MAKOLE
JF-Expert Member
- Feb 5, 2012
- 618
- 280
Nilibahatika kuwepo hapa Dodoma kwa muda wa majuma manne. Kwa kipindi nilichokuwepo katika mji huu wa Dodoma yapo mambo mengi ambayo kwa namna moja ama nyingine na pamoja na kuwa yanajulikanwa na baadhi ya wenye mamlaka katika nchi hii lakini bado iko haja ya Watanzania wayafahamu.
Hakika mji huu na wakazi wake wanashuhudia historia yenye kuuma na kutia uchungu mkubwa. Inawezekana pia Labda kwa sababu hii ndio maana Serikali bado kwa yakini haijaamua kuhamia rasmi Dodoma kama makao makuu yake. Kwa hili naomba kuwaalika watafiti wa masuala ya kisiasa kulitafiti hili la uhusiano kati ya nitakayoyaeleza na dhamira ya serikali ya kuhamishia makao yake makuu hapa Dodoma.
Nimeshaondoka Dodoma, walakini, bado kila nukta niwapo safarini naikumbuka hali ya aibu niliyoiona Dodoma, hakika yataka moyo mgumu kuweza kuvumilia yaliyopo mjini hapa.
Dodoma yapo haya yafuatayo:-
1. Asilimia kubwa sana ya wakazi wake ni MASIKINI wa kutupa, nadhani kila mtanzania analifahamu hili. Sio lengo langu kuwafahamisha suala hili. LAKINI
2. Asilimia kubwa ya ombaomba wa Dodoma ni watoto wadogo sana ambao kwa umri wao walitakiwa wawepo shuleni.
3. Watu hawa hawana makazi ya kudumu, hali hii hata katika mji wa Dar es Salaam pia ipo, kwani ifikapo usiku wengi wao hulala pale jua linapowachwea.
Nimepata fursa ya kutembelea sehemu inayoitwa Ng'ong'ona. Hapa ni jirani sana na kilipo kitivo cha Elimu Chuo kikuu cha Dodoma. Wanachuo wengi hufika kijijini hapo kupata mahitaji yao, hasa vyakula kwani kuna mlundikano wa migahawa mingi sana. Hapa ndipo nilipopata hisia za uchungu ambazo kwazo, nimeamua kuzitupa kwa Watanzania wenzangu:
1. Wengi wa wahudumu hapa ni watoto ambao pia ni wanafunzi wa Shule ya Msingi ama Sekondari ya Ng'ong'ona. Hawa huwa wanapanga siku za kunda shule na siku za kwenda kazini kutoa huduma kwa wanachuo kama vibarua..
2. Watoto wengine, kwa kukata tama ya hali ya maisha nyumbani huwa wanafika hapo ili kupata riziki zao. HAKIKA watanzania : Hawa hujitolea kuosha vyombo vinavyotumiwa kwa chakula na wateja kwa malipo ya AMA kula MABAKI YA VYAKULA VILIVYOBAKIZWA NA WATEJA au KUKWANGUA SUFURIA ambazo hupikia na kuloekewa maji ili zilainike, hivyo wao ndio wanapata ujira wao.
3. Kundi kubwa la watoto na wazee wao, hujongea maeneo ya mikahawa iliyopo ndani ya chuo mida ya chakula na husubiri hapo hadi pale watakapoitwa kwenda kuchukuwa mgao wao. Mgao huo aghalabu huwa ni "MAKOMBO" yaani mabaki ambayo yastahili wapewe mifugo kama mbwa, kuku nk. Wao hupewa huku wakiwa katika foleni.
4. Kwa watoto watukutu utawakuta badala ya kufikisha chakula nyumbani kwa kuwa kinasubiriwa na jamaa zao, wao huanza kutafuna mifupa njiani kwani wanajua fika kuwa watakapoifikisha nyumbani hawatapata mgao wa mfupa (kwa wao huo ndio mnofu).
5. Nimejaribu kumhoji kijana wa darasa la 3 hapa Ng'ong'ona p/r anasema kuwa wao wamezoea kula mara moja tu kwa siku, hivyo inawalazimu kuacha kwenda shule na kuranda randa ili apate riziki.
Hawa ndio watanzania ambao wakifeli mitihani tunalalamika, na pengine tunawalalamikia walimu.
Hawa ndio tunawaandaa waje kushika madaraka ya nchi baada ya sisi, waje kupambana na changamoto za mabadiliko ya dunia ya sasa.
Hii ni sehemu ndogo ya watanzania walioko msambweni, hapa ni eneo moja tu - Dodoma.
Tunawaandaa hawa wanafunzi katika mifumo dhaifu, Halafu tunaweka vikwazo katika elimu ya juu kuwa MIKOPO ITATOLEWA KULINGANA NA VIPAUMBELE, SAYANSI 100%. SIO HALALI, SIO HALALI.
