VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Niko hapa Dodoma tangu mwanzoni mwa juma hili. Nashuhudia mtifuano usio na mfano wa Wabunge wakiuliza maswali, wakichangia hoja na kadhalika. Nawashuhudia Wabunge ndani na nje ya Bunge hapa Dodoma.
Kumejitokeza Wabunge wa CCM wanaojichora kama wakosoaji wa utendaji wa Serikali ya Rais John Pombe Magufuli. Wabunge hao wamejichora kwa kauli, michango na hoja zao. Wabunge hao wanahatarisha kupitishwa kwa Muswada wa Sheria ya Vyombo vya Habari.
Dawa ya Wabunge hao imepatikana. Ndani ya CCM hakishindikani kitu. Maelekezo yametolewa kwa viongozi wa Wabunge wa CCM kuwasilisha majina na 'hoja-korofishi' za Wabunge hao ili wajadiliwe na 'kuonywa' kichama. Kuna mkutano maalum wa Wabunge wa chama (party caucus) utaitishwa kwa ajili yao.
Pamoja na hayo mambo ya kichama na udhibiti wake, naliona Bunge likirudi katika kuisimamia Serikali. Linarudi kwenye mstari!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
Kumejitokeza Wabunge wa CCM wanaojichora kama wakosoaji wa utendaji wa Serikali ya Rais John Pombe Magufuli. Wabunge hao wamejichora kwa kauli, michango na hoja zao. Wabunge hao wanahatarisha kupitishwa kwa Muswada wa Sheria ya Vyombo vya Habari.
Dawa ya Wabunge hao imepatikana. Ndani ya CCM hakishindikani kitu. Maelekezo yametolewa kwa viongozi wa Wabunge wa CCM kuwasilisha majina na 'hoja-korofishi' za Wabunge hao ili wajadiliwe na 'kuonywa' kichama. Kuna mkutano maalum wa Wabunge wa chama (party caucus) utaitishwa kwa ajili yao.
Pamoja na hayo mambo ya kichama na udhibiti wake, naliona Bunge likirudi katika kuisimamia Serikali. Linarudi kwenye mstari!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)