimba zaidi muziki wa siasa na kuigiza filamu mbalimbali.
Kwa sasa nimeweka muziki pembeni unajua tena mama yangu ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa(Nec) nimeona nimuunge mkono kuimba nyimbo za kampeni na zinazohusu CCM,alisema.
Pamoja na kuimba nyimbo za siasa alisema nia yake sio kuja kugombea Ubunge baadaye bali amevutiwa mwenyewe na Chama hicho kwani atakuwa anatumia kipaji chake cha uimbaji kuelimisha jamii masuala ya siasa.
Alisema pia pamoja na kuimba muziki wa siasa pia anaendelea na harakati za kuigiza katika filamu na sasa tayari wameshatoa filamu mbili zinazoitwa sista duu na machepele.
Alisema baada ya siku mbili filamu hizo zitakuwa sokoni hivyo mashabiki wake wasikate tamaa wataendelea kumuona katika filamu mbalimbali na kuomba wamuunge mkono kwa kununua kazi hizo.