Yatupasa kwa pamoja tupige kelele kwa vyombo husika, Jamii hii isaidiwe!
NAWASILISHA.
Hakika mji huu na wakazi wake wanashuhudia historia yenye kuuma na kutia uchungu mkubwa. Inawezekana pia Labda kwa sababu hii ndio maana Serikali bado kwa yakini haijaamua kuhamia rasmi Dodoma kama makao makuu yake. Kwa hili naomba kuwaalika watafiti wa masuala ya kisiasa kulitafiti hili la uhusiano kati ya nitakayoyaeleza na dhamira ya serikali ya kuhamishia makao yake makuu hapa Dodoma.
Nimeshaondoka Dodoma, walakini, bado kila nukta niwapo safarini naikumbuka hali ya aibu niliyoiona Dodoma, hakika yataka moyo mgumu kuweza kuvumilia yaliyopo mjini hapa.
Dodoma yapo haya yafuatayo:-
1. Asilimia kubwa sana ya wakazi wake ni MASIKINI wa kutupa, nadhani kila mtanzania analifahamu hili. Sio lengo langu kuwafahamisha suala hili. LAKINI
2. Asilimia kubwa ya ombaomba wa Dodoma ni watoto wadogo sana ambao kwa umri wao walitakiwa wawepo shuleni.
3. Watu hawa hawana makazi ya kudumu, hali hii hata katika mji wa Dar es Salaam pia ipo, kwani ifikapo usiku wengi wao hulala pale jua linapowachwea.
Nimepata fursa ya kutembelea sehemu inayoitwa Ng'ong'ona. Hapa ni jirani sana na kilipo kitivo cha Elimu Chuo kikuu cha Dodoma. Wanachuo wengi hufika kijijini hapo kupata mahitaji yao, hasa vyakula kwani kuna mlundikano wa migahawa mingi sana. Hapa ndipo nilipopata hisia za uchungu ambazo kwazo, nimeamua kuzitupa kwa Watanzania wenzangu:
1. Wengi wa wahudumu hapa ni watoto ambao pia ni wanafunzi wa Shule ya Msingi ama Sekondari ya Ng'ong'ona. Hawa huwa wanapanga siku za kunda shule na siku za kwenda kazini kutoa huduma kwa wanachuo kama vibarua..
2. Watoto wengine, kwa kukata tama ya hali ya maisha nyumbani huwa wanafika hapo ili kupata riziki zao. HAKIKA watanzania : Hawa hujitolea kuosha vyombo vinavyotumiwa kwa chakula na wateja kwa malipo ya AMA kula MABAKI YA VYAKULA VILIVYOBAKIZWA NA WATEJA au KUKWANGUA SUFURIA ambazo hupikia na kuloekewa maji ili zilainike, hivyo wao ndio wanapata ujira wao.
3. Kundi kubwa la watoto na wazee wao, hujongea maeneo ya mikahawa iliyopo ndani ya chuo mida ya chakula na husubiri hapo hadi pale watakapoitwa kwenda kuchukuwa mgao wao. Mgao huo aghalabu huwa ni "MAKOMBO" yaani mabaki ambayo yastahili wapewe mifugo kama mbwa, kuku nk. Wao hupewa huku wakiwa katika foleni.
4. Kwa watoto watukutu utawakuta badala ya kufikisha chakula nyumbani kwa kuwa kinasubiriwa na jamaa zao, wao huanza kutafuna mifupa njiani kwani wanajua fika kuwa watakapoifikisha nyumbani hawatapata mgao wa mfupa (kwa wao huo ndio mnofu).
5. Nimejaribu kumhoji kijana wa darasa la 3 hapa Ng'ong'ona p/r anasema kuwa wao wamezoea kula mara moja tu kwa siku, hivyo inawalazimu kuacha kwenda shule na kuranda randa ili apate riziki.
Hawa ndio watanzania ambao wakifeli mitihani tunalalamika, na pengine tunawalalamikia walimu.
Hawa ndio tunawaandaa waje kushika madaraka ya nchi baada ya sisi, waje kupambana na changamoto za mabadiliko ya dunia ya sasa.
Hii ni sehemu ndogo ya watanzania walioko msambweni, hapa ni eneo moja tu - Dodoma.
Tunawaandaa hawa wanafunzi katika mifumo dhaifu, Halafu tunaweka vikwazo katika elimu ya juu kuwa MIKOPO ITATOLEWA KULINGANA NA VIPAUMBELE, SAYANSI 100%. SIO HALALI, SIO HALALI.
Yatupasa kwa pamoja tupige kelele kwa vyombo husika, Jamii hii isaidiwe!
NAWASILISHA.