Hebu kajambe mbele siyo lazima kila thread ukate viuno wakati hujui lolote.
Lakini ndugu yangu Matola, hivi kwani ungeandika DMV ni jumuiya au chama cha watanzania wanaoishi, mji kuu wa Marekani yaani Washington DC kwa maana ya District of Columbia, jimbo la Maryland na la Virginia (DMV) ingekugharimu nini? Wakati mwingine sio kila mtu anayekuja hapa anaelewa hayo mambo makubwa ya huko uzunguni. Wengine wanauliza kwa ajili ya kuwasaidia wengine waelewe vizuri kile ulichotaka kieleweke, kwa hiyo ushirikiano ni muhimu ili ulicholenga kifike kwa hadhira yako kinafika ipasavyo.